Pre GE2025 Mashekhe wafanya ibada na kuomba majini yasaidie Rais Samia kushinda kwenye uchaguzi ujao

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Sasa wewe ulishaona majini yakaombwa halafu MUNGU akae hapo? Kama hatakaa shetani! Hakuna tofauti na mabaari-peor
Kwahiyo malaika ndio wanafaa kuombwa? Tatizo hamsomi kwa kuelewa mnakurupuka tu kisa mmeona wametajwa majini, nyie ndio mnatuambia kuwa hao majini ni malaika na kila mkiambiwa kuwa majini ni viumbe tofauti na malaika ambao hawamuasi Mungu hamuelewi.
 
Aje mwislamu hapa atufafanulie, kwanini masheikh na usomi wao wa dini ya haki,wanawataja majini kwenye maombi yao hayo!!?,,hii imekaaje?,je twaweza tofautisha vipi na zile kauli za docta sule!?kuhusu kuwatumia majini kwa namna mbalimbali.
Mkristo ni mtata sana. Muislamu akisema Yesu ndio Issa, mkristo anakataa katakata anasema hao ni watu wawili tofauti na ataweka hadi maandiko kuonyesha utofauti wao. Muislamu akisema jini ni kiumbe kilichoumbwa na Mungu na kwamba wapo majini wema na waovu, bado mkristo anakataa anasema jini ni malaika(aliyeasi) ila hapa hatoi maandiko kuonyesha huo ufanano au uthibitisho wa kimaandiko kuwa majini ndio malaika waliyoasi.

Sasa imekuwa muislamu akimzungumzia jini mkristo anachukulia ni malaika waliyoasi ila muislamu akimzungumzia Issa mkristo haoni kuwa anakusudiwa Yesu.
 
Wanaosema kuwa eti shekhe aliyeomba majini yamsaidie Samia kuupata Urais, siyo shekhe, bali ni mganga wa kienyeji, wanapotosha.

Huo mkutano ulikuwa wa viongozi wa dini ya kiislam, siyo mkutano wa waganga wa kienyeji. Kama aliyetoa kauli ile angekuwa ni mganga wa kienyeji, ina maana shekhe mkuu, mufti huwa anafanya ibada kwa kushirikiana na waganga wa kienyeji?
 
Nilikuwa namheshimu sana. Vizuri Allah amenionesha kabla ya kufa!
Hii inazidi kudhihirisha dunia ni 'ibtilaa' (majaribu) hakuna yeyote, hata Maaskofu au Mashekhe, ambaye anaweza kusema ameshinda mtihani huu..............hadi aondokapo dunia. Wote tuko sawa!
 
Majini gani
Kwani uislam unawasilisha maombi kwa majini?
 
Nilikuwa namheshimu sana. Vizuri Allah amenionesha kabla ya kufa!
Hii inazidi kudhihirisha dunia ni 'ibtilaa' (majaribu) hakuna yeyote, hata Maaskofu au Mashekhe, ambaye anaweza kusema ameshinda mtihani huu..............hadi aondokapo dunia. Wote tuko sawa!
 
MFUATILIE IMAM WA KIISLAM ALIYEKUFA NA KUFUFUKA NDIO UTAFAHAMU UKO CHAKA. KWA SASA ANAISHI MAREKANI AWALI ALIISHI IRAQ NA ALIKUWA NA MSIKITI KWA SASA AMEKIMBIA HADI MSIKITI. YUKO YOUTUBE!
 
Umeweka video mbili, video ya kwanza hao masheikh wanajulikana na kilichosmwa ni kutaka manini na MALAIKA kumuombea Samia kwa Mungu.
Video nyengine umeweka huyo mtu anayetaka kusoma Albadil na kuchinja mbuzi, huyo ndio kaitwa ni mganga.
 
Halafu tukiwaambia kuwa mungu wa waislamu ni shetani mwenyewe wanakasirika. Majini ni watumishi wa shetani hivyo, kama mnawaamini na kuwatumia ina maana mko upande mmoja nao na huo upande ni kinyume na Mungu.
 
unaelewa maana ya msaada? yaani hao majini yanamsaidia binadamu au yanamuonngoza bindamu akamchague ssh siyo yenyewe ndiyo yanapiga kura kwahiyo uzi huu umefeli kwa kiwango kikubwa sana
 
Halafu tukiwaambia kuwa mungu wa waislamu ni shetani mwenyewe wanakasirika. Majini ni watumishi wa shetani hivyo, kama mnawaamini na kuwatumia ina maana mko upande mmoja nao na huo upande ni kinyume na Mungu.
Lazima wakasirike kwa sababu unapotosha, wewe unaamini majini ni malaika na kwamba malaika wanamuasi Mungu ni tofauti na waislamu ambao wanaamini malaika hawamuasi Mungu na kwamba majini sio malaika ni viumbe tofauti na malaika.
 
Mkuu umeuliza mambo ya msimgi mpaka nimejikuta nacheka kijinga sana.

Nchi inapita wakati Mgum sana, sasa rasmi kwa kauli hii uchaguzi ujao ni kati ya watanganyika vs Majini , na kama ndivyo yatapelekewa moto mpaka yarudi kuzimu kwa vilio vingi sana.

Swali .
Hii nguvu kubwa inayotumika kwa upande wa kijani ni ya nini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…