Proved
JF-Expert Member
- Sep 10, 2018
- 32,639
- 42,908
Kama hutaki mbona hutekelezi ?... anyway kila laheri mkuu.Mkuu siyo kwamba sitaki kuoa ata mama, ndugu jamaa marafiki wananigusia sana hilo suala
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kama hutaki mbona hutekelezi ?... anyway kila laheri mkuu.Mkuu siyo kwamba sitaki kuoa ata mama, ndugu jamaa marafiki wananigusia sana hilo suala
😂😂😂😂😂Sasa ndugu bangi ina kosa gnBange ipigwe marufuku
Ki Afrika mlezi wa watoto( kwa ukaribu) ni nani?Kwaiyo ushoga unaharibu hadhi ya mwanamke na sio mwanaume?
WazaziKi Afrika mlezi wa watoto( kwa ukaribu) ni nani?
HunielewiMkuu hadhi ya mwanamke ina sifa zipi..
Afu kuolewa sio basic need bhana khaaaaaaHabari za muda huu marafiki,
Siku za hivi karibuni kumekuwa na hali ya kushangaza kustaajabisha kwenye jamii yetu na hasa huku mitandaoni.
Kumekuwa na wimbi la watu kuwasimanga, kuwakejeli na hata kuwacheka ndugu zetu, jamaa zetu na marafiki zetu wanaoonekana kwa vigezo, mitazamo na viwango vilivyowekwa kwenye jamii kuwa wamechelewa kuoa au kuolewa hivyo kuonekana wamepata watoto wa uzeeni.
Ni jambo linaloonekana kama la kawaida lakini kwa upande mwingine linasononesha na kuvunja mioyo ya watu walioamua kujenga familia.
Ni kauli za kitoto zinazoonyesha kuwa bado hawajakomaa kiakili kwenye ulimwengu huu uliojaa harakati na purukushani za kila aina.
Ningependa kuchukua nafasi hii kuwakumbusha hao wenye kuwakejeli wengine kwenye hili ya kuwa.
1) Maisha ni fumbo zito Sana ambalo mara nyingi ni wachache Sana wenye kufumbua. Mara nyingi mipango yako inaweza ikapishana na mipango ya Mungu.
2) Uhai na kifo ni vyake Mungu mwenyewe kwani hakuna ajuaye kuwa amebakisha muda gani wa kuishi hapa duniani. Wapo vijana wengi wametangulia mbele za haki wakiacha watoto wao na familia zao zikiteseka na kuwaacha wazee wakiendelea kulea watoto wao wa uzeeni mpaka wakijitegemea na kufurahia matunda yao. Hivyo kusema kuwa mwanaao akifika miaka kadhaa wewe utakuwa umeshachoka au umeshakufa ni maneno ya kufuru au ya mtu asiye na Imani kwa mola wake mlezi.
3) Kwenye maisha kila mtu Mungu amemuwekea wakati wake wa kufanya jambo lake kwa rehema zake. Wapo watu waliowahi kuoa lakini Mungu akawanyima watoto mpaka wanazeeka na wengine wanawapata uzeeni kabisa. Wapo watu wamejikuta wapo jela wakitumikia vifungo virefu na mpaka wanatoka umri umekwenda na wanaamua kujenga familia. Wapo watu walikuwa wanaugua kwa muda mrefu na hatimaye wakapona na kuanzisha familia. Hivyo basi kama wewe umewahi ni sahihi kwako lakini haiwezi kuwa makosa kwa anayeonekana amechelewa.
4) Changamoto za kifamilia na vifo.
Kuna mwingine anawahi kuoa lakini Kati Kati ya safari anawapoteza mke na watoto wote kwa pamoja Kwa ajali au maladhi ya kawaida na anaamua kuoa na kuanzisha familia upyaaa.
Kwa kifupi mambo na changamoto za kidunia ni nyingi zinazopelekea watu kuonekana wamechelewa kupata watoto au kuoa na kuolewa. Tujifunze kuwa wastaarabu kwenye maisha ya watu kwani hatujui matamshi yetu yanawaathiri vipi wenzetu.
Niko tayari kusahihishwa.
Nawasilisha.
Mzazi KE nafasi yake imepokwa na kunajisiwa na Beijing 1995...na athari mtambuka zi ndani ya jamii.Wazazi
Anaoaje na miaka 50, anamuoa nani?😂😂😂😂😂Sasa ndugu bangi ina kosa gn
Mama ni mama hata anatembelea fimbo na bibi ni Bibi hata kama anavaa kimini.......Kuna rafiki aliniambia kauli iliniuma kiasi, kwa kejeli eti watoto wataniita bibi badala ya mama 😪😪🙏
Inategemea na kipaumbele chako duniani Yesu pamoja na kukaa karibu na Mungu lakini hakuoa inashangazaFamilia ni kitu muhimu na ndio steji ya mtu aliyekamilika ijalishi ni muda gani?
Hilo sio tatizoAnaoaje na miaka 50, anamuoa nani?
Hii ndio ukweli wa mambo watu wanaogopa majukumu wanajitetea. Kazi ya jamii ni kusimamia maadili kwa hiyo lazima uulizwe tuu ukitaka usitake utaulizwa.Vijana wengi hatutaki kuoa bila hoja yoyote , hoja zinazojengwa zote ni sababu ya kukwepa majukumu sasa mwanaume kama unakwepa majukumu maana yake hujakamilika kujiita mwanaume
Hao walevi wachache hawaondoi uhalali kuoa ni heshima na ni maadili kwenye jamii. Vijana wengi tunaogopa majukumu na kumbuka hutakuwa kijana maisha yako yote tunajidanganya kwa muda tuuNyie mndio mnaoendekeza utamaduni wa kunyanyapaa watu wasiooa.
Yani uneshakariri. Kuoa = Heshima.
Wakati kuna walevi mbwa kibao wameoa na wanapiga wake zao kila siku na kufanya mambo ya kujivunjia heshima.
Halafu kuna watu poa tu hawajaoa.
Acha kuiga maisha ya kimagharibi Mungu amesema tuzaliane tujaze dunia na ni muhimu watoto wazaliwe kwenye ndoa ili kutunza maadiliKwani wapi nimesema kuoa si kitu cha heshima?
Unajua kusoma kwa ufahamu?
Kwanini unaweka false dichotomy kwamba kuoa lazima ni kitu cha heshima au si kitu cha heshima? Kwa nini unaona mtu akisema kuoa si lazima kiwe kitu cha heshima, basi amemaanisha kuwa kuoa ni lazima kiwe ni kitu kisicho cha heshima?
Do you not see this as a false dichotomy logical fallacy?