Mapinduzi ya Zanzibar: Mchango wa John Okello (Che Guevara wa Afrika Mashariki) umefutwaje?


We tapeli umemplipa Oluoch
 
Last edited by a moderator:
So notorious. Unatukebehi. Tungejuaje historia ya mapinduzi kama wale walioshiriki wasingetukalisha chini na kutusomesha. Tungeliyakuaje ya Kipumbwi na Sakura kama Victor Mkello na Mzee Mkwawa wasingetufungulia milango ya.siri ile nzito? Dr. Ghassany alifanya utafiti. Kapita maktaba nyingi America na Uingereza hadi nyumbani kwa Mzee Mkwawa Makorola Tanga na Nguvumali. Huko hakuonyeshwa nyaraka. Kule alielezwa kuhusu kambi ya askari mamluki wa Kimakonde wakata mkonge kutoka shamba la.Sakura waliokuwa wakifanya mazoezi porini. Regional Commissioner Jumanne Abdallah na Area Commissioner Ali Mwinyi Tambwe wote wakisimamia mpango ule. Dr. Ghassany hakuyakuta haya katika utafiti wake Library of Congress Washington wala Rhodes House Oxford. Haya kaja elezwa Tanga Makorola na Nguvumali na watu ambao hakuna aliyekuwa anajua mchango wao. Hakika kwa kiasi chetu tunaijua historia ya mapinduzi.
 
Tatizo ni kuwa ukweli wa mapinduzi anaujua Mohamed Said na Harith watu wengine wote walikuwa wajinga na vipofu wakati mapinduzi yanatokea

SoNotorious,
Unatukebehi.
Hii si dalili nzuri kwako.

Inaonyesha kushindwa na hoja zangu.
Mimi huwa sizungumzi kile nisichokijua naogopa kufedheheka.

Tungejuaje historia ya mapinduzi kama wale walioshiriki hasa
wasingetukalisha chini na kutusomesha?

Tungeliyakuaje ya Kipumbwi na Sakura kama Victor Mkello na
Mzee Mkwawa wasingetufungulia milango ya siri ile nzito ya
mamluki wa Kipumbwi?

Dr. Ghassany alifanya utafiti wa miaka.

Kapita maktaba nyingi Amerika na Uingereza hadi nyumbani kwa
Mzee Mkwawa Makorola Tanga na Nguvumali.

Huko hakuonyeshwa nyaraka.

Kule alielezwa kuhusu kambi ya askari mamluki wa Kimakonde
wakata mkonge kutoka shamba la Sakura waliokuwa wakifanya
mazoezi ya kuvamia Zanzibar porini.

Regional Commissioner Jumanne Abdallah na Area Commissioner
Ali Mwinyi Tambwe wote wakisimamia mpango ule.

Ali Mwinyi Tambwe alikuwa mmoja wa watu ambao hawakutaka
ijulikane kuwa alihusika katika mapinduzi.

Ali Mwinyi Tambwe alikataa kuzungumza na marehemu Prof.
Haroub Othman
alipomgusia habari ya mapinduzi.

Nafsi yake iliingia hofu kubwa alipokujajua watu waliouliwa katika
mapinduzi yale.

Dr. Ghassany hakuyakuta haya ya Sakura, Kipumbwi na mamluki
wa Kimakonde katika utafiti wake Library of Congress Washington
wala Rhodes House Oxford.

Haya kaja elezwa Tanga Makorola na Nguvumali na watu ambao
hakuna aliyekuwa anajua mchango wao.

Hakika kwa kiasi chetu tunaijua historia ya mapinduzi.

Ilimchukua miaka mitatu kwa Dr. Ghassany kuweza kumshawishi
Victor Mkello kumuamini kuwa likuwa ni mtafiti wa kweli na wala
hatoki International Criminal Court (ICC) Hague ndipo alipokubali
kuongea.

Mimi nilikuwapo katika mahojiano yote ya miaka mitatu ya nyuma
isipokuwa huu wa mwisho alipofunguka na kueleza ukweli wa yale
waliyofanya katika kuivamia Zanzibar kutoka Kipumbwi.

Mimi nilibaki nje nimeegesha gari yangu msikitini.

Nilijua kuwa hii ndiyo ile kubwa yake nilitaka Dr. awe na ''one on
one,'' na Mzee Mkello.

Baadae Dr Ghassany aliniambia kuwa mama yetu mkewe Mzee
Mkello
alikuwapokatika mazungumzo yale na sababu yake ni kuwa
Mzee Mkello alitaka ili akikosea au kusahau jambo amkumbushe.

Soma ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,'' umsikilize nini Mkello
alisema.

Baada ya Dr. Ghassany kueleza yale yaliyopitika Kipumbwi kati
ya 1961 na 1964 kwa watu kuvushwa kutoka Tanganyika kwenda
kuipigia kura ASP watafiti wengi wa nje wakataka kuja Tanga
kufanya uthibitisho.

Picha hiyo hapo chini mmoja wa watafiti kutoka Marekani akimhoji
Mama Mkello nyumbani kwake Nguvumali, Tanga.

 
Last edited by a moderator:

Philomon Mikael,
Nakuomba hebu linganisha maelezo uliyobandika na jibu langu kwa
SoNotorious.

Naamini utaona mpishano uliokuwapo.
Mapinduzi ya Okello ni mapinduzi ya kuzuka usiku mmoja.

Mapinduzi niliyoeleza mimi kwa kumnukuu Dr. Harith Ghassany ni
mapinduziyaliyopangwa na kuratibiwa na wajuzi wa mipango -
Abdullah Kassim Hanga,Oscar Kambona juu kwenye kinara.

Chini yao kwenye ''Zone of Operation,'' kuna maofisa wa serikali ya
Tanganyika-Jumanne Abdallah na Ali Mwinyi Tambwe.

Chini ya hawa kuna Mohamed Omar Mkwawa na Victor Mkello.

Hawa ndiyo walikuwa wakiwasiliana na mamluki wa Sakura na
Kipumbwi.

Nadhani hii ''Chain of Command,'' unaiona.
Nani anawajibika kwa nani na kwa kipi.

Mzee Mkwawa anasema hata siku moja Kambona wala si Hanga
walifika kambini Kipumbwi kuzungumza na ''askari.''

Simlazimishi mtu kuamini yale aliyoeleza Dr. Ghassany kwenye
kitabu chake, ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru'' lakini Waswahili
tuna msemo, "Penye ukweli uongo hujitenga.''
 
Last edited by a moderator:

Nmekisoma kitabu cha Dr.Ghassany nmejifunza mambo mengi kwenye icho kitabu...hata wewe mwenyewe nmesoma vitabu vyako nmejifunza mambo mengi....

Lakini mpo wabinafsi sana na hiyo inawezekana kwa makusudi au kutokana na historia ya maonevu ambayo umeyapointi kwenye maandiko yako mengi...mfano pale unaposema eti Okello akuweza kuandika kitabu kama kile napata wasiwasi na wewe.....hivi kuna tofauti gani kati ya kuandika wewe mwenyewe na kumuadithia mtu akaandika kile unachokijua...na wewe unatupa sababu gani ili tuziamini sources zako.

Historia imeamua iwe hivyo na kamwe hamuwezi kuibadilisha...niliposomaga kitabu cha mabadiliko cha uchina ya kale #i_ching nilijifunza mambo mengi sana.

Dr.ghassany na wewe ni wanaharakati wa kiislamu na icho kitu dunia imeshajua....pro Islamic wahhabism.

Ndio maana kila mnachoonge lazima mtaje uislamu.....ying yang....mmeshindwa kwa karne nyingi na huo ndio ukweli..
 

Chuma Cha Reli,
Hakika mimi ni Muislam na natafakhari na kumshukuru Allah kwa kunijaalia
Uislam iwe dini yangu.

Hilo kuwa mimi ni Mhabi...
Siyo na ningelikuwa ningelikufahamisha bila wasiwasi wowote.

Huwa sifichi kile ninachokiamini.

Kuwa mimi ni mbinafsi hilo umesema wewe na ni fikra zako siwezi kabisa
kukuingilia.

Ikiwa sasa unasema kuwa Okello hakuandika kitabu kile ila alimhadithia
mtu na yeye akaandika hapo tumekwenda kwengine.

Wewe umesogea mbele kutoka Okello mwandishi kwenda kwa Okello
muhadithiaji stori.

Hili la kuwa alimhadithia mtu yale aliyofanya Zanzibar sikuwa na haja ya
kuelezwa na mtu kwani lilikuwa dhahiri.

Alex Hailey aliandika "biography" ya Malcolm X...
Alibadilisha mambo mengi sana alipokufa Malcolm.

Hii ndiyo hatari ya kuandikiwa.
Nadhani sasa umenielewa.
 
Je Mwanamalundi vipi alifungwa kisiwa cha mwanamalindi pale bahari ya hindi si mbali sana na Dar lakini akaonyesha maajabu makubwa ya kutembea juu ya bahari kwenda Dar na kurudi, pia alipanda viazi vikakomaa kwa usiku mmoja tu. ndipo wakoloni walipoona power yake wakaamua kumuachia.
huyu ni shujaa wa kWELI MWANAMALUNDI . Alikuwa na uwezo wa kukusha miti kwa kunyoosha kidole tu yaani hizi historia zimefunikwa funikwa suji kwa nini. jamani tusaidiane kuziweka sawa.
 

Besty,
Sheikh Ali Muhsin Barwani wakati wa kupigania uhuru wa Zanzibar
alikuwa kiongozi wa Zanzibar Nationalist Party (ZNP) vilevile chama
hiki kikijulikana kama Hizbu. Kwa mapenzi makubwa wanachama
wa Zanzibar walikuwa wanamwita, "Zaim" yaani Kiongozi.

Ilikuwa ni ya Sheikh Ali Muhsin Zanzibar ipiganie uhuru wake chini
ya chama kimoja cha kizalendo chenye nguvu chama cha kitaifa
badala ya vyama vilivyojijenga katika misingi ya rangi.

Ilikuwa pigi kubwa sana kwake Abeid Amani Karume alipoasisi
Afro Shirazi Party, chama kilichosimama kwa maslahi ya Waafrika
na Washirazi.

Sheikh Ali Muhsin alipigania uhuru wa Zanzibar mpaka ukapatikana
tarehe 10 December 1963.

Sheikh Ali Muhsin alishiriki katika mkutano wa katiba Lancaster
House.

Baada ya mapinduzi yaliyotokea Zanzibar tarehe 12 Januari 1964
Sheikh Ali Muhsin alikamatwa na kusafirishwa Tanganyika ambako
alifungwa Ukonga na jela nyingine kwa kipindi cha miaka 10 na
miezi michache.

Katika kipindi alichokuwa kifungoni Sheikh Ali Muhsin aliandika
miswada kadhaa ambayo alikuja kuichapa kama vitabu baada ya
kutoka kifungoni.

Kabla hajafa mwaka 2006 Sheikh Ali Muhsin aliandika kitabu cha
maisha yake, ''Conflict and Harmony in Zanzibar,'' ambacho kilikuja
kufasiriwa kama ''Kujenga na Kubomolewa Zanzibar.''

Katika kitabu hiki cha maisha yake Sheikh Ali Muhsin anaeleza
yaliyopitika Zanzibar kabla na baada ya mapinduzi.

Baada ya kushindwa kupata pasi ya kusafiria, Sheikh Ali Muhsin
alitoroka nchini mwaka 1974.

Hadi anafariki siku zote Sheikh Ali Muhsin alikuwa akisema yale
hayakuwa mapinduzi bali mavamizi.
 

Mzee Said anabishana na video mbona Kambona na Hanga hatuwaoni hapo au ilikuwa haramu wao kujitokeza hadharani kuwa walisimamia mapinduzi na si Okello ? The problem the old guy wants to establish islamic connection in erything, hii sio sawa.
 
Mzee Said anabishana na video mbona Kambona na Hanga hatuwaoni hapo au ilikuwa haramu wao kujitokeza hadharani kuwa walisimamia mapinduzi na si Okello ? The problem the old guy wants to establish islamic connection in erything, hii sio sawa.

SoNotorious,
Hili la ''old guy wants to establish islamic connection in erything
(everything), hii sio sawa...''

Jibu la hilo ni dogo na fupi.

Ikiwa wewe una wengine zaidi waliofanya haya ambao si Waislam
tueleze weka taarifa zao hapa JF tutazisoma lakini usinilaumu mimi
kwa kuandika historia za watu ambao mimi nakua katika mitaa ya
Dar es Salaam nawaona na wengine wakiingia hadi majumbani kwa
wazee wetu.

Unauliza kwa nini Kambona na Hanga huwaoni kujitokeza hadharani...
Labda na mimi nikuongozee wengine kidogo ambao hawajajitokeza
hadharani hadi hii leo ingawa wako hai.

Hanga na Kambona wangelijitokeza hadharani kabla au baada ya
mapinduzi ingelijulikana kuwa Zanzibar ilivamiwa na mamluki kutoka
mashamba ya mkonge ya Sakura kwenda kupindua serikali ambayo
ilichaguliwa kihalali.

Isingeishia hapo dunia ingelitaka kujua nani alimtuma Kambona
kufanya yote aliyofanya na kusababisha mauaji ya maelfu ya watu.

Isingeishia hapo tu dunia ingelijua nani aulizwe kuhusu mauaji yale
yaliyotokea.

Hiki ndicho kilikuwa kitisho kikubwa.

Hii ndiyo sababu wote walikaa kimya pamoja na Victor Mkello,
Ali Mwinyi Tambwe
na Jumanne Abdallah.

Lililowatisha ni kuwa hawakutegemea kiasi kile cha mauaji.

Okello hakuwa chochote.
Okello alikuwa mpiga tarumbeta tu pale Raha Leo.

Viongozi wa mapinduzi na waliopanga mapinduzi yale Dr. Harith
Ghassany
kawaeleza katika kitabu chake, "Kwaheri Ukoloni Kwaheri
Uhuru.''

La mwisho.

Utapata tabu sana ikiwa kila unapoona majina ya Waislam katika
historia ya Tanganyika moyo unakuchoma.

Huwezi kuibadili historia hii.

Siku moja nilikuwa nazungungumza na Hamza Aziz basi kidogo
nikamchokoza kuhusu mapinduzi nikamwambia, ''Baba hebu nieleze
ukweli.''

Sikiliza jibu lake:

''Mimi nimekula kiapo cha kutunza siri siwezi kusema kitu ama
sivyo watanifunga. Mimi sasa nina miaka 74...''

Wakati ule wa mapinduzi Hamza Aziz ndiye alikuwa Inspector
General of Police (IGP).
 

Duh kumbe Sultan hakuwa mkoloni ? Kama alikuwa mkoloni kwa nini uone aibu na ujifiche kwa kufanya kitendo cha kishujaa cha kumtoa nduki mkoloni na kuwa Zanzibar huru ? Okello alivyojitokeza kama kiongozi wa mapinduzi mbona hakuguswa na mambo waliogopa kina Kambona na Hanga ? Hili la Aziz unamsingizia sijawahi kuona dying citizen at the age of 74 ambae hana cha kupoteza kuogopa jela tena mtu wa imani ambayo usipokuwa suicidal unakuwa assasin disciple.
 
SoNotorious,
Huko nyuma nilishamueleza Okello na nilisema alikuwa mtu mjinga...

Wajanja wote walikaa kimya.

Mtu mwerevu hajigambi katika hali ya mauaji kama yale yaliyotokea
Zanzibar.

Na kama Okello angeliendelea kuishi Zanzibar huenda angeliuliwa kwa
kulipiza kisasi.

Mimi sikulazimishi uniamini hata kidogo ikiwa unapenda kuamini kuwa
Hanga na Kambona sio walopanga mapinduzi au kambi ya Sakura na
Kipumbwi, Tanga haikuwako au mamluki wa Victor Mkello ni ndoto
zangu.

Yote kwangu sawa.

Lakini kaa ukijua pasi na shaka kuwa kuna watu wengi sana wanaamini
ninachowaeleza katika historia ya Tanganyika.
 

Mm mmoja wapo ktk mamilion ya watu tunaokuamini kwa parsent kubwa ya yale unayo tueleza na kukusoma ktk maandishi yako...m/zimungu akupe umri mrefu na afya njema zaidi akuzidishie upeo na ujasiri wa kutoficha ukweli amen.
 
Historia ipi ya nchi hii?si ndio hao maprofeseri waliobadilisha wauza watumwa kuwa mashujaa wetu.Historia hiyo ilindikwa sijui na wamanyema dar.Eti Mkwawa,kinjekitile,Abushir,Mirambo na makundi mengi ya kikabila km wamanyema, wayao etc walivyokuwa active kuuza watumwa na vita zao zilikuwa za kutetea uuzaji huo wa watumwa.Hadi leo Manyema wanajiona kuwa superior na miaka yao yote walijitenga na wabantu wengine kwa kujiona kuwa wao ni masters.Hadi leo hiyo tabia ya kuwapa majina mazuri maharamia ipo ndani ya ccm ..mafisadi,majambazi,wabakaji,wauaji wa wengine kwa risasi hadharani,etc ndio wanaoandika katiba,ndio wanaosimamia tume ,ndio wasafi.Wanaoamsha wengine kuhusu hayo,wanaitwa wazushi,wanaona wivu,wachonganishi na wanaotaka poteza amani yetu.Yote haya yameanzia ktk chuo cha kishetani UDSM chuo cha propaganda na tafiti za kisanii.
 
John Okelo hana historia wala ushujaa wowote - ni mwizi na jambazi ambae alipata fursa ya 'kupindua' serikali ya Zanzibar sababu ya hiana za waingereza tu.
 
Mnara mpya wa Michenzani wa kumbukumbu ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar mwaka 1964 uliogharimu mabilioni ya shilingi ungesherehesha zaidi kama ukapewa heshima ya jina la kiongozi mkuu wa Mapinduzi, Field Marshall John Okello. Mtu aliejitolea hali na mali kuwakomboa waafrika wenzake.

Historia itatuhukumu tukiliacha jina lake kupotea katika kumbukumbu za Mapinduzi ya Zanzibar. Kama Mapinduzi yale yasingelifanikiwa kichwa cha John Okello kingelikuwa cha kwanza kuchinjwa na kuangamizwa.

Nkweli yeye alikuwa si mzanzibari lakini mchango wake hauwezi kubezwa katika ukombozi na Mapinduzi ya Zanzibar.Che Guevara, mwana mapinduzi mwenzake kule Cuba amejengewa mnara wa kumbukumbu, kuthamini mchango wake wakati nae pia alikuwa sio Mcuba.
 
Last edited by a moderator:
Field Marshal John Okello ni "K.a.f.i.r.i" alieitoa Nchi ya Kislamu kutoka utumwani mwa Waislamu wenzao. Wampe haki yake.
 
Ngoja waje, shauri yako...unamzungumzia Yohana Mpambanaji John Okello aliyewasaidia waislamu watoke mikonon mwa utumwa wa waislamu wenzao? Huyu ------ mpambanaji aliyekuwa na upendo wa ajabu kwa watu ambao baada ya mapinduzi waliamua kumchukua na kumfuta kwenye historia yao? Laana hii itawaandama sana na mpaka siku wakija kutubu na kuutambua mchango wa yohana mpambanaji kidume ,jibaba mkombozi wa visiwa vya unguja na pemba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…