Mara ya mwisho kumwambia Mwanao unampenda ni lini?

Mara ya mwisho kumwambia Mwanao unampenda ni lini?

Salam Wakuu,

Katika malezi ni muhimu sana mtoto ajihisi kupendwa na wazazi wake ama na yoyote anayemlea. Ni ngumu kwa mzazi/mlezi kuwapenda watoto wote sawa, lakini ni muhimu kwa watoto wote kujihisi wanapendwa na kujaliwa na wazazi/walezi wao.

Mtoto anayepata mapenzi na upendo kutoka wa wazazi wake; kwanza anakuwa huru kueleza changamoto zake pale anapokwama, lakini pia ni rahisi kwa wewe mzazi kugundua mapema kama kuna tatizo kubwa linamsumbua hata asiposema, sababu tayari una ukaribu naye kiasi cha kuona tofauti pindi asipokuwa sawa.

Mtoto anafikisha mpaka miaka 15 hajawahi kusikia hata siku moja mama au baba yake wake anamwambia anampenda, mtoto huyu akikutana na mtu akaonyesha kumjali na kumpa upendo wa kuziba nafasi yako unafikiri atashindwa kumrubuni?

Na usitegemee kwamba wa kumrubuni anaweza akawa kwenye mazingira ya hapo karibu tu, mtoto wako anaweza kupata rafiki mtandaoni ambae ataona kuna mwanya huo akautumia vizuri. Mwanzo ataanza kumuonesha upendo na mapenzi, na mtoto akishamuamini ni rahisi kumfanyia chochote. Wengine wanaweza kwenda mbali kabisa mtoto akatekwa ukibahatika kumpata ni maiti, lakini hayo ilifikaje huko, ni kwa sababu mtu alipata mwanya ambao ni wajibu wako kuufanya akautumia vizuri.

Na ikishatokea hivyo mtoto wala hatakwambia kuwa nimekutana na mtu amesema moja, mbili, tatu kwasababu atakuwa mtu muhimu kwake anaemtendea vema kuliko wazazi wake, kwanini asimuamini zaidi na kuhamisha upendo, mapenzi na kumthamini mtu huyo kuliko wazazi wake?

Kibaya ni kwamba mtu huyo aliyeaminiwa anaweza kufanya ukatili kwa mtoto wako wala usijue, mpaka unakuja kushtuka unakuwa umechelewa, mtoto ameshaharibiwa kwa miaka na wewe upo hapo hapo, wakati ungetoa muda wako na kuonesha upendo kwa mtoto wako ungeweza kuepusha mambo mengi.

Kuna watu wapo azma yao ni kutafuta watoto kuwafanyia ukatili ama kuwafanya bidhaa kwa watu wengine wenye matamanio hayo maovu, wengine wanaweza kuwa ni wafanyabishara haramu ya viungo vya binadamu, anakuja kuziba nafasi yako vizuri, anampa mtoto upendo wako wote lakini lengo lake sio kusaidia, tuwe makini.

Mzazi unafurahi na kuhadithia kabisa, yaani mtoto wangu anampenda fulani kuliko mimi, nikimuacha kwake nafanya kazi zote hata hasumbui, JITAFAKARI. Wazazi hasa wanaume wanaona hili halina maana, tubadilike. Mtoto wako wa kike au wa kiume akijua baba na mama wananipenda unatengeneza ukaribu kati yenu na kufanya iwe ngumu kurubuniwa na watu wengine na kumuepusha na vitu vingine vibaya vinavyoweza kutokea, tuwe macho.

Narudisha swali kwenu wazazi na walezi, mara ya mwisho kumwambia mtoto wako unampenda ni lini?
Mnaiga umagharibi na hizo gender studies zenu halafu mnataka kuyaleta Africa. Magharibi kumeoza chakushangaza eti ndio mifano yetu. Unafikiri mtoto hana inteligensia kichwani, anayo tangu miaka 3.
 
Mi siwaambii ila wanajua nawapenda. Kuna huyu wa kiume ye ndo huwa kila mara lazima aniambie "mama nakupenda".Mdogo wake pia akimaliza ananiuliza "mama na we unanipenda?"
Umejuaje kama wanajua? Kama kila siku anakuuliza hivyo huoni kunashida yoyote?
 
haya mambo mnayatoa wapi hivi?
upendo wa wazazi kwa mtoto au watoto ni kimatendo zaidi
Mbali na matendo akisikia kutoka kwako ni vizuri zaidi.... Si kwa ubaya, ni kumhakikishia upo hapo kwa ajili yao. Inaweza ukawa unaashumu wao wanajua lakini ikawa siyo hivyo. Tujitahidi kuongea na watoto wetu
 
Mnaiga umagharibi na hizo gender studies zenu halafu mnataka kuyaleta Africa. Magharibi kumeoza chakushangaza eti ndio mifano yetu. Unafikiri mtoto hana inteligensia kichwani, anayo tangu miaka 3.
Kumwambia mtoto wako unampenda ni kuiga umagharibi? Halafu mtoto akikua akiwa anampenda mzazi mmoja mnaanza kulaumu. Mbali na kutimiza majukumu yako kuhakikisha anavaa, kula nk, unaongea na mwanao? Mtoto wako anafeel your presence kwao?
 
Kumwambia mtoto wako unampenda ni kuiga umagharibi? Halafu mtoto akikua akiwa anampenda mzazi mmoja mnaanza kulaumu. Mbali na kutimiza majukumu yako kuhakikisha anavaa, kula nk, unaongea na mwanao? Mtoto wako anafeel your presence kwao?

Mkuu moja ya sentensi za kinafiki dunia ni neno nakupenda. Sishauri umwambie mtoto hivi wewe zingatia vitendo watoto wanajifunza Kwa vitendo kuliko maneno na wanaona. Ndo maana wazazi wetu hawakutwambia haya maneno lakini tunawapenda mpaka kesho , mtoto anachapwana na mama yake ndani ya dk 20 keshasahau wanacheka, sasa mchape wewe stranger uone dogo atakuweka akilini milele, unajua hapa ni Kwa nini ? Mtoto anatambua upendo wa kweli wa mama yake kupitia vitendo

Nakupa Mfano mwingine , kuna wale masela unakuta wanapendana Kama ndugu lakini kamwe hutosikia neno nakupenda kati Yao hutosikia kamwe lakini they are there for each other iwe jua iwe mvua, bunafsi Nina marafiki wa hivi wachache sana hawazidi wanne.

Hata mbwa wako hapo nyumbani anajua Nani anampenda bila kumwambia maneno nakupenda

Zingatia vitendo achana na mambo ya nakupenda za asubuhi mchana na jioni . Nakupenda ni neno la kinafki sana
 
Jamani haya watamkieni,wato hata watakushangaa na wata anza kudeka, huyo mke tu kumwambia nakupenda nilimwambia kipindi cha uchumba ....upendo unaonyeshwa kwa matendo tu....hata uyo mke au mtoto umwambie nakupenda then chakula ndani hkn, nguo hawana, etc haisaidii
 
Wazaz wangu najua wananipenda balaa hasahasa mzee wangu. Ila hajawahi tamka hilo neno. Upendo wa mzazi huonekana tu hata ile closeness .
Nje wa mada kidogo .nimedate na wanawake kadhaa lkini neno nakupenda halijawahi kutoka kati yetu mwanzoni lbda baadae sijui ndo mnaitaga "love at first sight"?
 
Kuambia mtoto nakupenda so lazima kwa mtoto kujua anapendwa.
Haijawahi tokea ww kuliliwa either na mtoto wa jirani kila akikuona tu anakukimbilia ni kusema kwa sababu ulisema "nakupenda mtoto"?
No, ila issue ni ile "CLOSENESS".
 
Salam Wakuu,

Katika malezi ni muhimu sana mtoto ajihisi kupendwa na wazazi wake ama na yoyote anayemlea. Ni ngumu kwa mzazi/mlezi kuwapenda watoto wote sawa, lakini ni muhimu kwa watoto wote kujihisi wanapendwa na kujaliwa na wazazi/walezi wao.

Mtoto anayepata mapenzi na upendo kutoka wa wazazi wake; kwanza anakuwa huru kueleza changamoto zake pale anapokwama, lakini pia ni rahisi kwa wewe mzazi kugundua mapema kama kuna tatizo kubwa linamsumbua hata asiposema, sababu tayari una ukaribu naye kiasi cha kuona tofauti pindi asipokuwa sawa.

Mtoto anafikisha mpaka miaka 15 hajawahi kusikia hata siku moja mama au baba yake wake anamwambia anampenda, mtoto huyu akikutana na mtu akaonyesha kumjali na kumpa upendo wa kuziba nafasi yako unafikiri atashindwa kumrubuni?

Na usitegemee kwamba wa kumrubuni anaweza akawa kwenye mazingira ya hapo karibu tu, mtoto wako anaweza kupata rafiki mtandaoni ambae ataona kuna mwanya huo akautumia vizuri. Mwanzo ataanza kumuonesha upendo na mapenzi, na mtoto akishamuamini ni rahisi kumfanyia chochote. Wengine wanaweza kwenda mbali kabisa mtoto akatekwa ukibahatika kumpata ni maiti, lakini hayo ilifikaje huko, ni kwa sababu mtu alipata mwanya ambao ni wajibu wako kuufanya akautumia vizuri.

Na ikishatokea hivyo mtoto wala hatakwambia kuwa nimekutana na mtu amesema moja, mbili, tatu kwasababu atakuwa mtu muhimu kwake anaemtendea vema kuliko wazazi wake, kwanini asimuamini zaidi na kuhamisha upendo, mapenzi na kumthamini mtu huyo kuliko wazazi wake?

Kibaya ni kwamba mtu huyo aliyeaminiwa anaweza kufanya ukatili kwa mtoto wako wala usijue, mpaka unakuja kushtuka unakuwa umechelewa, mtoto ameshaharibiwa kwa miaka na wewe upo hapo hapo, wakati ungetoa muda wako na kuonesha upendo kwa mtoto wako ungeweza kuepusha mambo mengi.

Kuna watu wapo azma yao ni kutafuta watoto kuwafanyia ukatili ama kuwafanya bidhaa kwa watu wengine wenye matamanio hayo maovu, wengine wanaweza kuwa ni wafanyabishara haramu ya viungo vya binadamu, anakuja kuziba nafasi yako vizuri, anampa mtoto upendo wako wote lakini lengo lake sio kusaidia, tuwe makini.

Mzazi unafurahi na kuhadithia kabisa, yaani mtoto wangu anampenda fulani kuliko mimi, nikimuacha kwake nafanya kazi zote hata hasumbui, JITAFAKARI. Wazazi hasa wanaume wanaona hili halina maana, tubadilike. Mtoto wako wa kike au wa kiume akijua baba na mama wananipenda unatengeneza ukaribu kati yenu na kufanya iwe ngumu kurubuniwa na watu wengine na kumuepusha na vitu vingine vibaya vinavyoweza kutokea, tuwe macho.

Narudisha swali kwenu wazazi na walezi, mara ya mwisho kumwambia mtoto wako unampenda ni lini?
Nimwambie nampenda ili iweje? Ataambiwa na mama yake! Kwangu mimi ni utani kidogo na bakora kwa mbali..
 
Usimwambie mtoto unampenda. Are you a crazy Westerner,or what?
Makid ya now days. kizazi cha pampas. unawezaliambia litoto la kike likaona Mshua kaelewa Mzigo. Kifuatacho sasa!! hutakaa uamini. labda hizi zifanyike huko masaki,capripoint,forest, uhidini na place kaa hizo. lakini mbagala,bugalika,Matola, nyihogo, kanyenye,sombetini,Chogo au buzebazeba? utaishia kuchumishwa tunda na utalila tu kama Mwanangu Adamu wa pande za Eden mapindi yale
 
Unamuonyeshaje mapenzi ya baba Mkuu?
Hakikisha anapata mahitaji muhimu, nguo kali, shule nzuri english medium, chakula kizuri, kumtomkaripia bila sababu ya maana, outing, kumpenda mama yake,kumfundisha kazi, kumjenga kiimani, kumtengenezea vision nk. Sio eti mwanangu Benard nakupenda.....kwanza dogo wangu ataniona nimeanza kudata
 
Hakikisha anapata mahitaji muhimu, nguo kali, shule nzuri english medium, chakula kizuri, kumtomkaripia bila sababu ya maana, outing, kumpenda mama yake,kumfundisha kazi, kumjenga kiimani, kumtengenezea vision nk. Sio eti mwanangu Benard nakupenda.....kwanza dogo wangu ataniona nimeanza kudata
Unafikiri wanaolalamika watoto wao hawaoni mchango wao na kuona mchango wa mama pekee hawafanyi yote hayo?
 
Back
Top Bottom