Marekani huenda ikaiwekea China vikwazo kutokana na teknolojia ya kuponya ugonjwa wa kisukari

Marekani huenda ikaiwekea China vikwazo kutokana na teknolojia ya kuponya ugonjwa wa kisukari

Wagonjwa wa sukari hio habari ni njema kwao na siku zote UKiwa mzima wa afya utaleta zarau but ukiumwaa haswaa hata mkojo ukiambiwa dawa utakunywa
Ungesima na kuelewa nilichoandika usingekuwa unajibu haya unayojibu
 
Kwanza ni lazima mtambue kwamba Marekani au Ulaya siyo sawa na Tanzania na Afrika. Twende taratibu.

Sababu kuu zinazowezesha Marekani kutokukubaliana na tiba ya ugonjwa wa kisukari iliyogunduliwa nchini China zinaweza kujumuisha mambo yafuatayo
  1. Usalama na Ufanisi
    • Marekani ina viwango vya juu vya tathmini ya usalama na ufanisi wa matibabu yoyote mapya. Tiba mpya lazima zipitie mchakato mkali wa tathmini kupitia majaribio ya kitabibu na taratibu za udhibiti kabla ya kupitishwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa (FDA).
    • Ikiwa tiba mpya kutoka China haina data za kutosha au ushahidi wa kisayansi uliochapishwa katika majarida ya kimataifa yenye sifa, inaweza kuchukuliwa na Marekani kuwa haijathibitishwa vya kutosha.
  2. Tofauti za Udhibiti
    • Viwango vya udhibiti wa matibabu nchini China na Marekani vinaweza kutofautiana. Marekani inaweza kuwa na shaka juu ya ukali wa taratibu za majaribio ya kitabibu zilizofanyika nchini China.
    • Mchakato wa kibali nchini Marekani unaweza kuwa mrefu na mgumu, huku ukiangalia mambo mengi kama vile athari za muda mrefu, mwingiliano wa dawa, na hatari zinazoweza kutokea.
  3. Masuala ya Kibiashara na Kisiasa
    • Ushindani kati ya makampuni ya dawa za Marekani na China unaweza kusababisha upinzani wa tiba mpya kutoka nje. Makampuni ya Marekani yanaweza kushawishi dhidi ya bidhaa mpya za kigeni ili kulinda masoko yao.
    • Mahusiano ya kisiasa kati ya Marekani na China yanaweza kuathiri jinsi tiba za China zinavyokubaliwa. Matatizo ya kisiasa na kibiashara yanaweza kufanya Marekani kuwa na mtazamo mkali zaidi dhidi ya bidhaa za China. Mdiyo maana ya kuwa na nguvu na ushawishi, havijaja tu bure so ni lazima uheshimiwe maana aliwekeza kuvipata hivyo vyote.
  4. Matatizo ya Miliki
    • Marekani inaweza kuwa na wasiwasi juu ya masuala ya haki miliki inayohusiana na tiba mpya kutoka China. Ikiwa kuna shaka juu ya uhalali wa uvumbuzi au ikiwa haki miliki haziheshimiwi ipasavyo, hii inaweza kuathiri kukubalika kwa tiba hiyo. Hiyo kwao ni culture.
  5. Public Health
    • Afya ya watu wake na Usalama: Katika masuala yanayohusu afya ya watu, Marekani huchukua hatua za ziada kuhakikisha kuwa tiba mpya ni salama na haina madhara. Hii inajumuisha tathmini ya kina na majaribio zaidi ili kuhakikisha kuwa tiba mpya haitasababisha matatizo zaidi kwa wagonjwa.
Kwa hivyo, Marekani inaweza kuwa na sababu nyingi za tahadhari katika kukubali tiba ya ugonjwa wa kisukari kutoka China, zikihusisha masuala ya kisayansi, udhibiti, kibiashara, kisiasa, haki miliki, na afya ya umma.

Ninyi huko kwenu mnashangilia tu, lakini China atalazimika kufuata masharti yote ya US ili aweze kufaidika, maana soko lipo US, population ya US ina uwezo mkubwa sana wa kufanya purchasing ndiyo maana hata China kwake soko la US ndiyo soko analouza bidhaa zake na linampatia hela ndefu kuliko soko lingine lolote lile duniani.
Nninyi huko hata mkiletewa Chaki mtameza tu.
Hivi mgonjwa wa Kisukari mwenye pesa yake atashindwa kuifuata tiba China, kinachoweza kutokea ni wajanja kufungua Clinic karibu na marekani na wakapiga pesa au wakafanyiwa saboteji. Suala la vikwazo kwenye matibabu huwa lipo kwa mtu mwenye afya yake mkuu. Mgonjwa ataifuata popote.
 
Hivi mgonjwa wa Kisukari mwenye pesa yake atashindwa kuifuata tiba China, kinachoweza kutokea ni wajanja kufungua Clinic karibu na marekani na wakapiga pesa au wakafanyiwa saboteji. Suala la vikwazo kwenye matibabu huwa lipo kwa mtu mwenye afya yake mkuu. Mgonjwa ataifuata popote.
Upo sahihi, wanaweza wakafungua clinic Cuba, au Mexico lakini hawataruhusiwa kuingia nazo US, wagonjwa watalazimika kuhamia huko nchi jirani wakatibiwe.
Watu wanapinga tu, lakini kila nchi ina standards zake. Tanzania kuna maziwa ya watoto yanauzwa kimagendo sana, muuzaji asipokufahamu hakuuzii. Maziwa hayo yanatumika kwa wingi sana US, lakini kwa Tanzania hayaruhusiwi sababu mamkuka husika haijayathibitisha pamoja na kwamba mamlaka za US zimeyathibitisha kutumika nchini mwao.
 
Marekani hana njia nyingine ya kufanya zaidi ya kutoa vitisho!
 
Marekani haiwezi wekea vikwazo hayo makampuni ya madawa ya Kichina. Labda kuzuia dawa zao kwa visingizio vya uongo kuhusu usalama, ila si kuyawekea vikwazo vya kiuchumi.
Mfumo wao wa kisheria uko wazi hivyo vikwazo vitakataliwa.
Ubaya mtu mwenye nguvu na ushawishi duniani anaweza kukuzushia chochote ilimradi malengo yake yatimie na hakuna kitu tunaweza kumfanya , ndio dunia yetu ya leo ilipofika
urusi wakati wanapigna na taliban afghanistan, marekani walikuwa wanawaita talibans freedom fighters na kwamba russia wavamizi
Marekani huyo huyo alivyovamia afghanistan akawaita taliban terrorists na dunia nzima tukakaa kimya
 
Back
Top Bottom