Masikhara ya JK nyuma ya uwepo wa Makamba nionyeshe rafiki nikwambia wewe mtu wa aina gani

Masikhara ya JK nyuma ya uwepo wa Makamba nionyeshe rafiki nikwambia wewe mtu wa aina gani

Ungekuwa ni mtu wa CCM ningeweza kukuelewa lakini CHADEMA hata siku moja huwezi kuongea maongezi chanya lazima ukosoe tu.

Usisahau kipindi CHADEMA wanapiga kelele kuwa Magufuli amefariki mliwakebehi. Hadi walipotishia kufanya press conference ya kutangazwa kifo Cha Magufuli ndipo Mama Samiah akakurupushwa usiku wa manane.

Nina uhakika Magufuli akirudi leo Atawaomba msamaha CHADEMA, na ndio atagundua CHADEMA ndio marafiki zake wa kweli.
 
kuna Viongozi wengi tu wamefariki wakiwa madarakani ukianzia kwa Rais Karume Mkubwa, Sheikh Anri Abeid, Sokoine, Horace Kolimba, Salome Mbatia, n.k

kwanini tumekimbilia kuhisi kuwa kasemwa mtu fulani ?

Waovu Mara nyingi hujishuku. Sijasikia wafuasi wa Maalim Seif wakilalamika.
 
Wazungu wanao msema usemao nionyeshe rafiki yako nikwambie wewe ni mtu wa aina gani. Maana yake marafiki zako ndio wanaokutambulisha mbele ya wastaarabu. Ni msemo umekuwepo kwa miaka mingi japo unajulikana kwa wale wasomaji wa vitabu vya kingereza.

Mwalimu Nyerere alikuwa na Hayati Rashid Kawawa, wakati akihutubia hupenda kumtambulisha kwa kulitaja jina lake la kwanza la Rashid. Alikuwa ni msiri wake waliyeshibana vyema, nakumbuka miaka ile pale ikulu alikuwa akitamka Rashid atageuza shingo yake na kumtazama akiwa amekaa kushoto kwake.

Awamu ya nne ilipoingia ikulu Mheshimiwa Jakaya Kikwete akaja na katibu mkuu wa CCM ambaye ni mwanajeshi mwenzake mstaafu mzee Makamba, Kuonyesha alivyoshibana haraka sana akamuondoa Mzee Mangula kutoka katika nafasi ya ukatibu mkuu ili Makamba achukue cheo chake. Hawa wameshibana sana tangu ujanani wakiwa na siri nyingi wanazozifahamu za miaka na miaka.

JK ni mpenda mno masikhara, yapo ndani ya damu yake na hawezi kuongea bila ya kuchomeka maneno mawili matatu ya utani. Makamba nae ni mule mule anamopita JK. Kauli za kebehi kwa wajane wa marais waliokuwa pale ukumbini zilipokelewa kwa tabasamu lile lile la miaka yote la bosi wake wa zamani aliyemuamini na kumpa nafasi ya juu kabisa ndani ya CCM.

Labda ni kuteleza ulimi kwa mtu mzima mwenye miaka 84 na Rais SSH akatumia busara za hapo kwa hapo za kumfichia aibu mzee Makamba pale ukumbini akitumia kiswahili kile kile laini na neno moja la kingereza kwamba mzee alikuwa na emotions wakati anatoa hotuba yake, wenye akili tulimuelewa kwanini aliamua kumsitiri mtu wa umri wa Baba yake akimuita kaka yake.

Ni yale yale ya wazungu na msemo wao nionyeshe rafiki yako nikwambie wewe ni mtu wa aina gani. Bashiru Ally Kakurwa kwa kumtazama tu akiongea ni mtu makini na mwenye kuchagua aongee lipi na kwa wakati upi, anayo kauli yenye mamlaka na ujumbe wake unafikirisha kwa msikilizaji. JPM alituonyesha yeye ni mtu wa aina gani kwa kumpa kipaumbele Bashiru Ally. Tulimjua ni mtu wa aina gani pale tulipomtazama rafiki yake.

Pengine maneno ya mzee Makamba ni matokeo ya umri kuwa umesogea, mzee wa miaka 84 hawezi kupanda jukwaani akawa sawa na mwanasiasa mwenye miaka 45 hadi 60. Na nadhani ni sababu baadhi yetu tunamshauri mzee Wasira Stephen aachane na siasa, kwani ni rika hilo hilo la Makamba.

JK analo la kubeba katika kauli iliyochukuliwa kama ni dhihaka ya Mzee Makamba wakati akihutubia. Hawezi kukwepa lawama kutoka kwa wale wenye kufikiria masuala ya kisiasa kwa kina. Tumemuona yeye mwenyewe kupitia kwa haiba ya Mzee Makamba.
Kuna nini kipya ambacho kilikuwa hakijulikani? Kikwete, Kinana, Makamba na kundi lao lote walifurahia sana kutwaliwa kwaa bwana yule... Ni watanzania tu mnapenda kujadili mambo ambayo yako wazi na yale ambayo hayako wazi mnayaacha. Alichosema huyu Makamba ni sehemu ndogo tu ya undani wao.
 
Kuna nini kipya ambacho kilikuwa hakijulikani? Kikwete, Kinana, Makamba na kundi lao lote walifurahia sana kutwaliwa kwaa bwana yule... Ni watanzania tu mnapenda kujadili mambo ambayo yako wazi na yale ambayo hayako wazi mnayaacha. Alichosema huyu Makamba ni sehemu ndogo tu ya undani wao.
Kufurahia kutwaliwa kimya kimya wengi tu walifurahia, kuna waliofanya sherehe kabisa kwa kwenda disco usiku ule ule kujipongeza.

Tatizo ni hizi hekima mbovu za uzeeni za kusema kabisa kwamba umefurahi juu ya kifo cha JPM mbele ya mjane aliyefunga safari kutoka alipotoka kwenda mkutanoni pale. Inakuwa kama vile mnamsuta yeye kwa kuwa mahali pale na kwa kuolewa na marehemu. Mzee Makamba amefanya jambo la kipuuzi sana kuongea vile hadharani.

Kauli huwa inaumba, chunga sana kitokacho kinywani mwako huweza kukuharibia maisha yako yote. Kitokacho mdomoni mwako kinakushtaki moja kwa moja kwa Mungu. Pia upo msemo Mungu hadhihakiwi.
 
kuna Viongozi wengi tu wamefariki wakiwa madarakani ukianzia kwa Rais Karume Mkubwa, Sheikh Anri Abeid, Sokoine, Horace Kolimba, Salome Mbatia, n.k

kwanini tumekimbilia kuhisi kuwa kasemwa mtu fulani ?
Watu wamechukua mbili wakajumlisha na mbili jawabu likaja nne.
 
Kufurahia kutwaliwa kimya kimya wengi tu walifurahia, kuna waliofanya sherehe kabisa kwa kwenda disco usiku ule ule kujipongeza.

Tatizo ni hizi hekima mbovu za uzeeni za kusema kabisa kwamba umefurahi juu ya kifo cha JPM mbele ya mjane aliyefunga safari kutoka alipotoka kwenda mkutanoni pale. Inakuwa kama vile mnamsuta yeye kwa kuwa mahali pale na kwa kuolewa na marehemu. Mzee Makamba amefanya jambo la kipuuzi sana kuongea vile hadharani.

Kauli huwa inaumba, chunga sana kitokacho kinywani mwako huweza kukuharibia maisha yako yote. Kitokacho mdomoni mwako kinakushtaki moja kwa moja kwa Mungu. Pia upo msemo Mungu hadhihakiwi.
Nakubaliana na wewe kabisa mkuu. Na madaraka yanalevya kweli kweli. Sasa hivi kina Kikwete na Kinana na pia huyu mzee wameshasahau kuwa walikuwa wameshapotea mazima. Wamerudi kwa kiburi na dharau kali huku hawajui ya kesho.
 
Nakubaliana na wewe kabisa mkuu. Na madaraka yanalevya kweli kweli. Sasa hivi kina Kikwete na Kinana na pia huyu mzee wameshasahau kuwa walikuwa wameshapotea mazima. Wamerudi kwa kiburi na dharau kali huku hawajui ya kesho.
JK Kwa kuwa na upande anaoshabikia anajishushia heshima yake japokuwa anajaribu kadri awezavyo aonekane ni mstaarabu.
 
Huyo babu ni kawaida yake kuropoka sijui hata watu mnashangaa nini,na hilo jopo lake litashangaa siku ataporoka chanzo halisi cha kfo cha jiwe.endeleeni kumpandisha jukwaani huvyohivyo
 
Ushahidi wa mauaji aliyofanya ukiombwa uutoe mahakamani upo tayari kufanya hivyo? Yale yale ya maiti kuokotwa ndani ya viroba yalisemwa sana lakini cha ajabu ni kwamba mpaka leo bado miili inaokotwa ndani ya viroba. Na hawa nao mhusika mkuu ni JPM?.

Uovu wa kubuni tu akilini bila ya ushahidi wowote ni dhambi ya huyo anayetuhumu.
Nenda basi mahakamani, idiot
 
Ni yale yale ya wazungu na msemo wao nionyeshe rafiki yako nikwambie wewe ni mtu wa aina gani. Bashiru Ally Kakurwa kwa kumtazama tu akiongea ni mtu makini na mwenye kuchagua aongee lipi na kwa wakati upi, anayo kauli yenye mamlaka na ujumbe wake unafikirisha kwa msikilizaji. JPM alituonyesha yeye ni mtu wa aina gani kwa kumpa kipaumbele Bashiru Ally. Tulimjua ni mtu wa aina gani pale tulipomtazama rafiki yake.
"JPM alituonyesha yeye mi mtu wa aina gani kwa kumpa kipaumbele Bashiru Ally."
Inawezekana hapa ukawa umewachanganya wasomaji wako wengi kwa hayo maneno kumhusu JPM na Bashiru.

Binafsi sijui mfanano wa karibu kati ya hao wawili, ila ninakumbuka maneno aliyowahi kutamka Bashiru Ali kuhusu chama kinachounda serikali kulazimika kuachia madaraka kwa matakwa ya wananchi wakati wa uchaguzi.

Yeye kwa maoni yake haoni hilo likitokea huku chama kikishikilia dola na nyenzo zake zote! sijui kama kuna mfano mwingine wowote uliowaweka hawa watu wawili karibu zaidi.
 
Mwenyekiti Mstaafu na anayeendelea walishampatia twisheni mzee asiye na breki aongee nini na hakuna litakalotokea.

Natabiri, uchaguzi wa 2025 utakuwa baina ya CCM dhidi ya JPM. Wapinzani watakuwa watazamaji
Hilo likitokea,nchi itafaidika sana.

Lakini najua ni jambo lisilowezekana kwa walafi walioko CCM. Kwao maslahi ndio kila kitu. Wakilambishwa asali akili zote zinawaruka.
 
Wazungu wanao msema usemao nionyeshe rafiki yako nikwambie wewe ni mtu wa aina gani. Maana yake marafiki zako ndio wanaokutambulisha mbele ya wastaarabu. Ni msemo umekuwepo kwa miaka mingi japo unajulikana kwa wale wasomaji wa vitabu vya kingereza.

Mwalimu Nyerere alikuwa na Hayati Rashid Kawawa, wakati akihutubia hupenda kumtambulisha kwa kulitaja jina lake la kwanza la Rashid. Alikuwa ni msiri wake waliyeshibana vyema, nakumbuka miaka ile pale ikulu alikuwa akitamka Rashid atageuza shingo yake na kumtazama akiwa amekaa kushoto kwake.

Awamu ya nne ilipoingia ikulu Mheshimiwa Jakaya Kikwete akaja na katibu mkuu wa CCM ambaye ni mwanajeshi mwenzake mstaafu mzee Makamba, Kuonyesha alivyoshibana haraka sana akamuondoa Mzee Mangula kutoka katika nafasi ya ukatibu mkuu ili Makamba achukue cheo chake. Hawa wameshibana sana tangu ujanani wakiwa na siri nyingi wanazozifahamu za miaka na miaka.

JK ni mpenda mno masikhara, yapo ndani ya damu yake na hawezi kuongea bila ya kuchomeka maneno mawili matatu ya utani. Makamba nae ni mule mule anamopita JK. Kauli za kebehi kwa wajane wa marais waliokuwa pale ukumbini zilipokelewa kwa tabasamu lile lile la miaka yote la bosi wake wa zamani aliyemuamini na kumpa nafasi ya juu kabisa ndani ya CCM.

Labda ni kuteleza ulimi kwa mtu mzima mwenye miaka 84 na Rais SSH akatumia busara za hapo kwa hapo za kumfichia aibu mzee Makamba pale ukumbini akitumia kiswahili kile kile laini na neno moja la kingereza kwamba mzee alikuwa na emotions wakati anatoa hotuba yake, wenye akili tulimuelewa kwanini aliamua kumsitiri mtu wa umri wa Baba yake akimuita kaka yake.

Ni yale yale ya wazungu na msemo wao nionyeshe rafiki yako nikwambie wewe ni mtu wa aina gani. Bashiru Ally Kakurwa kwa kumtazama tu akiongea ni mtu makini na mwenye kuchagua aongee lipi na kwa wakati upi, anayo kauli yenye mamlaka na ujumbe wake unafikirisha kwa msikilizaji. JPM alituonyesha yeye ni mtu wa aina gani kwa kumpa kipaumbele Bashiru Ally. Tulimjua ni mtu wa aina gani pale tulipomtazama rafiki yake.

Pengine maneno ya mzee Makamba ni matokeo ya umri kuwa umesogea, mzee wa miaka 84 hawezi kupanda jukwaani akawa sawa na mwanasiasa mwenye miaka 45 hadi 60. Na nadhani ni sababu baadhi yetu tunamshauri mzee Wasira Stephen aachane na siasa, kwani ni rika hilo hilo la Makamba.

JK analo la kubeba katika kauli iliyochukuliwa kama ni dhihaka ya Mzee Makamba wakati akihutubia. Hawezi kukwepa lawama kutoka kwa wale wenye kufikiria masuala ya kisiasa kwa kina. Tumemuona yeye mwenyewe kupitia kwa haiba ya Mzee Makamba.
Hizi ni porojo zingine!

Bashiru hana hizo sifa unazompa. Ni mganga njaa tu ambaye alipopewa madaraka alilewa akaanza kutumia rasilimali za umma kulangua wapinzani!

Kwa viwango vyovyote Magufuli alikuwa kiongozi muovu. Munaomuona vinginevyo ni wale muliofaidika na uovu wake kwa kupata mlichokuwa hamsitahili.
 
Back
Top Bottom