Mara nyingine tena timu zetu za Afrika zinaenda kutuangusha Kombe la Dunia

Punyeto sana,nguvu magotini hawana
Nakubaliana nawe. Wachezaji wa Ghana wanaonekana kuwa na miili lakini wamekosa nguvu kabisa. Walikuwa wanaanguka anguka tu kipuuzi. Mexico hawana maumbo makubwa ila wana nguvu.

Jamaa wanapiga sana selfie.
 
Si kweli. Uingereza waligundua football lakini wana miaka hawajachukua. Sisi hatupo serious na kitu kingine zaidi ya Ngono.
 
Kwa Talent ya Mpira, wenzetu wametuacha mbali sana. Kuanzia Miundombinu ya mpira, vipaji, mbinu n.k wapo mbali sana kutuzidi.
 
Sjawai shabikia team za taifa za africa , sisi hatujui mpira. Yaan nishabikie Ghana akiwa anacheza Portugal lbda nimerogwa. Yaani nishabikie Ghana, Nigeria na upuuzi wa aina hiyo niache team za maana Brazil, Spain!! Huo uzalendo wa kijinga
 
Cameroon utakuta wanatolewa leo. Maana weupe wakipangwa na teams za africa wanachekelea sana. Wana uhakika wa kushinda
 
Timu za Africa hazijawahi kuwa na umakini. Hata kipindi kile cha kina Roger Milla, baadae Nigeria ya kina Kanu, Ghana iliyotolewa na Uruguay, nk pamoja na kuwa na timu nzuri sana zinazovutia kuangalia, zilishindwa kwa kukosa umakini. Tena unapojua haupendwi, ingebidi tuwe extra careful hasa katika kucheza rough.

Kina Kanu walionyesha katika Olympics kuwa Africa tunaweza mpira tukiamua.

Toka nishuhudie Cameroon na Nigeria wameenda World Cup wakaamua kufanya mgomo baridi kisa pesa zao za posho zimeliwa na viongozi wao, baadae nikaona Ghana anatolewa ki***ge kwa kukosa ile penalti, sijawahi kuwa na matumaini na timu za Africa. Senegal kidogo aliyemfunga Ufaransa alionekana anajua nini anatakiwa afanye.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…