Mapinduzi ya Zanzibar: Mchango wa John Okello (Che Guevara wa Afrika Mashariki) umefutwaje?

Mapinduzi ya Zanzibar: Mchango wa John Okello (Che Guevara wa Afrika Mashariki) umefutwaje?

Google utapata historia yake just type John Okello
 
Wana jf mimi kama kijana mzalendo mwenye kiu ya kujua historia ya nchi yangu, katika kufuatilia historia ya mapinduzi ya Zanzibar nimekutana na jina la JOHN OKELLO kwamba ni miongoni mwa wapiganaji katika kuitafuta Zanzibar huru. Naomba kwa mwenye historia japo kwa ufupi ya mtu huyu anisaidie ili niweke kumbukumbu zangu sawa.
Ngoja waje unataka kujua jinsi alivyo mchuviding..naniliuu nii!
 
Wana jf mimi kama kijana mzalendo mwenye kiu ya kujua historia ya nchi yangu, katika kufuatilia historia ya mapinduzi ya Zanzibar nimekutana na jina la JOHN OKELLO kwamba ni miongoni mwa wapiganaji katika kuitafuta Zanzibar huru. Naomba kwa mwenye historia japo kwa ufupi ya mtu huyu anisaidie ili niweke kumbukumbu zangu sawa.
Okelo ndiye aliyeongoza mapinduzi ya Zanzibar siyo Karume. Historia imechakachuliwa na watawala ili kumpa ujiko Karume kwakuwa Okelo hakuwa mzawa. Baada ya kufanikiwa kupindua wakamtimua na kumpa ujiko Karume kuwa ndiye alikuwa kiongozi wa mapinduzi hayo. Usisahau kuwa Karume naye asili yake ni Malawi
 
Okelo ndiye aliyeongoza mapinduzi ya Zanzibar siyo Karume. Historia imechakachuliwa na watawala ili kumpa ujiko Karume kwakuwa Okelo hakuwa mzawa. Baada ya kufanikiwa kupindua wakamtimua na kumpa ujiko Karume kuwa ndiye alikuwa kiongozi wa mapinduzi hayo. Usisahau kuwa Karume naye asili yake ni Malawi

Kweli historia inakawaida ya kujirudia, kumbe hizi ndio tabia za Wazanzibari, wanapenda mtu mwingine awafanyie kazi wao wale tu basi and then waje wajisifu kua wamefanya wao, barabara, umeme, mishahara ya viongozi wao na pesa za kuhudumia Wazenji zote zinatoka bara, mara baada ya mambo kua mazuri sasa wanadai wajitenge, kisa tu eti vipimo vya kijiolojia vinaonesha Zanzibar kuna mafuta! Sijui kwanini hawa watu hua hawana shukurani.
 
ngojea Shariff Ritz aje atuwekee historia ya huyu mzee wetu...
 
Last edited by a moderator:
Okelo ndiye aliyeongoza mapinduzi ya Zanzibar siyo Karume. Historia imechakachuliwa na watawala ili kumpa ujiko Karume kwakuwa Okelo hakuwa mzawa. Baada ya kufanikiwa kupindua wakamtimua na kumpa ujiko Karume kuwa ndiye alikuwa kiongozi wa mapinduzi hayo. Usisahau kuwa Karume naye asili yake ni Malawi

Kweli historia inakawaida ya kujirudia, kumbe hizi ndio tabia za Wazanzibari, wanapenda mtu mwingine awafanyie kazi wao wale tu basi and then waje wajisifu kua wamefanya wao, barabara, umeme, mishahara ya viongozi wao na pesa za kuhudumia Wazenji zote zinatoka bara, mara baada ya mambo kua mazuri sasa wanadai wajitenge, kisa tu eti vipimo vya kijiolojia vinaonesha Zanzibar kuna mafuta! Sijui kwanini hawa watu hua hawana shukurani.
Hamjui mnaloliongea. tafuteni vitabu msome msitegemee stori za vijiweni.
 
YAITWAYO "MAPINDUZI"​

John Okello alitoka kwao Uganda, Injin aliyetoka kwao Kenya na Mfaranyaki aliyetoka Tanganyika, na kuivamia nchi huru usiku wa manane wa kuamkia tarehe12 Januari 1964. Wananchi, mafisadi kwa sababu ya maslahi ya nafsi zao hawakuhisi uchungu kuipoteza nchi yao, wala kuzipoteza roho za wazee wao, za ndugu zao na za marafiki zao. Kwa mujibu wa kitabu cha huyo aliyejipa ujamadari wa hayo 'mavamizi' ya Januari 12, 1964, John Okello, amesema kuwa watu waliyokufa katika 'mavamizi' hayo ni 13,000. Hii ni idadi ndogo kabisa aliyopenda kuitaja.

Ukatili, ushenzi na unyama uliofanywa katika visiwa hivi vilivyokuwa na ustaarabu wa kupigiwa mfano, hauwezi hata kuhadithika. Wengi waliokuwa wanaijua Zanzibar, waliona taabu kuyaamini waliyokuwa wameyasikia yametokea Zanzibar kutokana na hayo yenye kuitwa 'mapinduzi'. Ilifika hadi, siku hiyo ya 'mavamizi' washenzi na makatili hao kuwanajisi maiti wa kike. Kitendo hicho hakijawai kufanyika katika nchi nyingi ulimwenguni zenye ubinaadamu na ustaarabu wake. Lenye kuzidi kushangaza na kusikitisha ni kumsikia mwananchi mwenye kujulikana kuwa yeye ndiye mwongozi wa hao wenye kujiita "progressives" akasema kuwa, watu waliyouliwa katika hayo yenye kuitwa 'mapinduzi' ni 491! Duh!

Mwenyewe Okello alieongoza hayo mauwaji amesema kuwa wamekufa wananchi 13,000. Hata wangekuwa watano tu, bali ni binaadamu, ni wananchi, jee, ndio wawe wamestahiki kuuliwa kwa kuvamiwa nchi yao na wageni ambao wewe na wenzio kama wewe mmechanganyika na hao wageni katika kuifisidi nchi na wananchi wake? La kustaajabisha zaidi - ni pale ilipojulikana kuwa haya yote yalipangwa kabla - kwa siku 30 tu yaaani Desemba 10 mpaka Januari 11 ilitosha kujuwa uovu wa Serikali hata ikastahiki kupinduliwa? Hata ingelikuwa ni ovu hivyo, bali njia za kuiondowa za kikatiba zilikuwepo ambazo zingaliweza kutumika, khasa na hao Wapinzani. Haikuhitaji hata kidogo kutumia nguvu. Lakini hakika khasa ni kuwa mambo yalikwisha pangwa zamani, hayo yalikuwa ni matekelezo tu!!

Taarifa yako sio sahihi,na imejaa uongo ambao hauvumiliki na hata mtoto ndogo.Tujiulize kidogo tu kwamba inawezekana vipi,mtu atoke kwao uganda usiku wa kuamkia tarehe 12 1 64,afanye mapinduzi bila kuwa na mipango au kushirikiana na wenyeji?
Alikwendaje Radio Zanzibar kutangaza mapinduzi?
Alipegaje picha na Waanzilishi wa Mapinduzi.
Alijuaje vituo vya jeshi la mwarabu.
Alijuaje uimara na udhaifu wa jeshi la mwarabu.
Alimtangazaje Karume kuwa rais.
Na kadhalika na kadhali.
 
Alikuwa ni Mzee wa mikwara Mbuzi na fulu muongo na mzushi kuwa aliwapindua wazungu kuipatia zanzibr uhuru
 
Mwka 1964 siku thelathini baada ya uhuru wa bandia wa Zanzibar, wanamapinduzi kumi na nne wakiongozwa na mpigania uhuru John Okello aliwaongoza kwenye mapinduzi ya Zanzibar yaliyokuwa na umwagaji mkubwa wa damu.

Baada ya mapinduzi kufanikiwa John Okello [kiongozi wa mapinduzi] alichukua jukumu la kutangaza mapinduzi kwenye radio Zanzibar, ikumbukwe pia wakati mapambano yakiendelea ..aliyekuja kuwa rais wa Zanzibar mzee Karume na Babu walikuwa mafichoni na hawakushika wala bisibisi kwenye mapinduzi na hata ukiangalia ile picha ya wanamapinduzi ya kwanza John Okello amevalia kipolisi na amekaa kama kiongozi rasmi.

Baada ya hali kutulia Okello anamtangaza Karume rais na Abdulrahman Babu kuwa Waziri mkuu. Na ndie aliyeenda kumpokea Karume kutoka alikokuwa amejificha kwa siku kadhaa.

Baada ya siku chache mzee Karume akamfukuza Zanzibar kama mbwa John Okello [Field Marshal] na bila kujali mchango wake anatokomea kusikojulikana na historiaa ya mapinduzi ikafutwa na nafasi ya Okello ikaja kuwa mkwezi, mpiga tofali ambaye alibahatika kupiga picha [akiwa amekaa kitini katikati tu kwa sababu ya kuwa na kipaji cha kuongea - (kumbuka kuwa hata kiswahili chake kilikuwa 0kibovu)]

Naomba kuchokoza mada kuhusu nafasi ya John Okello kwenye mapinduzi, kwa nini historia ilifunikwa?

Je aliishia wapi,..wapenda historia ya kweli wameshatamani hata kujua lilipo kaburi lake..kumbukeni wenzetu Kenya baada ya kugundua hila wanahaha kutafuta kaburi la Field Marshal Dedan Kimathi...mbona wapenda hitoria Zanzibar na Tanganyika kwa jumla hamumtendei haki JOHN OKELLO [FIELDMASHAL]?

Ukitaka kijua historia ya John Okelo na historia ya mapinduzi ya Zanzibar soma hichi kitabu http://kwaheri.files.wordpress.com/2010/05/kwaheri-ukoloni-kwaheri-uhuru.pdf, katika kitabu hichi utapa ufafanuzi wapi John Okello katokea na wapi kafia na kwanini alijitanganzi kuwa yeye ndio jemedari wa mapinduzi ya zanzibar

Unajua watanzania tuna tabia ya kubwabwaja mambo bila ya kufanya utafiti, humu katika JF wana jamvi watatoa stori na hisia tafauti bila hata ya kufanya utafiti kuhusu hilo jambo..

Soma hicho kitabu utafaidika sana mkuu,just download hiyo PDF files,enjow the show wangu...
 
Mnapoongelea kuhusu Ernesto Che Guevara na John Okello, munanikumbusha mbali sana kuhusu wana mapinduzi mashuhuri. Tuwakumbuke vilevile akina Ho Chin Minh (uncle Ho). Ebu rejeeni hii video kutoka youtube hapo chini ili muone who was incharge mara baada ya mapinduzi ya Januari 1964.
Che Guevara 17.jpg
 
Last edited by a moderator:
kwanini akina sheikh AMEIR BIN JUMA na wenzake wasiwe baba wa taifa wa Tanganyika baada ya kupigania uhuru kwa nguvu zote na gharama kwamiaka yote kumuondoa mkoloni wa kiingereza, hatimae he is been deported to Zanzibar without any reason.
 
Mwanamapinduzi John Okello kama ijulikanavyo katika Historia kwamba ndiye aliye ongoza kikundi kidogo cha Makamanda na kuipindua serikali ya Sultan Jemshid huko Zanzibar. Lakini, cha kushangaza huyu Mkombozi aliishia kufukuzwa Zanzibar...
 
Mwanamapinduzi John Okello kama ijulikanavyo katika Historia kwamba ndiye aliye ongoza kikundi kidogo cha Makamanda na kuipindua serikali ya Sultan Jemshid huko Zanzibar. Lakini, cha kushangaza huyu Mkombozi aliishia kufukuzwa Zanzibar...

Alipotelea mikononi mwa Field Marshal Idd, DSO, The conquerer of British Empire!
 
Huyu bwana alipotoka uganda alikwenda Kenya kama kawaida yake (ana itikadi za che -gwevara)akaend kusaidia mapambano dhidi ya wakoloni.baada ya kufanikiwa wakamtupa lipango kisha wakamtimua. Baada ya mapinduzi ya zanzibar inasemekana utawala wa kenya ukamwambia mwalimu kuwa huyo jamaa ni hatari hafai kuwepo zanzjbar hapo akapewa n persona granta-mtu asiyetakiwa zanzibar ndo akasepa
 
...nahisi alikumbwa na masaibu makubwa sana...
 
Back
Top Bottom