Masheikh wa Uamsho wafutiwa kesi, warejea uraiani
[emoji117]Unakaa jela zaidi ya miaka 9, unateseka weee familia inakosa huduma yako kwa muda wote huo

[emoji117]Baada ya miaka mingi kupita DPP Anafuta kesi yako na kukuruhusu uende nyumbani

[emoji117]Unaenda nyumbani ukiwa umeathirika kisaikolojia, biashara zako/kazi zinakuwa zimekufa na muda mwingine huna pesa kabisa hivi unaishije?

[emoji117]Huwa kuna kesi hazina dhamana mtu anakaa jela wee halafu baadae anashinda kesi au DPP anafuta hiyo kesi huyu nae anaambiwa aende nyumbani tu huko anaenda kuishije?

[emoji117]Wataalamu hebu mnisaidie huwa wanapewa pesa kufidia muda walio kaa gerezani?au wanaachwa tu? Kama wana waachwa tu hili liangaliwe wawe wanapewa fidia

[emoji117]Mtu anakaa gerezani miaka sita mfano kesi ikiwa anaendelea mwaka wa saba anapewa hukumu ya kufungwa miaka 15 jela (mfano).. Je, kuna fidia ya ile miaka sita aliyo kaa kabla ya hukumu?

~Karibuni
Hoja za msingi sana.

Tujadili.
 
..Mama Samia asipojihusisha na UKATILI ataacha legacy kubwa kuliko Magufuli. Watz ni watu rahisi sana kuwaridhisha.
Hakika mkuu.

Tunamuombea kwa Mungu awe msikivu na mnyenyekevu hivi hivi. Asijikweze na kujiona Mungu mtu. Ajue ataulizwa na dunia ni mapato tu.

Leo usiku ntaamka niswali swala maalum ya kumuombea yeye tu.
 
Hakika mkuu.

Tunamuombea kwa Mungu awe msikivu na mnyenyekevu hivi hivi. Asijikweze na kujiona Mungu mtu. Ajue ataulizwa na dunia ni mapato tu.

Leo usiku ntaamka niswali swala maalum ya kumuombea yeye tu.


..umfanyie DUA mikono yake isichafuke kwa damu za Watz wasio na hatia, pamoja na kashfa za ufisadi na rushwa.
 
Utaratibu wa fidia ukiwepo tena kwa kuwakata mafao yao watumishi wote wanaoweka watu ndani kabla ya ushahidi kukamilika itasaidia kupunguza utitiri watu kukaa mahabusu na kuokoa kodi zetu.

Kwa sababu hakuna utaratibu huo easy tu mtu kukaa ndani hata miaka zaidi ya hio. Hao ni mashehe tu je kuna wangapi Wana miaka zaidi ya hio ndani?

Ulimwengu wa Sasa hivi ni ngumu Sana huwezi jificha popote pasipojulikana kama upo nje kwa Dhamana. Ipo haja kama ushahidi haujakamilika mtu asikamatwe kama walivyo wenzetu.
Haswaaa.

Mtu akituhumiwa basi wachukue pasi ya kusafiria, na vitu vyake muhimu vizuiwe ila uhuru wake aachiwe.

Haya ni maoni yangu tu, upelelezi haujakamilika ni sababu ya kipuuzi na kiuonevu juu ya watuhumiwa
 
Hili ni jambo la faraja sana hasa ukichukulia hawa watu hawajahukumiwa kutokuwa na makosa bali kesi imefutwa. Kilio cha wengi kwa muda wote huu kilikuwa kwenye options 3, kwamba ushahidi uaptikane na wafungwe jela, kama ushahidi ulikuwa haupo basi wangepewa dhamana ili ukikamilika ndio waitwe Mahakamani au basi waachiwe huru kama ilivyotokea ....hii imesubiri miaka 9 (ajabu),
Huenda wapo wengine wengi kama hawa na wanapitia mateso haya haya.

Kuwekana sana, hili si tatizo la mwendazake maana naye aliwakuta ndani tayari na akawaacha. Sijui tunaweza kusema ni tatizo la ccm au vyovyote lakini lililo kubwa ni kupata aina ya KATIBA itakayotulazimisha kutendeana haki na hata tusipoitenda haki basi tuone haya.
Tujifunze sasa badala ya kutegemea huruma au 'ukatili' wa mtu binafsi eti sababu ya cheo chake basi tuitegemee Katiba walau kwa 60%
Very well said kiongozi.

Kama lilivyosikilizwa hili na serikali yetu sikivu ikiongozwa na Mama yetu Mheshimiwa rais Mama Samia Suluhu Hassan, ndivyo tunavyoamini kwamba hata la katiba mama amelisikia na analifanyia kazi.

Ndio maana tunasisitiza kwamba Mama aachwe afanye kazi na neema zitapatikana kwa kila mmoja wetu
 
Maskini machozi ya yule padre aliyemwagiwa tindikali, yule shehe mwenye asili ya tanga aliyemwagiwa tindikali, yule polisi aliyechinjwa hapo mwanakwwrekwe, wataliinwaliokuwa wanamwagiwa tindikali, makanisa yaliyokuwa yanachomwa , bar, pamoja na mabucha ya kitimoto[emoji2297][emoji2297]
Wana roho mbaya sana hao, wabadilike sasa!!
 
Maskini machozi ya yule padre aliyemwagiwa tindikali, yule shehe mwenye asili ya tanga aliyemwagiwa tindikali, yule polisi aliyechinjwa hapo mwanakwwrekwe, wataliinwaliokuwa wanamwagiwa tindikali, makanisa yaliyokuwa yanachomwa , bar, pamoja na mabucha ya kitimoto🙆‍♂️🙆‍♂️
aka kamama katakuja kutupeleka pabaya watu walikuwa na mashtaka ya wazi kabisa hata rohoni mwake huyu rais uchwara anajua walitenda
 
aka kamama katakuja kutupeleka pabaya watu walikuwa na mashtaka ya wazi kabisa hata rohoni mwake huyu rais uchwara anajua walitenda
Raisi Samia Suluhu anafuata Sheria, ninyi mlozowea vya kunyonga vya kuchinja hamviwezi, ni zamu yenu sasa mutafute Nchi inayotawaliwa na Dikteta muhamie na Magodoro yenu.
 
Back
Top Bottom