Nadharia yako iko sahihi kinadharia, ila uhalisia kutokea hili sio rahisi. Kwenye information technology bado teknolojia nyingi ni za US au washirika wake. Kutengeneza hizo chip like EMV or So unahitaji teknolojia ambazo kwa kiasi kikubwa ni za Marekani. So theoretically that can happen but practically... doubtful!
Na mimi nimesema hiki si kitu cha kutokea mara moja.
Ila, ukweli kwamba si rahisi nyumba kushika moto haukufanyi baba mqenye nyumba ucheze na mto ndani ya nyumba kwa kusema nyumba haiwezi kuungua moto kirahisi. Unaweza kushindwa ku u control moto, nyumba ikaungua.
Trump anachofanya sasa hivi ni kusema kwamba nyumba haiwezi kushika moto kirahisi, anacheza na moto. Na kibaya zaidi, ana alienate si tu maadui wa US, bali mpaka marafiki.
Anajiweka katika nafasi ya ku fight nchi kama China alone. Kitu ambacho si kizuri.
Rais wa zamani wa US, Thwodore Roosevelt alikuwa na msemo wake, alikuwa anasema "speak softly and carry a big stick". Kwamba Marekani inatakiwa kuongea kwa sauti nzuri, lakini vitendo vyake viwe kitisho.
Maana yake ni kwamba nchi inaheshimiwa sana kwa uwezo wake kiasi haihitaji kutoa vitisho, unashawishi kwa diplomasia, na ukitaka kuikosea, daflao lake ukilifikiria kwa kuangalia utakavyopatilizwa, unajirudi mwenyewe bila hata Mmarekani kufanya kitu.
Sasa hivi Trump anapiga kelele, halafu zaidi ya vikwazo (ambavyo wa Iran wanaonekana kuvikabili bila kutetereka) hana karata nyingine.
Dollar kuanguka ni vigumu. Ina mfumo wenye kina kirefu, lakini, Trump ana undermine nguvu za dollar kwa sababu shallow za kisiasa.