Marekani anatoa misaada kiduchu hataki Ukraine ashindwe wala kushinda sana, anataka vita iwe ndefu ili kumfanyia utafiti Urusi na Ukraine awe mdaiwa

Marekani anatoa misaada kiduchu hataki Ukraine ashindwe wala kushinda sana, anataka vita iwe ndefu ili kumfanyia utafiti Urusi na Ukraine awe mdaiwa

Ndicho nachokiona, Marekani anatumia misaada kidogo kidogo lengo ni Ukraine asishinde wala asipigwe, yani vita iwe neutral wawe wanatwangana na mrusi, Nipe nikupe, Marekani akiona Ukraine anazidiwa anamtumia silaha , akiona anakaribia kupata ahueni anazima data rais wa Ukraine anaanza kulalamika, Marekani anatuma misaada kidogo kidogo kwa maksudi kabisa, mpaka sasa imefikia dola bilioni 60 ambazo tunaweza kuzioma nyingi ila kwa marekani ambaye bajeti yake pekee ni dola bilioni elf 4 hii misaada ni KIDUCHU.

lengo kuu la mmarekani kutuma misaada kidogo kidogo ni kuirefusha vita iwe ndefu ili akusanye intelejensia , Mmarekani saizi yupo na daftari lake anamfanyia urusi utafiti anakusanya intelejensia kuhusu mabadiliko ya mbinu za kivita za kisasa anazotumia urusi, kumlazimisha urusi atumie teknolojia alizoficha ili azichunguze, kupima loyalty ya wanajeshi, kujua mbinu anazotumia urusi anapobanwa na vikwazo, reaction za Putin, n.k. kwa sasa kaenda mbali zaidi hata katika tafiti zake anawapa silaha Ukraine ila yeye ndie anaeminya rimoti ya kumtungua urusi huku wakifatilia kwa makini urusi huwa anajibu vipi mapigo.

Hii vita hadi iishe ni mpaka Marekan awe kachukua notes za kutosha kajaza counter books za quire 4 za intelejensia kumhusu Urusi. kiufupi Urusi anatumika, asahau kabisa kuhusu ushindi.

Pesa ikigoma kununua kitu tumia currency nyingine, wengine hutumia zawadi, wengine hutumia urafiki, wengine hutumia connection, n.k. Marekani inanunua utiifu kutoka Ukraine kwa njia ya kuilimbikizia madeni, vita ikiisha tutarajie Ukraine ikiwa moja ya ally mpya za Marekani katika kiwango cha juu cha utiifu.

Kuhusu Putin aliingia vitani kibabe sana na ni aibu kwake kuondoka hata akipigwa ataendelea hivyo hivyo na haitakiwa kitu cha ajabu kwa Putin kuanza kuwakamua wananchi wa nchi yake ili kuilipia vita na ndipo hapa warusi watachafukwa kutakuwa na maandamano kibao na majaribio ya kumpindua Putin, na muda huo ndipo Marekani nae ataongeza zaidi misaada kwa Ukraine, sasa sijui itakuwaje hapo, ukiweka nguvu ya kuzima maandamano na mapinduzi kule Ukraine anapeleka moto sio mchezo, ikiwekwa nguvu zaidi vitani basi humo nchini maandamano na majaribio ya mapinduzi yanashika kasi, Chagua moja


Mwisho wa yote zitatumika Nuclear.
 
Kabisa mkuu Kp. Halafu ww kuwa Pro USA haimaanishi kuwa kila kitu cha USA unasapoti unaweza pia ukapinga jambo kama halikupendezi au ukasifia upande wa pili kama umefanya sawa.

I wish we members were able to bend to any right direction and not to be forced out of shape just to be seen as A PRO SOMETHING, I wish we were flexible and not rigid.
Wengi sana tunaoitetea Ukraine humu ndani tunaonekana tunasapoti Ushoga, Tunaiona US ndo kila kitu n.k

Mimi nipo JF kitambo saana, ID hii nimeanza itumia toka 2011. Humu ndani kipindi cha nyuma nilikuwa nakandia saana US kuvunja amani mataifa mengine hasa hasa LIBYA.

Lakini hii haikunifanya nisapoti Russia kwa kuvamia Ukraine, ninaona ni kama Ukraine ananyimwa haki yake ya kuchagua kile anachokitaka. Hata US angevamia nchi yoyote bado nsingeunga mkono.

Kuwa neutral ni jambo zuri mno.

Ongera sana mkuu.
 
Wengi sana tunaoitetea Ukraine humu ndani tunaonekana tunasapoti Ushoga, Tunaiona US ndo kila kitu n.k

Mimi nipo JF kitambo saana, ID hii nimeanza itumia toka 2011. Humu ndani kipindi cha nyuma nilikuwa nakandia saana US kuvunja amani mataifa mengine hasa hasa LIBYA.

Lakini hii haikunifanya nisapoti Russia kwa kuvamia Ukraine, ninaona ni kama Ukraine ananyimwa haki yake ya kuchagua kile anachokitaka. Hata US angevamia nchi yoyote bado nsingeunga mkono.

Kuwa neutral ni jambo zuri mno.

Ongera sana mkuu.
Nikiweza nitafuatilia hoja zako za huko nyuma mkuu maana hapa kwa namna ulivyojibu tu nimeona wewe sio mbuyu kuwa ukishasimikwa ardhini unakaa hapo hapo na kukubaliana na jua mvua vumbi n.k Inaonekana Upo huru haufungwi na uchawa.
 
Nikiweza nitafuatilia hoja zako za huko nyuma mkuu maana hapa kwa namna ulivyojibu tu nimeona wewe sio mbuyu kuwa ukishasimikwa ardhini unakaa hapo hapo na kukubaliana na jua mvua vumbi n.k Inaonekana Upo huru haufungwi na uchawa.
Miaka ya nyuma kuna thread humu ilikuwa inahusu silaha ya s300 defenc system, kuna s18 balistic missiles, tulichangia mno na kuisifia Russia, tukasema ndio mbabe wa magharibi.

Kuna special thread inayohusu hiyo s300 ila jina silikumbuka, ina posts zaidi ya 2,000. Kipindi hiko Jukwaa hili kuna jamaa anaitwa Elungata, naona sasa hivi atakuwa amebadili ID. Huyu Bukyanagandi alikuwepo kipindi hiko. Anaweza akaja akathibitisha hili, jamaa huyu ni pro russia toka kipindi hiko JF. Huu mpambano wa vita wa sasa yeye kuwa Pro Russia hata sio kitu cha ajabu.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Ndicho nachokiona, Marekani anatumia misaada kidogo kidogo lengo ni Ukraine asishinde wala asipigwe, yani vita iwe neutral wawe wanatwangana na mrusi, Nipe nikupe, Marekani akiona Ukraine anazidiwa anamtumia silaha , akiona anakaribia kupata ahueni anazima data rais wa Ukraine anaanza kulalamika, Marekani anatuma misaada kidogo kidogo kwa maksudi kabisa, mpaka sasa imefikia dola bilioni 60 ambazo tunaweza kuzioma nyingi ila kwa marekani ambaye bajeti yake pekee ni dola bilioni elf 4 hii misaada ni KIDUCHU.

lengo kuu la mmarekani kutuma misaada kidogo kidogo ni kuirefusha vita iwe ndefu ili akusanye intelejensia , Mmarekani saizi yupo na daftari lake anamfanyia urusi utafiti anakusanya intelejensia kuhusu mabadiliko ya mbinu za kivita za kisasa anazotumia urusi, kumlazimisha urusi atumie teknolojia alizoficha ili azichunguze, kupima loyalty ya wanajeshi, kujua mbinu anazotumia urusi anapobanwa na vikwazo, reaction za Putin, n.k. kwa sasa kaenda mbali zaidi hata katika tafiti zake anawapa silaha Ukraine ila yeye ndie anaeminya rimoti ya kumtungua urusi huku wakifatilia kwa makini urusi huwa anajibu vipi mapigo.

Hii vita hadi iishe ni mpaka Marekan awe kachukua notes za kutosha kajaza counter books za quire 4 za intelejensia kumhusu Urusi. kiufupi Urusi anatumika, asahau kabisa kuhusu ushindi.

Pesa ikigoma kununua kitu tumia currency nyingine, wengine hutumia zawadi, wengine hutumia urafiki, wengine hutumia connection, n.k. Marekani inanunua utiifu kutoka Ukraine kwa njia ya kuilimbikizia madeni, vita ikiisha tutarajie Ukraine ikiwa moja ya ally mpya za Marekani katika kiwango cha juu cha utiifu.

Kuhusu Putin aliingia vitani kibabe sana na ni aibu kwake kuondoka hata akipigwa ataendelea hivyo hivyo na haitakiwa kitu cha ajabu kwa Putin kuanza kuwakamua wananchi wa nchi yake ili kuilipia vita na ndipo hapa warusi watachafukwa kutakuwa na maandamano kibao na majaribio ya kumpindua Putin, na muda huo ndipo Marekani nae ataongeza zaidi misaada kwa Ukraine, sasa sijui itakuwaje hapo, ukiweka nguvu ya kuzima maandamano na mapinduzi kule Ukraine anapeleka moto sio mchezo, ikiwekwa nguvu zaidi vitani basi humo nchini maandamano na majaribio ya mapinduzi yanashika kasi, Chagua moja
Unaweza kua sahihi. West wanaakili sana

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Miaka ya nyuma kuna thread humu ilikuwa inahusu silaha ya s300 defenc system, kuna s18 balistic missiles, tulichangia mno na kuisifia Russia, tukasema ndio mbabe wa magharibi.

Kuna special thread inayohusu hiyo s300 ila jina silikumbuka, ina posts zaidi ya 2,000. Kipindi hiko Jukwaa hili kuna jamaa anaitwa Elungata, naona sasa hivi atakuwa amebadili ID. Huyu Bukyanagandi alikuwepo kipindi hiko. Anaweza akaja akathibitisha hili, jamaa huyu ni pro russia toka kipindi hiko JF. Huu mpambano wa vita wa sasa yeye kuwa Pro Russia hata sio kitu cha ajabu.
Kuna mambo mengine huwa atuyasemi - FYI,mimi ni mwandisi(Engineer) niliyesoma vyuo vikuu vya Ulaya magharibi,nimefanya kazi na kuishi huko,masomo yangu na fedha za kujikimu pamoja na nauli ya ndege kwenda na kurudi nyumbani wakati wa likizo nikiwa masomoni nilikiwa nalipiwa na Serikali yao kutoka kwa fedha za walipa kodi wa taifa husika,nakumbuka vizuri walicho nishauri in privacy nifanye iwapo ntarudi nyumbani nikihitimu masomo - so I know these people modus operandi like back of my hand - si watu wema hata kidogo.

Msione si support matakwa yao ya kutaka kuitawala Dunia kinguvu kwa kutumia mbinu mbali mbali zikiwemo overt and covert tactics mkafikiri labda nasukumwa na chuki binafsi, hii si kweli hata kidogo.

Watu hawajui tu, hata mgogoro huu wa Ukraine ulisukwa vizuri siku nyingi tu na mataifa hayo hayo ya magharibi specifically US, walicho kuwa wanasubiri ni opportune time ya kuitumia Ukraine ipigane a proxy war kwa niaba ya US, lengo hasa ni kutaka kuisambaratisha Urusi in totality making sure she will never rise again to challenge the US militarily and Global influence, nikiona Biden ana shed crocodile tears namshangaa sana sana kwa kujitia ni mtetezi mkubwa wa Taifa la Ukraine na Raia wake - ulaghai mtupu, interest zake na wapambe wake zimejikita kwenye kuzitafutia soko kampuni za Merikani zinazo unda silaha, pili battlefield ya kufanyia majaribio ya silaha mpya za Merikani dhiidi ya defense systems za Urusi ili kukitokea vita baina ya Urusi na NATO wajue lipi la kufanya, la tatu ni kutumia kisingizio cha vita ya Ukraine kushiniki Bunge liidhinishe fedha fasta lakini kiasi alisi cha fedha zinazo kwenda Ukraine ni kidogo fedha nyingine zinaishia mifukoni mwa Biden,rafiki zake na wamiliki wa viwanda vya kuunda silaha (MIC)-kumbukeni mwanae wa Kiume wa Rais Biden aliwahi uajiriwa kwenye Serikali ya Ukraine kama mshauri mkuu wa Rais, vile vile alimilikishwa makumpuni ya mafuta na gesi ya huko Ukraine wakati baba yake akiwa ni makamu wa Rais Obama -hii inadhilisha wazi wazi kwamba familia ya Biden ina vested interest kwenye Taifa la Ukraine si ajabu ndio maana saula la Ukraine amelivalia njuga kweli kweli!!

Back to the main point - ushindani baina ya US na Russia, si ushindani tu bali na uadui hivyo vyote vipo deep seated kabisa, actually as far as western leaders specifically the US are concern cold war did not end in 1990s it is still on going in other words still alive and kicking!!! Next time ntaeleza kwa kina sababu zangu za kui-support Urusi.
 
Sijui mmekatwa vichwa?

Makanali 100 wa Urusi wameteketea na Misiba na mazishi Yao tunaoneshwa kwenye TV halafu unaropoka eti Russia hajatumia Majeshi Yake? Majeshi ya Urusi + Chechen Soldiers + Wagner fighters + DPR Fighters + LPR Fighters wote kwa Pamoja wako bega kwa bega wanapambana na Majeshi ya Comedian ambaye anapewa Silaha kiduchu Tena za Mgao na bado anawajambisha. Mpaka Sasa,Russia haijateka Donbass yote (Luhansk + Dotnensk). Wamefanikiwa Kuitena Luhansk TU. Kila wakisogea Mji mkuu was Jimbo la Dotnensk wa Krymatonsk wanafekwa Nyuma. Tangu HIMMARS ziingie nchini Ukraine siku 30 zilizopita,Urusi imeteka 10km Kule Dotnensk na 3km Kule Izyum na Kupoteza 38Km Kule Kherson.
Siyo tumekatwa vichwa tunaangalia kwa ukaribu saaana kinachoendelea huko!!!NATO ni bingwa wa propaganda km mjuavyo hii nayo ni siraha kali sana ya kumshinda adui!

ni ngumu kumuua jenerali wa kirusi!! NATO hata wakifa woote wataonyesha kuwa hao ni warusi! ndo tabia yao!...unadhania NATO wao watasemaje zaidi ya huo uongo!
 
Putin alijazwa akajaa sasa ndio anaanza kugundua mtego alioingia kibaya ni kujitoa anaona aibu.
China walijua hilo wakakwepa mtego
Ziara ya spika wa bunge la Marekani aliyeingia kimabavu Taiwani kutembelea wachina wakaweka mkwara lakini wakashtuka kuanzisha vita wakajua ya Urusi yatawakuta!! Mali zote za wachina nje kutaifisha nk wakaamua kuwa wapole sababu uchumi wa China kwa sasa unategemea dola zaidi na wao ndio wakopeshaji wakubwa wa Serikali ya Marekani!! Wakaona pesa itayeyuka hewani mchana kweupe!! Wakarudisha majeshi nyuma kutoshambulia Taiwani

Humu mmojawapo mimi nilitamka wazi kuwa Putin Bwege hadi ma moderators humu walifuta nyuzi zangu zilizokuwa na comment mwanzo kabisa wa vita za kusema kuwa Putin ,Hopeless na bwege hakufanya analysis ya kutosha kabla kujitosa hiyo vita na Ukraine!! Sasa hivi ushahidi kuwa.Putin hakuwa na akili kuanzisha hiyo vita uko wazi
 
Kwa taarifa yako Ukraine hakopi kupigana vita nafikiri hufuatilii pesa na misaada ya kivita bunge la Marekani linapoindhinisha linatamka wazi kuwa ni msaada

Uwe unafuatililia wanatoa nini.na wanachotoa ni msaada au mkopo? Mleta mada umeandika utoto
 
Huwezi kusema marekani inatoa msaada kiduchu!! Mpaka sasa marekani imeshatoa zaidi ya dola bilioni 60!! Huo ni msaada kiduchu!!! Ni zaidi ya bajeti ya Tanzania kwa miaka mitatu!! Halafu bila aibu unasema ni msaada kiduchu!!!
Hizo pesa silaha bado halafu mtu anaita kiduchu

Kombora moja la Himars la masafa marefu na Laucher yake ni dola milioni sita na laki tano sawa na shilingi bilioni 13 za Tanzania

Marekani imewapa Ukraine makombora ya Himars kibao ukichukulia kombora moja gharama yake sawa na shilingi za kitanzania bilioni 13 bado mtu ataita msaada kiduchu? Akili anakuwa hana
 
China walijua hilo wakakwepa mtego
Ziara ya spika wa bunge la Marekani aliyeingia kimabavu Taiwani kutembelea wachina wakaweka mkwara lakini wakashtuka kuanzisha vita wakajua ya Urusi yatawakuta!! Mali zote za wachina nje kutaifisha nk wakaamua kuwa wapole sababu uchumi wa China kwa sasa unategemea dola zaidi na wao ndio wakopeshaji wakubwa wa Serikali ya Marekani!! Wakaona pesa itayeyuka hewani mchana kweupe!! Wakarudisha majeshi nyuma kutoshambulia Taiwani

Humu mmojawapo mimi nilitamka wazi kuwa Putin Bwege hadi ma moderators humu walifuta nyuzi zangu zilizokuwa na comment mwanzo kabisa wa vita za kusema kuwa Putin ,Hopeless na bwege hakufanya analysis ya kutosha kabla kujitosa hiyo vita na Ukraine!! Sasa hivi ushahidi kuwa.Putin hakuwa na akili kuanzisha hiyo vita uko wazi
Ni kweli kulikuwa hamna dalili zozote zile Putin kushinda Ukraine ili hali mataifa ya Magharibi G7, Canada pamoja na US wapo na Ukraine. Sasa tayari wameshaanza kuijenga Ukraine kwa mabillion ya dola yanayomiminika kila siku.

Silaha za watu wa Magharibi na US ni balaa, itoshe kusema tu kwamba Ukraine anapimiwa silaha, zile ambazo wanaona zinaweza kumsabaratisha kwa haraka hawazitumii ili kwanza kumdhoofisha na kumsogeza kwenye meza ya mazungumzo ya amani akiwa hoi.

Technologia na Silaha za viwango vya juu duniani inamilikiwa na US pamoja na mshirika wake wa karibu Israel.

Pole kwa Putin, maana wanakwenda kuichukua na CRIMEA - recording maneno yangu leo tarehe 12/09/22
 
China walijua hilo wakakwepa mtego
Ziara ya spika wa bunge la Marekani aliyeingia kimabavu Taiwani kutembelea wachina wakaweka mkwara lakini wakashtuka kuanzisha vita wakajua ya Urusi yatawakuta!! Mali zote za wachina nje kutaifisha nk wakaamua kuwa wapole sababu uchumi wa China kwa sasa unategemea dola zaidi na wao ndio wakopeshaji wakubwa wa Serikali ya Marekani!! Wakaona pesa itayeyuka hewani mchana kweupe!! Wakarudisha majeshi nyuma kutoshambulia Taiwani

Humu mmojawapo mimi nilitamka wazi kuwa Putin Bwege hadi ma moderators humu walifuta nyuzi zangu zilizokuwa na comment mwanzo kabisa wa vita za kusema kuwa Putin ,Hopeless na bwege hakufanya analysis ya kutosha kabla kujitosa hiyo vita na Ukraine!! Sasa hivi ushahidi kuwa.Putin hakuwa na akili kuanzisha hiyo vita uko wazi
Hii nakubali mkuu, moja ya watu mliojitokeza hadharani kutamka wazi wazi ni wewe pamoja na nyamizi.
 
Back
Top Bottom