Matrillioni ya pesa yanayokusanywa na makampuni ya Bima kupitia mawakala wao ni za serikali au ni za nani?

Ni muda muafaka kodi ya ‘third party’ ianze kuwasilishwa serikalini
 
Biashara ya bima ni biashara Kama zingine ina faida na hasara. Wewe unasemea faida hujajua kwamba kuna malalamiko (claims) ambazo hulipwa na bima!!

Serikali ina NIC insurance, lakini haizuii makampuni mengine ya bima kukosa mapato,

Point yako haina mashiko
 
Tumeshajadili sana hiki kwenye uzi. Bima ya third party sio biashara kama biashara zingine, maana ni lazima (compulsory) , utake au usitake lazima ulipe. Tena wanaoifanya hii biashara ifanikiwa ni traffic police ambao nao wanalipwa kwa kodi za wanachi. Ninkama useme biashra anayofanya Tanesco ni biashara kama biashara zingine, sio kweli. Wewe utafanyabkazi kama wakala wa Tanesco tu, ila umeme lazima umpe Tanesco ndio asambaze. Hali kadhalika, mawakala wakusamye tu hizi pesa za third party kwa niaba ya serikalinna wachukue commission zao tu, ila pesa ziwasilishwe serikalini.

Pili ni ngumu sana kwa third party kuja kufanya claim, wengi huamua kumalizana na waliemwaribia mali yake ili kuepuka jail time, mwisho wa siku hii kodi inaishia mifukoni mwa wahindi tu. Hivyo ni vyema hii kodi iemde serikalini, kisha kama kutakuwa na third party claim yeyote, NIC itakuwa ikitengea kafungu kidogo toka kwenye hayo makusanyo ili kusettle.
 
Bima kuwa compulsory ni kwa faida ya watumiaji wa barabara, nchi zingine hata bima ya afya ni lazima.

Unafikiri NIC anao uwezo wa kuinsure risk zote? Ulizia watu wa actuarial watakupa majibu.

Pamoja na kwamba third party insurance ni lazima unajua idadi ya watanzania wenye bima walau moja?

Bado penetration iko chini Sana!!
 
1.) Sijasema bima haina faida, na sijasema isiwe Compulsory, nimesema ilipwe Serikalini na sababu nimeshakupa.

2.) Sijasema NIC afanye insuramce zote, bali ‘third party tu’, na sababu nimeshakupa.

3.) Sizungumzi bima kwa watZ, nazungumiza bima ya magari ya aina ya ‘third party’ tu, na sababu nimeshakupa.
 
Jana kuna dogo dereva boda boda wa kampuni ya Dume Condom alipasua taa ya nyuma ya gari, kuwapigia ofisini wakamwambia aite traffic, traffic kufika akaandaa mchoro wa ajali. Dogo akajua ndio tayari hapo Bima wanalipa ili aondoke zake, anashangaa anaambiwa akalale ndani ili kesi iende mahakamani baada ya upelelezi kukamilika. Kuona hivyo akapigia simu ndugu zake wakamtumia pesa akalipa taa.
Yaani pesa ambayo ilikuwa ilipwe na bima imelipwa na ndugu. Hivyo watu wa bima wanabaki na pesa za bima karibu zote kwa upande wa third party. Nasisitiza, hii kodi ya third party iwasilishwe serikalini, mawakala wabaki na commission zao tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…