Masikhara ya JK nyuma ya uwepo wa Makamba nionyeshe rafiki nikwambia wewe mtu wa aina gani

Masikhara ya JK nyuma ya uwepo wa Makamba nionyeshe rafiki nikwambia wewe mtu wa aina gani

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2015
Posts
18,487
Reaction score
13,611
Wazungu wanao msema usemao nionyeshe rafiki yako nikwambie wewe ni mtu wa aina gani. Maana yake marafiki zako ndio wanaokutambulisha mbele ya wastaarabu. Ni msemo umekuwepo kwa miaka mingi japo unajulikana kwa wale wasomaji wa vitabu vya kingereza.

Mwalimu Nyerere alikuwa na Hayati Rashid Kawawa, wakati akihutubia hupenda kumtambulisha kwa kulitaja jina lake la kwanza la Rashid. Alikuwa ni msiri wake waliyeshibana vyema, nakumbuka miaka ile pale ikulu alikuwa akitamka Rashid atageuza shingo yake na kumtazama akiwa amekaa kushoto kwake.

Awamu ya nne ilipoingia ikulu Mheshimiwa Jakaya Kikwete akaja na katibu mkuu wa CCM ambaye ni mwanajeshi mwenzake mstaafu mzee Makamba, Kuonyesha alivyoshibana haraka sana akamuondoa Mzee Mangula kutoka katika nafasi ya ukatibu mkuu ili Makamba achukue cheo chake. Hawa wameshibana sana tangu ujanani wakiwa na siri nyingi wanazozifahamu za miaka na miaka.

JK ni mpenda mno masikhara, yapo ndani ya damu yake na hawezi kuongea bila ya kuchomeka maneno mawili matatu ya utani. Makamba nae ni mule mule anamopita JK. Kauli za kebehi kwa wajane wa marais waliokuwa pale ukumbini zilipokelewa kwa tabasamu lile lile la miaka yote la bosi wake wa zamani aliyemuamini na kumpa nafasi ya juu kabisa ndani ya CCM.

Labda ni kuteleza ulimi kwa mtu mzima mwenye miaka 84 na Rais SSH akatumia busara za hapo kwa hapo za kumfichia aibu mzee Makamba pale ukumbini akitumia kiswahili kile kile laini na neno moja la kingereza kwamba mzee alikuwa na emotions wakati anatoa hotuba yake, wenye akili tulimuelewa kwanini aliamua kumsitiri mtu wa umri wa Baba yake akimuita kaka yake.

Ni yale yale ya wazungu na msemo wao nionyeshe rafiki yako nikwambie wewe ni mtu wa aina gani. Bashiru Ally Kakurwa kwa kumtazama tu akiongea ni mtu makini na mwenye kuchagua aongee lipi na kwa wakati upi, anayo kauli yenye mamlaka na ujumbe wake unafikirisha kwa msikilizaji. JPM alituonyesha yeye ni mtu wa aina gani kwa kumpa kipaumbele Bashiru Ally. Tulimjua ni mtu wa aina gani pale tulipomtazama rafiki yake.

Pengine maneno ya mzee Makamba ni matokeo ya umri kuwa umesogea, mzee wa miaka 84 hawezi kupanda jukwaani akawa sawa na mwanasiasa mwenye miaka 45 hadi 60. Na nadhani ni sababu baadhi yetu tunamshauri mzee Wasira Stephen aachane na siasa, kwani ni rika hilo hilo la Makamba.

JK analo la kubeba katika kauli iliyochukuliwa kama ni dhihaka ya Mzee Makamba wakati akihutubia. Hawezi kukwepa lawama kutoka kwa wale wenye kufikiria masuala ya kisiasa kwa kina. Tumemuona yeye mwenyewe kupitia kwa haiba ya Mzee Makamba.
 
Actions Speaks Louder than words..., Hata ukifanya masikhara huku matendo yako yana outcome nzuri watu hawatajali...

Haya yote wangeyafanya hata mabovu zaidi ya huyu ya kuitana kwamba watanzania tunapenda vya dezo wakati gharama ya maisha haijapanda wala hatuhitaji kununua mishumaa kwa kuwa na umeme wa uhakika nadhani dhahika zozote tungecheka tu tukijua kwamba ni utani....
 
Wazungu wanao msema usemao nionyeshe rafiki yako nikwambie wewe ni mtu wa aina gani. Maana yake marafiki zako ndio wanaokutambulisha mbele ya wastaarabu...
Makamba mbona kasema vizuri tu, Magu was evil na ni kweli MTU MWOVU HAISHI na hakuna sababu aishi

Imagine angekuwa hai leo tungeshakufa wangapi? Maelfu kwa Maelfu
 
Wazungu wanao msema usemao nionyeshe rafiki yako nikwambie wewe ni mtu wa aina gani. Maana yake marafiki zako ndio wanaokutambulisha mbele ya wastaarabu. Ni msemo umekuwepo kwa miaka mingi japo unajulikana kwa wale wasomaji wa vitabu vya kingereza.

Mwalimu Nyerere alikuwa na Hayati Rashid Kawawa, wakati akihutubia hupenda kumtambulisha kwa kulitaja jina lake la kwanza la Rashid. Alikuwa ni msiri wake waliyeshibana vyema, nakumbuka miaka ile pale ikulu alikuwa akitamka Rashid atageuza shingo yake na kumtazama akiwa amekaa kushoto kwake.

Awamu ya nne ilipoingia ikulu Mheshimiwa Jakaya Kikwete akaja na katibu mkuu wa CCM ambaye ni mwanajeshi mwenzake mstaafu mzee Makamba, Kuonyesha alivyoshibana haraka sana akamuondoa Mzee Mangula kutoka katika nafasi ya ukatibu mkuu ili Makamba achukue cheo chake. Hawa wameshibana sana tangu ujanani wakiwa na siri nyingi wanazozifahamu za miaka na miaka.

JK ni mpenda mno masikhara, yapo ndani ya damu yake na hawezi kuongea bila ya kuchomeka maneno mawili matatu ya utani. Makamba nae ni mule mule anamopita JK. Kauli za kebehi kwa wajane wa marais waliokuwa pale ukumbini zilipokelewa kwa tabasamu lile lile la miaka yote la bosi wake wa zamani aliyemuamini na kumpa nafasi ya juu kabisa ndani ya CCM.

Labda ni kuteleza ulimi kwa mtu mzima mwenye miaka 84 na Rais SSH akatumia busara za hapo kwa hapo za kumfichia aibu mzee Makamba pale ukumbini akitumia kiswahili kile kile laini na neno moja la kingereza kwamba mzee alikuwa na emotions wakati anatoa hotuba yake, wenye akili tulimuelewa kwanini aliamua kumsitiri mtu wa umri wa Baba yake akimuita kaka yake.

Ni yale yale ya wazungu na msemo wao nionyeshe rafiki yako nikwambie wewe ni mtu wa aina gani. Bashiru Ally Kakurwa kwa kumtazama tu akiongea ni mtu makini na mwenye kuchagua aongee lipi na kwa wakati upi, anayo kauli yenye mamlaka na ujumbe wake unafikirisha kwa msikilizaji. JPM alituonyesha yeye ni mtu wa aina gani kwa kumpa kipaumbele Bashiru Ally. Tulimjua ni mtu wa aina gani pale tulipomtazama rafiki yake.

Pengine maneno ya mzee Makamba ni matokeo ya umri kuwa umesogea, mzee wa miaka 84 hawezi kupanda jukwaani akawa sawa na mwanasiasa mwenye miaka 45 hadi 60. Na nadhani ni sababu baadhi yetu tunamshauri mzee Wasira Stephen aachane na siasa, kwani ni rika hilo hilo la Makamba.

JK analo la kubeba katika kauli iliyochukuliwa kama ni dhihaka ya Mzee Makamba wakati akihutubia. Hawezi kukwepa lawama kutoka kwa wale wenye kufikiria masuala ya kisiasa kwa kina. Tumemuona yeye mwenyewe kupitia kwa haiba ya Mzee Makamba.
Huyo mzee mpumbavu tu kama wewe mwenyewe,mbona kina mzee Malechela, Warioba wapo na watulivu?
Hawa wazee wapumbavu endeleeni kuwatetea nchi inaangamia kwa kujifanya wanahati miliki ya chama na nchi,kiama chao chaja
 
Makamba mbona kasema vizuri tu, Magu was evil na ni kweli MTU MWOVU HAISHI na hakuna sababu aishi

Imagine angekuwa hai leo tungeshakufa wangapi? Maelfu kwa Maelfu
Huyo mzee mpumbavu tu kama wewe mwenyewe,mbona kina mzee Malechela, Warioba wapo na watulivu?
Hawa wazee wapumbavu endeleeni kuwatetea nchi inaangamia kwa kujifanya wanahati miliki ya chama na nchi,kiama chao chaja
 
Wazungu wanao msema usemao nionyeshe rafiki yako nikwambie wewe ni mtu wa aina gani. Maana yake marafiki zako ndio wanaokutambulisha mbele ya wastaarabu...

Tunashukuru kwa bandiko lako la kucheza na maneno, lakini ukweli utabaki palepale kuwa Magufuli hakuwa kiongozi bora au makini, bali katili, mwenye jazba na mlevi wa madaraka.

Kwa bahati mbaya Bashiru akaiga tabia za Magufuli. Na Msoga gang wanachofanya sasa ni kutoa mrejesho wa siasa zao za ulevi wa madaraka chini ya Magufuli.
 
Huyo mzee mpumbavu tu kama wewe mwenyewe,mbona kina mzee Malechela, Warioba wapo na watulivu?
Hawa wazee wapumbavu endeleeni kuwatetea nchi inaangamia kwa kujifanya wanahati miliki ya chama na nchi,kiama chao chaja

Hao wazee unaoita watulivu, si ndio hao wakionya kuhusu mwenendo mbovu wa CCM mnaishia kuwaambia wakae kimya?

Ngoja hao waropokaji waongee, na hamna chochote cha kuwafanya maana hata nyie sukuma gang hamna ushawishi kwa umma zaidi ya ulevi wa muda mfupi madarakani.
 
Huyu Mzee wakati ni kiongozi nilikuwa kijana mdogo sikuwa najua chochote, lakini kauli yake inanipa picha kwamba ujana wake mpaka utu uzima alikuwa ni mropokaji kama wale tuliowaona awamu ya tano
Ndivyo alivyo tangu kwenye Chama hadi ukuu wa mkoa

Huwa anadhani kuwa mtata mtata ndio Dili
 
Wazungu wanao msema usemao nionyeshe rafiki yako nikwambie wewe ni mtu wa aina gani. Maana yake marafiki zako ndio wanaokutambulisha mbele ya wastaarabu...
Mwenyekiti Mstaafu na anayeendelea walishampatia twisheni mzee asiye na breki aongee nini na hakuna litakalotokea.

Natabiri, uchaguzi wa 2025 utakuwa baina ya CCM dhidi ya JPM. Wapinzani watakuwa watazamaji
 
Huyu Mzee wakati ni kiongozi nilikuwa kijana mdogo sikuwa najua chochote, lakini kauli yake inanipa picha kwamba ujana wake mpaka utu uzima alikuwa ni mropokaji kama wale tuliowaona awamu ya tano
Nilimfahamu zaidi alipokuwa mkuu wa mkoa.
Ndiye muanzilishi wa soko la kila wiki la barabara inayopitia Lumumba.
Kuna kipindi nilimuona mtetezi wa wanyonge alipowapigania wafanyakazi wabangua korosho kiwanda flani pale Waliita Abestozi pale karibu na Kibo complex.
Alitoa speech nzuri sana kuwatetea.

Kumbe asali huleta kiburi
 
mbona kina mzee Malechela, Warioba wapo na watulivu?
Asa km hawana cha kusema waseme nini?? af bangi zingine za ukubwani bana wala si nzuri! Mtu aseme seme tu km taahira aau! eti tu kwa sababu makamaba kasema??
 
Back
Top Bottom