Mapinduzi ya Zanzibar: Mchango wa John Okello (Che Guevara wa Afrika Mashariki) umefutwaje?

Mkuu Gsana, wewe ulimsikia kwa masikio yako mwenyewe Mama Fatma Karume akiongea hayo?.
Mimi pia niliwahi kumuona na kumsikia Mama Fatma Karume akiongea haya kuhusu siku ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar.

P
 
OKELO ALIRUDI KWAO UGANDA NA KUFIA HUKO KWA WACHOLI WENZAKE, NYERER ALIMZAWADIA GARI NA PESA ZA MAFUTA ILI ARUDI NYUMBANI SALAMA ,LAKINI ALIPATA AJALI NJIANI NA AKANUSURIKA KUFA ILA GARI IKAWA RIGHT OFF,HAPO AKALA BODA KWA MABASI HADI ACHOLI.
 
OKELO ALIRUDI KWAO UGANDA NA KUFIA HUKO KWA WACHOLI WENZAKE, NYERER ALIMZAWADIA GARI NA PESA ZA MAFUTA ILI ARUDI NYUMBANI SALAMA ,LAKINI ALIPATA AJALI NJIANI NA AKANUSURIKA KUFA ILA GARI IKAWA RIGHT OFF,HAPO AKALA BODA KWA MABASI HADI ACHOLI.

okelo alikua mkenya
 
Kwadwo. Unataka watu wa Unguja na watu wa Pemba wamtambuwe Okello? Okello hakutambuliwa na ASP wala TANU leo atatambuliwa na Wazanzibari. Hebu nioneshe wapi alipotajwa na vyama hivyo kwamba yeye ndie shujaa. Okello alikua mdini na ndio kilichomponza eti anasema kwamba kapindua kwaajili ya Ukristo?.
 
sawa sawa
 
ev uyu chegevara nimtu ainagan mwalabu mcyopia au
 
Kumbe?
 
Uongo,kwanza Acholi ni kabila siyo sehemu
OKELO ALIRUDI KWAO UGANDA NA KUFIA HUKO KWA WACHOLI WENZAKE, NYERER ALIMZAWADIA GARI NA PESA ZA MAFUTA ILI ARUDI NYUMBANI SALAMA ,LAKINI ALIPATA AJALI NJIANI NA AKANUSURIKA KUFA ILA GARI IKAWA RIGHT OFF,HAPO AKALA BODA KWA MABASI HADI ACHOLI.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yan bro the article is there natumesoma na tumeelewa kwamba okello was not who u think he is was crazy we can that say that in accordance with the the article so why don't we shut up and believe that I know u just want to talk abt him even after knowing the truth just because u want to push the talk LETS BE CIVILIZED

 
OKELLO BABA WA TAIFA LA ZANZIBAR .ALIYEWAOKOA WAZANZIBAR TOKA ITUMWANI NA BADO HAWAMTAMBUI.


 
Leo tarehe 12 January ni Sikukuu ya Mapinduzi ya Zanzibar, nachukua nafasi hii kuwatakia nyote heri na fanaka za Mapinduzi na kukutakieni maadhimisho mema ya sherehe ya kumbukumbu ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kwa watakao shereheka kwa wale wenye kumbukumbu njema, na kwa vile Mapinduzi Matukufu yale pia yaliandamana na umwagaji damu, natoa pole kwa wenye kumbukumbu chungu.
P
 
Field Marshall John Okello, baba wa mapinduzi ya Zanzibar, mbabe wa Sultan Jamshid.

Angalau sasa tunajua kuwa mapinduzi ya Zanzibar yalifanywa na vijana wa ASP lakini hayakuongozwa na viongozi wa ASP, bali yaliongozwa na Jemedari John Okello, mganda aliyepatiwa mafunzo ya kijeshi huko Cuba.

Tunajua pia viongozi wa bara, akina Oscar Kambona walipanga kufanya mapinduzi dhidi ya Sultan Jamshid, lakini walichelewa. Watu wawili waliotumwa kuomba silaha huko London walitumiwa ujumbe mfupi kwa njia ya telegramu na kuambiwa wasitishe shughuli hiyo kwani mapinduzi yamekwishafanyika.

Kumbe, vijana waliokuwa wakipatiwa mafunzo kwenye mashamba ya mikonge kule Tanga ili wakamng'oe Sultan, hawakuwahi kufanya kazi waliojiandaa nayo.

Badala yake John Okello akatumia hasira za vijana wa ASP na kufanikiwa kumg'oa Sultan Jamshid aliyekuwa na ulinzi dhaifu. Silaha ambazo Sultan Jamshid aliagiza kutoka Misri, hazikufika, na waingereza nawo walimuacha bila ulinzi wa maana. Ikawa kazi rahisi kwa Jemedari John Okello.

Hivyo ndivyo! Watu wanaongea mengi lakini ni ukweli kwamba mapinduzi ya Zanzibar yalikuwa 'Surprise' kwa viongozi wa bara na visiwani. Nyerere, Kambona, Karume, Babu, Hanga, Moyo, Kawawa walishuhudia tu, Sultan kakimbilia Mombasa na John Okello akijimwambafai katikati ya viyunga vya Stone Town! Sultan mpya alikuwa mjini. Mapinduzi yaliyopangwa hayakufanyika, yaliyofanyika yalikuwa ya ghafla na ya kushangaza waliopanga.

Wakati mapinduzi yakiendelea, kiongozi wa ASP, Abeid Aman Karume alikuwa amejihifadhi kwenye kijumba kimoja huko Zanzibar. (Taarifa zingine zinadai Dsm).

Akihojiwa na TBC, siku ya Tarehe 12 Januari 2012 mjane wa mzee Karume, Bi Fatuma Karume alikiri kuwa yeye na Karume walihifadhiwa kwenye kijumba huko Zanzibar. Baada ya muda walisikia sauti ya gari ikaribia huko walipohifadhiwa; ndipo Karume akamwmbia mkewe;

'Unasikia hilo gari? Wanakuja hapa. Kama mapinduzi yamefanikiwa basi mimi nitakuwa Rais, Kama hayajafanikiwa basi nitachukuliwa na hutaniona tena' maneno ya Bi Fatuma Karume, Januari 12, 2012 TBC.

Ikiwa maneno hayo ni ya kweli, basi itoshe kusema Karume alipata taarifa kuhusu mapinduzi, lakini hakushiriki kimwili. Na kama si msaada kutoka bara (baada ya mapinduzi) basi John Okello, mtu mbabe, bwanavita na jemedari mjinga angetawala Zanzibar.

Kutoka kwa,
Christopher Cyrilo
 
Imekuwa kawaida kwa gazeti la Monitor la Uganda kuadhimisha mapinduzi ya Zanzibar kwa kutoa makala zinazomtambulisha Field Marshall John Okello kama kiongozi pekee wa mapinduzi ya Zanzibar.

Mwaka huu wametoa makala iliyoandaliwa na mwandishi Felix Ocen inayomtambulisha John Okello akiwa na miaka 25 akiongoza kikosi cha watu 600 kwa muda wa masaa tisa tu na kufanikisha kumpindua Sultani.

John Okello aliyeingia Zanzibar miaka minne kabla ya mapinduzi, alikuwa mzaliwa wa familia ya kawaida katika wilaya ya Alebtong kaskazini mwa Uganda.

Okello, baada ya harakati zake za mapinduzi aliandika kitabu alichokipa jina The Revolution in Zanzibar, lakini kilipigwa marufuku kuchapishwa na serikali zote za Afrika Mashariki.

Gazeti linasema kuwa Okello aliongoza D-Day na wafuasi wake bila uwepo wa watu tunaoambiwa waliongoza mapinduzi hayo yaani Abeid Karume na Abdurahman Babu. Hawa wawili walikuwa wamefukuzwa visiwani na utawala wa Sultan, na walishangazwa sana kusikia kuna mapinduzi Zanzibar.

Okello alifanya siri mpango wake wa D-Day mpaka ilipofika usiku wa tarehe 11 January 1964, alipowakusanya wafuasi wake na kuwaamuru kuivamia kambi ya silaha ya Ziwani wakiwa na silaha za jadi.

Baada ya kufanikiwa kuiteka kambi ya silaha huku walinzi wa kambi wakitoroka, Okello na wafuadi wake walielekea mji mkongwe wakiwa wamejiimarisha kwa silaha kali. Kwa masaa machache walifanikiwa kuuteka mji mkongwe huku Sultan akikimbilia Dar es salaam kuomba hifadhi kwa Nyerere, lakini Nyerere alikataa na ikamlazimu Sultani kuelekea Mombasa kisha Uingereza.

Mpaka kufika asubuhi, Okello na wafuasi wake walikuwa wameshikilia vituo vyote vya muhimu huku akiwaamsha wazanzibari kwa tangazo "This is John Okello, the Field Marshall of Pemba and Zanzibar. Wake up you imperialists, there is no more imperialist government. Wake up you Blacks, pick the weapons and clear out the remnants of the imperialist government.... I am giving the Sultan 20 minutes to kill his children and wives and later himself, or else Okello will do it."

Mpaka kufika jioni watu takribani 13,000 walikuwa wameuliwa, huku zaidi ya 12,000 wakiwa waarabu. Viongozi wote ambao hawakufanikiwa kutoroka zahama ya Okello walitangaza kujisalimisha na kumuunga mkono Okello.

Okello aliunda kikosi cha wapiganaji wa mapinduzi kilichoitwa "Freedom Military Force" au Jeshi la Uhuru. Pia aliunda baraza la kwanza la mapinduzi, lakini walipompendekeza kuwa rais wa baraza alikataa. Badala yake aliwaita akina Karume kutokea Tanganyika, akampendekeza Karume kuwa Rais na Babu kuwa waziri mkuu.

Mengine fungua link usome wenyewe.

How Ugandan led revolution that ended Arabs reign over Zanzibar



Hapa kuna maswali kadhaa.

1. Kwanini CCM wanatudanganya watanzania na kuidanganya dunia?

2. Kuna faida gani tunazopata kwa kukataa kumtambua Okello kama kiongozi na baba wa taifa la Zanzibar?

3. Kwanini viongozi wa Afrika Mashariki walimwogopa Okello?

4. Inaonekana Okello alitekwa na watu wasiojulikana wakati wa utawala wa Iddi Amini na hajulikani alipopotelea mpaka leo. Serikali ya Zanzibar imefanya juhudi zipi ili haki za huyu Field Marshall zipatikane zikiwepo za kupewa heshima anayostahili?

Nawasilisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…