Mashindano makubwa ya "drafti" Dar: Noel Namaloe atwaa ubingwa baada ya kumshinda Ronaldo katika fainali

Mashindano makubwa ya "drafti" Dar: Noel Namaloe atwaa ubingwa baada ya kumshinda Ronaldo katika fainali

Aisee kumbe sikuhizi mafundi wamebadilika enzi zetu nilikuwepo mimi mangwelele juma mchafu na mafundi wengine wengi vijiwe buguruni,mbagala tmk
Hao watu huwa wanasahau kula na kuoga kwa ajili ya draft. Nakumbuka tulipandishiana dau na Mangwelele nizuie sare mbili, nikapata sare moja.

Juma Mchafu nilikuwa namuweza.
 
Heshima kwa Wanzilishi wakongwe wa huu mchezo wa Drafti ninao wakumbuka wachache ni pamoja na.
Fundi Kikwa
Fundi Amiri
Fundi Noa Mkubwa
Fundi Bedui
Fundi Mavumba
Endelezeni kutaja mafundi wa zamani na sio hawa wanaocheza leo ambao mdogo kabisa ni Shaaban katoto, aliitwa "katoto" kwakuwa alikuwa ndiye mchezaji mdogo zaidi wakati leo ndiye mwalimu wa akina Nduli. tajeni wale manguli wa zamani.
 
Nasikia game za mitoano ilikuwa zinapigwa 14; 7 anaanza huyu na 7 anaanza mwingine.

Na kwenye kuanza kila game unaanza kete tofauti na ile ya mwanzo, kwa michezo hiyo 7 yote unaanza kete tofauti.
 
Ile miondoko ya drafti iliyoshinda kuanzia hatua ya robo fainali ilibidi irekodiwe ili tusiohudhuria tuiangalie hata U-tube, au Wasap App.
Tuone miguu ya Ushindi ilitembeaje kuanzia robo fainali.
 
Back
Top Bottom