Martin Ngoga wa Rwanda achaguliwa Spika Bunge la Afrika Mashariki. Tanzania na Burundi wasusia uchaguzi huo

Martin Ngoga wa Rwanda achaguliwa Spika Bunge la Afrika Mashariki. Tanzania na Burundi wasusia uchaguzi huo

Mwanzo siku zote unakuwaga mgumu, lakini naamini kizazi kijacho kitatambua umuhumu wa hii jumiya.
Huu sio mwanzo wa East Africa community, ilianza ikafa, na hii ya sasa ina zaidi ya 20 yrs huwezi kusema ndio mwanzo
 
Huu sio mwanzo wa East Africa community, ilianza ikafa, na hii ya sasa ina zaidi ya 20 yrs huwezi kusema ndio mwanzo
Ile ya mwanzo inatofauti kubwa sana na hii ya sasa hivi, maana ya mwanzo iliuwa ni ushirikiano wa kiuchumi tuu na sio wa kiasisa au kijamii au kibunge. Hivi sasa tumeingeza na nchi nyingine tatu labda na zingine zitajiunga baadae. Hii ya sasa inakwenda na changamoto za karne hii, vitu kama siasa, mawasiliano ya haraka, uhusiano wa kiusalama na kijeshi havikuwepo huko nyuma. Kwahiyo sio vyema kulinganisha jumuiya ya zamani na hii ya sasa.
 
Ninayetoa haya maoni ni mimi, na kila ninaloliongea hapa ni mtazamo wangu binafsi. Hivyo sio sahihi kusema kauli yangu ni conclusive wakati mimi natoa maoni kama raia wa kawaida!

Hata hivyo bado narudia kusema huo utaratibu haufai, haijalishi ni wake binafsi au ni sheria; Maana hata ikiwa sheria kuna mda inaonekana inahitaji kubadilishwa kuendana na mahitaji.

Msingi wangu uko kwenye kufanya kazi kama mfumo badala ya mtu mmoja mmoja,

Toyota Escudo naona umekutana na Joto la jiwe [emoji1].Nimeufuatilia ubishi wenu na kuona kuna dalili za uchama au U-Team.Mi napita.
 
Ok, sasa nimekuelewa kwamba unahisi haufai, ila mimi ninaona unafanya kazi na kufikia malengo yanayokusudiwa, japo ni kweli kwamba sio njia nzuri kutumika mara zote, ila kumbuka duniani kote kuna njia nyingi tu za kufanya watu wawajibike, Kikwete alitumia njia kama hizo unazopendekeza za kiuungwana matokeo yake tuliyaona, subiri kidogo jamaa awanyooshe kidogo ili wajue kwamba business in unusual nowdays.
Huo utaratibu haujawahi kufikia malengo yaliyokusudiwa, labda umesaidia kufikia matakwa binafsi! Kama ungekuwa umesaidia kufikia hayo malengo basi mambo kama hayo tungekuwa hatuyaoni, kuendelea kuyaona maana yake ni kuwa hauna matokeo chanya ya kiutendaji, labda unajenga hofu.

Naendelea kusisitiza kuwa yapo mambo mengi ninayokubaliana na rais wangu! Lakini yale ninayopishana naye, ni pamoja na hili!
 
Huo utaratibu haujawahi kufikia malengo yaliyokusudiwa, labda umesaidia kufikia matakwa binafsi! Kama ungekuwa umesaidia kufikia hayo malengo basi mambo kama hayo tungekuwa hatuyaoni, kuendelea kuyaona maana yake ni kuwa hauna matokeo chanya ya kiutendaji, labda unajenga hofu.

Naendelea kusisitiza kuwa yapo mambo mengi ninayokubaliana na rais wangu! Lakini yale ninayopishana naye, ni pamoja na hili!
Kaka katika hili sikubaliani na wewe kabisa, Magufuli amefanikisha mambo Mengi sana kwa kutumia mtindo wake huu wa kuwafanya watu wapate hofu, mfano mzuri ni utafiti wa TWAWEZA wa hivi karibuni ulioonyesha kati ya watu kumi waliohojiwa 8 wamesema rushwa imepungua sana, wengi wanakiri watumishi serikalini wamekuwa wakiwajibika, makusanyo ya nchi yameongezeka kufuatia kuziba mianya ya upotevu, Jumuiya za Kimataifa zinaridhishwa kwa jinsi serikali inavyotumia pesa za misaada, matukio ya ujambazi katika miji mikubwa yamepungua sana.

Kujenga hofu kwa watu wenye nia mbaya ni jambo zuri sana, lazima mtu ajue kwamba akifanya jambo kinyume na sheria za nchi au kazi lazima atapata msukosuko, hata Mungu pia ametujengea hofu kwamba tukifanya mambo mabaya hatotuacha salama.
 
Kaka katika hili sikubaliani na wewe kabisa, Magufuli amefanikisha mambo Mengi sana kwa kutumia mtindo wake huu wa kuwafanya watu wapate hofu, mfano mzuri ni utafiti wa TWAWEZA wa hivi karibuni ulioonyesha kati ya watu kumi waliohojiwa 8 wamesema rushwa imepungua sana, wengi wanakiri watumishi serikalini wamekuwa wakiwajibika, makusanyo ya nchi yameongezeka kufuatia kuziba mianya ya upotevu, Jumuiya za Kimataifa zinaridhishwa kwa jinsi serikali inavyotumia pesa za misaada, matukio ya ujambazi katika miji mikubwa yamepungua sana.

Kujenga hofu kwa watu wenye nia mbaya ni jambo zuri sana, lazima mtu ajue kwamba akifanya jambo kinyume na sheria za nchi au kazi lazima atapata msukosuko, hata Mungu pia ametujengea hofu kwamba tukifanya mambo mabaya hatotuacha salama.
Hofu sio lazima itolewe hadharani mkuu! Kwenye sehemu muafaka, yeye afoke kama anavyojua lakini viongozi wake awape stahi zao!.

Nadhani utofauti wangu na wewe katika hili ni kuwa ni sehemu gani hasa hiyo hofu inafaa kujengewa! Mimi napendekeza kwenye vikao au ofisini, hapo aongee, agonge meza na aandike barua za maonyo kadri awezavyo! Wakija huku nje wanakuwa kitu kimoja.

Kufokeana hadharani kwanza kunapunguza heshima kwa wananchi, kila mwananchi anakuona ukikoromewa hadharani, kila atakalokuwa anafanya watu watasema hawezi kitu ndo maana anakoromewa kila siku na mkuu wake!

Kwani shida iko wapi, kama ukimpa waziri guidelines unazozitaka na timeframe na kumwambia akishidwa kutekeleza anafukuzwa?

Shida ya huu utaratibu unasababisha waziri anajihami ili kumfurahisha mteuzi wake! Ngoja nikupe mfano, wakati waziri wa uvuvi anateuliwa alisema akiwa kagera kuwa uvuvi haramu usipoisha anajiuzuru! Hebu nenda kanda ya ziwa uliza kuhsu huo uvuvi kama umeisha au huyo waziri kajiuzuru!
Alichokifanya ni kutoa tamko la uoga maana kateuliwa huku akiwa hana mkakati muafaka wa kumaliza uvuvi haramu!

Halafu tukiongea kuhusu kujenga hofu simaanishi kwa watu wote, namaanisha kwa viongozi hasa walio chini yake wasifanye kazi kwa hofu! Maeneo mengine hofu inaweza kutumika, najua hilo na nalitambua. Mfano kumjengea jambazi hofu ni njia mojawapo ya kumshinda!

Hofu tunayoijadili hapa ni tofauti kidogo.
 
Hofu sio lazima itolewe hadharani mkuu! Kwenye sehemu muafaka, yeye afoke kama anavyojua lakini viongozi wake awape stahi zao!.

Nadhani utofauti wangu na wewe katika hili ni kuwa ni sehemu gani hasa hiyo hofu inafaa kujengewa! Mimi napendekeza kwenye vikao au ofisini, hapo aongee, agonge meza na aandike barua za maonyo kadri awezavyo! Wakija huku nje wanakuwa kitu kimoja.

Kufokeana hadharani kwanza kunapunguza heshima kwa wananchi, kila mwananchi anakuona ukikoromewa hadharani, kila atakalokuwa anafanya watu watasema hawezi kitu ndo maana anakoromewa kila siku na mkuu wake!

Kwani shida iko wapi, kama ukimpa waziri guidelines unazozitaka na timeframe na kumwambia akishidwa kutekeleza anafukuzwa?

Shida ya huu utaratibu unasababisha waziri anajihami ili kumfurahisha mteuzi wake! Ngoja nikupe mfano, wakati waziri wa uvuvi anateuliwa alisema akiwa kagera kuwa uvuvi haramu usipoisha anajiuzuru! Hebu nenda kanda ya ziwa uliza kuhsu huo uvuvi kama umeisha au huyo waziri kajiuzuru!
Alichokifanya ni kutoa tamko la uoga maana kateuliwa huku akiwa hana mkakati muafaka wa kumaliza uvuvi haramu!

Halafu tukiongea kuhusu kujenga hofu simaanishi kwa watu wote, namaanisha kwa viongozi hasa walio chini yake wasifanye kazi kwa hofu! Maeneo mengine hofu inaweza kutumika, najua hilo na nalitambua. Mfano kumjengea jambazi hofu ni njia mojawapo ya kumshinda!

Hofu tunayoijadili hapa ni tofauti kidogo.
Nadhani tunakwenda vizuri. Kwanza ninaomba tukubaliane kwamba mambo yanaenda kama anavyotaka yeye, ile kauli kwamba hayaendi ninaomba uachane nayo, sasa kuhusu huyo waziri aliyetoa ahadi na hakujiuzulu, ndiyo hao vichwa ngumu ambaa Magufuli anawatafuta, kumbuka waziri wa Maji na umwagiliaji alipotoa ahadi kule Lindi kwamba maji yangetoka kabla ya muda flani, Magu aliwaambia wananchi yasipotoka atamuwajibisha waziri, na ndicho kilichotokea, kwa hiyo mawaziri wengine wanajua kwamba ukitoa ahadi mbele ya rais na usipotimiza utatumbuliwa, inatuma ujumbe mzito kwa mawaziri wengine.

Ninarudia kusema, hii sio njia nzuri, lakini kama kuna mawaziri wanaambiwa in private na hawasikii wala kujirekebisha, ina maana hawajiheshimu na hawawajibiki, kwahiyo kukoromewa hadharani ni sehemu ya punishment, akiendelea atafukuzwa kazi, na kama anadhani amedhalilishwa, basi ajiuzulu ili asidhalilishwe tena.

Mimi sikubaliani na Magufuli katika masuala ya demokrasia, hasa kuminya uhuru wa vyama vya siasa, lakini katika utendaji yupo vizuri sana, hana tofauti sana na Kagame, nani anapinga kwamba Kagame anafanya vizuri katika maendeleo japo wanyarwanda wanaishi kwa hofu kubwa, kuanzia Janeth Kagame hadi mwanafunzi wa chekechea hakuna asiye na hofu, ila nchi inapiga hatua za maendeleo, Japo Magufuli hajafikia huko, lakini anaelekea huko.
 
Sasa inakuwaje Kimbisa amepata kuwa sufuri (0)?
Sasa hivi ilikuwa zamu kati ya Burundi , Rwanda au South sudani , Lakin Burundi na Rwanda waliingia Siku moja. Nani achukie kiti hicho cha Uspika? Kutokana na madai ya Burundi Na Tanzania anaestahili ni Burundi , Sababu zinazotolewa ni kwamba pamoja kwamba Burundi na Rwanda waliingia Siku moja , Katika Alfabetical order anatakiwa aanza Burundi , Hata Siku ya kuapisha wabunge Walifuata alfabetical order . Ila kina kinachoonekana yanataka kuingia masuala ya mwaka 2013 ya ule umoja Wa waliotayari EAC yaani Kenya, Uganda na Rwanda ndo maana Tanzania na Burundi wamepinga uchaguzi Wa spika.
 
Sasa hivi ilikuwa zamu kati ya Burundi , Rwanda au South sudani , Lakin Burundi na Rwanda waliingia Siku moja. Nani achukie kiti hicho cha Uspika? Kutokana na madai ya Burundi Na Tanzania anaestahili ni Burundi , Sababu zinazotolewa ni kwamba pamoja kwamba Burundi na Rwanda waliingia Siku moja , Katika Alfabetical order anatakiwa aanza Burundi , Hata Siku ya kuapisha wabunge Walifuata alfabetical order . Ila kina kinachoonekana yanataka kuingia masuala ya mwaka 2013 ya ule umoja Wa waliotayari EAC yaani Kenya, Uganda na Rwanda ndo maana Tanzania na Burundi wamepinga uchaguzi Wa spika.

..Kenya, Tanzania, na Uganda, nazo zilijiunga EAC wakati mmoja.

..sasa mbona Uspika ulianzia Tanzania, badala ya Kenya, kama Uspika unapatikana kwa alphabetical order?

..zaidi, kwanini Tanzania imeweka mgombea wakati ilishatoa Spika?

..pia kuna hoja kwamba Burundi wanaongoza sekretariat kwa hivyo ili kuleta usawa Bunge linapaswa kuongozwa na nchi nyingine.

..Wasikilize wabunge toka nchi wanachama wakijenga hoja zao hapa chini.


 
..Kenya, Tanzania, na Uganda, nazo zilijiunga EAC wakati mmoja.

..sasa mbona Uspika ulianzia Tanzania, badala ya Kenya, kama Uspika unapatikana kwa alphabetical order?

..zaidi, kwanini Tanzania imeweka mgombea wakati ilishatoa Spika?

..pia kuna hoja kwamba Burundi wanaongoza sekretariat kwa hivyo ili kuleta usawa Bunge linapaswa kuongozwa na nchi nyingine.
Suala ni mazungumzo , bila shaka mawaziri wakikutana mambo yatakaa vizuri sana.
 
Suala ni mazungumzo , bila shaka mawaziri wakikutana mambo yatakaa vizuri sana.

..mazungumzo yalipaswa kufanyika ndani ya bunge.

..sasa wabunge wetu wamekimbia mjadala.

..Burundi waliwasilisha barua kwa Katibu wa Bunge inayoeleza mambo ambayo hawakubaliani nayo, lakini kitu cha ajabu wakatoka nje ya kikao na hivyo kukosa nafasi ya kutetea hoja zao.
 
..mazungumzo yalipaswa kufanyika ndani ya bunge.

..sasa wabunge wetu wamekimbia mjadala.

..Burundi waliwasilisha barua kwa Katibu wa Bunge inayoeleza mambo ambayo hawakubaliani nayo, lakini kitu cha ajabu wakatoka nje ya kikao na hivyo kukosa nafasi ya kutetea hoja zao.
Barua nahic haikufanyiwa KAZI Na wakubwa wale
 
Back
Top Bottom