Masaki, Dar: Adam Malima atishiwa kwa Bunduki, Risasi zarindima kama Njugu

Masaki, Dar: Adam Malima atishiwa kwa Bunduki, Risasi zarindima kama Njugu

HESHIMA NA BUSARA MUHIMU SANA! HERI MBWA ANAYE ISHI KULIKO SIMBA ALIYE KUFA! Choose wisely my people!
 
Kumbe kapiga risasi ushabiki, kisa kaambiwa hana mamlaka... Dah, vijana wamekosa weledi wa kazi... Mtu kaweka mikono mfukoni kabisa wewe ka li 10Kg unajiona mwanaume....
Elimu
Elimu
Elimu
Weledi hupatikani kama elimu ulipatia kazi ni dogo na wagumu kujiendeleza kaka....
 
Kuna haja ya mafunzo ya hawa vijana kutazamwa upya. Yani Askari yeye ndio alikua anaprovoke na sio raia. Askari ndio kapanick anamsukuma mtu aliyeweka mikono kiunoni.

Nadhani alikua anataka jamaa ajibu mapigo kumsukuma au arushe ngumi.

Askari wa pili mbona amekuja kwa busara zaid ya huyo mwenzake.
 
Kukam
Hata kusoma hujui ndugu, Majembe alitaka kukamata gari alipoambiwa atoe kitambulisho akagoma
kukamata gari kwa kosa lipi? La kodi au wrong parking etc.
Halafu Hiyo risasi imepigwa kumtishia malima ili afanyeje ? Au ilikuwa ni kwa ajili ya kumuokoa aliyezaniwa ni jambazi? Au polisi alikuwa ana mpendelea mmojawapo
 
Shida yao inaanzaje sasa?
Wamepewa kiburi cha kipuuzi kwa kuwa mtamani u-IGP ana roho mbaya. Kwani mtu akifanya kosa barabarani ndio umtolee magobore? Anasema yeye ameapa. Pumbavu, hajaapa kuwa mtiifu kwa serikali yake? Ningekuwa mkubwa wake angekuwa hana kazi by muda huu. Hana hekima za kiuaskari kiasi cha kuaminiwa kupewa Silaha huyu. Full viroba
 
Kabisa wakiwa siriaz huyu kazi hana, kavunja pakubwa mno taratibu/sheria za matumizi na kubehave ukiwa na siraha ya moto mkononi,
Hajavunja sheria yoyote hapo kupiga risasi juu kwenye msongamano wa watu ambao walitaka kuvunja sheria.
 
Watanzania tumezoea kuongea kwa fashion ya upepo wa kisiasa.

Kwa mtazamo wa haraka haraka wananchi walipomzingira mtu walijua ni mwizi na wangeweza kumuua sasa polisi kupiga risasi juu ni kwa nia ya kutawanyisha watu ili kuepusha kifo cha jamaa.
Fashion zingine zinatuvua nguo ni vema tukaachana nazo.

Tazama heading ya hii habari, risasi zarindima! Katika maelezo risasi moja ndiyo imepigwa hewani sasa risasi zirizolindima ni ngapi na ziko wapi katika maelezo?

Mwanzoni mwa habari, mleta mada anasema kumekuwepo na majibizano ya risasi, mwishoni anasema risasi moja ndiyo imefyatuliwa hewani, sasa hayo majibizano ya risasi ni baina ya polisi na nani? ikiwa mmiliki wa gari hakua na silaha na wananchi hawakua na silaha!
umeona video zote mbili mkuu kabla ya kuchangia
 
Kwa maelezo haya, polisi hajafanya kosa kabisa kufyatua risasi hewani.

Kwa sababu, naona maelezo hapo yanasema wananchi walikuwa Karibu kujichukulia sheria mikononi.

Hivyo, polisi kuokoa maisha ya aliyedhaniwa ni jambazi ili asitolewe roho.

Au mi nimeelewa tofauti!?
Hujaelewa kabisa. Gari iliyopaki na dereva akiwa ndani
 
Wamepewa kiburi cha kipuuzi kwa kuwa mtamani u-IGP ana roho mbaya. Kwani mtu akifanya kosa barabarani ndio umtolee magobore? Anasema yeye ameapa. Pumbavu, hajaapa kuwa mtiifu kwa serikali yake? Ningekuwa mkubwa wake angekuwa hana kazi by muda huu. Hana hekima za kiuaskari kiasi cha kuaminiwa kupewa Silaha huyu. Full viroba
Ndiyo maana huweze kua mkubwa wake.
Utaishia kupiga kelele JF
 
Unajua ni watu wa namna gani wanatakiwa kupigiwa salute, mbuge bado hajafikia hatua ya kupigiwa salute
 
Kufyatua risasi hewani sio issue kwa huyo askari, issue ni hayo maneno na mikwara aliyokuwa anatoa sijui "sijui nimeapa, sijui nimevaa bendera anaonyesha mkanda huku anafyatua alafu mbaya zaidi anaetishwa ametulia tuli huku jamaa anamgusagusa na kufyatua risasi hewan", hapo asingekuwa Malima ingekuaje au kama angekuwa mtu mwingine ambae hafahamiki kwenye jamii wangefanya mchezo huo walioufanya wa kupiga hewani risasi huku unamtolea mkwara mtuhumiwa? Ila baadae wakajishitukia ikabidi wamwambie kwamba yupo chini ya ulinzi
 
Tuheshimu mamlaka na mamlaka ituheshimu.
Tusizoweshwe milio ya silaha tunaweza izoea.
Wrong Parking ni kosa linalozungumzika.
Majembe na Yono mambo mengine tumieni busara.
 
Mchana huu pamesikika milio ya risasi maeneo ya Masaki karibu na Double tree Hotel.

Yalikuwa ni majibizano kati ya Majembe Auction Mart waliokuwa wameambatana na Polisi walipojaribu kukamata gari lilokuwa limeegeshwa pembeni ya barabara hali ya kuwa Dereva yupo ndani.

Inasemekana gari lilikuwa la Mwanae Kigoma Malima aliyeenda IOM kufatilia ishu zake.

Mtu wa Majembe akavamia gari hilo na alipodaiwa kuonyesha vitambulisho aligoma kutoa ndio wananchi walipolizingira gari wakitaka kumpiga wakijua ni jambazi.

Polisi aliingilia kati na katika majibizano akafyatua risasi juu kumtishia ndugu Malima aliyekuwa hana hata silaha wala hakukuwa na mwananchi aliyekuwa na silaha.

Tunakoelekea siyo kuzuri hata kidogo!. Muda siyo mrefu kwa staili hii hali ya hewa inaweza kuchafuka!
Kulikuwa na sababu zipi za risasi kupigwa?Iko siku atauliwa mtu mbele ya kamnasi kiasi hiki kwa ulevi tu wa kuwa na silaha !
 
Ndiyo athari za vyeti feki. Halafu Adam na yeye mijegeje si anayo angewachejia na yeye
 
Back
Top Bottom