Marlaw: Sina mpango wa kushiriki kampeni za kisiasa tena

Marlaw: Sina mpango wa kushiriki kampeni za kisiasa tena

Wote mnaounga mkono utetezi huu wa Marlow ni wapotoshaji wa hali halisi, anachohitaji Marlow hapa kuhurumiwa na kupata ushauri wa nini cha kufanya...hakuna uhusiano wowote wa yeye kuanguka kimuziki na kampeni za chama.

Na tusitumie mate wakati wino upo....Marlow si yupo, akapige kampeni kwa chadomo tuone ni nini kipya atakuja nacho.

Uwepo wa Sugu cdm imemsaidia vipi kimuziki ? kama huna jipya huna jipya tu.

Wapi kina Saida Karoli, Mr Nice, TID, Twenty pa, Q Chilla, Stara Thomas, Muumini, Ray c, Madojo na Domo, haya na Kanda Bongo man je ? nao walifanya kampeni za nani ? acheni kuwajaza vijana ujinga.

Kila mtanzania anajua vijana wakiingia kwenye kampeni ni njia nyingine ya kujitengenezea mkwanja, na wala hatosusiwa kwa sababu hiyo.

Tena nawashauri wachangamkie tenda sio kwa kuchagua chama bali kwa kuchagua mwenye dau refu, na msanii mwenye kisu kikali (anayekubalika zaidi) ale nyama kwa kwenda mbele hakuna kuremba......iwe ni nccr, ccm, cdm, dp, udp,ccj,cuf, chamudata etc...waingie mfukoni vijana wapigie kazi.
 
Mimi mwenyewe nilishangaa sana, msanii ni kioo cha jamii, kitendo kuimba nyimbo za ccm kwenye kampeni, kulidhihilisha jinsi gani asivyojielewa, time is steel allow turn back.
 
Baada ya watu kuweka hadharani account za ccm zikiwa hazina kitu watu wameingiwa woga
 
pi pi pi pi tupishe ww mku.da....

Nilikuwa nampenda sana huyu msanii nilikuwa na kazi zake cd & dvd hata kwenye cm nilikuwa na nyimbo zake nyingi sana!

Ila baada ya kuanza kujishaua na Mizigo fc nili-delete nyimbo zake zoteee...

dvd & cd nilizipiga moto zoteeee.....

Go to Hell Gambaz!
 
Hivi watu kama Mzee Yusuph, Ngwasuma, Twanga, Diamond na wengine wenye mafanikio ni wa vyama gani????!!!!

Hahaa ngwasuma timu ya taifaaaa...hatare wajameni sikilizeni machereografe yanasumbuaga maana mimbo ni za kitambo sana ...elombe kichinjaaa
 
attachment.php


Msanii aliyepata kuvuma sana kabla ya mwaka 2010 alimaarufu kwa jina la Marlaw, amejutia uamuzi wake wa kukipigia kampeni chama cha ccm kwani kimemporomosha kimuziki.

"Unajua mimi mwaka 2010 nimeburudisha ktk kampeni za ccm lakini nimeambulia kushuka kimuziki sijui ni siasa imehusika au la kwa sababu toka hapo nimetoa nyimbo nyingi lakini hazivumi tena, sasa sitaipigia ccm tena labda chama kingine si unajua vijana wako wapi mzee ha ha haaa si kwamba nimejitoa ccm hapana mi ni msanii naburudisha watu wote"

Mwananchi lilipotaka kujua ni chama gani amekilenga kukipigia kampeni kwa malipo alisema bado muda wa kukiweka hadharani.

Wasanii someni alama za nyakati msije jikuta mko njia panda kimuziki huu ni mfumo wa vyama vyama vingi.
Umesikika Marlaw.. jamaa atakuboreshea maslahi hawatakubali uipigie Chama kingine kampeni
 
Uccm wake umemmaliza kijana mdogo anashabikia magamba njaa mbaya sana.
 
attachment.php
Msanii aliyepata kuvuma sana kabla ya mwaka 2010 alimaarufu kwa jina la Marlaw, amejutia uamuzi wake wa kukipigia kampeni chama cha ccm kwani kimemporomosha kimuziki. "Unajua mimi mwaka 2010 nimeburudisha ktk kampeni za ccm lakini nimeambulia kushuka kimuziki sijui ni siasa imehusika au la kwa sababu toka hapo nimetoa nyimbo nyingi lakini hazivumi tena, sasa sitaipigia ccm tena labda chama kingine si unajua vijana wako wapi mzee ha ha haaa si kwamba nimejitoa ccm hapana mi ni msanii naburudisha watu wote" Mwananchi lilipotaka kujua ni chama gani amekilenga kukipigia kampeni kwa malipo alisema bado muda wa kukiweka hadharani. Wasanii someni alama za nyakati msije jikuta mko njia panda kimuziki huu ni mfumo wa vyama vyama vingi.
Huyo jamaa analalamika nini wakati ana mgao wa buku 7 pale Lumumba kila siku kwa mkataba wa miaka 5(2010-2015)
 
Baada ya watu kuweka hadharani account za ccm zikiwa hazina kitu watu wameingiwa woga
safi sana...CCM ni shombo..mbaya zaidi hana wa kumdai kwani aliyemshawishi pengine hayupo tena ktk chat..bila kujali km kijana kapokea chake au alah
 
Baada ya watu kuweka hadharani account za ccm zikiwa hazina kitu watu wameingiwa woga
haha..mwigulu anakwenda ongea na wa wafanyabiashara ili akawatishe watoe hela bila hivyo anawatuma TRA...
 
mbona diamond bado yuko juu..huyu kilaza asitafute mchawi,,mziki umemshinda anataka kukimbilia kwenye chama cha wahuni kama afande sele...anataka kugombea ubunge huyu
 
Ashirik kampein kwa wimbo wake upi unaoheat? Nape na wenzake wanaaakil sana,hawashindwi zunguka na Diamond platnum nchi nzima mwisho wa siku ushind kwao
 
kachelewa yeye aendelee kutumika ila hata mimi binafsi niliekuwa shabiki wake mkubwa tangua wakati ule nililazimika kuvunja cd zake zote sikuona hata umhimu wa kugawia mtu
 
Binafsi nampinga maamuzi yake kama akiyatekeleza, napenda nimshauri asifungamane na upande wowote ule asimamie Ngawira tu ndo iwe kaulimbiu yake.
 
aache umbumbu mbona Diamond anashiriki mikutano ya siasa na bado hajachuja? yeye aseme tu uwezo umeshuka wasanii wanatakiwa wafanye kazi zao kibiashara zaidi wakiitwa na CCM CDM au CUF waende tu ila iwe ni kibiashara zaidi tatizo wengine wanaenda pengine kwa kutegemea labda kupewa hata ukuu wa wilaya hapo ndo watachemsha vibaya
 
mbona diamond bado yuko juu..huyu kilaza asitafute mchawi,,mziki umemshinda anataka kukimbilia kwenye chama cha wahuni kama afande sele...anataka kugombea ubunge huyu

Ccm bwana ndo mmeishiwa hoja!! Kutoka chama cha kikabila, kidini, kikanda sasa ni cha kihuni.
 
marlow ccm ndo wamechangia kushuka kimziki kwani nyimbo zake alibadilisha zikawa za ccm watanzania hawapendi chama cha wahuni ndo amekosa soko na kushuka kiwango kimuziki ...
 
Huyu nae amechuja halafu anatafuta wa kumtupia lawama,mbona diamond anazidi kupanda chati?
 
Back
Top Bottom