Marufuku Mtanzania kujiunga Jeshi la nchi nyingine

Marufuku Mtanzania kujiunga Jeshi la nchi nyingine

Ccm wanavunja sheria za nchi hii kila siku,mi nikipata nafasi najiunga na jeshi lolote hata kama ni somalia,!!
Yaani upate nafasi ya kujiunga na jeshi la Marekani,ukatae kisa uraia wa TZ!!!?aaaah wapi,hiyo passport yenu natupa,nachukua uraia mwingine
Naunga mkono hoja.
 
Tax apiga marufuku kwa watazania kujiunga na la jeshi la nchi nyengine. Alisema kwa mujibu wa sheria zao Mtanzania yoyote haruhusiwi kujiunga na jeshi la nchi yoyote isipokuwa jeshi la Tanzaia tu na kufanya hivyo kuvunja sheria za nchi.

---

SERIKALI: ‘Fuateni sheria na taratibu mkiwa nje ya nchi’

View attachment 2495178


Serikali imewataka Watanzania kuzingatia na kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi walizopo ili kulinda taswira nzuri ya nchi yao.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Stergomena Tax kuhusu kifo cha Nemes Tarimo, Mtanzania aliyefariki dunia nchini Urusi, alisema:

“Nitoe rai kwa Watanzania kuhakikisha wanazingatia sheria kanuni na taratibu za nchi walizopo, na pia wawe mabalozi wazuri wa kulinda taswira ya Tanzania.

Ikumbukwe kwa mujibu wa sheria zetu, Mtanzania yeyote haruhusiwi kujiunga na jeshi la nchi yoyote isipokuwa Jeshi la Tanzania na kufanya hivyo ni kuvunja sheria,” amesema Waziri huyo.

Amesema Mtanzania huyo alikwenda nchini Urusi mwaka 2020 kwa lengo la kujiunga na Chuo Kikuu cha Moscow Technological University (MIREA) kwa masomo ya Shahada ya Uzamili katika fani ya Business Informatics.

Ameongeza kuwa Mwezi Machi 2022, Mtanzania huyo alitiwa hatiani kwa kuhusika na vitendo vya uhalifu na kwa mujibu wa sheria za Urusi alihukumiwa kifungo cha miaka saba jela.

Waziri Tax ameongeza kuwa Tarimo akiwa gerezani alijiunga na kikundi cha kijeshi cha Urusi cha Wagner kwa ahadi ya kulipwa fedha na kuachiwa huru, baada ya kumaliza muda wa kutumika vita na alifikwa na umauti akiwa nchini humo.

Waziri Tax amesema kuwa mwili wa marehemu umeondoka nchini Urusi leo Januari 24, 2023 na unatarajiwa kuwasili nchini muda wowote kuanzia sasa na kuongeza kuwa Serikali imekuwa ikiwasiliana na Serikali ya Urusi, ili kuhakikisha mwili wa marehemu Tarimo unarejeshwa nchini na kukabidhiwa kwa familia yake kwa ajili ya taratibu za mazishi.

Waziri ametoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na Watanzania kwa msiba huo.

Waziri Tax amewauhakikishia umma na Diaspora wa Kitanzania wakiwemo wanafunzi walioko masomoni duniani kote kuwa serikali itaendelea kuwapa ushirikiano wakati
Kabla ya kukemea muangalie nafasi ya vijana nchi mwao kwenye majeshi yetu haya.

Kuna rushwa nyingi hadi kupenya huko nafasi zinatoka kwa upendeleo na nafasi nzuri zinatolewa kwa watoto wa vigogo mojakwamoja.

Then tuangalie na nchi za huko zilizoendelea nafasi za jeshi ni haki ya kila mtu hata asiwe raia, mshahara marupurupu kama yote alafu mwakataze vijana ni mjinga tu ndio ataacha hizo chance.

Jeshi la USA lina vijana wa tz kibao tu na huko Russia ni huyo aliyeuwawa ndio imegundulika ila wapo wengi pia..we imagine vikundi km alshabab na the like vinaveza kuwashawishi vijana wetu na wakajoin huko bila senti na kupigana bila vifaa vya maana sembushe minchi mikubwa na matajiri.

Ukweli ni kwamba vijana hawana namna ya kuchoropoka kwenda huko ila kama kungejuwa na upenyo kidogo kungekuwa na mafuriko makubwa kukimbilia huko.

Muhimu ni sera nzuri kwa vijana nchi zitazowavutia kuendelea kupambana nchini hapa hapa na sio tofauti hapo.

Njaa haina bausa na hakuna anayependa kunuka umasikini.
 
Kuna watanzania wengi nawafahamu ni wanajeshi wa marekani lakini badala ya kutoa kauli kali atueleze balozi zetu zinafanya Nini pale watanzania wanapopata matatizo wakiwa nje ya nchi.
Wanahakikisha wanapata mawakili pia wanapata muda wa kuwatembelea ni wazi Kuna uzembe kwenye wizara yake.
Sasa hao tayari ni raia wa marekani
Siyo watanzania tena
Point kuu ni hawa wanajiunga na majeshi kama mamluki(mecenaries)
Na kwa upande sioni kama ni shida maana ni moja ya utafutaji tu wa maisha

Ova
 
Wakuu nadhani tunamtafsiri waziri visivyo, marufuku mtanzania kujiunga na jeshi LA NCHI NYINGINE, hapa catch ni NCHI, ila kujiunga na vikundi vya kupiganaji sioni ni tatizo, ni ajira kama ajira zingine, nikiwa ni professional fighter Nina haki ya kutafuta ajira kwenye hivi vikundi vya kupiganaji ila sio NCHI
 
Huyu bi mkubwa anaongea ushubwada kabisa. Shenzi taipu!

Eti nipewe nafasi ya kujiunga na Jeshi la Marekani, Uingereza, Urusi, Uchina halafu nikatae kwa sababu ya visheria vyenu vya madafu? Mbwaaaaaaa! Yani immediately siwazi mara mbili mimi huyoooooo naenda kuvaa gwanda, to hell with your https://jamii.app/JFUserGuide#ng laws!
 
Sheria gani imevunjwa nikijiunga na jeshi la nchi nyingine.
Good observation , Kama waziri ingekuwa vyema angetaja kabisa hiyo Sheria na kifungu husika.
Mimi mwenyewe ndio mara ya kwanza
Ya uhamiaji na makazi. Kama uko interested na majeshi ya nchi zingine, ukane uraia wa tz kisheria then chukua uraia wa nchi husika ambapo utataka kujiunga na jeshi hilo

Embu taja hiyo Sheria na kifungu husika.
Tanzania hakuna Sheria inayoitwa Uhamiaji na ukazi
 
Kuna watanzania wengi nawafahamu ni wanajeshi wa marekani lakini badala ya kutoa kauli kali atueleze balozi zetu zinafanya Nini pale watanzania wanapopata matatizo wakiwa nje ya nchi.
Wanahakikisha wanapata mawakili pia wanapata muda wa kuwatembelea ni wazi Kuna uzembe kwenye wizara yake.

Mi namjua mmoja yupo France legion
Huyu Mama nadhani kakurupuka
 
Back
Top Bottom