Masaa 10 ya Jehanamu nyumbani kwa Sister

Masaa 10 ya Jehanamu nyumbani kwa Sister

Last Jumamosi nilipata mualiko kumtembelea Sister Home kwake Mikocheni. Nilienda na Mke Wangu na Mtoto wetu mmoja wa miaka 4.5
Wewe umefata yako ya wenzako yaache kama ulivyoyakuta. Umeyaleta hapa ili iweje?

Kama makosa ni ya mama'ko ndio hajamfunda dada'ko vyema. Unamtutukanisha mzazi wako tu. Mlezi ni mama, ndio maana hata wewe hukulelewa vyema unakuja kuyaanika mambo ya kifamilia hadharani. "Like sister like brother".
 
Sipendi watoto watundu watundu, kuna siku nipo hosp. Kuna mtoto kama miaka 6 hivi akaja kavamia Mkoba anataka kuufungua nikamshika mkono kwa upole, nikauminya ule mkono huku namwongelesha nikimkazia macho, “Unaitwa nani? Ninachapaaaaa! Kakae pale utulie, nilimminya kweli kweli na hakurudi tena kwangu.
Hahhahahaha
 
Last Jumamosi nilipata mualiko kumtembelea Sister Home kwake Mikocheni. Nilienda na Mke Wangu na Mtoto wetu mmoja wa miaka 4.5

Saa nne tulikuwa tumefika home maana tuliambiwa siku hiyo hata kinywa tukafungulie pale na jioni tukifungie pale pale. Waswahili wanasema mtu hakatai wito.
Familia ya futuhi 😁

Nilishaenda sehemu niko bored sebuleni kwa watu na ka Lumia changu nikawa nacheza game flan gumu la akili ...vitoto vikaanza lilia afu wakubwa tu ..na wazazi wake wanasema wanapenda game sana hao watoto..nikawaambia hili hawawezi cheza zaidi ya kugusa gusa tu mzazi wake anasema we wape uone hao watoto wana akili sana dhhu nikawanyima ..unaeka simu charge unakuta wametoa wanabofya bofya...nilitoa onyo kali mbele ya wazazi wao ..ni marufuku kushika hio simu bila ruksa yangu
 
Hilo jina tu linasadifu...watoto wenye mijina ya kizungu wanalelewa kijinga sana
Ni ugenini mkuu unapaswa kuficha uhalisia wako.
Imagine linakuja unazungumza linakupiga kofi la mdomo kwa kukushitukiza na linaambiwa " We Ivan jamani mbona hivyo" linaanza kulia kisa limeambiwa hivyo 😟
 
Huwezi kukurupuka kuchukua hatua kwa mtoto au familia isiyokuhusu!

Nilifanya hivyo sababu nawajua vyema na wananijua vyema kifupi nawamudu!!

Hata hivyo kabla ya kuchukua hatua nilishauliza mbona analialia sana? Wakajibu anadeka, nikawaambia wazi ngoja nimnyooshe kidogo apunguze ujinga!!

Alipokosea mtoto kujichanganya kwangu na kilio bila kujua plan iliyopo!!
Safi kabisaa
 
Siku moja niko na mzee wangu(a.k.a osama) tulienda kutembea kwa bamdogo, sasa vile vitoto vya bamdogo mideko mingi vikawa vinaturukia rukia, nikasema ngoja nione dingi atafanya nini maana anajikutaga serious [emoji23]
Kwan ata dakika tano zilipita sasa, kuna kitoto kikamrukia mgongoni et "bamkubwa nibebe", akakibeba hadi nje akachukua kiboko tulisikia tu mtu analia huko alipo rudi ndani akasema wachezeen hao mlio wazoea mmesikia eeh, kuanzia hapo fujo zikaisha.
 
Wewe umefata yako ya wenzako yaache kama ulivyoyakuta. Umeyaleta hapa ili iweje?

Kama makosa ni ya mama'ko ndio hajamfunda dada'ko vyema. Unamtutukanisha mzazi wako tu. Mlezi ni mama, ndio maana hata wewe hukullelewa vyema unakuja kuyaanika mambo ya kifamilia hadharani. "Like sister like brother".
Bi Faiza kama Faiza....nilikuwa natafuta mtu wa kutofautiana na wengi hatimaye nimempata...japo hii story ya Chizi Maarifa 98% ni ya kutunga ila hata kama Ina ukweli ndani yake sio mbaya Sana maana wengi tuko na fekero...shida itakuja pale ambapo ni ya kweli na dada mtu au shemeji yupo pia Jf...haitapendeza kwa kweli maana chizi kama chizi hata kama hakuwa na ubavu wakuwakemea watoto kwa yale waliyokuwa wanayafanya basi haya makasiriko yako aliyoyaleta hapa alitakiwa ayawakilishe kwa dada yake na hata shemeji ikiwezekana...ila bado naamini hii story ni ya kutunga 98% japo Kuna familia Zina malezi ya ajabu ajabu Sana kwa watoto wao.

Kuna dada mmoja ni single mother...mtoto wake wa kiume mgeni akija kwao Akiondoka lazima atamfuata mama yake na kumuuliza..."mama huyu mtu amekuja kufafuata nn kwetu". Sasa siku moja huyo single mother akaniadithia kuhusu hyo tabia ya mtoto wake. Mimi nilimchana tu kuwa asipoikemea hyo tabia mapema itafika muda huyo mtoto atakuwa asubiri tena mgeni aondoke ili aulize swali lake Bali atamuuliza kabisa mgeni kuwa umekuja kufuata Nini kwetu??

Basi huyo dada akawa mbishi kuwa haiwezi tokea kitu ka hcho...juzi Kati kanipigia ananiambia yale niliyomwambia yametokea...nikamjibu si nilikuambia..alichonijibu akasema sijui alipata wapi ujasiri wa kumchapa mtoto wake maana baada ya mgeni kuondoka alimchapa kisawasawa...nikamwambia hapo Sasa ndo umekuwa mama wala husijisikie vibaya kumchapa mtoto wako. Nikakata simu.
 
Kuna siku nilimtembelea shemeji yango hapa dar 2012 mtoto wao ana alikuwa na miaka 3 nDhani sikumbuki anapenda sana simu akachukua simu ya mama mkubwa wake Eheee kilichokotea nilipata cold feet wakatianaambiwa junia nirudishie simu akaitumbukiza kwenye beseni la maji.....
 
Nakumbuka mwaka flan hv enzi za JK kuna waziri wake mmoja alikuwa ndugu yetu akatualika kwake tukaenda. Kufika tu tukapokelewa na mtoto wake wa kiume nadhan alikuwa na miaka 5-6 hv, baada ya kutuona akaenda kuvaa jez ya taifa stars na kuanza kucheza mpira pale sitting room tulipokaa.

Sasa hizo fujo zake mpira mara umetupita kushoto mara utake kutupiga usoni tunakwepa yani ikawa vurugu vurugu Mama yake anajisemesha acha jamani yani ww ni mtundu sana acha badae mama yake akaenda nje mtoto akaendelea na mashuti ya mpira nusura mpira unipige usoni nikamuita akaja na mpira wake nikamfinya kifinyo kitakatifu mgongoni akajifanya anataka kupiga kelele kwa kilip nikamsindikizia na jicho kali akanyamaza na kutulia kwenye sofa kama sio yeye.

Mama yake alivyokuja anajifanya kumsemesha flan mbona huchezi tena mpira kakawa kanamuangalia tu hapo na mm nakakata jicho kali balaaaa.
 
Watoto wanajifunza- kama wazazi let train our kids vile tunataka wawe angali wakiwa wadogo as now sisi ndiyo role models wao na rafiki zao. Wakifikia uteenage- inaweza kuwa ngumu sana kuwin akili na mioyo yao kama wanavyokuwa hawajabalehe.

Let train our kids.
 
Watoto wako kwao, ukiona wanakufanyia fujo ondoka wewe, usepe zako. Kwanini uanze kuwafinya, kuwakazia macho sijui kuwachapa, wanakuhusu nini watoto wa wenzio?

Mtoto kuja kucheza au kufanya fujo kwako ni "friendly gesture" na kukukaribisha na kukufahamisha "instictively" kuwa "feel free in our territory". Elewa kuwa bado hawana upeo ulio nao wewe kwa umri wako na hiyo ya kimchezo mchezo ndio upeo wao ulipo, Hawana cha kuogopa au kuwa na hofu na wewe mpaka wahisi au wuwatie hofu.

Kumpiga mtoto, kumbadilishia hisia, kumkazia macho na au hata kutoonesha upendo kwake ni udhaifu kwa upande wako sio upande wa watoto na ufanyapo hivyo umeshajenga uadui na hyo mtoto maisha wa kutoweza kuwa karibu nawe tena, ni nani atataka kuwa karibu na adui ambae unamkaribisha kwako mcheze, mfurahi anakuumiza?

Hivi hamuelewi kuwa ni haki ya mtoto kucheza na ni kumjenga ki akili na kimawazo kumuachia ajisikie huru kwao? Boundaries na watoto haziwekwi kwa ukali au kukurupuka zinawekwa kwa kusemeshwa kirafiki na tone nzuri kama vile unaongea na mtu mzima mwenzio unaempenda. Mtoto atajifunza haraka na kukuelewa haraka na kuwa rafiki wako wa maisha ukifanya hivyo.

Ni mijitu mijinga inayokwenda nyumba za watu ikakuta watoto wanafanya utundu kwa kuwakaribisha, ki namna yaoa, ikaanza kuwashambilia. Si umite mwenyeji wako pembeni umueleze kuhusu wanawe na awaondoe hapo karibu yako kwaani hukuja kwa ajili ya kucheza na watoto, mwenyeji wako atakuelewa na atafahamu namna ya kuwazuia watoto.

Na walezi wanatakiwa waelewe kuwa ukimualika mtu, hujamualika kuja kucheza na wanao, kwa hiyo unawafahamisha kabisa watoto, kuwa kunakuja wageni na mkisha salimia mkae mbali na wageni, hususan wanaowazidi umri. Na wakija na watoto wenzenu, mtatumia, sehemu hii kuchezza nao, mtawaonesha kabisa sehemu watakayokuwa na wenzao.

Yote ni malezi tu.

Tuna safari ndefu sana ya kwenda Tanzania.
 
Bi Faiza kama Faiza....nilikuwa natafuta mtu wa kutofautiana na wengi hatimaye nimempata...japo hii story ya Chizi Maarifa 98% ni ya kutunga ila hata kama Ina ukweli ndani yake sio mbaya Sana maana wengi tuko na fekero...shida itakuja pale ambapo ni ya kweli na dada
Sijaona tatizo la mtoto ni lipi hapo na kauliza swali valid kabisa. Si unamjibu tu ulichokifata kwao? Tatizo lamtptp liko wapi hapo? na watoto wote duniani kuongea kwao ni kwa kuuliza na kuulizwa.

Tanzania tuna safari ndefu sana ya kwenda.
 
Sijaona tatizo la mtoto ni lipi hapo na kauliza swali valid kabisa. Si unamjibu tu ulichokifata kwao? Tatizo lamtptp liko wapi hapo? na watoto wote duniani kuongea kwao ni kwa kuuliza na kuulizwa.

Tanzania tuna safari ndefu sana ya kwenda.
Duuu haya bi Faiza...ila kwa kweli Mimi mtoto wa miaka minne aniulize nimeenda kufuata Nini kwao ....au mtoto wangu amuulize mgeni wangu amefuata nini kwao..???.duuu hapana aisee sitajisikia vzuri kabisa...yaani mtoto hata salamu hatoi...salamu ni swali kuwa umeenda fuata nini kwao??? Hii safari kweli itakuwa bado ni ndefu Sana kwangu...
 
Duuu haya bi Faiza...ila kwa kweli Mimi mtoto wa miaka minne aniulize nimeenda kufuata Nini kwao ....au mtoto wangu amuulize mgeni wangu amefuata nini kwao..???.duuu hapana aisee sitajisikia vzuri kabisa...yaani mtoto hata salamu hatoi...salamu ni swali kuwa umeenda fuata nini kwao??? Hii safari kweli itakuwa bado ni ndefu Sana kwangu...
Kwani anakosa lipi? Kwanini usimfahamishe mapema kuwa kuna mgeni anakuja kwa sababu hii na hii. Sio tu akija mgeni, mtoto unatakiwa uwe na mawasiliano nae, hata unapotoka nyumbani unatakiwa umuage unakwenda wapi na kufanya nini.

Ni ujinga tu kumhukumu mtoto mdogo bila kosa lolote. Mtoto akimuuliza mgeni wangu, kafata nini kwake, kuna kosa lipi hapo? Si amjibu tu kwa kilichomleta.

Wewe unafikiri pale ni kwako, na mtoto anafahamu pale ni kwao, vipi aje mtu na yeye asielewe yule mtu kafata nini? Kwani hana haki ya himaya yake? Kuwa na haki na himaya ni "natural instinct," sio ya kufundishwa.

Wewe mgeni akija kwenu huelewi kafata nini?
 
Home kwa mama.
mdogo wangu anao wa3 na ni singo maza.
Anaishi hapo home.
Sasa nikienda kumsalimu bi mkubwa ni kero tu,kwanza vinakuangalia kwa kukunyali na ni hivi vidogo kurwa na doto.
Mkubwa wao mtulivu nampenda sana.
Baba yao kasepa mama yao ndio hivyo tia maji tia maji.
Namsaidia mpk nimechoka hasaidiki.
Sasa siku niko pale naongea na bi mkubwa naona hivyo vinaletwa,vimeshikiwa fimbo vimeiba huko mtaani.
Yaani siku hiyo viliiona mbingu chafu.
Nilipiga mbele bibi yao kipigo kitakatifu.
Si tunahangaika kuwalea hapa libaba lenu limekimbia majukumu mnaleta wizi tena.
Mwisho pigisha magoti kwenye kokoto masaa kadhaa mpk bibi yao akaviombea poo.
Vikala mateke ya mwisho vikaondoka kulala.
Tokea hapo vikiskia mjomba kaja vitajifungia gheto kwao kimya amani imepatikana.
Ilikua kero tupu.
Mara vijilize,mara vigombane,mara sijui vinacomplaini nini.
Mama yao ananijua akijua nipo pale anakimbia hata wiki.
 
Back
Top Bottom