Maridhiano yanayoendelea ni hadaa kwa Taifa. Vyama vijitoe kabla havijakaangwa

Maridhiano yanayoendelea ni hadaa kwa Taifa. Vyama vijitoe kabla havijakaangwa

The Palm Beach ,

..Mbowe inabidi aende kwa wananchi azungumze nao kabla hajarudi kwa wananchi.

..Wananchi wanaelekea kukosa imani na vikao vya maridhiano. Mbowe akasikilize wananchi nchi nzima, na kuwapa mrejesho.

.."Honey moon" ya kuwa Ccm na Cdm wanazungumza imekwisha. Wananchi wanataka kuona maazimio au hatua za utekelezaji wa kinachozungumzwa.

Hilo ndio suluhisho sio kujikomba kana kwamba mama Samiah ana jema Sana.
 
Hakuna chama chochote cha upinzani ambacho hakina mapandikizi,ccm ni habari nyengine upinzani wa kweli utatoka ndani ya ccm sio cuf,act wala nani uko

Acha kauli zilizopitwa na wakati.

Una maanisha utakatifu utaletwa na shetani?. Yani ccm ( shetani) ndio ataleta upinzani wa kweli (utakatifu). Tuache kuongea mambo ambayo siyo realistic.
 
Huyu mama Ni majanga. Sijui wanampendea Nini? Nilidhani atakuja na mambo tofauti kumbe naye ni mnafiki unazuia wapinzani kufanya siasa halafu unakopa Trilioni 91 na tozo juu.
 
Acha kauli zilizopitwa na wakati.

Una maanisha utakatifu utaletwa na shetani?. Yani ccm ( shetani) ndio ataleta upinzani wa kweli (utakatifu). Tuache kuongea mambo ambayo siyo realistic.
Kwa hiyo unakataa kuwa chadema hakuna mapandikizi ya ccm?
 
Maridhiano ya nini? Awaambie wananchi wameongea nini kwenye maridhiano
Ameongea Marekani huko ndio walipa kodi wapo?
Heche kanyaga twende!
Huku ni kupotezeana muda na kuwadanganya wananchi…
Kundi kubwa limeenda Marekani kufanya nini? Mwenyekiti na Makamu why?
Kuna watakaochukia but tusidanganyane lipo jambo…
 
Dj anajua ila maridhiano ambayo hayana time frame ni kama kuhadaa watu
 
Mengine yote uko sahihi na nakubaliana na wewe ndugu Msanii

Hata hivyo sikubaliani na ushauri/pendekezo lako la watu wanatofautiana au wanaogombana au wanaosagiana kunguni kuacha kukaa chini pamoja ili kumaliza tofauti zao kwa njia ya majadiliano au kama mnavyoiita "maridhiano..."

Kama unashauri watu wasimalize tofauti zao kwa mazungumzo, then watumie njia gani? Wapigane ngumi...?

HAPANA..!!

Tunachotakiwa ni kushauri namna njema ambayo majadiliano haya yanapaswa kuendelea kufanyika. Ubabe haujawahi kuleta suluhu popote pale duniani isipokuwa adha na mateso kwa wananchi...

Mashauriano au maridhiano ya kitaifa yaendelee. Na ndugu Freeman Mbowe - Mwenyekiti wa CHADEMA (T) alifafanua vyema kabisa juu ya hili siku mbili zilizopita akiwa huko Marekani na mimi kwa kweli nilimwelewa vizuri kabisa...
Mbowe aache kuitumia CDM kufanya maridhiano ya kitapeli. Kama ana maslahi yake binafsi na hayo maridhiano, basi aachie uenyekiti lakini sio kugeuza watu kuwa mateka wa CCM. Machafuko pekee ndio njia ya kuheshimiana sio zaidi ya hapo.
 
HAKI NA WAJIBU
  1. Katiba na sheria vinatoa haki na kila upande yaani raia na dola wana wajibu wa kufana ili sheria itekelezeke.
  2. Rais anamsema mtangulizi wake kuhusu utawala wa mabavu na vitisho lakini yeye hajafanya lolote kufuta mabavu hayo anataka maridhiano yaendelee huku akiagiza vyombo vya dola kuzuia mikutano ya kisheria ya vyama.
  3. Vyama vinaitwa meza ya maridhiano kana kwamba sheria zinazoruhusu shughuli za siasa zimekosewa na hazitekelezeki.
  4. CCM imeweka mapandikizi ndani ya vyama hivyo kasoro kimoja hivyo wanajiona wapo salama kushiriki maridhiano ambayo ni HADAA kubwa kwa Taifa.
  5. Bunge linatumika kuchafuana wenyewe kwa wenyewe badala ya kuisimamia nchi. Siass imezuiwa kufanyika na hakuna tamko wala azimio la Bunge kuhusu hili.
  6. CCM inafanya mikutano yake na maabdamano huku ikipewa ulinzi lakini vyama vingine wanazuiwa wakiambiwa hakuna ulinzi lakini jeshi hilo hilo lina kikosi cha mauaji kinachoenda kuwashambulia kwa silaha za kivita endapo watakaidi agizo haramu la kusitisha mikutano yao.
  7. Mahakama ambayo ndiyo inawajibu wa kutafsiri sheria inapokea mashtaka na kutoa hukumu kwa wanaokaidi maagizo haramu yanayokiuka sheria na katiba kuhusu mikutano na maandamano
Serikali ya CCM imepoteza ushawishi na uhalali. Vyama viachane na hayo maridhiano. Vijitoe sasa kwa sababu wanaohitaji maridhiano ni Watanzania ambao wameishi kwenye mkwamo wa kipuuzi zaidi ya miaka 60 ya Uhuru.

Vyama vinavyoendelea na maridhiano ni vile ambavyo ni ngazi na busati la CCM kuendelea kuwahadaa Watanzania ili iendelee kuwatawala kwa minajili ya kulinda ukwasi wa kikundi cha watawala kinachokwapua rasilimali za nchi na kujimilikisha uhalali wa kuamua nani aishi na nani afe ndani ya Tanzania.

Maridhiano tanayoendelea yanakiuka Katiba na Sheria za nchi. Yasitishwe.
kumbe hata huyajui maridhiano.
maridhiano ni baina ya ccm na CHADEMA wewe unasema vyama vyote.

jichunguze kwanza
 
Mbowe aache kuitumia CDM kufanya maridhiano ya kitapeli. Kama ana maslahi yake binafsi na hayo maridhiano, basi aachie uenyekiti lakini sio kugeuza watu kuwa mateka wa CCM.
Nakubaliana na wewe kwenye hili👆👆👆
Machafuko pekee ndio njia ya kuheshimiana sio zaidi ya hapo.
Lakini kwa hili 👆 👆👆, HAPANA KUBWA KABISA..!!

Na nakukemea waziwazi kabisa kuwa, kwa wazo hilo umekeunga ndugu yangu Tindo. Na kwa hiyo namuapiza shetani aliyeweka roho ya ugomvi na machafuko ndani yako ashindwe kwa Jina la Yesu Kristo wa Nazareth...!

Kwa hili, una maana ya kuwa Freeman Mbowe atangaze mapigano kati ya walio madarakani serikalini na bunduki zao dhidi ya wananchi wasio na silaha...!

Is this what you want Tindo...?

Hili halimhitaji Mbowe kukuambia anza kupigana nao kwa nguvu za mwili wa damu na nyama...

Wewe kama unaona njia sahihi ya mazungumzo ya amani mezani inakuchelewesha, unaweza tu kuanza wewe kupigana nao na wakitokea watakao kuunga mkono, basi mnaliendeleza kwa pamoja....!!

But I am strongly sure that, kwa njia hii Mbowe na CHADEMA together are in the right track....

Labda ungeweza kushauri kuwa, CHADEMA wanapaswa kuwa aggressive a little bit kwa kuilazimisha serikali na chama kilicho kwenye dola yaani CCM kufanya vitu fulani fulani especially kutoyafanya mazungumzo kuwa ni siri kati ya viongozi wa CHADEMA na CCM/SERIKALI...

Tuwaambie kuwa maridhiano hayo wanayoyafanya ni mali ya wananchi na wao tumewapa dhamana na nafasi tu ya kuzungumza kwa niaba yetu sote...

Na kwa hiyo lazima kuwe na updates za mara kwa mara ya nini kinaendelea na kuwe na framework ya process yote ya dialogue hiyo kuonyesha yameanza na yanatakiwa kuisha lini...

Isiwe ni mazungumzo yasiyo na mwisho. Mazungumzo ya namna hiyo ni mchezo usio na tija huku yakila fedha ya umma tu....

Lakini kuomba kutokee machafuko kwa sababu iwayo yoyote is not an alternative solution ya changamoto za nchi hii zaidi kwamba italeta adha na maumivu yasiyo na sababu kwa watoto wetu bure.....

Tindo, CCM hii itatoka madarakani bila ya wananchi kupigana sisi kwa sisi. Hawa taratibu wameshaanza kujinyonga wenyewe na mwisho watakata roho kabisa...!
 
HAKI NA WAJIBU
  1. Katiba na sheria vinatoa haki na kila upande yaani raia na dola wana wajibu wa kufana ili sheria itekelezeke.
  2. Rais anamsema mtangulizi wake kuhusu utawala wa mabavu na vitisho lakini yeye hajafanya lolote kufuta mabavu hayo anataka maridhiano yaendelee huku akiagiza vyombo vya dola kuzuia mikutano ya kisheria ya vyama.
  3. Vyama vinaitwa meza ya maridhiano kana kwamba sheria zinazoruhusu shughuli za siasa zimekosewa na hazitekelezeki.
  4. CCM imeweka mapandikizi ndani ya vyama hivyo kasoro kimoja hivyo wanajiona wapo salama kushiriki maridhiano ambayo ni HADAA kubwa kwa Taifa.
  5. Bunge linatumika kuchafuana wenyewe kwa wenyewe badala ya kuisimamia nchi. Siass imezuiwa kufanyika na hakuna tamko wala azimio la Bunge kuhusu hili.
  6. CCM inafanya mikutano yake na maabdamano huku ikipewa ulinzi lakini vyama vingine wanazuiwa wakiambiwa hakuna ulinzi lakini jeshi hilo hilo lina kikosi cha mauaji kinachoenda kuwashambulia kwa silaha za kivita endapo watakaidi agizo haramu la kusitisha mikutano yao.
  7. Mahakama ambayo ndiyo inawajibu wa kutafsiri sheria inapokea mashtaka na kutoa hukumu kwa wanaokaidi maagizo haramu yanayokiuka sheria na katiba kuhusu mikutano na maandamano
Serikali ya CCM imepoteza ushawishi na uhalali. Vyama viachane na hayo maridhiano. Vijitoe sasa kwa sababu wanaohitaji maridhiano ni Watanzania ambao wameishi kwenye mkwamo wa kipuuzi zaidi ya miaka 60 ya Uhuru.

Vyama vinavyoendelea na maridhiano ni vile ambavyo ni ngazi na busati la CCM kuendelea kuwahadaa Watanzania ili iendelee kuwatawala kwa minajili ya kulinda ukwasi wa kikundi cha watawala kinachokwapua rasilimali za nchi na kujimilikisha uhalali wa kuamua nani aishi na nani afe ndani ya Tanzania.

Maridhiano tanayoendelea yanakiuka Katiba na Sheria za nchi. Yasitishwe.

Rahisi kupinga ! Tupe mawazo yangu tutaenda vipi mbele kama taifa ukizingatia Watanzania ni waoga sana hata kuandamana ni shida
 
Rahisi kupinga ! Tupe mawazo yangu tutaenda vipi mbele kama taifa ukizingatia Watanzania ni waoga sana hata kuandamana ni shida
Kwani wewe Kamundu siyo mtanzania..?

Kama ni mtanzania, kwanini unajitoa? Ina maana na wewe ni mwoga vilevile, au siyo...?

Kama jibu ni HAPANA, basi kumbe unaweza kuanza kuvaa wewe ujasiri wa kuanzisha maandamano or any other kind of physical confrontations dhidi ya watawala ili ku - achieve political ambitions zenu...!

Yaani nyie ni kama vimbwa koko vile vioga. Mnabweka mkiwa pembeni kwa kuhimiza wengine waanzishe vurugu za kisiasa huku nyie wenyewe mkiwa mmejificha vyumbani msiguse sekeseke hilo hata kwa vidole vyenu...!

Mnakosea. Vita hivi vinapiganwa kwa HEKIMA na MAARIFA.. Tundu Lissu kalisema hili several times sijui kwa nini hamuelewi...

Mtawezaje kupigana na watu wenye silaha huku nyie mkiwa mikono mitupu? Mtakuwa hamna akili kuingia kwenye vita ya namna hiyo...!!

Acheni watu wazungumze ili kumaliza tofauti zao za kisiasa. Kama kuna mahali wanakosea, shaurini namna ya kuboresha ili mwisho wa siku nchi hii ubaki salama na yenye umoja...

Nchi na wananchi wa nchi hawana shida. Shida ni baadhi ya viongozi wachache ndani ya CCM...

Hatuhitaji kutumia bomu la nuclear kuua panya ndani ya nyumba yetu....!
 
Maridhiano ya nini? Awaambie wananchi wameongea nini kwenye maridhiano
Ameongea Marekani huko ndio walipa kodi wapo?
Heche kanyaga twende!
Huku ni kupotezeana muda na kuwadanganya wananchi…
Kundi kubwa limeenda Marekani kufanya nini? Mwenyekiti na Makamu why?
Kuna watakaochukia but tusidanganyane lipo jambo…
Aliyetengeneza uwepo wa jambo hilo anajulikana ni CCM.

Tusishangae haya
 
Nakubaliana na wewe kwenye hili👆👆👆

Lakini kwa hili 👆 👆👆, HAPANA KUBWA KABISA..!!

Na nakukemea waziwazi kabisa kuwa, kwa wazo hilo umekeunga ndugu yangu Tindo. Na kwa hiyo namuapiza shetani aliyeweka roho ya ugomvi na machafuko ndani yako ashindwe kwa Jina la Yesu Kristo wa Nazareth...!

Kwa hili, una maana ya kuwa Freeman Mbowe atangaze mapigano kati ya walio madarakani serikalini na bunduki zao dhidi ya wananchi wasio na silaha...!

Is this what you want Tindo...?

Hili halimhitaji Mbowe kukuambia anza kupigana nao kwa nguvu za mwili wa damu na nyama...

Wewe kama unaona njia sahihi ya mazungumzo ya amani mezani inakuchelewesha, unaweza tu kuanza wewe kupigana nao na wakitokea watakao kuunga mkono, basi mnaliendeleza kwa pamoja....!!

But I am strongly sure that, kwa njia hii Mbowe na CHADEMA together are in the right track....

Labda ungeweza kushauri kuwa, CHADEMA wanapaswa kuwa aggressive a little bit kwa kuilazimisha serikali na chama kilicho kwenye dola yaani CCM kufanya vitu fulani fulani especially kutoyafanya mazungumzo kuwa ni siri kati ya viongozi wa CHADEMA na CCM/SERIKALI...

Tuwaambie kuwa maridhiano hayo wanayoyafanya ni mali ya wananchi na wao tumewapa dhamana na nafasi tu ya kuzungumza kwa niaba yetu sote...

Na kwa hiyo lazima kuwe na updates za mara kwa mara ya nini kinaendelea na kuwe na framework ya process yote ya dialogue hiyo kuonyesha yameanza na yanatakiwa kuisha lini...

Isiwe ni mazungumzo yasiyo na mwisho. Mazungumzo ya namna hiyo ni mchezo usio na tija huku yakila fedha ya umma tu....

Lakini kuomba kutokee machafuko kwa sababu iwayo yoyote is not an alternative solution ya changamoto za nchi hii zaidi kwamba italeta adha na maumivu yasiyo na sababu kwa watoto wetu bure.....

Tindo, CCM hii itatoka madarakani bila ya wananchi kupigana sisi kwa sisi. Hawa taratibu wameshaanza kujinyonga wenyewe na mwisho watakata roho kabisa...!

Sipingi unachoamini, lakini narudia tena, bila machafuko ni kupotezeana muda. Sihitaji kuambiwa na Mbowe maana tayari Mbowe ameshasalimu amri. Kenya hapo baada ya machafuko leo hii heshima ni tele. Mazungumzo ya mezani wakati wapinzani wanaonekana ni waoga, hakuna maridhiano hapo bali ni kuchorana.
 
Rahisi kupinga ! Tupe mawazo yangu tutaenda vipi mbele kama taifa ukizingatia Watanzania ni waoga sana hata kuandamana ni shida
MAandamano yanaweza kuwa suluhisho na labda yakawa chanzo cha shida mpya.

Kwa hali yetu Tanzania tunapaswa kuanza kujenga misingi kuanzia chini. Kuondokana na siasa za uharanakati na kupalilia siasa za mikakati.

CCM imejitwalia mamlaka ya kupenya kwenye viapo vya majeshi yetu halafu sisi wananchi tumebung'aa na kushadidia propaganda hatarishi za nchi yetu.

Ninaongea kwa dhati moyoni kwamba. Vita ama machafuko nchini havitaletwa na upinzani bali watawala ambao watayapigania maslahi yao na siyo maslahi ya nchi.


Nimewaza kwamba. Hadaa ya maridhiano inatumika kama taswira ya nia njema ya serikali iweze kukopesheka huko duniani.


Wananchi wanahitaji kujengwa na siyo kupelekeshwa. Mwisho wa siasa za kiushabiki ni mchezo wa mauti kwetu sote.
 
Back
Top Bottom