Masikini Lowassa, nilihisi haya yatamkuta, yamemkuta

Masikini Lowassa, nilihisi haya yatamkuta, yamemkuta

Bwashee niko mjini kitambo Sana na kinywaji nilikuwa napata hapo Puma wakati huo ikiwa Bar

Wadanganye Wagogo Wenzako huko Kongwa 😂😂
Kwa taarifa yako hapo mahala palikuwa BP, tukinywa supu ya ghoulash hapo na kina mzee Bob Makani.
Na kama unafikiri kuifahamu BP miaka hiyo ndo long time basi wewe bado pusi hapa mjini.
 
Kuyataja maovu yako ni kukuhukum? Endeleni na viwanda vya dhambi huko makanisani kwenu eti mkionywa mnahukumiwa.

Mnapoteza muda bora mkanywe pombe tu.
Wewe unaonywa na nani? Na hayo mamlaka ya kuonya amekupa nani?
 
Masikini Mh Edward Ngoyai Lowassa, mwanasiasa machachari tuliyemjua kwa miaka mingi, ametangulia mbele za haki.

Si vizuri kumuongelea vibaya marehemu, lakini hata Rais Mwinyi aliwahi kusema, maisha ni kitabu, tuishi vyema ili watakao kisoma kitabu chako cha maisha, wafurahie hadithi ya maisha yako.

Hisia zangu ni ile miaka ya 94-2000 ambapo Lowassa alikuwa waziri wa Ardhi.
Alitenda kosa ambalo kimsingi nikajiambia, huyu mzee kajichotea laana isiyosameheka.
Lowassa kama watu wengi wa kaskazini wanapenda sana ardhi, iwe ya kudhulumu au haki.
Katika hili nasikitika kusema alidhulumu ardhi ya KKKT Mbezi Beach, pale Tangi Bovu.

Mzee mmoja maarufu anaitwa Arnold Kileo, alikuwa Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni ya Breweries. Mzee Kileo alitoa ardhi yote karibia eka tatu au nne kwa kanisa, kama sadaka yake.
Naamini kabla ya kutoa ardhi hiyo ,mzee Kilewo aliomba kwa Mungu.

Maaombi yalipoenda wizarani kubadili jina, kiwanja kikakatwa nusu bin nusu.
Nusu moja akajimilikisha kwake Lowassa, ndugu zake na marafiki, kina Kimbisa, na nusu ndiyo akakibakishia kanisa.

Waumini wa hapo walishangaa kwani walijua Lowasa ni Mluteri, kwa nini afanye vile?
Wakamwomba Baba Askofu Sendoro akamwone waziri na kumsihi arudishe ile nusu ya eneo, Lowassa alikataa.

Alipokataa Baba Askofu alishukuru na kumtakia heri, Lawassa asijue kuwa hapo tayari ndipo laana ilipotoka.

Cha kushangaza, kila aliyeweka mradi katika kile kiwanja kilichoporwa, mradi ulikufa, TANESCO walikodi ofisi pale wakaishia kuhama. Ilikuwepo supermarket ya Imalaseko, Dry Cleaner na Gym , vyote vimekufa.
Hata jengo lililo na benki ya NMB pale nayo linakosa wapangaji.

Tukija kwa ndugu yetu Lowassa ,safari yake ya kisiasa ilienda kusuasua. Hata zlipochaguliwa waziri Mkuu, hakudumu.
Lowassa akakosana na rafikiye mkubwa, Jakaya Kikwete, na marafiki hao wakawa maadui.
Mwisho alihama CCM kabisa, na uamuzi bado haukuwa na tija, akarudi.
Lowassa akawa kama mwanasiasa anayetangatanga nyikani.

Pale kanisa la Mbezi KKKT, Lowassa hakuwahi kuslikwa shughuli yoyote ya harambee, ingawaje Sumaye alialikwa mara nyingi.

FUNZO, jamani tumwogope Mungu na tumtumikie hata tukiwa na vyeo vikubwa.
Kwa kufariki akiwa na miaka 70, Lowassa alikuwa bado mdogo mwenye miaka si chini ya 15-20 mbele. Lakini yote ni mapenzi ya Mungu RIP Edward Ngoyai Lowassa.
Mpumbavu wewe, kwanza Lowassa siyo masikini
Pili, Magufuli, Maalim Seif, Anna Mghwira hawa wagombea 2015 wamefariki walizulumu viwanja wapi na wakalaaniwa na nan
 
nimekupa Like kaka!
Inasemekana YESU alikufa Akiwa na 36yrs!
Nadhani jambo la Msingi ni Malengo!
MUNGU huwapangia watu malengo ktk kuishi…
Ukishayatimiza Malengo Then anakuchukua!
Unaweza Ishi Miaka 49 lakini ukafanya Mengi makubwa sawa au zaidi na Alieishi miaka 79Kaka!
Masahihisho kidogo:

✍️Yesu Kristo aliishi miaka 33½ pekee na siyo 36 hapa duniani.

✍️Mgawanyo wa miaka ya maisha yake ni;

• Miaka 30 ni ya kuishi maisha ya kawaida ya kujifunza na kujiandaa kwa ajili ya huduma yake ya kuukomboa ulimwengu na wanadamu kutoka ktk dhambi na matokeo yake

• Miaka 3½ ilikuwa miaka ya kutimiza kusudi la kuja kwake duniani. Ilikuwa ni miaka ya kutangaza habari njema ya wokovu na ukombozi wa ulimwengu. Ilikuwa ni miaka ya vita na mapambano dhidi ya utawala wa shetani hadi kupatikana kwa ushindi pale msalabani Golgotha. Akafa na dhambi zote za ulimwengu. Akazikwa nazo chini. Siku ya tatu akafufuka kwa ushindi mkuu akiziacha dhambi zote chini. Shetani na kazi zake akawa ameshindwa totally.

Mtu yeyote akikiri kwa mdomo wake na kuamini moyoni mwake kuwa haya yalifanyika kwa ajili yake ya kuwa Yesu Kristo aliteswa, akafa, akazikwa na siku ya tatu alifufuka toka kwa wafu, naye mtu huyu ataokolewa!.

Yesu Kristo ameketi juu ya kiti chake cha enzi. Ni mfalme wa wafalme wote duniani na mbinguni!
 
 
Dunia hii haina mbabe. Na siku zetu zinahesabika. Mpaka leo hii watu wachache bado wanawadhulumu watanzania kwa kutumia mali na madaraka wanayopewa kwa hila na dhuluma. Kama vile wao na wajukuu zao wataishi milele.

Muda unafundisha mengi. Baadae tunajikuta tunabaki kujilaumu na kusikitika. Majuto mjukuu. Cha kushangaza ni kama vile bado hatujifunzi.
RIP Mzee Lowasa. It has never been easy anyway...ndio maisha
Huwa hatujifunzi kwa sababu huwa hatuamini yanayowatokea wenzetu nasi siku moja yatatutokea tena even worse kuliko yao !!
Wenye Nguvu waache kudhalilisha watu maana siku yao ya majuto itafika tu !!🙏🙏🙏
 
Du.... nyumba ya Sanaa, ule msonge, wewe kweli kijana mwenzangu wa siku nyingi!
Wengi kiuhalisia hawamjui Lowassa, umemuelezea kiukweli kabisa.
wengi nadhani humu hawajakuelewa. sidhani kama umeleta mada kwa nia mbaya ya kumchafua mwendazake Edo. Umeeleza uhalisia. naamini wengi tulikuwa tunam admire Edo kama kiongozi. Lakini alikuwa na makando kando mengi. Na kwa vile alikuwa kiongozi wa serikali, haya madudu yake hayakwepeki. Especially kwa sababu mengi aliyafanya akiwa na dhamana ya madaraka.

In all, binadamu wote tuna makandokando yetu. Ingawa pia, kama Masanja niliwahi kupewa dhamana ya uongozi ndani ya nchi yangu, nikitangulia mbele ya haki, watu watanizungumzia kadri ya walivyonifahamu. Kama niliwahi kumzulumu mtu, yes watasema. Kama nilikuwa fisadi....Yes they are free to say it. Kwangu mimi sioni shida ipo wapi, kama watu wanaongelea yale uliyoyafanya ukiwa hai au kwenye nafasi fulani. Ni maisha yako. Wacha watu waongee. Kama wanaweza kuongelea mazuri yangu, wacha hata mabaya yangu wayaongee.

Kujificha chini ya kivuli cha "leta ushahidi" we all know, nchi yetu inafanyaje kazi. Mwisho wa siku, kila mtu humu ana story yake kuhusu viongozi wetu wa umma. refer stories za akina Makonda, Sabaya nk. kwamba wamepata second chance....haitawahi kufuta ujinga na udhalimu waliowafanyia wasio na hatia. ni kanuni ya maisha.

Nikiishi kwa wizi na utapeli, kwa kuwadhulumu. watu, hata kesho nikiokoka, nikaanza kuchangia mamilion kanisani, au msikitini.. haitafuta story ya utapeli wangu. Ingawa waumini/wanausharika wenzangu hawatapenda "hiyo dark side" iongelewe.

Ndugu yetu Edo apumzike alipoaandaliwa na Muumba wake.

Masanja
 
wengi nadhani humu hawajakuelewa. sidhani kama umeleta mada kwa nia mbaya ya kumchafua mwendazake Edo. Umeeleza uhalisia. naamini wengi tulikuwa tunam admire Edo kama kiongozi. Lakini alikuwa na makando kando mengi. Na kwa vile alikuwa kiongozi wa serikali, haya madudu yake hayakwepeki. Especially kwa sababu mengi aliyafanya akiwa na dhamana ya madaraka.

In all, binadamu wote tuna makandokando yetu. Ingawa pia, kama Masanja niliwahi kupewa dhamana ya uongozi ndani ya nchi yangu, nikitangulia mbele ya haki, watu watanizungumzia kadri ya walivyonifahamu. Kama niliwahi kumzulumu mtu, yes watasema. Kama nilikuwa fisadi....Yes they are free to say it. Kwangu mimi sioni shida ipo wapi, kama watu wanaongelea yale uliyoyafanya ukiwa hai au kwenye nafasi fulani. Ni maisha yako. Wacha watu waongee. Kama wanaweza kuongelea mazuri yangu, wacha hata mabaya yangu wayaongee.

Kujificha chini ya kivuli cha "leta ushahidi" we all know, nchi yetu inafanyaje kazi. Mwisho wa siku, kila mtu humu ana story yake kuhusu viongozi wetu wa umma. refer stories za akina Makonda, Sabaya nk. kwamba wamepata second chance....haitawahi kufuta ujinga na udhalimu waliowafanyia wasio na hatia. ni kanuni ya maisha.

Nikiishi kwa wizi na utapeli, kwa kuwadhulumu. watu, hata kesho nikiokoka, nikaanza kuchangia mamilion kanisani, au msikitini.. haitafuta story ya utapeli wangu. Ingawa waumini/wanausharika wenzangu hawatapenda "hiyo dark side" iongelewe.

Ndugu yetu Edo apumzike alipoaandaliwa na Muumba wake.

Masanja
Waswahili Wanasemaga Maneno kuntu !
 
wengi nadhani humu hawajakuelewa. sidhani kama umeleta mada kwa nia mbaya ya kumchafua mwendazake Edo. Umeeleza uhalisia. naamini wengi tulikuwa tunam admire Edo kama kiongozi. Lakini alikuwa na makando kando mengi. Na kwa vile alikuwa kiongozi wa serikali, haya madudu yake hayakwepeki. Especially kwa sababu mengi aliyafanya akiwa na dhamana ya madaraka.

In all, binadamu wote tuna makandokando yetu. Ingawa pia, kama Masanja niliwahi kupewa dhamana ya uongozi ndani ya nchi yangu, nikitangulia mbele ya haki, watu watanizungumzia kadri ya walivyonifahamu. Kama niliwahi kumzulumu mtu, yes watasema. Kama nilikuwa fisadi....Yes they are free to say it. Kwangu mimi sioni shida ipo wapi, kama watu wanaongelea yale uliyoyafanya ukiwa hai au kwenye nafasi fulani. Ni maisha yako. Wacha watu waongee. Kama wanaweza kuongelea mazuri yangu, wacha hata mabaya yangu wayaongee.

Kujificha chini ya kivuli cha "leta ushahidi" we all know, nchi yetu inafanyaje kazi. Mwisho wa siku, kila mtu humu ana story yake kuhusu viongozi wetu wa umma. refer stories za akina Makonda, Sabaya nk. kwamba wamepata second chance....haitawahi kufuta ujinga na udhalimu waliowafanyia wasio na hatia. ni kanuni ya maisha.

Nikiishi kwa wizi na utapeli, kwa kuwadhulumu. watu, hata kesho nikiokoka, nikaanza kuchangia mamilion kanisani, au msikitini.. haitafuta story ya utapeli wangu. Ingawa waumini/wanausharika wenzangu hawatapenda "hiyo dark side" iongelewe.

Ndugu yetu Edo apumzike alipoaandaliwa na Muumba wake.

Masanja
Ni kweli mkuu, wengi wanafikiri nalimfahamu Lowasa kupitia Luninga. Wengi hawajui kuwa alikuwa na kampuni yake ikiitwa Barare, na nilifanya kazi nao.
Hili nililobandika si uzushi wala majungu, ni kweli tupu.
 
Masahihisho kidogo:

✍️Yesu Kristo aliishi miaka 33½ pekee na siyo 36 hapa duniani.

✍️Mgawanyo wa miaka ya maisha yake ni;

• Miaka 30 ni ya kuishi maisha ya kawaida ya kujifunza na kujiandaa kwa ajili ya huduma yake ya kuukomboa ulimwengu na wanadamu kutoka ktk dhambi na matokeo yake

• Miaka 3½ ilikuwa miaka ya kutimiza kusudi la kuja kwake duniani. Ilikuwa ni miaka ya kutangaza habari njema ya wokovu na ukombozi wa ulimwengu. Ilikuwa ni miaka ya vita na mapambano dhidi ya utawala wa shetani hadi kupatikana kwa ushindi pale msalabani Golgotha. Akafa na dhambi zote za ulimwengu. Akazikwa nazo chini. Siku ya tatu akafufuka kwa ushindi mkuu akiziacha dhambi zote chini. Shetani na kazi zake akawa ameshindwa totally.

Mtu yeyote akikiri kwa mdomo wake na kuamini moyoni mwake kuwa haya yalifanyika kwa ajili yake ya kuwa Yesu Kristo aliteswa, akafa, akazikwa na siku ya tatu alifufuka toka kwa wafu, naye mtu huyu ataokolewa!.

Yesu Kristo ameketi juu ya kiti chake cha enzi. Ni mfalme wa wafalme wote duniani na mbinguni!
Amen.
 
Back
Top Bottom