Maswali na ushauri kwa Malinzi

Maswali na ushauri kwa Malinzi

Vp kuhusu timu zinazomilikiwa na Majeshi?? Je mliweka utaratibu wowote kuzihusu??
Manake isifike kipindi Kwenye timu 16 kwenye Ligi za JKT,JW,MAGEREZA,POLISI ni 10..Hapo patakuwa na tatizo kwenye soka letu la Tz...
PILI Ndugu Malinzi hili suala la Ligi yetu kusimama kwa kipindi kirefu katikati ya msimu kana kwamba tunapisha Msimu wa Baridi mnalichukuliaje??

Hapa kama kuna conflict of interests au ni macho yangu? hizo timu zote nne zipo chini ya wizara kama 2, si kuna kipengele cha FIFA/CAF kinachozuia haya?
CC Malafyale, Jamal Malinzi
 
Hapa kama kuna conflict of interests au ni macho yangu? hizo timu zote nne zipo chini ya wizara kama 2, si kuna kipengele cha FIFA/CAF kinachozuia haya?
CC Malafyale, Jamal Malinzi

Tumsubiri Rais wa TFF ajibu hili kwa ukamilifu!Post yangu ya mwanzo kabisa niliongelea hili!Kuwa na team zaidi ya 2 za jeshi moja kwenye league yetu inapunguza msisimko na ni rahisi kwao kupanga matokeo!
Jamal Malinzi kwa sababu hata CAF/FIFA wanakataza team za mmiliki mmoja zaidi ya moja kwenye ligi;Lini mtaziondoa team hizi za majeshi nyingii kwenye ligi zetu hapa TZ?
 
Last edited by a moderator:
Nikusaidie Malafyale na born again pagan mshazari na wengine
Awali CAF waliamua Afcon qualifiers for Morocco 2015 ziwe twelve groups na zichezwe Sept to Nov 2014.Ilikuwa kila group winner aende Morocco plus two best losers na host,total 16,na hadi mashindano ya CHAN south africa mwanzoni mwa mwaka huu hali ilikuwa hivyo,kipindi hicho hata website ya CAF ilisema hivyo.Tulipomtoa Poulsen ( kwa sababu ambazo kimaadili si vyema kumsema mtu ambaye hawezi kujitetea jf)tulijua tunajipanga for september 2014,ghafla CAF wakabadili utaratibu na kusema kutakuwa na pre qualifiers and then group stage,hatukuwa na njia zaidi ya kufumua mipango yetu na kujipanga upya,hiyo ndiyo dhamana ya uongozi.
Mpango wa maboresho ya Taifa stars (ambao unfortunately unauita bonanza),ulibuniwa Novemba mwaka jana tukiamini vijana hao tungewaandaa kuelekea qualifiers septemba,haikuwa hivyo.
Neverthe less hakuna kilichoharibika,wapo ambao Nooij karidhika nao amewachukua National team,waliobaki amewatengenezea program maalum ya mafunzo ataitangaza mwenyewe soon.All in all TFF tumeridhika na tulichokifanya.

Maelezo murua kama haya ndiyo huwa tunayakosa kutoka kwa watawala wetu!Umenieleza vyema na nimekuelewa na uwe unafanya hivi kila ukiulizwa na wala usichukulie maswali yetu kama chuki binafsi!
Chukua "like"yangu!
 
Last edited by a moderator:
Utekelezaji wa Hiyo kanuni Itaanza Msimu upi?? Bado tunaona mmiliki mmoja (Mfano JKT) Akiwa na club 3 kwenye Ligi yetu?
PILI; Hongereni Sana kwa kuwa na Website Nzuri...manake bado Taasisi nyingi zinaendeshwa ki-anolojia zaidi Tanzania...Ila Jitahidini ku-update ili tuwe tunapata habari nyingi na Muhimu za masuala ya Soka letu/Timu ya Taifa...Manake nimejaribu kutafuta taarifa kuhusu mechi yetu inayokuja ila nimeambulia patupu...

CAF kwa sasa wanasisitiza tuanze utekelezaji wa kanuni ya club licencing,hasa kwa vilabu vinavyoshiriki champions league na confederation cup Africa.Muda ukifika tuta comply kwa vilabu visivyocheza Africa championship.
Club licencing regulation lengo lake ni kuboresha uendeshaji wa vilabu vyetu kwa kuvilazimisha viwe na viwanja vya mazoezi,viwe na ofisi,viajiri mtunza fedha,viwe na youth programme nk
 
Hivi sisi wana-Kagera tusio wahaya tulishirikishwaje katika kuchagua jina la timu ya mkoa nasema hivi kwa sababu according to you jina lipo kihaya inaelekea hali-represent wana-kagera wote. Just concerns sio ukabila.
Pili sioni sababu ya kubadili jina la Taifa Stars sababu lipo kiswahili na kiswahili ndo kinachotuunganisha Watanzania (Bara na Visiwani) wote.
CC Malafyale

La Lweru eagles hilo nalo neno.Taifa cup ikirudi tutaliangalia,ila kumbuka timu ya mkoa wa shinyanga inaitwa IGEMBENSABO
 
Maelezo murua kama haya ndiyo huwa tunayakosa kutoka kwa watawala wetu!Umenieleza vyema na nimekuelewa na uwe unafanya hivi kila ukiulizwa na wala usichukulie maswali yetu kama chuki binafsi!
Chukua "like"yangu!

Thanks.
Liberia nao yamewakuta,jana kocha wao mpya ndo karipoti kambini.
 
La Lweru eagles hilo nalo neno.Taifa cup ikirudi tutaliangalia,ila kumbuka timu ya mkoa wa shinyanga inaitwa IGEMBENSABO

Kwa hili nakusaidia;nadhani mikoa mingi ilichukua majina yao kutokana na kabila kubwa ktk mkoa wao!Sisi team yetu ya Mbeya inajulikana kama "BANYAMBALA" yaani mwanamme wa shoka,typical from my nyakyusa vernacular ambalo ndiyo kabila kubwa Mbeya!
 
CAF kwa sasa wanasisitiza tuanze utekelezaji wa kanuni ya club licencing,hasa kwa vilabu vinavyoshiriki champions league na confederation cup Africa.Muda ukifika tuta comply kwa vilabu visivyocheza Africa championship.
Club licencing regulation lengo lake ni kuboresha uendeshaji wa vilabu vyetu kwa kuvilazimisha viwe na viwanja vya mazoezi,viwe na ofisi,viajiri mtunza fedha,viwe na youth programme nk

Siku hii kanuni ikianza kutumika Tanzania naacha kushabikia Mpira wa Ulaya na kuhamia wa ndani..Hatuna wachezaji nje ya nchi,Club zetu haziendeshwi Kisasa..Timu bora ya Taifa itatoka wp??
TUTAKUKUMBUSHA JUU YA HILI SUALA HAPO MBELENI...
PILI; Ndugu Rais kuna hili suala la Diaspora..Naona Taasisi unayoongoza ipo kimya sana na ni moja kati ya waathirika wakubwa...Mfano kuna kijana wetu Nditi yupo UK (CHELSEA) Ilikuwa ni wakati wenu kama wadau wa Mpira kulipigia kelele suala la Uraia Pacha hususani kipindi hiki cha katiba ili Tuweze kunufaika nalo...
Tumueni ushawishi mlionao kuishauri serikali juu ya Faida tutakazozipata kupitia Mpira...
 
La Lweru eagles hilo nalo neno.Taifa cup ikirudi tutaliangalia,ila kumbuka timu ya mkoa wa shinyanga inaitwa IGEMBENSABO

Timu ya mkoa wa Shinyanga hainihusu,natoka Kagera. Let watu watokao Shinyanga wasio Wasukuma walalamikie hilo jina. BTW sijawahi kusikia kabila lingine originally toka mkoa wa Shinyanga zaidi ya wasukuma. Anyway, ili kuonyesha ukomavu wako katika nyanja za uongozi nakushauri ujiudhuru madaraka ya KRFA. Kuwa Rais wa KRFA na TFF wakati mmoja ni kuleta conflict of interests zisizo na mpango vile vile kuendelea kuchafua jina la Kagera na watu wake(regardless ya makabila).
 
La Lweru eagles hilo nalo neno.Taifa cup ikirudi tutaliangalia,ila kumbuka timu ya mkoa wa shinyanga inaitwa IGEMBENSABO

Mkuu hujajibu ni sababu au kanuni zipi ambazo TFF imetumia katika suala la Domayo ku-sign Azam iliyopeleka wewe kama Rais kuajiri lawyer kuchunguza hilo suala.je ni kosa kisheria mchezaji kusajiliwa akiwa timu ya taifa? Je tutaamini vp kwamba hujaongozwa na mahaba yako binafsi kwa maana ya conflict of interest since you are Yanga member ?
 
Kaka Jamal; sasa nafasi ya #122 au sivyo?
Mkakati ungefanywa angalau timu ifike # 100 alaf mambo mengine yazungumzwe wakati huo.
Kwa sasa punguzeni kufanya majaribio na team ya taifa. Mpira wa timu ya taifa ni matokeo ya muda mfupi. RAha ya mashabiki ni ushindi.
Kinyume na hapo timu itakosa support!

Mwacheni kocha achague wachezaji 'the best' for the job.
Haiwezekani mtu anawekwa benchi kwenye yake; akija timu ya taifa anapata namba.
let's be serious kidogo.

Aliyekutangulia amewahi kuifikisha hii timu karibu na #100.
Be focused. mambo mengine mtafanya muda ukiruhusu. Kwa sasa irudishe 'timu' #100.🙂
Unategemea 100% perfection katika uongozi wa Malinzi? Duniani humu hakuna kiongozi ambaye ni mkamilifu assilimia mia.We always try our best,kikubwa ni kuwa na nia thabiti na ujasiri wa kutoa maamuzi unayoamini ni sahihi.
 
sasa JAMAL MALINZI huku ndiko unapaswa kuelekea;
mambo ya majaribio tupunguze: Timu ikae pamoja muda mrefu, itazoea kucheza kwa pattern fulani. Kama mnafanya maboresho mnaboresha kidogo kidogo.

huwezi kuongeza wacheza 10 kwa wakati mmoja. inavuruga pattern ya timu.
MIFANO:

Brazil iliyocheza kombe la Mabara na Brazil iliyoteuliwa juzi ni ileile.
Hispania imeendelea kuwa ileile: Xavi, Iniesta, Fabregas, Ramos, Cassilas, Pique, ..huwezi kuona wanabadili timu nzima. Hiyo itasaidia kuwa na 'stability' kwenye timu.
🙂
timu ya taifa ni tofauti na klabu.
mzee Ndolanga mchango wake kwenye mpira wa Tanzania ni mkubwa na ninamuheshimu sana.Kumbuka pamoja na kutokuwa na udhamini kwenye 90's Tanzania ilifikia namba 65 kwenye FIFA rankings.
 
Mh rais mpira wa Taifa stars na Zimbabwe unacheza mbeya hii n kulingana na taarifa zilizopatikana baada ya kufanyika ukaguzi kwenye uwanja wa sokoine mjini mbeya,labda unitoe mashaka nn hasa kigezo ulichotumia mh rais? Unahis timu ikicheza dar itakosa mapato kwa kuwa haina mvuto??
 
Mkuu hujajibu ni sababu au kanuni zipi ambazo TFF imetumia katika suala la Domayo ku-sign Azam iliyopeleka wewe kama Rais kuajiri lawyer kuchunguza hilo suala.je ni kosa kisheria mchezaji kusajiliwa akiwa timu ya taifa? Je tutaamini vp kwamba hujaongozwa na mahaba yako binafsi kwa maana ya conflict of interest since you are Yanga member ?

born again pagan kinachogomba hapa sio usajili wa mchezaji (hilo ni suala la players status commitee) na muda wa kushughulikia usajili bado,kinachochunguzwa na wakili ni kwamba je kulikuwa na ukiukwaji wa miiko ya maadili ya National Team camp? Ni hilo tu.
 
Last edited by a moderator:
sasa JAMAL MALINZI huku ndiko unapaswa kuelekea;
mambo ya majaribio tupunguze: Timu ikae pamoja muda mrefu, itazoea kucheza kwa pattern fulani. Kama mnafanya maboresho mnaboresha kidogo kidogo.

huwezi kuongeza wacheza 10 kwa wakati mmoja. inavuruga pattern ya timu.
MIFANO:

Brazil iliyocheza kombe la Mabara na Brazil iliyoteuliwa juzi ni ileile.
Hispania imeendelea kuwa ileile: Xavi, Iniesta, Fabregas, Ramos, Cassilas, Pique, ..huwezi kuona wanabadili timu nzima. Hiyo itasaidia kuwa na 'stability' kwenye timu.
🙂
timu ya taifa ni tofauti na klabu.

Nakubaliana na wewe,mwalimu Nooij atalizungumzia na kuelezea mkakati wake wa uboreshaji timu na uendelezaji wa vipaji vilivyoibuliwa.
 
Mh rais mpira wa Taifa stars na Zimbabwe unacheza mbeya hii n kulingana na taarifa zilizopatikana baada ya kufanyika ukaguzi kwenye uwanja wa sokoine mjini mbeya,labda unitoe mashaka nn hasa kigezo ulichotumia mh rais? Unahis timu ikicheza dar itakosa mapato kwa kuwa haina mvuto??

TFF haijatangaza Tanzania vs Zimbabwe itafanyika wapi,maandalizi yakikamilika tutasema
 
Kaka Jamal; sasa nafasi ya #122 au sivyo?
Mkakati ungefanywa angalau timu ifike # 100 alaf mambo mengine yazungumzwe wakati huo.
Kwa sasa punguzeni kufanya majaribio na team ya taifa. Mpira wa timu ya taifa ni matokeo ya muda mfupi. RAha ya mashabiki ni ushindi.
Kinyume na hapo timu itakosa support!

Mwacheni kocha achague wachezaji 'the best' for the job.
Haiwezekani mtu anawekwa benchi kwenye yake; akija timu ya taifa anapata namba.
let's be serious kidogo.

Aliyekutangulia amewahi kuifikisha hii timu karibu na #100.
Be focused. mambo mengine mtafanya muda ukiruhusu. Kwa sasa irudishe 'timu' #100.🙂

performance ya Kiemba uliiona mechi ya Malawi?
Mwalimu ana mamlaka kamili na timu,tumwache afanye kazi yake
 
born again pagan kinachogomba hapa sio usajili wa mchezaji (hilo ni suala la players status commitee) na muda wa kushughulikia usajili bado,kinachochunguzwa na wakili ni kwamba je kulikuwa na ukiukwaji wa miiko ya maadili ya National Team camp? Ni hilo tu.

Na tusubiri matokeo ya uchunguzi wa wakili na adhabu itakayotolewa kama ni kwa player au timu (Azam).
 
Last edited by a moderator:
Hivi ni lazima kila kitu kibadilike hata mechi muhimu kama ya zimbabwe mnataka ichezwe mbeya?
Nimemsika manager wa timu kituo kimoja charadio akisema mngependa ichezwe mbeya kisa timu ipo kambini mbeya na hali ya hewa ni baridi mngependa wacheze mbeya hapa mnachemka rudisheni mechi dar
 
Back
Top Bottom