Masoud Kipanya anafanya biashara gani hadi aendeshe magari ya kifahari? Mwenyewe amejibu..

Masoud Kipanya anafanya biashara gani hadi aendeshe magari ya kifahari? Mwenyewe amejibu..

Uanze we utambie una biashara gani.

Umwage humu vielelezo vyote

Kisha, tuendelee na masoud

Huo umbea wako, bakisha huko huko kibarazani.

Hili taifa linahitaj wachapa kazi na sio wachapa umbea.

Fanya kazi,ingiza kipato chako.

Umbea, wivu wa kijinga na roho ya kwanini havikusaidii chochote.

###pambana na hali yako####
Mzee wa ubuyu povu limemtoka
 
Huna akili wewe, badala ya kufanya kazi umekazana kuchunguza maisha ya watu. Tulikuwa tunasema wanawake ni wambea ila baadhi ya wanaume kama wewe ni zaidi ya mwanamke kwa umbea. Fanya kazi Acha kufuatilia maisha ya watu, Eti hummer. ... wewe unashangaa Hummer! Jifunze kuwekeza, tumia muda wako kama pesa, achana na starehe Muamini Mungu huo utajiri utaona asubuhi. .ACHANA NA MAJUNGU ETI AHOJIWE WEWE NI NANI KWANZA?
tapatalk_1492087126596-jpeg.503773
 
Habari yenu wakuu,
View attachment 686139
Mimi nmeanzisha hii thread kutaka kujua ni biashara gani huyu Masoud Kipanya anafanya Mjini Dar. Haiwezekani mtoto mdogo awe anaendesha magari ya kifahari kwa kipato cha kuchora Katuni za Mwananchi.

Juzi kati alinipita na gari la kifahari la aina yake, nikajaribu kumpiga picha akaniacha alikuwa speed. Sasa leo nimemuona nikamzoom akaingia kati nikamfotoa kwa mbali.

Je katuni zinalipa kiasi hicho? Au naye ana wafadhili? Mbona hajioneshi kama anahela za kununua magari ya kifisadi?

Mwenye kujua katoa wapi hela. Au Mambosasa amuite amhoji tujue.

Juzi kati alitekwa. Hajasema kwanini alitekwa, hajasema walikuwa wanamdai nini wala hajasema amewapa nini wakamuachia.
Masoud is around 44 inakuwaje unamwita mtoto mdogo? Kwani Hummer H2 bei gani hadi uone ni ajabu?
 
Humvee?Ni gari aina gani hii mkuu.

Nahisi itakua hybrid version ya zile gari zetu za Nyumbu
Humvee ni USA military vehicles ndio chanzo cha Hummer kutengenezwa kwa ajili ya raia.
 
Tunaweza kumuona mleta mada kama mmbea ila huenda kuna mtu anawindwa hapa na kupitia huu Uzi taarifa zake zote zikawa disclosed.
 
Ana project nyingi Sana , hujui project ile iliyokuwa inaoneshwa na vituo vya tv jina nimeisahau
 
Je katuni zinalipa kiasi hicho? Au naye ana wafadhili? Mbona hajioneshi kama anahela za kununua magari ya kifisadi?
Kwa kauli hii inaonesha ni namna gani watanzania wengi wana kaliba ya ulimbukeni; Ajionyeshe ili iweje? kwani kuna ulazima mtu ajionyeshe? Kama una hela always money talk, huna haja ya kuongea kama unayo...

Vijana mnapotea sana siku izi, nasikitika kauli kama hizi zinatolewa na kijana.
 
Una hilo tu au masoud najua ana yard ya magari jangwani toto kanko kitu kama hichi lbda ww umekuja mjini juzi kutoka kolomije ndio.mnaofnya kumbi za stareh kutufungia saa 6
Halafu jamaa inaonekana hamjui vizuri Masoud Kipanya. Huyo jamaa sio kijana mdogo kama mwonekano wake ulivyo huyo jamaa ni mhenga ila ana umri mkubwa tu na kama ni mfanyakazi wa serikalini basi abnawaza kustaafu. Masoud ni mpiganaji wa miaka mingi sana na alikuwa na ma-coaster yanaitwa Tonto Kanko miaka ya nyuma sana Enzi hizo kina Prof J bado wako sekondari. Pia amewahi kuwa na duka kubwa sana la nguo pale Millenium Tower lilikuwa linaitwa KP Wear na amefanya miradi mingi sana kama kulima, ufugaji nyuki na program kama Maisha Plus nk. Kwa ufupi jamaa ni mpiganaji hicho kigari ulichokipiga picha wala sio kielelezo cha utajiri wake. Ni kama kumpiga picha mbuzi mmoja kwa mfuga ng'ombe 100
 
Hehhehhhhhh. .......wa Tz bwana kwa wivu hatujambo. ....mtoa mada unadhihirisha ulivyo na wivu mbaya kama ulikua unataka kujua ungeuliza ki ustaarabu ungejibiwa sio kumuita mwenzio kijana mdogo et ana gari la kifisadi wakati humjui ni kutaka kumchafua mtanzania mwenzio heshimu hustle zake......najua umelewa umaskini kwahiyo kila kitu unahis hakiwezekani pole sana aiseee
 
Hivi hujui kama michoro inalipa sana huko majuu?
Masudi anashiriki kwenye maonesho yote makubwa ya michoro duniani,fanyeni kazi
 
Back
Top Bottom