Maswali yote kuhusu mechi ya Simba kuchezwa saa 4 usiku asiachiwe Ahamed Ally kuyajibu

Maswali yote kuhusu mechi ya Simba kuchezwa saa 4 usiku asiachiwe Ahamed Ally kuyajibu

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Mechi kati Simba vs US Gendamarie itachezwa saa 4 usiku siku ya jumapili kuamkia jumatatu siku ya kazi.

Hii ni mara yetu ya kwanza kuwa na kitu kama hiki nchini kwetu. Inafahamika kuwa Uwanja wa Mkapa uko pembeni mwa jiji hasa kwa watu wanaotoka Ilala, Kinondoni, Ubungo, Kawe, Bagamoyo, Kibaha, Kisarawe, Mlandizi na sehemu nyingine nchini.

Inafahamika kuwa maeneo yale ya Keko, Tandika, Mbagala na vitongoji vinavyouzunguuka uwaja kuna vibaka wengi hata siku za kawaida tu mchana sembuse usiku wa saa 6? Hawa ni watu ambao wanapora, wanachomoa mifukoni, ndani ya magari na hata vifaa vya magari kama taa, power window, rims, redio, nk.

Inafahamika pia usafiri wa umma kwenye routes zote ndani ya jiji na vitongoji vyake haufiki saa 6 usiku, na hata kama utalazimisha ufike saa 6 usiku basi utahangaika na madereva waliochoka sana wenye usingizi, au sivyo madaladala yataendeshwa na madei waka na kusababisha ajali.

Hivyo uhakikisho wa usalama wa watanzania watakaokwenda kutizama mechi saa 4 usiku na kutoka saa 7 usiku ni vizuri utolewe na serikali kupitia waziri wa michezo, mambo ya ndani, Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya Temeke, IGP, RPC na kiongozi wa umoja wa madaladala Dar badala ya kuachiwa Simba kupitia msemaji wao Ahmed Ally kusema ooooh usalama utakuwepo, oooo usafiri mpaka kibaha utakuwepo, oooo msiwe na hofu, oooo hivi oo vile.

Ni vizuri watu wakashauriwa wale ambao hawana usafiri binafsi wakachanga kukodi magari kwa bei ya makubaliano ili wawe na uhakika wa kuja na kuondoka na usafiri wao bila kulazimika kugombania magari ambayo obvious yatakuwa machache sana, baadhi ya maeneo hayatakuwa na usafiri kabisa. Na vibaka wanapendelea sana watu wanapokuwa kwenye msongamano wa kugombea kuingia uwanjani au kwenye magari. Badala ya Ahmed kuwaaminisha yeye watu kuwa usalama na usafiri utakuwa wa kutosha ni heri tu kuwaambia ukweli watu waangalie mechi kwenye luninga zao nyumbani na vibanda umiza.
 
IMETUMIKA SIASA KUBWA SANA BAADA YA KUCHUKUA HELA ZA VIINGILIO WANAKUJA NA KAULI NYEPESI SANA Kusema ooooh usalama utakuwepo, oooo usafiri mpaka kibaha utakuwepo, oooo msiwe na hofu, oooo hivi oo vile.

Magari yenyewe kwa usiku ule usitarajie nauli itakuwa 400, 500, 600 na 750 hizi tulizozoea, hapo ni kuanzia buku, 2000, 3000 hadi 5000 huko na mida hiyo watu wamechoka sana sijui umakini utakuwepo wa namna gani tena ndio bahati mbaya 'thimba atolewe" ndio kabisa mvurugano

Usalama utakaokuwepo sidhani kama utatosha na ndio maana nahofu watu wengi wataangalia majumbani au kwenye vibandaumiza kuliko kuchoma nauli na kiingilio hadi Taifa

Ukimuuliza msemaji barua ya makubaliano ya kubadili muda utaanzisha vita ingine😀
 
IMETUMIKA SIASA KUBWA SANA BAADA YA KUCHUKUA HELA ZA VIINGILIO WANAKUJA NA KAULI NYEPESI SANA Kusema ooooh usalama utakuwepo, oooo usafiri mpaka kibaha utakuwepo, oooo msiwe na hofu, oooo hivi oo vile.

Magari yenyewe kwa usiku ule usitarajie nauli itakuwa 400, 500, 600 na 750 hizi tulizozoea, hapo ni kuanzia buku, 2000, 3000 hadi 5000 huko na mida hiyo watu wamechoka sana sijui umakini utakuwepo wa namna gani tena ndio bahati mbaya 'thimba atolewe" ndio kabisa mvurugano

Usalama utakaokuwepo sidhani kama utatosha na ndio maana nahofu watu wengi wataangalia majumbani au kwenye vibandaumiza kuliko kuchoma nauli na kiingilio hadi Taifa

Ukimuuliza msemaji barua ya makubaliano ya kubadili muda utaanzisha vita ingine😀

Hakuna barua, mechi za mwisho lazima zichezwe muda mpya ili kupunguza nafasi ya kupanga matokeo. Muda waliocheza simba na waarabu ndio huo huo siku iyo tutaangalia kwa hapa bongo
 
IMETUMIKA SIASA KUBWA SANA BAADA YA KUCHUKUA HELA ZA VIINGILIO WANAKUJA NA KAULI NYEPESI SANA Kusema ooooh usalama utakuwepo, oooo usafiri mpaka kibaha utakuwepo, oooo msiwe na hofu, oooo hivi oo vile.

Magari yenyewe kwa usiku ule usitarajie nauli itakuwa 400, 500, 600 na 750 hizi tulizozoea, hapo ni kuanzia buku, 2000, 3000 hadi 5000 huko na mida hiyo watu wamechoka sana sijui umakini utakuwepo wa namna gani tena ndio bahati mbaya 'thimba atolewe" ndio kabisa mvurugano

Usalama utakaokuwepo sidhani kama utatosha na ndio maana nahofu watu wengi wataangalia majumbani au kwenye vibandaumiza kuliko kuchoma nauli na kiingilio hadi Taifa

Ukimuuliza msemaji barua ya makubaliano ya kubadili muda utaanzisha vita ingine😀
Kindiga
 
Kwa hiyo unachotaka kuuambia ulimwengu ni kwamba Tanzania siyo salama kwa watu kutembea usiku kuanzia saa 4?
 
Mechi kati Simba vs US Gendamarie itachezwa saa 4 usiku siku ya jumapili kuamkia jumatatu siku ya kazi.

Hii ni mara yetu ya kwanza kuwa na kitu kama hiki nchini kwetu. Inafahamika kuwa Uwanja wa Mkapa uko pembeni mwa jiji hasa kwa watu wanaotoka Ilala, Kinondoni, Ubungo, Kawe, Bagamoyo, Kibaha, Kisarawe, Mlandizi na sehemu nyingine nchini.

Inafahamika kuwa maeneo yale ya Keko, Tandika, Mbagala na vitongoji vinavyouzunguuka uwaja kuna vibaka wengi hata siku za kawaida tu mchana sembuse usiku wa saa 6? Hawa ni watu ambao wanapora, wanachomoa mifukoni, ndani ya magari na hata vifaa vya magari kama taa, power window, rims, redio, nk.

Inafahamika pia usafiri wa umma kwenye routes zote ndani ya jiji na vitongoji vyake haufiki saa 6 usiku, na hata kama utalazimisha ufike saa 6 usiku basi utahangaika na madereva waliochoka sana wenye usingizi, au sivyo madaladala yataendeshwa na madei waka na kusababisha ajali.

Hivyo uhakikisho wa usalama wa watanzania watakaokwenda kutizama mechi saa 4 usiku na kutoka saa 7 usiku ni vizuri utolewe na serikali kupitia waziri wa michezo, mambo ya ndani, Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya Temeke, IGP, RPC na kiongozi wa umoja wa madaladala Dar badala ya kuachiwa Simba kupitia msemaji wao Ahmed Ally kusema ooooh usalama utakuwepo, oooo usafiri mpaka kibaha utakuwepo, oooo msiwe na hofu, oooo hivi oo vile.

Ni vizuri watu wakashauriwa wale ambao hawana usafiri binafsi wakachanga kukodi magari kwa bei ya makubaliano ili wawe na uhakika wa kuja na kuondoka na usafiri wao bila kulazimika kugombania magari ambayo obvious yatakuwa machache sana, baadhi ya maeneo hayatakuwa na usafiri kabisa. Na vibaka wanapendelea sana watu wanapokuwa kwenye msongamano wa kugombea kuingia uwanjani au kwenye magari. Badala ya Ahmed kuwaaminisha yeye watu kuwa usalama na usafiri utakuwa wa kutosha ni heri tu kuwaambia ukweli watu waangalie mechi kwenye luninga zao nyumbani na vibanda umiza.
Mechi haikuhairishwa muda na Simba, imebadilishwa na CAF kuepusha match fixing. Ikumbukwe kuwa yeyote kwenye kundi anaweza kufuzu.
 
Mechi haikuhairishwa muda na Simba, imebadilishwa na CAF kuepusha match fixing. Ikumbukwe kuwa yeyote kwenye kundi anaweza kufuzu.
Ukiwa shabiki wa yanga akili kidogo inakuwa sio nzuri CAF wamesema kama ulivyoandika hvyo ila yanga wanavyotoa taarifa ya kuarisha mechi ni kama wapo Cairo vile.
 
Hivi ni lazima ukiwa shabiki wa Yanga uwe unabweka tu kama mbwa au kupiga kelele kama nyani? Huwa naona yanga kama kutoutoa mwiko nyuma kumewaathiri sana. Manara alisema wenye akili yanga ni wawili tu....nakubaliana naye
IMETUMIKA SIASA KUBWA SANA BAADA YA KUCHUKUA HELA ZA VIINGILIO WANAKUJA NA KAULI NYEPESI SANA Kusema ooooh usalama utakuwepo, oooo usafiri mpaka kibaha utakuwepo, oooo msiwe na hofu, oooo hivi oo vile.

Magari yenyewe kwa usiku ule usitarajie nauli itakuwa 400, 500, 600 na 750 hizi tulizozoea, hapo ni kuanzia buku, 2000, 3000 hadi 5000 huko na mida hiyo watu wamechoka sana sijui umakini utakuwepo wa namna gani tena ndio bahati mbaya 'thimba atolewe" ndio kabisa mvurugano

Usalama utakaokuwepo sidhani kama utatosha na ndio maana nahofu watu wengi wataangalia majumbani au kwenye vibandaumiza kuliko kuchoma nauli na kiingilio hadi Taifa

Ukimuuliza msemaji barua ya makubaliano ya kubadili muda utaanzisha vita ingine😀
V
 
Kwa hiyo unachotaka kuuambia ulimwengu ni kwamba Tanzania siyo salama kwa watu kutembea usiku kuanzia saa 4?
Vishandu wanapora mchana kweupe sembuse saa 7 usiku. Dalili kuu ya nchi au mtaa usio salama ni kuona kila nyumba Ina grill za chuma kuanzia madirisha mpaka milango.
 
Mechi haikuhairishwa muda na Simba, imebadilishwa na CAF kuepusha match fixing. Ikumbukwe kuwa yeyote kwenye kundi anaweza kufuzu.
Hatulalamiki mechi kuanza saa 4 usiku kwakuwa sababu za kuchezwa saa 4 usiku kwa saa za kwetu zinafahamika, bali tunachohofia ni usalama wa watazamaji na wadau wengine maeneo ya uwanja na huko kwao waendako kuhusu usafiri. Je nikienda na gari langu litalindwa?
 
Watu wa Dar mbona waoga hivyo mnawaogopa vibaka tena vibaka wenyewe ni mateja mtama mmoja anazinduka siku ya 3.
Njooni huku mikoAni daily tunapishana na simba, fisi, chui na wachawi kibao usiku wa manane tukitokea kwenye pombe na madisco.
Acheni kunangusha bwana wanadaslama nendeni mkamcheki mnyama hyo kesho.
 
Mechi haikuhairishwa muda na Simba, imebadilishwa na CAF kuepusha match fixing. Ikumbukwe kuwa yeyote kwenye kundi anaweza kufuzu.
Kwa kundi lilivyokaaa vile nani wa kufanya mtach fixing vitu vingine ni ujinga ....
 
Watu wa Dar mbona waoga hivyo mnawaogopa vibaka tena vibaka wenyewe ni mateja mtama mmoja anazinduka siku ya 3.
Njooni huku mikoAni daily tunapishana na simba, fisi, chui na wachawi kibao usiku wa manane tukitokea kwenye pombe na madisco.
Acheni kunangusha bwana wanadaslama nendeni mkamcheki mnyama hyo kesho.
Unasema huko hakuna panyaroad? Huku Kuna baiskeli tu huku kwetu hata watu wazima wanaokota chupa tupu za maji, bia, soda. Huku Kuna magari ya kawaida na ghari sana Lakini spea za wizi, wasiokiwa na kazi huku ni wengi kuliko huko, huku ukizubaa kidogo unashikishwa ukuta.
 
TFF iruhusu watu waingie na shuka zao kwa anaetaka kubaki kulala uwanjani baada ya mechi alale kwa usalama wake
 
Hatulalamiki mechi kuanza saa 4 usiku kwakuwa sababu za kuchezwa saa 4 usiku kwa saa za kwetu zinafahamika, bali tunachohofia ni usalama wa watazamaji na wadau wengine maeneo ya uwanja na huko kwao waendako kuhusu usafiri. Je nikienda na gari langu litalindwa?
Kwani Tanzania kuna waasi? Kuna vita? Nchi nyingine wanawezaje?
 
Huelewi mpira na unashabikia usivyovijua. Taarifa ikufikie kuwa yeyote anaweza kufuzu.
Nipe Scenerio zote za uvukaji wa kundi hili ... Katika Poisonous Probability distribution ni pale tu atakaposhinda akishinda Berkane..ndio wote wamepotea... Jikite na mdako....
 
Hakuna barua, mechi za mwisho lazima zichezwe muda mpya ili kupunguza nafasi ya kupanga matokeo. Muda waliocheza simba na waarabu ndio huo huo siku iyo tutaangalia kwa hapa bongo
Mbona champions League wamecheza jana na leo wanacheza?

Hakuna barua, mechi za mwisho lazima zichezwe muda mpya ili kupunguza nafasi ya kupanga matokeo. Muda waliocheza simba na waarabu ndio huo huo siku iyo tutaangalia kwa hapa bongo

Screenshot_2022-04-02-17-54-35-748_com.android.chrome.jpg
 
Back
Top Bottom