Tunawashukuru,sababu hawajaanza kutusaidia leo
Walianza zamani sana,ile miaka ya chakula cha yanga,na vile vyakula vilitwa bruga,miaka ya hivi karibu wakahamia kwenye ARVs,TB,Malaria,huduma za afya kwa mama na mtoto, mengi.hao hao ndiyo wanaoingiza fedha TASAF,chanjo ya surua,polio,.sikuelewaaga kabisa kwamba sasa hiv wana nia ya kutuua kupitia chanjo ya covid 19.sijui hiyo nia ya sasa iwe ni kwa sababu gani. sababu ukweli nchi yetu imeishi kwa misaada kwa kiasi kikubwa kutoka kwao saana,na inaendelea kutusaidia pakubwa
labda wale wajuvi watuambie sababu ni nini?
ni makinikia au ni gesi?au mbuga za wanyama? wanataka kutua kwa chanjo kwa sababu ya nini eti?