Maswali ninayojiuliza kwenye huu mgogoro wa DRC

Maswali ninayojiuliza kwenye huu mgogoro wa DRC

Kwa miaka ya karibuni Rwanda vs Burundi ...Rwanda imetulia kwa kiasi chake.

Anzia miaka ya mwishoni mwa 90 hadi sasa......labda kama umepitwa hapo karibuni.

Kutulia kisiasa kuna jumuisha.
1. Ulinzi wa nchi
2. Kutokuwa na vita ya wenyewe kwa wenyewe
3. Kukuza uchumi n.k
Nimekuuliza swali nijibu. Kama Rwanda imetulia FDRL wako wapi? Je kuna kikundi chochote cha uasi Burundi?
 
Je, suala la Watutsi wanaoishi mpakani na Congo kuilalamikia serikali nalo tulipuuze?
Jiulize wamasai wa Ngorongoro walihanishwa lakini halikutoka tamko la Kenya wala Ethiopia kuonesha "Masaaiiis solidarity"

Kwa nini Kagame awe invested na watutsi wa Congo ilhali kuna burundi ambao wapo karibu zaidi with the same ethnicity?....

Ni issue ya ubaguzi tu ya watutsi wa Congo au kuna la zaidi kwenye frame
 
Hapo Goma haugombaniwi uraia, ni madini ndo yanagombaniwa..!!
Kungekuwa hakuna madini kila raia angerudi kwenye nchi yake..!

Hata wewe huo usomali unaopewa ungeufurahia km Somalia kusingekuwa na vita..!! Lazima ushtuke na ukasirike coz unajua watakuchukulia km gaidi.. sidhani km Somalia kungekuwa na amani na nchi nzuri ya kuishi ungebaki bongo….!!
Nisingeutamani Usomali maana mimi sio msomali..... vizazi viwili vizaliwa Tanzania.... nimeoga Mila na desturi za kitanzania.

I don't know how to explain this.... upendo wa nchi hauna uhusiano na rasilimali wala vita....ni feeling isiyoelezeeka. Nimeishi nje ya Tanzania miaka kibao na ndani ya nchi iliyoendelea kuliko Tanzania ila sijawahi kuwa na feelings niliyonayo kwa Tanzania.

Haijalishi familia yako inaumaskini wa namna gani hata ukiishi kwa tajiri Namba moja duniani...mapenzi uliyonayo kwa Familia yako ya damu hayaelezeki.
 
Nisingeutamani Usomali maana mimi sio msomali..... vizazi viwili vizaliwa Tanzania.... nimeoga Mila na desturi za kitanzania.

I don't know how to explain this.... upendo wa nchi hauna uhusiano na rasilimali wala vita....ni feeling isiyoelezeeka. Nimeishi nje ya Tanzania miaka kibao na ndani ya nchi iliyoendelea kuliko Tanzania ila sijawahi kuwa na feelings niliyonayo kwa Tanzania.

Haijalishi familia yako inaumaskini wa namna gani hata ukiishi kwa tajiri Namba moja duniani...mapenzi uliyonayo kwa Familia yako ya damu hayaelezeki.
Unaongea hayo yote sababu Tanzania kuna amani..!!
Vipi ungekuwa na vinasaba na USA?

Okay, nimekuelewa una moyo wa upendo sana na familia yako..!!
 
Unaongea hayo yote sababu Tanzania kuna amani..!!
Vipi ungekuwa na vinasaba na USA?

Okay, nimekuelewa una moyo wa upendo sana na familia yako..!!
Utaipenda tu USA kwasababu inakupa pesa na afadhali ya maisha. Ila kindakindaki kamoyo Kako kana kumbuka madhila ya Bongo.

Huoni wabongo kibao wanaoishi USA wanavyochangia mijadala hapa jukwaani? Wanauchungu na nchi zaidi ya waliopo nyumbani.
Ukiwa mbali na nchi yako unaimiss na maumivu yake ni kama ya X aliyekuacha bila kavita....hujui kama ni moyo au bandama linauma ila maumivu unayaskia.
 
1.Watsi wanachikifanya ni kama anchokifanya Israel dhidi ya Palestine,watsi akiwemo Kagame ni wahamiaji kutoka Ethipians ndio maana unaona huu ukanda wote hao watsi ndio wana maumbi na sura tofauti.
2.Walijatawalia maeno huko kongo iliyopo jirani na rwanda na kuanzisha makazi.
3.M23 ni wabaki ya wapiganaji wa kagame aliokuwa nao huko Uganda,na badaye Kagame akawapandikiza huko Kongo kwa lengo la kuvuna rasilimali.
4.Kabila mkubwa aliingia makubaliano na Paul Kagame na kuwatumia M23 kupindua Serikali ya Mobutu kwa ahadi kuwa atawapa hayo maeno wanayoyakalia M23 yawe yao kisheria na kuwapa madaraka.Badaye Kabila Mkubwa hakufanya hivyo aliwapa vyeo lakini hakuwapa eneo-badaye Kagame akamu assassinate kabila.
5.Kagame anatumiwa na mataifa ya USA na Ulaya kuharibu amani ya kongo na kuiba rasilimali za kongo.

Kwa kuwa mgogoro huu unahusisha western countries,njia pekee ya kongo kutoka kwenye mgogoro kama huu ni kiongozi wao kuungana na Russia au ant-west countries na nchi iendeshwe kijeshi dawa ya moto ni moto.
umemsikia Trumph anasema mambo haya ya Congo ni makubwa sana bila kufafanua na kuwa haifai kuyazungumza kwa sasa. akamaliza. Hapa kuna kitu.
 
Zinapitia wapi?

Kagame hajawahi kujibu swali la kutowasaidia waasi moja kwa moja....! Uso humbadilika.
Containers za silaha za M23 hupitia bandari za Dar es Salaam na Mombasa, hivi huwa wanasemaje kuhusu hilo.
 
Nadhani Kagame anawapa ufadhili wa silaha na wanajeshi ili kumsaidia Mtutsi mwenzake anayebaguliwa Congo.

Pia Nadhani, anawapa msaada waasi kwasababu Congo iliwaunga mkono waasi wa kihutu. Unaiunga mkono FDLR basi Nami nitawaunga mkono M23.

Sasa kama Kama ni kweli Rwanda inahusika
1. Kwanini hatuoni vijana wa kikongoko wakiipigania nchi Yao kwa kufa na kupona? Morale ya vita sio silaha au miundombinu bora bali cha kwanza ni ule munkari wa watu kujitolea kufa na kupona....kwanini Wacongo hawana hili???

2. Au ambayo yamekuwa yanalalamikiwa na M23 ndiyo yanayopitiwa na Wacongo wote?

3. Kwanini Kabila yupo kimya? Anamkono gani kwenye hili. Kumbuka makubaliano yake na Hawa waasi March 2009.

4. Je, Nangaa ni mtutsi?
Hakuna hisia mbaya kama za kukataliwa na nchi yako. MTUTSI ambaye vizazi na vizazi vimezaliwa Congo Kisha serikali inamwambia sio Mcongomani kisa tu anazungumza Kinyarwanda.

Mfano mdogo: Mimi Mama mzaa bibi yangu ni Msomali. Simfahamu hata.

Kwa muonekano ukiniona tu japo hadi uwe mdadisi utagundua ninavinasaba vya Kisomali. Lakini mimi sio msomali na hata sipajui.

Mara nyingi nikikutana na wale wabongo wajuaji wananiambia wewe sio mtanzania. Huwa najiskia Vibaya saana kila sehemu ya mwili wangu husisimka. Sasa huyo ni mtu baki....fikiria serikali iniambie hivyo...unafikiri nini kitafuata???
Mkuu, kiaje?

Kwa kuwa Nangaa katoa kauli (kwamba lengo ni kuchukua Kinshasa) basi ni kutokana na uelewa wake wa kilotokea mwaka 2018 kwenye uchaguzi.

Mashine za kupigia kura 8000 ziliungua moto zote kwenye ile bohari zilikohifadhiwa na baadae kukawa na makubaliano (fulani) kati ya Kabila na Tsisekedi. ina uhakika wa asilimia 110 kwamba Rwanda Intel wanafahamu yale yote yalotokea 2018 na makubaliano yote kati ya Kabila na Tshisekedi.

Hivyo tusijeshangaa yakatokea yalotokea kwa Kabila Senior.

Nangaa akisema wataelekea Kinshasa amaanisha kwamba akumbushia yale ya 2018.

Pia hata raisi Kagame lugha na kauli kuhusu Tshisekedi zaashiria kuwa kuna mpango kabambe na wakubwa wa Dunia watakuwa wamepewa "Brief" tayari kwamna what will come next na ni kwa kiwango gani.

Umeona jinsi jeshi la mamluki lilivyoshughulikiwa na pia wengi wa askari wa Congo DRC wamejisalimisha, hii ni ishara tosha kwamba "disarmament" ipo kwenye process kabla ya major push.
 
1. Lakini jamii nyingi zimehamia maziwa makuu kutokea sehemu tofauti tofauti. Huyu Mtutsi hakuwa hapo kabla ya uhuru wa Congo? Huyu ni raia wa wa wawapi sasa?

2. Historia inapingana kidogo na wewe....Watutsi wapo Mashariki mwa Congo kabla hata ya ukoloni. Koloni la Mbelgiji liliwatumia watutsi na kuwapa vyeo huku ndiko kuliwafanya watutsi kujiona bora kuliko makabila mengine.

Ni kweli Kagame atakuwa ametake advantage na kutumia mgogoro wa Watutsi na Serikali ya Congo kama fursa....lakini kwanini tuwakatae wamasai na tuseme ni wakenya kisa tu wanavinasaba vya kimasai?
Isitoshe ni Wabelgiji ndo waloamua kuwapa kipaumbele Watutsi kwa kuangalia uwezo wao wa akili na hata kupima pua zao na urefu wao, waliwahusudu sana hawa Watutsi na ndo ukawa mwanzo wa Watutsi kutawala eneo hilo khasa kijeshi.
 
Nadhani Kagame anawapa ufadhili wa silaha na wanajeshi ili kumsaidia Mtutsi mwenzake anayebaguliwa Congo.

Pia Nadhani, anawapa msaada waasi kwasababu Congo iliwaunga mkono waasi wa kihutu. Unaiunga mkono FDLR basi Nami nitawaunga mkono M23.

Sasa kama Kama ni kweli Rwanda inahusika
1. Kwanini hatuoni vijana wa kikongoko wakiipigania nchi Yao kwa kufa na kupona? Morale ya vita sio silaha au miundombinu bora bali cha kwanza ni ule munkari wa watu kujitolea kufa na kupona....kwanini Wacongo hawana hili???

2. Au ambayo yamekuwa yanalalamikiwa na M23 ndiyo yanayopitiwa na Wacongo wote?

3. Kwanini Kabila yupo kimya? Anamkono gani kwenye hili. Kumbuka makubaliano yake na Hawa waasi March 2009.

4. Je, Nangaa ni mtutsi?
Hakuna hisia mbaya kama za kukataliwa na nchi yako. MTUTSI ambaye vizazi na vizazi vimezaliwa Congo Kisha serikali inamwambia sio Mcongomani kisa tu anazungumza Kinyarwanda.

Mfano mdogo: Mimi Mama mzaa bibi yangu ni Msomali. Simfahamu hata.

Kwa muonekano ukiniona tu japo hadi uwe mdadisi utagundua ninavinasaba vya Kisomali. Lakini mimi sio msomali na hata sipajui.

Mara nyingi nikikutana na wale wabongo wajuaji wananiambia wewe sio mtanzania. Huwa najiskia Vibaya saana kila sehemu ya mwili wangu husisimka. Sasa huyo ni mtu baki....fikiria serikali iniambie hivyo...unafikiri nini kitafuata???
Vipi zile elements za asira,visasi na kujiona waarabu na sio waafrica ulirithi pia? Maana wasomali ukiwaona utasema wema kumbe,..............!!!!????
 
Zinapitia wapi?

Kagame hajawahi kujibu swali la kutowasaidia waasi moja kwa moja....! Uso humbadilika.
Mi si mwanasiasa, lakini nakujibu kwa mfano hai: Russia wakati inaanza vita na Ukraine, kila mtu aliamini haitakaa hata wiki kabla Russia haijaiponda Ukraine. Mpaka leo hii, ni vuta nikuvute. Lakini, hatimae, ukweli ulijulikana, na hakika Russia inapigana na USA, na EU. Russia ingekuwa ya kawaida, tayari.
Sasa kwa hili, kabla ya kujiuliza swali hilo, anzia kwenye historia ya miaka ya 1885. Miaka zaidi ya 200 ni kipindi kirefu sana. Kumbuka watu wanafarijiana, wanaoana na kuzaliana. Hivyo unajikuta mtu sehemu moja ameshapata ukoo sehemu nyingine. Jiulize, wanauliwa wakwe labda mkoa x. Utakaa kimya!?
Mimi(ni kwa uelewa wangu si kwa uhalisia wa kidiplomasia au kisiasa):

-uwezekano wa kuungwa mkono upo. Ila tatizo la huu mgogoro ambalo baso linawachanganya vichwa watu, ni kwamba wanyarwanda wa Congo na wa Rwanda, asilimia kubwa yao, ni lugha moja. Hivyo, kumtambua mtu wa M23 umtofautishe na wa Rwanda, ni jambo lisilowezekana. Ndio maana, wanaosema yawepo mazungumzo ya amani, ndo naona wana tija.

- wanyarwanda wa Congo(kumbuka ni mchanganyiko wa wahutu na watutsi). Baada ya migogoro hiyo, wengi wao waliweza kupata visa permanent nchi za nje. Diaspora yao, hakika inafadhili pakubwa. Tofauti yao na watu wengine, hawa watu wana upendo wa dhati kati yao. Hivyo kuumia alipo lakini asaidia kutafutia wenzake amani, lazima.

-Kama ilivyo kwa makundi mengine, haiwezekani M23 isimiliki machimbo. Tunalishwa tu matango, lakini kwenye biashara, tutadanganyana. Hakunaga uadui. Pesa ipo, wanaokufa watajua wenyewe, we nipe mzigo na mi nikupe pesa.

-Viwanda vingi, vilipiga marufuku kununua madini ya ukanda wa mashariki mwa DRC kutokana na mzozo huo. Majuzi serikali ya DRC, iliishitaki apple. Je, unadhani watu watafunga viwanda vyao kisa vita!? Haiwezekani. Na siraha mkitaka mtapata, kikubwa yeye apate mzigo, aendeshe viwanda vyake.

-Watutsi na Wahutu, kiuhalisia si makabila kama ilivyo kwa jamii nyingine duniani ukiondoa tu Rwanda na Burundi. Hivyo, watu wa Congo huko, baada ya wanajeshi wa serikali iliyoondolewa mwaka 1994, na waliouwa watutsi, walimuinda kila anaeitwa mtutsi ili auwawe nae. Kumbuka, haya makabila mara nyingi hutambulika tu kimaumbile. Hivyo, kuna wengine walipoteza maisha pasi na kuwa watutsi hao.

- ni nadra sana kwa mwanajeshi kuamini kama kweli ameshindwa. Atakufa na mipango akilini ya kurudi alikokuwa. Baada ya miaka yote hiyo, waliohusika na mauaji au na wanajeshi hao, hawapo tena. Watoto waliozaliwa mapolini huko, leo hii ndo wapiganaji. Walishaambiwa characteristics za mtutsi. Wanajua akikuwahi anakuua. Kwa hiyo wao ndo huhakikisha wanamuua.
Hawa watu(wahutu au FDLR), wao wana siraha. Kuua na kupora mifugo ni kugusa.

-Hii jamii, kabla ya miaka ya 1994, ilikuwa sawa na jamii nyingine nchini, hivyo jeshini walipokelewa. Ambao kwa sasa, wengi wao wana vyeo vya juu jeshini. Wengi wao waliamua kujitenga na serikali, na kuanzisha makundi yao ya kujihami. Baada ya kuamua kujiunga na kuwa M23, ni kundi lenye uzoefu wa kijeshi. DRC hasa mashariki, ni mapoli. Hivyo mafunzo ni rahisi kupata. Kupata warimu wa kijeshi kimataifa, halikuwa jambo gumu, kikubwa pesa wanapata. Hapa jambo la kujiuliza tu litakuwa siraha zinawafikiaje. Lakini mwanajeshi ni mwanajeshi na ana mbinu zake.
Kupeleka watu kujifunza, ni kazi ndogo.

-Leo hii ukiangalia arsenal ya siraha walizopola serikali, huwezi amini. Na kila aina ya siraha, kuna watu wanajua kuzitumia. Hii ina maana zilizotoka china, hakika kuna watu walijifunza huko au wengine waliletewa wataalam wa kuwafundisha. Russia hivo hivo, na mataifa mengine yanayotengeneza silaha.
Kwa hiyo, wakikamata silaha 10, wakasema zimepatikana 1000, utakubali. Nani ataenda kuhakikisha!? Na kumbuka, vitani kila silaha uliyoweza kupola, ni mali yako.

Je, mfano, SADC na wengine nani aliekubali kuwa vitani na M23!!! Lakini mwishoe wote wameumbuka.

Kwa kuhitimisha, vita bya Congo viangaliwe kwa masirahi ya mataifa makubwa pia. Kama yanapata chochote, kuuwana kwa watu si shida kwa wanaojitaji mali. Isimgelikuwa hivyo, huu mzozo usingekuwepo.
 
1.Watsi wanachikifanya ni kama anchokifanya Israel dhidi ya Palestine,watsi akiwemo Kagame ni wahamiaji kutoka Ethipians ndio maana unaona huu ukanda wote hao watsi ndio wana maumbi na sura tofauti.
2.Walijatawalia maeno huko kongo iliyopo jirani na rwanda na kuanzisha makazi.
3.M23 ni wabaki ya wapiganaji wa kagame aliokuwa nao huko Uganda,na badaye Kagame akawapandikiza huko Kongo kwa lengo la kuvuna rasilimali.
4.Kabila mkubwa aliingia makubaliano na Paul Kagame na kuwatumia M23 kupindua Serikali ya Mobutu kwa ahadi kuwa atawapa hayo maeno wanayoyakalia M23 yawe yao kisheria na kuwapa madaraka.Badaye Kabila Mkubwa hakufanya hivyo aliwapa vyeo lakini hakuwapa eneo-badaye Kagame akamu assassinate kabila.
5.Kagame anatumiwa na mataifa ya USA na Ulaya kuharibu amani ya kongo na kuiba rasilimali za kongo.

Kwa kuwa mgogoro huu unahusisha western countries,njia pekee ya kongo kutoka kwenye mgogoro kama huu ni kiongozi wao kuungana na Russia au ant-west countries na nchi iendeshwe kijeshi dawa ya moto ni moto.
Kwa hiyo Russia wao hawaitaji madini na hawana kazi huko kwao mpaka waje wawalinde wakongo man wao wakae tu kukatika viuno si ndio hivyo mkuu?
 
Utaipenda tu USA kwasababu inakupa pesa na afadhali ya maisha. Ila kindakindaki kamoyo Kako kana kumbuka madhila ya Bongo.

Huoni wabongo kibao wanaoishi USA wanavyochangia mijadala hapa jukwaani? Wanauchungu na nchi zaidi ya waliopo nyumbani.
Ukiwa mbali na nchi yako unaimiss na maumivu yake ni kama ya X aliyekuacha bila kavita....hujui kama ni moyo au bandama linauma ila maumivu unayaskia.
Umeongea vizuri D ulivyofika kwa X nimeacha kusoma 😔😥😹😹
 
Zinapitia wapi?

Kagame hajawahi kujibu swali la kutowasaidia waasi moja kwa moja....! Uso humbadilika.

..silaha zao zinaweza kuwa na njia zifuatazo.

1. Dsm Kigali Congo.

2 Dsm Kampala Congo.

3.Mombasa Kigali Congo.

4.Mombasa Kampala Congo.
 
1.Watsi wanachikifanya ni kama anchokifanya Israel dhidi ya Palestine,watsi akiwemo Kagame ni wahamiaji kutoka Ethipians ndio maana unaona huu ukanda wote hao watsi ndio wana maumbi na sura tofauti.
2.Walijatawalia maeno huko kongo iliyopo jirani na rwanda na kuanzisha makazi.
3.M23 ni wabaki ya wapiganaji wa kagame aliokuwa nao huko Uganda,na badaye Kagame akawapandikiza huko Kongo kwa lengo la kuvuna rasilimali.
4.Kabila mkubwa aliingia makubaliano na Paul Kagame na kuwatumia M23 kupindua Serikali ya Mobutu kwa ahadi kuwa atawapa hayo maeno wanayoyakalia M23 yawe yao kisheria na kuwapa madaraka.Badaye Kabila Mkubwa hakufanya hivyo aliwapa vyeo lakini hakuwapa eneo-badaye Kagame akamu assassinate kabila.
5.Kagame anatumiwa na mataifa ya USA na Ulaya kuharibu amani ya kongo na kuiba rasilimali za kongo.

Kwa kuwa mgogoro huu unahusisha western countries,njia pekee ya kongo kutoka kwenye mgogoro kama huu ni kiongozi wao kuungana na Russia au ant-west countries na nchi iendeshwe kijeshi dawa ya moto ni moto.
Watusi ni Wabantu, chanzo cha wabantu na Africa ya kati. Hakuna Wabantu Ethiopia.
 
Nadhani Kagame anawapa ufadhili wa silaha na wanajeshi ili kumsaidia Mtutsi mwenzake anayebaguliwa Congo.

Pia Nadhani, anawapa msaada waasi kwasababu Congo iliwaunga mkono waasi wa kihutu. Unaiunga mkono FDLR basi Nami nitawaunga mkono M23.

Sasa kama Kama ni kweli Rwanda inahusika
1. Kwanini hatuoni vijana wa kikongoko wakiipigania nchi Yao kwa kufa na kupona? Morale ya vita sio silaha au miundombinu bora bali cha kwanza ni ule munkari wa watu kujitolea kufa na kupona....kwanini Wacongo hawana hili???

2. Au ambayo yamekuwa yanalalamikiwa na M23 ndiyo yanayopitiwa na Wacongo wote?

3. Kwanini Kabila yupo kimya? Anamkono gani kwenye hili. Kumbuka makubaliano yake na Hawa waasi March 2009.

4. Je, Nangaa ni mtutsi?
Hakuna hisia mbaya kama za kukataliwa na nchi yako. MTUTSI ambaye vizazi na vizazi vimezaliwa Congo Kisha serikali inamwambia sio Mcongomani kisa tu anazungumza Kinyarwanda.

Mfano mdogo: Mimi Mama mzaa bibi yangu ni Msomali. Simfahamu hata.

Kwa muonekano ukiniona tu japo hadi uwe mdadisi utagundua ninavinasaba vya Kisomali. Lakini mimi sio msomali na hata sipajui.

Mara nyingi nikikutana na wale wabongo wajuaji wananiambia wewe sio mtanzania. Huwa najiskia Vibaya saana kila sehemu ya mwili wangu husisimka. Sasa huyo ni mtu baki....fikiria serikali iniambie hivyo...unafikiri nini kitafuata???
Jambo jengine Rwanda na Umoja wa Ulaya wamesign deal la Madini, Umoja Wa Ulaya utanunua Madini muhimu ya ku power Green technologies, ila hayo Madini Rwanda Hana yapo Kongo, sasa jiulize kwanini kuna huo mkataba na Rwanda atayatoa wapi kama sio kuteka maeneo yanapozalishwa.

 
Jambo jengine Rwanda na Umoja wa Ulaya wamesign deal la Madini, Umoja Wa Ulaya utanunua Madini muhimu ya ku power Green technologies, ila hayo Madini Rwanda Hana yapo Kongo, sasa jiulize kwanini kuna huo mkataba na Rwanda atayatoa wapi kama sio kuteka maeneo yanapozalishwa.

UONGO,
Glencore ni kampuni la Ulaya na linachimba madini kwa kibali cha serikali ya Congo.
Ivanhoe Mines ya Canada inachimba madini ya Congo kwa kushirikia na South Africa kwa kibali cha serikali ya Congo
AngloGold Ashanti ya South Africa wanachimba madini Congo.
 
UONGO,
Glencore ni kampuni la Ulaya na linachimba madini kwa kibali cha serikali ya Congo.
Ivanhoe Mines ya Canada inachimba madini ya Congo kwa kushirikia na South Africa kwa kibali cha serikali ya Congo
Hii website ya EU ikireport same thing


So mpaka EU wenyewe waliosaini huo mkataba ni waongo?

Mahaba Niue.
 
20250201_022655.jpg
 
Ila kwanini Watutsi wanabaguliwa/wanaona wanabaguliwa kila sehemu waishio? Labda tatizo ni wao!!!!!
Nayo yaweza kuwa propaganda. Wenye asili ya kitusi wamekuwemo kwenye serekali karibia zote za Congo kwenye nyadhifa mbalimbali za juu.
 
Back
Top Bottom