Mapokezi ya Tundu Lissu yapamba moto, apangiwa kuhutubia taifa jukwaani siku hiyo hiyo Temeke

Mapokezi ya Tundu Lissu yapamba moto, apangiwa kuhutubia taifa jukwaani siku hiyo hiyo Temeke

Dereva yupo wapi , mbona amefichwa miaka nenda rudu au na yeye amemalizwa chini kwa chini!?? Kwa jinsi mlivyo na agenda za chini kwa chini za RED BRIGADE
Mlitaka na yeye mmpoteze kama mlivyowafanya wengine.

Kwa dereva wa Lisu mmeshindwa. Atakaa mahali salama mpaka siku akina Bashite (msimamiaji wa operesgeni), Kisandku (mfyatuaji wa risasi), Ziro (mtoaji ulinzi kwa wauaji), watakapokamatwa, na atakuja kutoa ushahidi.

Mwiglu pia atakuwa shahidi muhimu maana kuna maelekezo alipewa na marehemu baada ya tukio. Bahati mbaya Mahig hayupo, naye angekuwa shahidi muhimu maana alishirikishwa na Mwglu kwa yale maelekezo aliyopewa na marehemu. KAalmni naye ni shahidi muhimu maana ana maelkz ya kuondoa CCTV.

Kama mnategemea kupoteza ushahidi kwa kumwondoa dereva kama mlivyoondoa CCTV, hapo mmegonga mwamba. Kuna siku mtasimama mahakamani tu, na mtashangaa mashahidi walivyo wengi. Siku hiyo mtapenda ardhi ipasuke ili iwameze.

JINAI HAIFI.
 
Jeshi la polisi lianzie eneo la tukio lilipopaswa kuwa lindoni na kuna ushahidi usiotia shaka wa CCTV cameras, simple and straight.
Servers huwa zinaweka kumbukumbu hata kama cameras zimeng'olewa, sasa kigugumizi kilitokea wapi kuweka hadharani footages za tukio zima?
Unapoteza nguvu zako kulijibu zuzu

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Sass kwanini risasi hazikumpata dereva ???? Hata kama cctv hazikuwepo on spot!?? Unajuaaa nyinyi mnafanya mazuzu.com , matahira.com yasiyojielewav,,,,,,, uki reply sema kwanini risasi zili miminwa upande wa dereva na zikafika kwa abiria hata hazikumchubua dereva ngoziii ...the. Dereva akafichwa kipindi kile wakati wa. Siro alisema dereva aletwe. CENTRAL either amechubuliwa na risasi huku anahema au kafa kwa risasi ....


What next is surprising......
Ungenyamaza tuu maana maandiko yako ni kichefuchefu. Risasi zilipigwa upande wa dereva? Hebu kamfulie nguo shemeji anatekutunza

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Taarifa ikufikie kwamba Maandalizi ya Mapokezi kabambe ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu yamekamilika, ambako wanachama wa CHADEMA na wapiga kura wake waliomchagua kwa kishindo 2020 kabla ya Sarakasi za Dr. Mahera, wametakiwa kujipanga kuanzia uwanja wa ndege hadi Temeke.

Habari zaidi kutoka kwenye Kamati ya Mapokezi zinasema kwamba, baada ya kuwasili, Tundu Lissu ataenda moja kwa moja kwenye Mkutano wa Hadhara ulioandaliwa na chama chake Viwanja vya Bulyaga -Temeke, mkoani DSM, ambako anatarajiwa kuhutubia taifa.

Binafsi nimesikia gari la matangazo likipita mitaani kwetu huku Tandika Mwembeyanga likihamasisha Wananchi kumpokea Shujaa wao.

Usiondoke JF kwa taarifa zaidi.

View attachment 2493397
Ikiwezekana nitoke mkoani kuja jijini kumpokea Mwamba huyo. Karibu Lissu mapambano dhidi ya udhalimu yanaendelea.
 
Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa Mchungaji Peter Msigwa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ndogo ya Kamati Kuu inayoratibu mapokezi ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu amesema kesho mchana Tundu Lissu akishatua uwanja wa Ndege wa J.K Nyerere Dar es salaam akitokea Ubelgiji ataelekea moja kwa moja Temeke kwenye mkutano mkubwa wa hadhara wa Chama hicho.

Mchugaji Msigwa amesema ajenda ya Mkutano huo anayo Tundu Lissu mwenyewe baada ya kukaa Ughaibuni "maandalizi yote yamekamilika kwa ajili ya mapokezi hayo, ni matumaini yetu kwamba Watu wengi watajitokeza kwenye uwanja wa Ndege na kama haitoshi tunawakaribisha Wananchi wa Dar es salaam na mikoa jirani kwenye mkutano huo"
 

Ngwear FT Mirror - Maskini WENZANGU


Intro: cowwizy ,ybm

Verse 1:
wachache ndo wanaishi wengi wetu ma escorts,
twiga wanapanda pipa hata bila ya passports,
mikoa mingi bado haina hata airports,
zaidi ya migodini madini kuya export,
bila ya wazawa kufaidika,
ndo mana wazanzibara wamechoka kutanga na nyika,
big up Mandela leo South sio Africa,
waliotangulia kupata uhuru bado wanapigika,
bidhaa zilizo expire kutubambika,
meli zinazidi zama wengi daily tunawazika,
wenye hali duni ndo tunao athirika,
wao ma vx yao ni special order uhakika,
tutalia machozi ya damu mpaka yata form bahari,
na tutaogelea wenyewe na watu hawajali,
leta mgomo baridi uijue serikali then muulize Ulimboka umuhimu wa Madaktari let's go

Chorus
(bado nalia tu na Tanzania yangu/kweli mali ni nyingi wale wachache wenzangu/me nalia na masikini wenzangu/eeh baba Mungu sikia kilo changu/issue is harder tuna suffer/sikia kilio changu/issue is harder tuna suffer/me nalia like..........)

Verse 2:
viongozi wa siasa kama viongozi wa dini,
mengi wanaongea coz silaha yao ni ulimi,
mh.spika Tanzania huru inazidi zeeka tayari ni miaka 50,
mengi mmetuahidi pia ahadi ni deni,
pia tunatambua umuhimu wa UN,
kupinga h.I.v,umaskini na rushwa and,
mabilioni yanayotumika kwa campgain,
kama za kupinga unyanyasaji wa watoto,
zisiishie kwenye promo na kuwalisha bado ndoto,
ishu sio kutupiana maneno bungeni,
bali watoto watoke mtaani warudi shuleni
,mkulima shambani anahitaji usafiri wa treni,
nyie piteni angani mazao yake muuzieni,
mpeni bei nzuri aweze mudu zaidi ya trector,
ni mawazo tu DIC usione nakuTATOR

(chorous)

Verse 3.
Tanu ilifanya kazi kubwa 61,
solution sio labda nchi wachukue upinzani,
bali mtanzania wa chini anaishi maisha gani,
watu wanakufa kwa njaa iweje tujivunie amani,
ni mengi tu mazuri yamefanyika mpaka sasa,
ila naamini bado tungekuwa mbali(hivi babu wa Loliondo nae inawezekana tu ilikuwa ni siasa)NO !(Lakini iko wapi hii kaburi ya Balali !?) Men ! Jibu unalo so usiulize swali,una dini ?
Mkristu sali na Muislam swali coz,
bado tunaishi ki mungu mungu,
Baada ya m weka z usikie kizungu zungu jinsi ukoloni unafanya mambo mpaka leo,
kuongoza jamii sio kumtawala mkeo,
najiuliza maisha yangekuwaje bila mziki,
hivi mtaani ingekuwa vp ? Ingekuwa mziki ...

(Chorous)

outro yeah chamber squad baby,one love,Tanzania,Muro jr I see ya ......
Till fade
 
Hongera zake... bora ameamua kurudi maana ugenini shida tu unabaki unamic tu home..
 
Lissu alikuwa Al Jazeera dakika chache zilizopita anadai kuruhusiwa kwa mikutano ya siasa ni pressure yao baada miaka 6 ya ukandamizaji wa Magufuli na Samia.

Kwa mujibu wa Lissu si kwamba Bi Tozo karuhusu tu alikuwa hana namna ya kuzuia nguvu ya umma kutaka mikutano ya hadhara.

Vita yake kuu akirudi ni katiba ya kidemokrasia.

Source: Tundu Lissu kupitia mahojiano yake na Al-Jazeera.
atakua kaanza vzr hivi, akianza kumsifia Bi Matozo naye tunatia kwenye kapu la taka
 
CCTV camera ziko wapi??
Vipi dereva yuko wapi !!! Kwann yeye risasi hazikumchubua hata. Kipande , chan ngozi


Na alitoka mzima mzima wakati risasi zote zili miminwa kwa upande wake zikamfikia abiria , dah hapa ni changa la macho ,,,paaaaaàh mazuzu.com hayoooooooooooooooooooooooo




Jeshi la polisi likikomalia hapa hakyanaani. Mate yaliyokuwa yanatupiwa kule chato hahhahaha yataokotwa tuuu....
 
Taarifa ikufikie kwamba Maandalizi ya Mapokezi kabambe ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu yamekamilika, ambako wanachama wa CHADEMA na wapiga kura wake waliomchagua kwa kishindo 2020 kabla ya Sarakasi za Dr. Mahera, wametakiwa kujipanga kuanzia uwanja wa ndege hadi Temeke.

Habari zaidi kutoka kwenye Kamati ya Mapokezi zinasema kwamba, baada ya kuwasili, Tundu Lissu ataenda moja kwa moja kwenye Mkutano wa Hadhara ulioandaliwa na chama chake Viwanja vya Bulyaga -Temeke, mkoani DSM, ambako anatarajiwa kuhutubia taifa.

Binafsi nimesikia gari la matangazo likipita mitaani kwetu huku Tandika Mwembeyanga likihamasisha Wananchi kumpokea Shujaa wao.

Usiondoke JF kwa taarifa zaidi.

View attachment 2493397
Mungu Ibariki CHADEMA [emoji1545]
 
Back
Top Bottom