Pre GE2025 Masheikh 12, waliokaa gerezani miaka 10, kwa tuhuma za Ugaidi waachiwa huru

Pre GE2025 Masheikh 12, waliokaa gerezani miaka 10, kwa tuhuma za Ugaidi waachiwa huru

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kuna huyu bwana siku akiitisha habari na wahandishi wa habari mwijaku hana subiri kusifia sasa
IMG_0749.jpeg
 
Nani kakuambia hawana hatia?? Mpaka uje uthibitishe kuwa hawana hatia, utakuta makanisa yameschomwa, mapadri wameuliwa na ushenzi kibao.

Namna ta kudeal na religious fundamentalists ni hivyo tu. Hata USA pale Guantanamo ndivyo walivyowasomba.

Dini ni kama bangi ukiipokea ndivyo sivyo. Hawa wameshikishwa adabu. HAWATOFURUKUTA tena
Naunga hoja
 
Shura ya Maimamu Tanzania

KUTOKA MAHAKAMA KUU LEO TAREHE 4/3/2025

MASHEIKH 12, WATOKA GEREZANI. WATANO NI FAMILIA MOJA YA ULATULE.

MASHEIKH 12, walio kaa gerezani miaka 10, (2015-2025), kwa tuhuma za Ugaidi wameachiwa huru leo. Uamuzi huo umetolewa na Jaji wa Mahakama Kuu Mheshimiwa Kirekiano.

Kabla ya hukumu hiyo Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP, aliambia Mahakama upande wa Jamhuri hauna haja ya kuendelea tena na shauri hilo.

Akitoa uamuzi huo mheshimiwa jaji amesema amekubali ombi hilo la Mwendesha Mashtaka wa serikali.

Kwa muda mrefu Shura ya Maimamu Tanzania imekua ikimuomba Mkurugenzi wa Mashtaka DPP kulifuta shauri hilo kwa sababu za upande wa Jamhuri kushindwa kuthibitisha tuhuma dhidi ya Masheikh hao.

Walioachiwa huru ni:

1. Ali Mohammed Ulatule (70).
2. Khamisi Mohammed Ulatule (61).
3. Nassoro Suleiman Ulatule (41),
4. Rajab Ali Mohammed Ulatule (34).
5. Na Ramadhani Khamisi Mohammed Ulatule (29).

Wengine ni:

6. Saidi Abdallah Chambeta.
7. Fadhili Shaabani Lukwembe.
8. Mnemo Qassim Mwatumbo.
9. Abdallah Bushiri kalukula.
10. Khamisi Ally Masamba.
11. Omari Abdallah Makota.
12. Na Mohammed Hassan Ungando.

Katika kundi la Masheikh walioachiwa leo, 5, ni wa familia moja ya Ulatule. Wao walikamatwa familia moja watu 16, na baada ya masiku kadhaa (ya kutofahamika walipo), hatimaye 7, walikutwa katika gereza la Segerea jijini Dar es Salaam baada ya kufikishwa Mahakamani na kusomewa shtaka la ugaidi.

Aidha wenzao 9, hawajulikani walipo mpaka leo. Kati ya 7, waliokua gerezani 2, Sheikh Suleima Mohammed Ulatule (99), na Sheikh Saidi Mohammed Ulatule (79), wamefariki dunia wakiwa gerezani.

Kufuatia kuachiwa kwa masheikh hao 12, idadi ya mahabusu wenzao waliobaki katika gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam ni 39.

Shura ya Maimamu Tanzania inawashukuru wale wote wanaoshiriki ipasavyo harakati za kutetea haki za binadamu.

Okay,hiv huwezi kuishitaki jamhuri kwa kukusababishia usumbufu.maana ikibaki kama hivyo DPP anaweza kuitumia vibaya ofisi yake.ni sawa na juzi Dr.Slaa ameachiwa kwa mtindo huo huo.kwambA DPP anaweza tu kuacha kuendelea na kesi just that simple.
 
Uzuri kila anayetoka anaanza maisha upya. Toka wale wa UAMSHO akina Farouk na Mselem, hakuna tena anayeendekeza UJINGA.

Kweli gereza ni chuo cha mafunzo au ulaya wanaita correctional centre.

Hongera Kikwette kwa kuwadhubiti hawa "Siasa Kali wa Kiislamu. La sivyo nchi yetu ingekuwa kichaka cha Alshabab
Dunia Haina HurumA.
Kuna Sehemu Umekaa Unajiaminisha Ujinga Huku Ukijiona Mjanja Na Chuki Zako Uchwara.
Jera Ni Haina Mwenyewe Hata Uwe Rais Wa Nchi Tegemea Linaweza Likukute Jambo Iwe Kwa Kutenda Au Kwa Kusingiziwa.Chunga Ulimi Wako Dogo.
 
Hii nchi in sheria za hovyo sana. Yaani unawashikilia watu kwa miaka 10 halafu from nowhrre unawaaambia huna nia ya kuendelea kuwashikilia. Kwa hiyo wapo huru. Na bado ukiamua unaweza kuwakamata tena! Na hapo hakuna cha fidia wala nini!!

DPP!! Bila shaka hiki ni kichaka cha uonevu na kinachotakiwa kufanyiwa marekebisho haraka iwezekanavyo.
 
Nani kakuambia hawana hatia?? Mpaka uje uthibitishe kuwa hawana hatia, utakuta makanisa yameschomwa, mapadri wameuliwa na ushenzi kibao.

Namna ta kudeal na religious fundamentalists ni hivyo tu. Hata USA pale Guantanamo ndivyo walivyowasomba.

Dini ni kama bangi ukiipokea ndivyo sivyo. Hawa wameshikishwa adabu. HAWATOFURUKUTA tena
Hii Inaweza Kuwa Ndo Chanzo Cha Chuki Dhidi Ya Kile Ulichokitaja.
Hawa Wanahitaji Kitu Kidogo Tu Kuwafanya Magaidi.

Dhulma Ndo Chanzo Cha Kisasi Ila Ukiwa Na Akili Za Kikanisa Kanisa Huwezi Kuelewa.
Wametumikia Miaka Kumi Bila Sababu Za Msingi Alafu Kuna mtu Anashangilia Binadam Mwenzie Kuonewa Kisa Ni Mwislam Kaonewa Ila Tambua Mambo Hubadilika.
 
Uzuri kila anayetoka anaanza maisha upya. Toka wale wa UAMSHO akina Farouk na Mselem, hakuna tena anayeendekeza UJINGA.

Kweli gereza ni chuo cha mafunzo au ulaya wanaita correctional centre.

Hongera Kikwette kwa kuwadhubiti hawa "Siasa Kali wa Kiislamu. La sivyo nchi yetu ingekuwa kichaka cha Alshabab
Hao muamsho issue yao ilikuwa kisiasa zaidi na wala sio udini.
Kuna watu wale walisombwa tu hawajui a wala ba. Na wengi walikuwa wapemba na ni Wafuasi wa CUF kwa kipindi kile kabla CUF kusambaratika na wengi kujiunga na ACT
 
Back
Top Bottom