Maridhiano yanayoendelea ni hadaa kwa Taifa. Vyama vijitoe kabla havijakaangwa

Maridhiano yanayoendelea ni hadaa kwa Taifa. Vyama vijitoe kabla havijakaangwa

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
HAKI NA WAJIBU
  1. Katiba na sheria vinatoa haki na kila upande yaani raia na dola wana wajibu wa kufana ili sheria itekelezeke.
  2. Rais anamsema mtangulizi wake kuhusu utawala wa mabavu na vitisho lakini yeye hajafanya lolote kufuta mabavu hayo anataka maridhiano yaendelee huku akiagiza vyombo vya dola kuzuia mikutano ya kisheria ya vyama.
  3. Vyama vinaitwa meza ya maridhiano kana kwamba sheria zinazoruhusu shughuli za siasa zimekosewa na hazitekelezeki.
  4. CCM imeweka mapandikizi ndani ya vyama hivyo kasoro kimoja hivyo wanajiona wapo salama kushiriki maridhiano ambayo ni HADAA kubwa kwa Taifa.
  5. Bunge linatumika kuchafuana wenyewe kwa wenyewe badala ya kuisimamia nchi. Siass imezuiwa kufanyika na hakuna tamko wala azimio la Bunge kuhusu hili.
  6. CCM inafanya mikutano yake na maabdamano huku ikipewa ulinzi lakini vyama vingine wanazuiwa wakiambiwa hakuna ulinzi lakini jeshi hilo hilo lina kikosi cha mauaji kinachoenda kuwashambulia kwa silaha za kivita endapo watakaidi agizo haramu la kusitisha mikutano yao.
  7. Mahakama ambayo ndiyo inawajibu wa kutafsiri sheria inapokea mashtaka na kutoa hukumu kwa wanaokaidi maagizo haramu yanayokiuka sheria na katiba kuhusu mikutano na maandamano
Serikali ya CCM imepoteza ushawishi na uhalali. Vyama viachane na hayo maridhiano. Vijitoe sasa kwa sababu wanaohitaji maridhiano ni Watanzania ambao wameishi kwenye mkwamo wa kipuuzi zaidi ya miaka 60 ya Uhuru.

Vyama vinavyoendelea na maridhiano ni vile ambavyo ni ngazi na busati la CCM kuendelea kuwahadaa Watanzania ili iendelee kuwatawala kwa minajili ya kulinda ukwasi wa kikundi cha watawala kinachokwapua rasilimali za nchi na kujimilikisha uhalali wa kuamua nani aishi na nani afe ndani ya Tanzania.

Maridhiano tanayoendelea yanakiuka Katiba na Sheria za nchi. Yasitishwe.
 
HAKI NA WAJIBU
  1. Katiba na sheria vinatoa haki na kila upande yaani raia na dola wana wajibu wa kufana ili sheria itekelezeke.
  2. Rais anamsema mtangulizi wake kuhusu utawala wa mabavu na vitisho lakini yeye hajafanya lolote kufuta mabavu hayo anataka maridhiano yaendelee huku akiagiza vyombo vya dola kuzuia mikutano ya kisheria ya vyama...
Maridhiano hayana faida yoyote kama yule anayeratibu maridhiano lengo lake ni kuendelea kukandamiza haki za vyama vingine.
 
Mengine yote uko sahihi na nakubaliana na wewe ndugu Msanii

Hata hivyo sikubaliani na ushauri/pendekezo lako la watu wanatofautiana au wanaogombana au wanaosagiana kunguni kuacha kukaa chini pamoja ili kumaliza tofauti zao kwa njia ya majadiliano au kama mnavyoiita "maridhiano..."

Kama unashauri watu wasimalize tofauti zao kwa mazungumzo, then watumie njia gani? Wapigane ngumi...?

HAPANA..!!

Tunachotakiwa ni kushauri namna njema ambayo majadiliano haya yanapaswa kuendelea kufanyika. Ubabe haujawahi kuleta suluhu popote pale duniani isipokuwa adha na mateso kwa wananchi...

Mashauriano au maridhiano ya kitaifa yaendelee. Na ndugu Freeman Mbowe - Mwenyekiti wa CHADEMA (T) alifafanua vyema kabisa juu ya hili siku mbili zilizopita akiwa huko Marekani na mimi kwa kweli nilimwelewa vizuri kabisa...
 
HAPANA..!!

Tunachotakiwa ni kushauri namna njema ambayo majadiliano haya yanapaswa kuendelea kufanyika. Ubabe haujawahi kuleta suluhu popote pale duniani isipokuwa adha na mateso kwa wananchi...

Mashauriano au maridhiano ya kitaifa yaendelee. Na ndugu Freeman Mbowe - Mwenyekiti wa CHADEMA (T) alifafanua vyema kabisa juu ya hili siku mbili zilizopita akiwa huko Marekani na mimi kwa kweli nilimwelewa vizuri kabisa...
Naam
Wananchi wanawakilishwaje kwenye haya maridhiano?

Unasema tushauri namna bora ya majadiliano hayo. Upo serious kweli?
Tuishauri serikali hii au nani haswa?

Ushauri unaotolewa kila kukicha kwamba Serikali iheshimu Katiba na sheria za nchi zinazoruhusu vyama kukusanyika na kufanya siasa kihalali, lini walitekeleza?

Wanajadiliana masuala ya kisheria kwa njia za kisiasa.
Kimsingi Katiba mpya ni msingi
 
HAKI NA WAJIBU
  1. Katiba na sheria vinatoa haki na kila upande yaani raia na dola wana wajibu wa kufana ili sheria itekelezeke.
  2. Rais anamsema mtangulizi wake kuhusu utawala wa mabavu na vitisho lakini yeye hajafanya lolote kufuta mabavu hayo anataka maridhiano yaendelee huku akiagiza vyombo vya dola kuzuia mikutano ya kisheria ya vyama.
  3. Vyama vinaitwa meza ya maridhiano kana kwamba sheria zinazoruhusu shughuli za siasa zimekosewa na hazitekelezeki.
  4. CCM imeweka mapandikizi ndani ya vyama hivyo kasoro kimoja hivyo wanajiona wapo salama kushiriki maridhiano ambayo ni HADAA kubwa kwa Taifa.
  5. Bunge linatumika kuchafuana wenyewe kwa wenyewe badala ya kuisimamia nchi. Siass imezuiwa kufanyika na hakuna tamko wala azimio la Bunge kuhusu hili.
  6. CCM inafanya mikutano yake na maabdamano huku ikipewa ulinzi lakini vyama vingine wanazuiwa wakiambiwa hakuna ulinzi lakini jeshi hilo hilo lina kikosi cha mauaji kinachoenda kuwashambulia kwa silaha za kivita endapo watakaidi agizo haramu la kusitisha mikutano yao.
  7. Mahakama ambayo ndiyo inawajibu wa kutafsiri sheria inapokea mashtaka na kutoa hukumu kwa wanaokaidi maagizo haramu yanayokiuka sheria na katiba kuhusu mikutano na maandamano
Serikali ya CCM imepoteza ushawishi na uhalali. Vyama viachane na hayo maridhiano. Vijitoe sasa kwa sababu wanaohitaji maridhiano ni Watanzania ambao wameishi kwenye mkwamo wa kipuuzi zaidi ya miaka 60 ya Uhuru.

Vyama vinavyoendelea na maridhiano ni vile ambavyo ni ngazi na busati la CCM kuendelea kuwahadaa Watanzania ili iendelee kuwatawala kwa minajili ya kulinda ukwasi wa kikundi cha watawala kinachokwapua rasilimali za nchi na kujimilikisha uhalali wa kuamua nani aishi na nani afe ndani ya Tanzania.

Maridhiano tanayoendelea yanakiuka Katiba na Sheria za nchi. Yasitishwe.
TATIZO LENU MNAPENDA KUANDIKA NA KULAUMU KUSHIRIKI MNAKAA NYUMA MNAJIFICHA
 
TATIZO LENU MNAPENDA KUANDIKA NA KULAUMU KUSHIRIKI MNAKAA NYUMA MNAJIFICHA
Waliojitokeza wote waulize kama shetani aliwaacha waishi vyema.

Nitajificha nyuma ya keyboard hadi kieleweke.

Ukikua utaelewa
 
The Palm Beach ,

..Mbowe inabidi aende kwa wananchi azungumze nao kabla hajarudi kwa wananchi.

..Wananchi wanaelekea kukosa imani na vikao vya maridhiano. Mbowe akasikilize wananchi nchi nzima, na kuwapa mrejesho.

.."Honey moon" ya kuwa Ccm na Cdm wanazungumza imekwisha. Wananchi wanataka kuona maazimio au hatua za utekelezaji wa kinachozungumzwa.
 
Cdm wanatakiwa kuwa makini Sana katika hili la sivyo credibility ya chama itakuwa katika mashaka makubwa Sana kwa wananchi.

Kuna ulazima wa CDM kusikia wananchi wanasema nini kuhusu maridhiano sio cdm kutaka wasikilizwe wao tu na wananchi ili kutimiza matakwa yao na sio matakwa ya wananchi.

"Maneno bila matendo hakuna kitu "
 
Kwenye kila kikao cha maridhiano kuna bahasha inapita na tabasamu juu, chadema endeleeni kukaa kwenye vikao.
 
The Palm Beach ,

..Mbowe inabidi aende kwa wananchi azungumze nao kabla hajarudi kwa wananchi.

..Wananchi wanaelekea kukosa imani na vikao vya maridhiano. Mbowe akasikilize wananchi nchi nzima, na kuwapa mrejesho.

.."Honey moon" ya kuwa Ccm na Cdm wanazungumza imekwisha. Wananchi wanataka kuona maazimio au hatua za utekelezaji wa kinachozungumzwa.
Nakubaliana na wewe ndugu JokaKuu...

Hotuba yake ya juzi kule USA kidogo ilitushangaza kwenye baadhi ya hoja zake...

Kwamba, wamekubaliana mambo mengine yasiwe disclosed (kwamba ni siri) kati yao baadhi viongozi wa CHADEMA na CCM..

Hii ni hapana. Hakuna siri tunapozungumza mambo ya nchi na wananchi..!

Kwa hiyo, nakubaliana na wewe kwamba, M/Kiti ndugu freeman Mbowe na CHADEMA kwa ujumla watoke kila wakati watuambie;

1. Hoja za maridhiano zilizo mezani ni zipi na zipi..

2. Kila moja ina maendeleo ya kukubaliana au kutokukubaliana kwa kiwango gani..

3. Nini changamoto za majadiliano hayo wanayokabiliana nayo...

4. Mwisho wawe wanatuambia wananchi tufanye nini paliposhindikana kupatana na kwa yale waliyokubaliana..

NB: Wakumbuke tu kuwa CHADEMA na CCM hawajadiliani kuhusu maslahi yao viongozi na vyama vyao. Wanajadiliana kuhusu mustakabali wa nchi hii na wananchi wake...
 
The Palm Beach ,

..Mbowe inabidi aende kwa wananchi azungumze nao kabla hajarudi kwa
Ansendaje kwa wananchi wakati mikutano ya vyama na wananchi imeharamishwa na madiktekta miungu watu?
  1. Vyama vijitoe maridhiano
  2. Serikali itimize wajibu wake wa utawala wa katiba na sheria
  3. Vyama na CCM wabebe agenda ya maridhiano na amani kwenye mikutano yao.
KInachoendelea ni sawa na mtu mzima kukuambia mtu mzima jambo la kitoto akikutaka ulikubali. Atakupuuza daima ukiendelea kuambatana naye.

CCM inaleta hadaa nyingi sana
 
Hakuna chama chochote cha upinzani ambacho hakina mapandikizi,ccm ni habari nyengine upinzani wa kweli utatoka ndani ya ccm sio cuf,act wala nani uko
 
HAKI NA WAJIBU
  1. Katiba na sheria vinatoa haki na kila upande yaani raia na dola wana wajibu wa kufana ili sheria itekelezeke.
  2. Rais anamsema mtangulizi wake kuhusu utawala wa mabavu na vitisho lakini yeye hajafanya lolote kufuta mabavu hayo anataka maridhiano yaendelee huku akiagiza vyombo vya dola kuzuia mikutano ya kisheria ya vyama.
  3. Vyama vinaitwa meza ya maridhiano kana kwamba sheria zinazoruhusu shughuli za siasa zimekosewa na hazitekelezeki.
  4. CCM imeweka mapandikizi ndani ya vyama hivyo kasoro kimoja hivyo wanajiona wapo salama kushiriki maridhiano ambayo ni HADAA kubwa kwa Taifa.
  5. Bunge linatumika kuchafuana wenyewe kwa wenyewe badala ya kuisimamia nchi. Siass imezuiwa kufanyika na hakuna tamko wala azimio la Bunge kuhusu hili.
  6. CCM inafanya mikutano yake na maabdamano huku ikipewa ulinzi lakini vyama vingine wanazuiwa wakiambiwa hakuna ulinzi lakini jeshi hilo hilo lina kikosi cha mauaji kinachoenda kuwashambulia kwa silaha za kivita endapo watakaidi agizo haramu la kusitisha mikutano yao.
  7. Mahakama ambayo ndiyo inawajibu wa kutafsiri sheria inapokea mashtaka na kutoa hukumu kwa wanaokaidi maagizo haramu yanayokiuka sheria na katiba kuhusu mikutano na maandamano
Serikali ya CCM imepoteza ushawishi na uhalali. Vyama viachane na hayo maridhiano. Vijitoe sasa kwa sababu wanaohitaji maridhiano ni Watanzania ambao wameishi kwenye mkwamo wa kipuuzi zaidi ya miaka 60 ya Uhuru.

Vyama vinavyoendelea na maridhiano ni vile ambavyo ni ngazi na busati la CCM kuendelea kuwahadaa Watanzania ili iendelee kuwatawala kwa minajili ya kulinda ukwasi wa kikundi cha watawala kinachokwapua rasilimali za nchi na kujimilikisha uhalali wa kuamua nani aishi na nani afe ndani ya Tanzania.

Maridhiano tanayoendelea yanakiuka Katiba na Sheria za nchi. Yasitishwe.

Unafanyaje maridhiano na CCM. Wao wanawaza madaraka Yani wao wanawaza Tanzania ni Mali yao.
 
Mengine yote uko sahihi na nakubaliana na wewe ndugu Msanii

Hata hivyo sikubaliani na ushauri/pendekezo lako la watu wanatofautiana au wanaogombana au wanaosagiana kunguni kuacha kukaa chini pamoja ili kumaliza tofauti zao kwa njia ya majadiliano au kama mnavyoiita "maridhiano..."

Kama unashauri watu wasimalize tofauti zao kwa mazungumzo, then watumie njia gani? Wapigane ngumi...?

HAPANA..!!

Tunachotakiwa ni kushauri namna njema ambayo majadiliano haya yanapaswa kuendelea kufanyika. Ubabe haujawahi kuleta suluhu popote pale duniani isipokuwa adha na mateso kwa wananchi...

Mashauriano au maridhiano ya kitaifa yaendelee. Na ndugu Freeman Mbowe - Mwenyekiti wa CHADEMA (T) alifafanua vyema kabisa juu ya hili siku mbili zilizopita akiwa huko Marekani na mimi kwa kweli nilimwelewa vizuri kabisa...

Tatizo sio maridhiano, tatizo uanfanya maridhiano na nani?. Je huyo unayefanua naye maridhiano anaaminika?. Hawezi kuvunja makubaliano huko mbeleni?. Ichukue Zanzibar Kama case study.
 
Vyama viachane na hayo maridhiano. Vijitoe sasa kwa sababu wanaohitaji maridhiano ni Watanzania ambao wameishi kwenye mkwamo wa kipuuzi zaidi ya miaka 60 ya Uhuru.
Wakisusa Ccm watakula kila kitu peke yao.
 
TATIZO LENU MNAPENDA KUANDIKA NA KULAUMU KUSHIRIKI MNAKAA NYUMA MNAJIFICHA
A
Kosa ni la Polisi na JWTZ kuwachukia waandamanaji kuliko mafisadi. Kipindi CHADEMA waanaandaa UKUTA polisi nchi nzima wakaanza mazoezi na JWTZ wakaanza nao kutembea njiani. Wakawa wanashindana na CHADEMA?.

Sasa Kama JWTZ wameamua kuwa upande wa mafisadi wa CCM wananchi wafanyeje?. Siki vyombo vya dola vikalilinda taifa na sio CCM , Basi siku hiyo ndio utajua watanzania wanaogopa maandamano au la.
 
Back
Top Bottom