Marekani yamtishia China: Eti Marekani itaipigania Taiwan kama China ikitaka kuichukua kwa nguvu

Kina watu hata akili hawana kabisa eti naye anajiona mjanja kuanzisha mada ya kipumbavu kiasi hiki.Akumbuke tu hapa Duniani hakuna Taifa la kuishinda USA kivita
Nyinyi mlio anza kufuatia siasa za kimataifa mwaka 2018 ndio mnatusumbua kwa kutujazia pumba humu.

Si ni huyu huyu Marekani alipata kipigo cha mbwa koko na cha aibu kutoka kwa Vietnam ,miaka 8 yuko vitani lakini hakufanikiwa kuteka hata kijiji.
 
Alafu si ndiye yule mchina aliyetaka kumpiga tafu Russia ,Marekani akamchimba mkwara mchina akarudisha mkia nyuma, bila shaka marekan anajua udhaifu wa China .alafu mbona China hapig hata mkwara marekani kuotetea Taiwan? Au kumsaidia Ukraine?
Tuliwahi kusema humu, china anaihitaji US na Ulaya ktk uchumi wake kuliko kitu chochote kile. Tukisema kwamba uchumi wa china ni kutokana na nguvu kubwa ya ulaya kununua bidhaa zake pamoja kuwekeza pale china wanatuona hatujaenda shule kama wao. China hawezi furukuta kwa namna yoyote ile mbele ya mabeberu.
 
Marekani imesema ipo tayari kuishambulia China kijeshi ikiwa taifa hilo litaishambulia Taiwan, hayo yamesemwa na Rais wa Marekani, Joe Biden akiwa katika ziara Tokyo, Japan, leo Mei 23, 2022.

Kauli hiyo ya Biden imeonekana kwenda kinyume na utaratibu wa Marekani wa kukwepa kuzungumzia mgogoro ulipo baina ya China na Taiwan uliodumu kwa miaka mingi.

Mara baada ya kutolewa kwa kauli hiyo China imejibu mapigo kwa kusema kuwa Marekani inacheza na moto na kudai suala la Taiwan ni mambo ya ndani ya China na kumuonya Biden kutodharau azimio juu ya suala la Taiwan ambayo China inachukulia kama sehemu ya eneo lake.


Source: DW
 
Trump mwenyewe aliwalima sunctions China, Hadi Huawei wakaenda na maji, China walikasilika Hadi wakamuwekea vikwazo Pompeo,wakamuacha Trump [emoji2]
 
Marekani hawezi kupigana na Taifa atalohisi litamjibu kwa kias kikubwa au karibia na kile alichofanya.

Utakumbuka mara baada ya kumuua Qasim Suleiman kamanda wa Iran, Iran ilisema italipa kisasi, siku wanamaliza mazishi usiku Iran ikapeleka makombora kwenye Base ya jeshi la Marekani pale Iraq.

Nakupa siri kuwa pale mashariki ya kati base kubwa ya jeshi iko Iraq, ile base ina technology zote za kijeshi pamoja ulinzi wa anga wa kutisha lakini makombora ya Iran yaliweza kupita na kupiga target na mwisho wa siku ulisikia matokeo japo taarifa za vifo walificha ila wale waliothirika kwenye bongo zao atleast walionekana ila vifo vya wanajeshi wasiopungua 100 walikufa palepale.

Baada ya ili tukio Donald Trump alitishia ataennda kuitandika Iran, ila unajua ule mpango ulifia wapi? Basi nakuambia mpaka leo hii Marekan anajiuliza Iran aliwezaje kupitisha mabomu yake tusiyaone mpk yaje kufika tulipo?

Sasa Marekan hawez kwenda vitan kwa taifa analoona limeendelea kitekinolojia ya jeshi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Trump mwenyewe aliwalima sunctions China, Hadi Huawei wakaenda na maji, China walikasilika Hadi wakamuwekea vikwazo Pompeo,wakamuacha Trump [emoji2]
Sasa jiulize ulaya iseme haipokei bidhaa za china na inafunga kabisa viwanda vyao vya pale china na kuvipeleka kwingine, watalia kilio kizito.
 
Kwahiyo mkuu hii siri waijua wewe? Wataalamu wengine hawaijui ila wewe ndo waitambua?
 
Na china anajua nguvu ya US alowekeza hapo taiwan, China anachoogopa ni uchumi wake tu. Ukimwambia aingia kwenye hilo bifu anajua kabisa anaweka uchumi wake kwenye risk.
Kuna mda utafikia ataona hakuna jinsi! Kumbuka US lengo lake kwa Taiwan iwe chini yake na mwisho wa siku ataenda kuweka mpk Base yake ya Jeshi! Hapo ndo pataa za kuwa pagumu!

Wenzetu wameendelea kijasusi, usione anaitetea Taiwan ila lengo kuu ni kuwa aitumie Taiwan kumchunguza na kumuharibu kabisa adui yake China.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha ujinga wewe, mbona USA mwenyewe yuko hapo kwa sababu ya tech ya Israel?

Amka usingizini wewe....[emoji847]
 
Marekani anashindaga vita kwenye sinema tu. Kitu alisi kwa sasa kipo Ukraine, kama ana ubavu atie mguu basi tumalize ubishi. Mimi naona anabwekabweka tu kama mbwakoko
 
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]marekani walificha Ila we ulijua kuwa wanajeshi 100 walikufa
 
Hawa madogo naona sasa wanavuka mpaka hadi kuzichezea saharubu. China asijifananishe na Russia, akae akijua Russia, USA, na hao wamangaribi hao ni kitu kimoja (wazungu).

Marekani kumchakaza mchina ni faida kwake kwani lile taifa lililokuwa likimnyatia kiuchumi litakuwa limesambaratishwa na stil ata kama uchumi wake utashuka nusu bado hakuna atakayemtisha.

Mchina achunge sana mdomo wake kwani atapata kichapo heavy asichokitegemea
 
Ngoja waje Waarabu wa kwa mtogole uwatambue vizuri [emoji16]
 
Alafu si ndiye yule mchina aliyetaka kumpiga tafu Russia ,Marekani akamchimba mkwara mchina akarudisha mkia nyuma, bila shaka marekan anajua udhaifu wa China .alafu mbona China hapig hata mkwara marekani kuotetea Taiwan? Au kumsaidia Ukraine?
Ulikuwa wapi mwaka jana China alipopigwa mkwara na USA afu Rais mstaafu wa USA Barrack Obama aliwakataza USA kutojihusisha vita kabisa na CHINA sababu China ni Taifa kubwa na linajiweza kiuchumi, hata kivita na ole wake USA ajipendekeze kijinga kwa CHINA kwani atatandikwa vizuri hasa [emoji848][emoji2]
 
Marekan anachonganisha Ili apate faida mbili, moja kuuza silaha na pili ili China ishuke kiuchumi Ila so kweli kua marekan anaipenda sana China kiasi hicho
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…