Uchaguzi 2020 Marekani: Kuanzia leo, tunaweka vizuizi kwa waliohusika na kuvuruga Uchaguzi nchini Tanzania

Uchaguzi 2020 Marekani: Kuanzia leo, tunaweka vizuizi kwa waliohusika na kuvuruga Uchaguzi nchini Tanzania

Ni mwanzo mzuri sana, hawa wapuuzi akina jiwe na genge lake ni lazima wakutane na ombwe la demokrasia ya kweli kutoka kwa Rais Joe Biden. Good.
 
Kwa Taarifa yako waliozuiliwa wengi ni viongozi wako japo wa Tume nao wamo , kuna lundo la viongozi wanaokutumikisha , halafu kingine unachopaswa kufahamu ni kwamba ukizuiliwa na USA , basi kuna mataifa mengine kama 10 hivi hutakanyaga , omba Mungu msiugue Tezi dume au maradhi mengine ya kukata viungo
Mbona Makonda kazuiliwa na maisha yanaendelea manka?

Marekani kitu gani bhana dunia iko kiganjani!
 
Si chini ya mwezi mmoja, Bunge la Umoja wa Ulaya limependekeza na kuridhia taratibu za vikwazo vinavyowekwa na Marekani kutumika pia Umoja wa Ulaya.

Nadhani wewe ni Mchanga sana na hujui impact ya travel Ban. Kwa taarifa yako ni kuwa hao watu na familia zao wataweza kwenda Asia na nchi na Africa tu. Na ikitokea wamepigwa na Ban za kufanya miamala ya kifedha ndo wameumia maana systems za kibank duniani karibu zote ziko chini ya hao hao.

Kikubwa kwa sasa ni watu wasali wasiwepo kwenye hiyo list Ila wakiwepo tu wameumia.
 
Na msiseme Makonda alifungiwa kwa kukataa mashoga, Museveni hataki hata kuwasikia mashoga Uganda lakini Marekani anakwenda.
Basi ujue hao jamaa zenu wana lao jambo na tanzania, mbona hawazungumzii uchaguzi wa uganda ila wao wanaleta ujinga tanzania?
 
Ni mwanzo mzuri sana, hawa wapuuzi akina jiwe na genge lake ni lazima wakutane na ombwe la demokrasia ya kweli kutoka kwa Rais Joe Biden. Good.
Pompeo mwenyeqe anatupwa nje baada ya biden kuapishwa.
 
Hapo inatakiwa diplomacy ya hali ya juu sana hasa kwa serikali ya Biden!!! Kabudi hana diplomacy ni mtu wa maguv na hapo ndio tunawakumbuka watu kama marehemu Mahiga na uzoefu wao!!

..njia rahisi zaidi ni kuishi vizuri na jumuiya ya kimataifa.

..hivi kuna ubaya gani kwa vyombo vya dola na tume ya uchaguzi kutenda HAKI sawa kwa vyama vyote vya siasa?

..2015 tulipoharibu uchaguzi wa Znz Wamarekani walitukatia msaada wa program yao ya MCC.

..serikali inafanya mambo ya hovyo ambayo sidhani kama yanaweza kurekebishwa kwa kuwa na waziri wa mambo ya nje mwenye weledi.
 
Kupitia akaunti yake ya Twitter, Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje, Mike Pompeo ameandika "Kuna matokeo ya kuingilia mchakato wa kidemokrasia. Kuanzia leo, tunaweka vizuizi vya visa kwa wale wanaohusika na uvurugaji wa uchaguzi nchini Tanzania. Tunabaki kujitolea kufanya kazi pamoja kuendeleza demokrasia na ustawi wa pande zote kwa nchi zetu zote mbili."

View attachment 1681412

Soma pia: Visa Restrictions on Tanzanians for Undermining the Democratic Process and Human Rights - United States Department of State
___________________________________________________

Marekani imetangaza kuwawekea vikwazo vya vya kuingia nchini humo maafisa wa Tanzania ambao nchi hiyo inawatuhumu kwa kile wanachokitaja kuwa kuharibu uchaguzi mkuu wa Oktoba 28, mwaka 2020.

Maofisa hao wanatajwa kuhusika kuingilia mchakato wa uchaguzi na kuminya utekelezaji wa demokrasia.

Hata hivyo taarifa hiyo ya wizara ya mambo ya nje ya Marekani haijabainisha ni viongozi gani hasa kutoka Tanzania waliowekewa vikwazo vya kuingia Marekani.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na waziri wa mambo ya Nje wa Marekani Mike Pompeo, Waangalizi wa uchaguzi na mashirika ya kiraia wanadai kuwepo kwa udanganyifu katika uchaguzi huo pamoja na uvunjifu wa haki za binadamu wakati na baada ya uchaguzi.

Marekani inasema kuzimwa ama kuzimika kwa mitandao, kuminywa kwa waandishi wa habari na nguvu kubwa iliyotumiwa na jeshi la Polisi kunafanya uchaguzi huo kutokua huru na wa haki.

Katika uchaguzi huo, baadhi ya wagombea kutoka vyama vya upinzani walienguliwa kwa sababu mbalimbali na wengine kukamatwa.

Tume ya uchaguzi nchini humo na hata Serikali kupitia waziri wake wa mambo ya nje, Palamagamba Kabudi ilieleza kwamba uchaguzi ulikua huru na wa haki.

Marekani inasema pamoja na hatua hii iliyochukua dhidi ya maafisa wa Tanzania, inaendelea kufuatilia kwa karibu maendeleo ya hoja hiyo, huku ikisema haitasita kuchukua hatua zaidi dhidi ya wale wanaominya demokrasia na kuvunja haki za binadamu.

''Tunaitaka Tanzania, kuwachukulia hatua wale wote waliohusika kuvuruga uchaguzi, kufanya vurugu na kuleta vitisho'' ilisema sehemu ya taarifa hiyo.

Juhudi za kumpata msemaji wa serikali ya Tanzania kuzungumzia suala hilo mpaka sasa hazijazaa matunda, na tutaendelea kuwatafuta kwa ajili ya kuzungumzia suala hilo

Haya ni moja ya maamuzi ya mwisho ya utawala wa rais Donald Trump ambaye amebakiza saa chache kuachia mamlaka ya urais. Mpaka sasa haijafahamika iwapo utawala wa rais mpya Joe Biden kama utatekeleza maamuzi hayo. Tayari ofisi ya Biden imetangaza kuwa itatengua sera kadhaa za Trump mara tu baada ya kuingia ofisini kesho.

BBC.
Msiwe na wasiwasi; jamaa bado ana saa 20 tu madarakani. Jana alipokuwa Europe alisusiwa!
 
Hata aibu hauoni! Sisi hii tunaita last kick of 'dying animal'!!

"US baby group" naona kiswahili mfukoni! !!! Kwishiney habari yenu. Ha ha ha ha aa!!!Nisikie tena kelele zenu za haki ya kujieleza na demokrasia wakati walezi wenu wa hiyo liberty hawawezi kufanya hayo waagizayo yafanywe na nchi nyingine.
No justification for violation of human rights!
 
Biden aje apige vikwazo kabisa tena kama vile vya Iran ili akili ziwakae sawa MATAGA na wananchi wanyonge wa ccm
 
Nilitamani maneno haya angesema Meko sio wewe alafu tuone majibu ya Marekani Taifa kubwa watasemaje?
 
Mbona Makonda kazuiliwa na maisha yanaendelea manka?

Marekani kitu gani bhana dunia iko kiganjani!
Acha ubishi we MATAGA, siku jiwe atakapochapwa na TEZI DUME ndipo utakapoona madhara ya hiyo "statement" ya Pompeo. Utarudi hapa na kulia lia tu.
 
Uongo mtupu na story za matango pori ya vijiweni.Mara ya mwisho mgombea wa Democrat kushinda Texas ni mwaka 1976. Texas ni red state pimbi
"Massive" does not mean " Total" hence waliweza kuchagua you NUT! Ndio maana Democrats walishindwa TEXAS ambako voter suppression ilikuwa very significant compared to Georgia ambako Stacey Abrahams na network yake waliweza kuthibiti voter suppression significantly na hivyo Democrats kushinda!!
 
Acha ubishi we MATAGA, siku jiwe atakapochapwa na TEZI DUME ndipo utakapoona madhara ya hiyo "statement" ya Pompeo. Utarudi hapa na kulia lia tu.
Kwai india haipo au unadhani marekani ndo wajanja zaidi?
Ujinga umewafunga macho.
 
..njia rahisi zaidi ni kuishi vizuri na jumuiya ya kimataifa.

..hivi kuna ubaya gani kwa vyombo vya dola na tume ya uchaguzi kutenda HAKI sawa kwa vyama vyote vya siasa?

..2015 tulipoharibu uchaguzi wa Znz Wamarekani walitukatia msaada wa program yao ya MCC.

Kama nchi siku hizi ule utamaduni wa kushauriana juu ya mambo muhimu ya nchi hakuna tena!! Tumemuachia mtu mmoja asiyekuwa na hulka ya kushauliana afanye maamuzi peke yake!!! Maendeleo ya nchi hupatikana kwa haraka zaidi kama wananchi wana uhuru wa kutoa maoni yao juu ya nchi yao! Hata ndani ya chama tawala ule uhuru wa mawazo umepokwa na ndio maana Mwenyekiti wao ndio anachagua nani atagombea katika chaguzi zote tofauti na huko nyuma!!
 
Back
Top Bottom