Pre GE2025 Mashekhe wafanya ibada na kuomba majini yasaidie Rais Samia kushinda kwenye uchaguzi ujao

Pre GE2025 Mashekhe wafanya ibada na kuomba majini yasaidie Rais Samia kushinda kwenye uchaguzi ujao

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hao ni watu waliofahamu vibaya maana ya istikhara!
Istikhara aliyofundisha mtume صلى الله عليه وآله وسلم Haina muda maalumu.
Unaweza kuifanya asubuhi , mchana, jioni au usiku .!
Muda wowote, huyo anayesema wakati wa kulala saa nyingine ni katika hao wanaotegemea kuoteshwa! Hadithi ya istikhara nitaileta hapa muda si mrefu na kutoa maelezo yake inshaa Allaah.
Si kwamba wamesema istikhara hufanywa usiku bali baadhi ya hao waja wema huifanya kabla ya kulala. Hata hivyo lengo langu si kuijadili sana istikhara bali kuonyesha tu kwamba yapo mambo mengi tu ambayo tunaweza kuyafanya pasina kutumia njia za shirki na uchawi na ukapata matokeo yale yale.

Kwahiyo hata kwenye kuwasiliana na jini si lazima zitumike njia za kichawi.
 
kwa hiyo majini kwako wewe ni masafi, matakatifu, ndio maana mnaswali nayo. ajabu sana. sasa mbona tukitamka JIna la Yesu yanakimbia hadi yanajisaidia?
Kama ilivyo utakatifu na uovu ni matokeo ya matendo ya binaadamu basi majini ni hivyo hivyo, kwahiyo kama ukifanya maombi mchawi akakimbia ndio utasema binaadamu wote wachawi?

Unachotakiwa kuelewa ni kwamba majini ni viumbe ambao ni tofauti na binaadamu na malaika hivyo majini si kundi la malaika (waliyoasi)

Kwahiyo issue sio majini kuwa wazuri au wabaya, jiulize kipi kilichofanya hao malaika (waliyoasi) kuitwa majini na je hawa majini huendana sifa zao na malaika (waliyoasi)?
 
Sisi binadamu tunamapungufu mengi sana, na huwenda hizi dini zetu kunaupande ni kama huwa tunadanganyana saana

Hawa hawa Mashekhe kipindi Rais Samia anaingia madarakani, walitusomea aya kuwa, Mwanamke kuwa kiongozi mwenye maamzi, yaani Mtawala, Kitabu na Dini ya Mnyaazi Mungu haikubali

Embu ona tena leo walivyomugeuka Huyu Mnyaazi Mungu na Kitabu chake!

Kuna mahali hata Mungu akitutazama anacheeeka na kutudharau sana kwa sababu huwa hatuna tujuacho kumhusu
Khaa! Umenivunja mbavu mkuu
 
Hili haliwezi kufanya waislamu wakamuwajibisha huyp sheikh jongo?? Angeweza kumpigia kampeni Samia bila kuhusisha majini na uislamu

Nategemea waislamu mtaandamana kwa hili la huyu sheikh kudhalilisha dini
Kivipi wakati dini ya myaaazimungu na majini ni Pete na kidole
 
Nilijua verified people are clever, but here you are the dumbest. What is 10 commandments? Aren’t they, the laws governing how you should live?

Okay, for the sake of your fellow dumb people,
In islam “worship/ibada ” is simply means obedience or devotion to God. It includes everything you do, say etc they should fall under the rule of Tawheed.
Unaijua tofauti ya kuagiza na kuabudu?. Na inaonekana haujanielewa nilichokizungumzia kabisa hapo.

Siku nyingine jitahidi uwe unaelewa kwanza kitu kabla ya kukizungumza au kukijibia, sawa Mkuu.
 
Si kwamba wamesema istikhara hufanywa usiku bali baadhi ya hao waja wema huifanya kabla ya kulala. Hata hivyo lengo langu si kuijadili sana istikhara bali kuonyesha tu kwamba yapo mambo mengi tu ambayo tunaweza kuyafanya pasina kutumia njia za shirki na uchawi na ukapata matokeo yale yale.

Kwahiyo hata kwenye kuwasiliana na jini si lazima zitumike njia za kichawi.
SWALI LA KWANZA kwako, ni kwanini baadhi ya hao waja wema wafanye istikhara kabla ya kulala na si wakati mwingine?!
SWALI LA PILI, ni njia gani ambazo unaweza kutumia kuwasiliana na majini bila kutumia njia zilizotajwa katika vitabu vya uchawi?!
SWALI LA TATU. Tukiachana na manabii nitajie mtu mwema mmoja tu ambaye alikuwa akiwasiliana na majini na alikuwa anataka nini kwa hao majini ambacho hawezi kukipata kwa wanaadamu wenzake?!
SWALI LA NNE. Majini hatuna uwezo wa kuwaona kwa macho japo wao wanatuona kama Quran ilivyoeleza kwenye suuratul Aaraafu Aya ya 27:
{ إِنَّهُۥ يَرَىٰكُمۡ هُوَ وَقَبِيلُهُۥ مِنۡ حَيۡثُ لَا تَرَوۡنَهُمۡۗ إِنَّا جَعَلۡنَا ٱلشَّيَٰطِينَ أَوۡلِيَآءَ لِلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ }
Hakika yeye (shetani )na kabila yake wanakuoneni, na nyinyi hamuwaoni. Hakika Sisi tumewafanya Mashetani kuwa ni marafiki wa wasio amini."

Na suuratul jinni imebainisha kuwa Kuna majini wema kwa waovu , waislamu na makafiri.
Na waislamu tunakatazwa kutafuta ushauri na msaada kwa watu waovu hata kama ni binadamu wenzetu wachilia mbali kutafuta ushauri kwa jini muovu.!
Sasa SWALI NI KWAMBA , IKIWA JINI MPAGANI AU MKRISTO AU MYAHUDI AKIKUDANGANYA KUWA YEYE NI MUISLAMU NA ANASWALI SWALA TANO NA ANAENDA HIJA KILA MWAKA.
Ni njia gani utatumia kujua kuwa huyu jini ni MUONGO?!
Kumbuka ikiwa kuna binadamu waongo majini waongo pia wapo kutokana na yanayopatikana katika baadhi ya Aya katika suuratul Jinni hasa Aya ya 11 na 14.
Na MWISHO ni jinsi gani utajua kuwa ushauri au maelekezo uliyopewa na jini ni sahihi wakati hujui jini huyo kama ni mwema au muovu?! Au unadhani jini muovu anaweza yeye mwenye kujitaja kuwa ni muovu.
Je unakumbuka maneno ambayo ibilisi aliyatumia kuwapoteza wazazi wetu Adamu na Hawaa hadi kufukuzwa peponi yalikuwa mazuri hadi Ibilisi aliapa kwamba anawapa nasaha na ushauri mzuri ?!
Allaah kalitaja tukio hili ndani ya suuratul Aaraafu Aya ya 21 hadi 22 kwa kusema:
{ وَقَاسَمَهُمَآ إِنِّي لَكُمَا لَمِنَ ٱلنَّٰصِحِينَ }
NAYE (Ibilisi )AKAWAAPIA (Adamu na Hawaa akawaambia ) KWA YAKINI MIMI NI MIONGONI MWA WANAOKUNASIHINI . (wanaokupeni nasaha na ushauri mzuri)
{ فَدَلَّىٰهُمَا بِغُرُورٖۚ فَلَمَّا ذَاقَا ٱلشَّجَرَةَ بَدَتۡ لَهُمَا سَوۡءَٰتُهُمَا وَطَفِقَا يَخۡصِفَانِ عَلَيۡهِمَا مِن وَرَقِ ٱلۡجَنَّةِۖ وَنَادَىٰهُمَا رَبُّهُمَآ أَلَمۡ أَنۡهَكُمَا عَن تِلۡكُمَا ٱلشَّجَرَةِ وَأَقُل لَّكُمَآ إِنَّ ٱلشَّيۡطَٰنَ لَكُمَا عَدُوّٞ مُّبِينٞ }
Basi akawateka (Adamu na Hawaa) kwa KHADAA. Walipo uonja ule mti, tupu zao zilifichuka na wakaingia kujibandika majani ya Bustanini. Mola wao Mlezi akawaita: Je, sikukukatazeni mti huo, na kukwambieni ya kwamba Shet'ani ni adui yenu wa dhaahiri?"

HUYO NDIYE SHETANI .
Anapotaka kukupoteza atakwambia yeye ni mwema na anakupendanna anataka upate kheri na mafanikio duniani na akhera kumbe ndiyo anakipoteza kidogo kidogo!.
 
SWALI LA KWANZA kwako, ni kwanini baadhi ya hao waja wema wafanye istikhara kabla ya kulala na si wakati mwingine?!
SWALI LA PILI, ni njia gani ambazo unaweza kutumia kuwasiliana na majini bila kutumia njia zilizotajwa katika vitabu vya uchawi?!
SWALI LA TATU. Tukiachana na manabii nitajie mtu mwema mmoja tu ambaye alikuwa akiwasiliana na majini na alikuwa anataka nini kwa hao majini ambacho hawezi kukipata kwa wanaadamu wenzake?!
SWALI LA NNE. Majini hatuna uwezo wa kuwaona kwa macho japo wao wanatuona kama Quran ilivyoeleza kwenye suuratul Aaraafu Aya ya 27:
{ إِنَّهُۥ يَرَىٰكُمۡ هُوَ وَقَبِيلُهُۥ مِنۡ حَيۡثُ لَا تَرَوۡنَهُمۡۗ إِنَّا جَعَلۡنَا ٱلشَّيَٰطِينَ أَوۡلِيَآءَ لِلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ }
Hakika yeye (shetani )na kabila yake wanakuoneni, na nyinyi hamuwaoni. Hakika Sisi tumewafanya Mashetani kuwa ni marafiki wa wasio amini."

Na suuratul jinni imebainisha kuwa Kuna majini wema kwa waovu , waislamu na makafiri.
Na waislamu tunakatazwa kutafuta ushauri na msaada kwa watu waovu hata kama ni binadamu wenzetu wachilia mbali kutafuta ushauri kwa jini muovu.!
Sasa SWALI NI KWAMBA , IKIWA JINI MPAGANI AU MKRISTO AU MYAHUDI AKIKUDANGANYA KUWA YEYE NI MUISLAMU NA ANASWALI SWALA TANO NA ANAENDA HIJA KILA MWAKA.
Ni njia gani utatumia kujua kuwa huyu jini ni MUONGO?!
Kumbuka ikiwa kuna binadamu waongo majini waongo pia wapo kutokana na yanayopatikana katika baadhi ya Aya katika suuratul Jinni hasa Aya ya 11 na 14.
Na MWISHO ni jinsi gani utajua kuwa ushauri au maelekezo uliyopewa na jini ni sahihi wakati hujui jini huyo kama ni mwema au muovu?! Au unadhani jini muovu anaweza yeye mwenye kujitaja kuwa ni muovu.
Je unakumbuka maneno ambayo ibilisi aliyatumia kuwapoteza wazazi wetu Adamu na Hawaa hadi kufukuzwa peponi yalikuwa mazuri hadi Ibilisi aliapa kwamba anawapa nasaha na ushauri mzuri ?!
Allaah kalitaja tukio hili ndani ya suuratul Aaraafu Aya ya 21 hadi 22 kwa kusema:
{ وَقَاسَمَهُمَآ إِنِّي لَكُمَا لَمِنَ ٱلنَّٰصِحِينَ }
NAYE (Ibilisi )AKAWAAPIA (Adamu na Hawaa akawaambia ) KWA YAKINI MIMI NI MIONGONI MWA WANAOKUNASIHINI . (wanaokupeni nasaha na ushauri mzuri)
{ فَدَلَّىٰهُمَا بِغُرُورٖۚ فَلَمَّا ذَاقَا ٱلشَّجَرَةَ بَدَتۡ لَهُمَا سَوۡءَٰتُهُمَا وَطَفِقَا يَخۡصِفَانِ عَلَيۡهِمَا مِن وَرَقِ ٱلۡجَنَّةِۖ وَنَادَىٰهُمَا رَبُّهُمَآ أَلَمۡ أَنۡهَكُمَا عَن تِلۡكُمَا ٱلشَّجَرَةِ وَأَقُل لَّكُمَآ إِنَّ ٱلشَّيۡطَٰنَ لَكُمَا عَدُوّٞ مُّبِينٞ }
Basi akawateka (Adamu na Hawaa) kwa KHADAA. Walipo uonja ule mti, tupu zao zilifichuka na wakaingia kujibandika majani ya Bustanini. Mola wao Mlezi akawaita: Je, sikukukatazeni mti huo, na kukwambieni ya kwamba Shet'ani ni adui yenu wa dhaahiri?"

HUYO NDIYE SHETANI .
Anapotaka kukupoteza atakwambia yeye ni mwema na anakupendanna anataka upate kheri na mafanikio duniani na akhera kumbe ndiyo anakipoteza kidogo kidogo!.
Nitajibu swali la pili na la tatu kwa pamoja. Naposema kuwasiliana na jini si kwamba ni lazima kuwasiliana huko kuwe kwa kumuona yeye mwenyewe au kumsikia sauti yake, ndio sawa na ule mfano niliyotoa wa kwamba hata sisi binaadamu tunaweza kuwasiliana na mtu ambaye yupo nchi nyengine huko ila ukaweza kuwasiliana nae pasina kumuona wala kumjua, hiyo ni teknolojia.

Kwahiyo baadhi ya njia ambazo unaweza kuwasiliana ni kupitia ndoto au meditation, wala haihitajiki ufanye aina fulani uchawi ili kuweza kuwasiliana.
 
Kwahiyo tutaongozwa na majini? Daa Mungu anadhihakiwa balaa majini ndiyo yatawale watu ! Mungu aamue kati ya binadamu na majini
 
Kwahiyo tutaongozwa na majini? Daa Mungu anadhihakiwa balaa majini ndiyo yatawale watu ! Mungu aamue kati ya binadamu na majini
Wewe umepata wapi hizo habari za majini kutuongoza? Wametajwa malaika na majini kwamba waombe kwa Mungu.
 
Wewe umepata wapi hizo habari za majini kutuongoza? Wametajwa malaika na majini kwamba waombe kwa Mungu.
Sasa wewe ulishaona majini yakaombwa halafu MUNGU akae hapo? Kama hatakaa shetani! Hakuna tofauti na mabaari-peor
 
Ndio maana huwa hakuna njia ya kumtenganisha shehe.......na shehena...........ukiondoa kuwa kigezo cha kuwa shehe sio shule bali majini basi shehena hana namna ya kulikataaa shehena popote atakapo hitwa
 
Hawa wangejua kuwa wanaitukanisha dini kwa vitendo hivi, wangeacha kumix dini na siasa. Siku hizi ndio imekuwa too much kwa Bakwata ya Sheikh Zuberi kuwa ni ya siasa tuuu. Aibu zao. Nchi si ya kidini hii. Matamko kama haya yakemewe. Mambo haya yanakuwa yanaamsha hisia na chuki za kidini, na haimsaidii Samia zaidi ya kumuharibia.
 
Mimi ni muislamu.
Uislamu unatutaka tunapozungumza tuwe waadilifu.
Katika uadilifu ni kwamba mtu akisema ukweli hata kama ni adui yako mwambie kwahilo umesema kweli!
Na mtu akisema uongo hata kama ni rafiki yako mwambie kwahilo rafiki yangu umesema uongo.
Mimi kwa sasanina umri wa miaka 48.
Tangu nikiwa mtoto wa miaka 12 nilikuwa nikisikia tuhuma kutoka kwa wakristo wakisema sisi waislamu tunafuga majini na uislamu ni dini ya majini nikawa napinga kwa nguvu zote.
Baada ya kukua , kusoma na kutembea na kukutana na makundi mbalimbali ya waislamu wenye Imani, itikadi na misimamo tafauti nikagundua kwamba ni kweli kuna baadhi ya waislamu wanashirikiana na majini waovu ( mashetani ) katika kazi zao za uganga, uchawi na ushirikina na hao ndio wamechafua jina la uislamu na waislamu kuonekana katika macho ya jamii ya wakristo kuwa uislamu ni dini ya majini.
Kinachotakiwa sio kukataa jambo hili , bali ni kufafanua kuwa hao waislamu wenzetu wanaoshirikiana na mashetani wanakosea na dini yetu kupitia Quran na hadithi za mtume صلى الله عليه وآله وسلم inakataza mambo ya ushirikina wa aina zote ila Hawa wenzetu ambao wengine ni maimamu katika baadhi ya misikiti wamekengeuka na kumfuata shetani na kuyapa mgongo mafundisho ya uislamu yanayopiga vita aina zote za matendo ya ushirikina.
Mfano wa waislamu wanaoendekeza mambo hayo ni Dr sule anayefikia hatua ya kumsingizia mtume Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم kwa kutangaza kwamba HATA MTUME MUHAMMAD صلى الله عليه وآله وسلم ALIFUGA MAJINI.
Mfano mwingine wa waislamu wanaofanya vitendo vya kishirikina hadharani ni huyu anayejiita Maallim kingu anayetangaza kusoma Albadiri na kuchinja mbuzi ili mama Samia apate mitano tena.
Huu ni ushirikina wa wazi unaofanywa na baadhi ya wanaojiita waislamu na huko sirini husema na kufanya mabaya zaidi ya hayo.
Kwanza ww sio Muislam wewe ni ktk Wale wale wanaodanganya Watu na Kufanya Propaganda kuusu Majini yapo Na Waislam manake Bado ata Majibu yako Yamedhihilisha ilo ilo ndio mana Wenzako Wenye Akili Wamekwepa Kunijibu kwakua Wamekosa Majibu

kuusu Hoja Yangu!! Kusema ww pia Muislam !!! kusema umegundua ni kweli wapo Waislam Wenye Majini apo nilitumia Neno Debe Tupu

Mana Wewe nawenzio kama ww na Wachungaji Ndio mnadanganya Watu uku mkifanya iyo Propaganda ya Kidini Sijuu ndio kumsaidia YESU awe mkuuu kwa kuisingizia Iman Pinzani Uwongo !!!! iyo Dhana kuusu Waislam na Majini,,,,

mm Nilitaka Tutoke kwa Maneno Tupu au Nilisikia Au Wewe Umeona Au Umesimuliwa na Babu yako kuwa Waislam Wanapenda Majini

SASA TUJE KWENYE UKWELI HOJA yangu inaseme kama ni kweli Waislam Ndio wanapenda au Wanafuga Majini kama mnavyotuambia mbona Matendo ya Kishilikina Zao la Majini atuyaoni Pwani ya Waislam

Badala yake Matendo ya kishilikina na majini Uchawi yapo Zaid kwenye Mikoa yenye Wakristo Wengi mfano Nikatoa sio Maneno matupu Debe Tupu kuwa mbona iyo Mikoa ya Wakristo ndio inaongoza kwa METENDO YA KISHILIKINA
Mfano

Sumbawanga Shinyanga Mbeya Mwanza ( 1 ) uko ndiko Vibibi vizee wenye macho mekundu Wanauwawa sababu kuu Ushilikina unaambiwa ETI kauwa mjukuu wake!!!!

( 2)
Watu Wanachunwa ngozi ili ikatumike kwenye Ushilikina (3)
Wanaume wanakatwa Mapumbu yao Yakatumike kwenye Ushilikina (4)
albino ndiko Wanauwawa ndiko Wanakatwa Viungo vyao ETI vikatumike kwenye ushilikina majin Uchawi matukio ayo 4 nimekupa

sio Debe tupu sio maneno Matupu ohh nimesikia kwa mjomba Hooo mchungaji katwambia aya nimekwambia sikusikia kwa shekh wala kwa Babu wala kuambiwa na mtu ila ayo matukio yametokea MEDIA imetuambia na Dunia inajua,,,,

mm nimeomba tukio la kishilikina kutoka kwa Waislam wa pwani mana aya maneno na Propaganda zenu mala nyinyi mnafanyia apa Dar es salaam au pwani yote!!!!i

Kazi kwenu leteni majibu wasomaji Walidhike lkn ulivojibu bado ukujibu kwa Hoja na Ushaidi umeishia tu kufanya yaleyale ya Propaganda hoo namm pia Muislam ni kweli yapo!!! tunawaomba matukio ili tuuunganishe na izi Propaganda zenu karibuni kujibu Wakristo???.???
 
Mashekhe waliokutana chini ya Shekhe Mkuu Mufti Abbakari, kwenye msikiti wa kwa Mtoro, jijini Dar es Salaam wamefanya ibada maalum ya kumwombea Rais Samia ashinde kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Shekhe mkuu akiwa kwenye ibada hiyo ameagiza kuwa mashekhe wa mikoa yote, wilaya hadi kwenye kata, wafanye ibada ya kumwombea Samia ashinde kwenye uchaguzi ujao.

Shekhe mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam amesema kuwa anayaagiza majini yote yahakikishe Rais Samia anashinda kwenye uchaguzi wa urais mwaka huu.

SWALI:
Tukiyaamini maneno ya mashekhe hawa, ina maana uchaguzi wa safari hii utakuwa ni ushindani kati ya wanadamu na majini? Kama majini yakishinda, huyu Rais atakuwa wa wanadamu wa Tanzania au atakuwa Rais wa majini?

Wananchi wanapomchagua kiongozi wao, matarajio yao ni kuwa huyo wanayemchagua atawaongoza katika jitihada zao za kuyafikia maendeleo, sasa kama majini yatamchagua mgombea kuwa Rais, hayo majini yanatarajia kunufaika vipi na huyo yaliyempigania?

Wataalam wa majini tunaomba litoleeni ufafanuzi hili la mashekhe kuomba majini yamsaidie Rais Samia, inamaanisha nini katika tafsiri pana?
View attachment 3222655
View attachment 3222658
Baada ya dua, mbuzi ng'ombe
 

Attachments

  • images-6.jpeg
    images-6.jpeg
    13.9 KB · Views: 1
Acha ubwabwajaji...kwasasa mpo vizuri kwenye hayo mambo vijana wa Mwamedi
Kwaiyo mtu akivaa kislamu ndio Muslimu mizwazwa mzigo kwa taifa!!! Akuna nchi ya kislamu iliopitisha sheria kuwatambua Mashoga zaid utapata ni nchi za Wakristo ata Africa utapata Africa kusini Zimbabwe zote za wakristo

Nchi inaruusu kisheria USHOGA sio unarusha vipicha vyako mtu yoyote anaweza kuvaa nguo lkn sio Muislam!!!! Propaganda zenu kwasasa mmetatizika kila mkiongopea watu yale mambo yanakuja milangoni kwenu tena kiushaidi wa kisheria!!!!!!!
 
Aje mwislamu hapa atufafanulie, kwanini masheikh na usomi wao wa dini ya haki,wanawataja majini kwenye maombi yao hayo!!?,,hii imekaaje?,je twaweza tofautisha vipi na zile kauli za docta sule!?kuhusu kuwatumia majini kwa namna mbalimbali.
 
Back
Top Bottom