Matukio ya Kushangaza Duniani Yanayodaiwa Kusababishwa na Uchawi

Matukio ya Kushangaza Duniani Yanayodaiwa Kusababishwa na Uchawi

Hiyo mifano kama Salem witch trials zilikuwa zama za giza.. jiulize leo hii kwa nini wazungu wameacha kuhukumu na kuua wachawi ?
Sababu mojawapo ya kuacha ni kutokana na sauti kubwa za mashirika ya kutetea haki za binadamu yaliyopo sasa. Sababu nyingine ni kwamba mahakama za leo ili mtu ahukumiwe lazima uwepo ushahidi usiotia shaka. Ni nani sasa anayeweza kuthibitisha mbele ya jaji kuwa amemuona shetani akiingia nyumbani mwake. Katika uzi huu nimekueleza kuwa matendo ya kichawi yanatokana na shetani na mapepo. Shetani huwezi kumuona kwa macho. Hivyo kuacha kuhukumu sio kwamba uchawi haupo.

Hata hivyo bado kuna nchi zinatoa hukumu dhidi ya wachawi. Kwa mfano, Saudi Arabia – Sheria za Kiislamu zinaelezea uchawi kuwa ni kosa kubwa, na kuna watu waliohukumiwa kifo kwa madai ya uchawi. Mfano halisi wa hukumu ya uchawi nchini Saudi Arabia ni kesi ya Amina bint Abdulhalim Nassar, ambaye alihukumiwa kifo kwa madai ya uchawi na uganga mnamo mwaka 2011.
Una ujasiri wa kusema Saudi Arabia bado wanaishi zama za giza?
 
Tuko pamoja. Katika bandiko langu nimeeleza kuwa uchawi unatokana na shetani na mapepo(majini). Mchawi ni mtu anayeshirikiana kiutendaji na majini/mapepo
Nachomaanisha ni kwamba yapo mambo ni uchawi na mengine ni vitimbi tu vya majini wenyewe sio uchawi, lakini sio kila uchawi unafanywa na mchawi kwa maana hata wewe usiye mchawi unaweza ukafanya kitu kidogo tu na ukawa umemfanyia mtu uchawi pasina kushirikiana na majini.
 
Hapa naona ni lugha Tu inayotumika kwao wanadeclare ni uchawi kwetu Tz mazingaombe .Ati jamaa kachezea wanafunzi wamepagawa na si kawaloga .
 
Kwahiyo mkuu unataka kusema hakuna tiba yeyote ya mambo ya kichawi wala majini isipokuwa tiba hiyo inapatikana kwa wakristo tu?
Swali lako ni zuri sana. Kama kuna wengine wana tiba watuelezee hizo tiba zao tuzijue. Mimi nimeongea kulingana na imani yangu. Mimi naamini kwamba nguvu ya kushinda wachawi na mashetani inapatikana kwa uwezo wa Yesu Kristo aliyepewa mamlaka yote mbinguni na duniani (Mathayo 28:18) na kwamba kwa jina lake, waumini wanaweza kushinda nguvu za giza (Luka 10:19, Wakolosai 2:15).
 
Thibitisha kwa hoja kuwa uchawi haupo


Anayesema kitu kipo ndiye mwenye mzigo wa kuthibitisha kitu kipo.

Kwa sababu kilichopo ndicho kinathibitika kipo.

Kisichopo, nje ya nadharia tupu, hakithibitiki hakipo, kwa sababu hakipo na kama hakipo, hakithibitishiki kwamba hakipo.

Ukitaka mtu anayesema uchawi haupo athibitishe uchawi haupo, ni sawa na kumwambia mtu ambaye hajavamiwa na wezi na kuibiwa athibitishe kwamba hajavamiwa na wezi na kuibiwa.

Atathibitishaje?

Anayeweza kuthibitisha ni yule anayesema jambo limetokea. Anayesema kavamiwa na wezi na kaibiwa anaweza kuthibitisha kwa alama za vidole za hao wezi, anaweza kutoa video ya kuonesha wezi wakiingia kwake.

Sasa mtu anayesema hakuna wezi walioingia kwake unamtaka athibitishaje kuwa hakuna wezi walioingia kwake?

Unataka atoe alama za vidole za wezi ambao hawapo? Unataka atoe video ya wezi ambao hawapo?

Polisi wakisema una madawa ya kulevya nyumbani kwako, wao ndio wana wajibu wa kuyasaka na kuyapata.

Hawakuambii wewe mtuhumiwa ambaye unasema huna madawa ya julevya uthibitishe huna madawa ya kulevya.

Utathibitishaje huna madawa ya kulevya?

You can't prove a negative.

Wewe unayesema uchawi upo ndiye mwenye wajibu wa kuthibitisha uchawi upo.

Anayesema uchawi haupo yeye kazi yake ni kutaka uthibitisho tu kuwa uchawi upo.
 
Kama huiamini Biblia una haki ya kusema uliyoyasema, sio kosa lako.

Kama kuna kitabu kinachoharibu akili ni Bibilia .

Biblia imeandika Eti nyoka aliongea na Hawa hivi toka lini nyoka huwa anaongea. huku Nyoka hana Vocal cords

hivi wewe na akili yako unaamini nyoka huwa anaongea ?

Eti Samson aliua Simba kwenye jangwa la Palestina toka lini simba anaishi Jangwani,
 
Swali lako ni zuri sana. Kama kuna wengine wana tiba watuelezee hizo tiba zao tuzijue. Mimi nimeongea kulingana na imani yangu. Mimi naamini kwamba nguvu ya kushinda wachawi na mashetani inapatikana kwa uwezo wa Yesu Kristo aliyepewa mamlaka yote mbinguni na duniani (Mathayo 28:18) na kwamba kwa jina lake, waumini wanaweza kushinda nguvu za giza (Luka 10:19, Wakolosai 2:15).
Kwa sababu unasema jini hawezi kutolewa na jini lenzake hapo ndio pamenishangaza kidogo.
 
Anayesema kitu kipo ndiye mwenye mzigo wa kuthibitisha kitu kipo.

Kwa sababu kilichopo ndicho kinathibitika kipo.

Kisichopo, nje ya nadharia tupu, hakithibitiki hakipo, kwa sababu hakipo na kama hakipo, hakithibitishiki kwamba hakipo.

Ukitaka mtu anayesema uchawi haupo athibitishe uchawi haupo, ni sawa na kumwambia mtu ambaye hajavamiwa na wezi na kuibiwa athibitishe kwamba hajavamiwa na wezi na kuibiwa.

Atathibitishaje?

Anayeweza kuthibitisha ni yule anayesema jambo limetokea. Anayesema kavamiwa na wezi na kaibiwa anaweza kuthibitisha kwa alama za vidole za hao wezi, anaweza kutoa video ya kuonesha wezi wakiingia kwake.

Sasa mtu anayesema hakuna wezi walioingia kwake unamtaka athibitishaje kuwa hakuna wezi walioingia kwake?

Unataka atoe alama za vidole za wezi ambao hawapo? Unataka atoe video ya wezi ambao hawapo?

Polisi wakisema una madawa ya kulevya nyumbani kwako, wao ndio wana wajibu wa kuyasaka na kuyapata.

Hawakuambii wewe mtuhumiwa ambaye unasema huna madawa ya julevya uthibitishe huna madawa ya kulevya.

Utathibitishaje huna madawa ya kulevya?

You can't prove a negative.

Wewe unayesema uchawi upo ndiye mwenye wajibu wa kuthibitisha uchawi upo.

Anayesema uchawi haupo yeye kazi yake ni kutaka uthibitisho tu kuwa uchawi upo.
Sasa utasemaje tu kitu fulani hakipo hali ya kuwa hauna uhakika? Hivi kipi chenye kufanya watu waseme hakuna uchawi?
 
Kila siku nauliza swali hapa, kama uchawi upo kwanini babu zenu wakabebwa na kuvushwa bahari kwenda kupigwa mijeledi na kufanyishwa kazi za shamba huko nchi za mbali, na hili limefanyika karne na karne, hadi uingereza ilipoleta mapinduzi ya viwanda ndipo hayo mambo yakaisha.

Hao babu zenu wataalamu wa kuroga walishindwa kuroga wazungu? kama uchawi upo waitwe wachawi wote waroge team ya taifa ichukue kombe la dunia...

Hayo mambo ni imani, wenzenu wametoka huko, Mobutu world cup 1974 alienda Germany world cup na wachawi kama wote kutoka Zaire(Congo), huko ndiko wanasema kuna wachawi, kawaambia waroge wafunge magoli, badala yake Zaire ilipigwa jumla mabao 8...

so the qn is Why cant we use this juju thing we claim can do anything win ordinary world cup?

Kama uchawi upo na hao warogaji, kwanini wasiroge viongozi wala rushwa hii nchi wafe?
Kwanini wasiroge TANESCO wanaokata umeme hovyo ili wasirudie tena kukata umeme?
Kwanini wasiroge kuwepo na uchaguzi wa uhuru na haki?
Watoto wa waganga na wachawi watumie uchawi wanao washinde mitihani...

Thats because these things dont work, they dont exist.. mtu anaye amini huu upuuzi huwa namuona ni mjinga..
 
Sasa utasemaje tu kitu fulani hakipo hali ya kuwa hauna uhakika? Hivi kipi chenye kufanya watu waseme hakuna uchawi?
Wapi nimesema sina uhakika ?

Ukitaka mtu anayesema uchawi haupo athibitishe uchawi haupo, ni sawa na kumwambia mtu ambaye hajavamiwa na wezi na kuibiwa athibitishe kwamba hajavamiwa na wezi na kuibiwa.
Atathibitishaje?

Ninasema kitu hakipo sababu hakionekani kwenye na organ za utambuzi.. ambazo ni macho, pua na sikio, etc
 
Wapi nimesema sina uhakika ?

Ukitaka mtu anayesema uchawi haupo athibitishe uchawi haupo, ni sawa na kumwambia mtu ambaye hajavamiwa na wezi na kuibiwa athibitishe kwamba hajavamiwa na wezi na kuibiwa.
Atathibitishaje?

Ninasema kitu hakipo sababu hakionekani kwenye na organ za utambuzi.. ambazo ni macho, pua na sikio
Mbona athari za uchawi tunaziona kwa macho mkuu kama tunavyoona athari za stress au addiction, au wewe unaelewa uchawi ni nini?
 
. Tambua uchawi ni haupo, ila imani juu ya uchawi ipo kwenye vichwa vya watu

There is no scientific evidence to support the existence of witches.

Imani juu ya uwepo wa uchawi ni aawa na Imani juu ya uwepo Upako wa kiroho maana vyote ni non scientific proven
 
Kila siku nauliza swali hapa, kama uchawi upo kwanini babu zenu wakabebwa na kuvushwa bahari kwenda kupigwa mijeledi na kufanyishwa kazi za shamba huko nchi za mbali, na hili limefanyika karne na karne, hadi uingereza ilipoleta mapinduzi ya viwanda ndipo hayo mambo yakaisha.

Hao babu zenu wataalamu wa kuroga walishindwa kuroga wazungu? kama uchawi upo waitwe wachawi wote waroge team ya taifa ichukue kombe la dunia...

Hayo mambo ni imani, wenzenu wametoka huko, Mobutu world cup 1974 alienda Germany world cup na wachawi kama wote kutoka Zaire(Congo), huko ndiko wanasema kuna wachawi, kawaambia waroge wafunge magoli, badala yake Zaire ilipigwa jumla mabao 8...

so the qn is Why cant we use this juju thing we claim can do anything win ordinary world cup?

Kama uchawi upo na hao warogaji, kwanini wasiroge viongozi wala rushwa hii nchi wafe?
Kwanini wasiroge TANESCO wanaokata umeme hovyo ili wasirudie tena kukata umeme?
Kwanini wasiroge kuwepo na uchaguzi wa uhuru na haki?
Watoto wa waganga na wachawi watumie uchawi wanao washinde mitihani...

Thats because these things dont work, they dont exist.. mtu anaye amini huu upuuzi huwa namuona ni mjinga..
Haupo sahihi kwa sababu unachomaanisha ni kwamba unataka kusema ili uchawi uwepo ni hadi hayo mambo uliyoyataja yangefanyika au yafanyike ndio tukubali uwepo wa uchawi, cha ajabu hapo ukitajiwa yanayofanyika kwa uchawi utakataa utasema sio uchawi ni imani tu.

Kuna mambo mengi tu yanahusishwa na uchawi na ni makubwa tu, sasa kwanini uchague kutaja hayo mambo ili kutaka ionekane hakuna uchawi kisa hayo tu hayajafanyika?
 
Yoyote anayesema uchawi haupo basi hajaizunguka hii nchi. Uchawi upo na matendo yake yapo sana. Hata maeneo ambayo hauwezi kufikiria kama uchawi upo huko napo umetamalaki.

Kuna maeneo mtu akikiangalia chakula unachokula hata kama ulisali kabla ya kula hiyo siku utaumwa tumbo hadi ukome na ukifanya mchezo watu wanaimba buriani. Ila sasa ajabu ni kabla ya kula ukimwaga chini kidogo mtu yule yule akikuangalia haudhuriki. Na wenyeji wanajuana vizuri.
 
Mimi ningependa tujadiliane kuwepo ama kutokuwepo kwa uchawi kwa kuangalia mazingira yetu halisi ya afrika, si sahihi mtu anasema hakuna uchawi kwa sababu tu kwa wenzetu nchi zilizo endelea watu wengi hawaamini uchawi.
 
Haupo sahihi kwa sababu unachomaanisha ni kwamba unataka kusema ili uchawi uwepo ni hadi hayo mambo uliyoyataja yangefanyika au yafanyike ndio tukubali uwepo wa uchawi, cha ajabu hapo ukitajiwa yanayofanyika kwa uchawi utakataa utasema sio uchawi ni imani tu.

Kuna mambo mengi tu yanahusishwa na uchawi na ni makubwa tu, sasa kwanini uchague kutaja hayo mambo ili kutaka ionekane hakuna uchawi kisa hayo tu hayajafanyika?
Kama uchawi kweli una nguvu, mbona hautumiki kuleta maendeleo ya maana na kubadili mambo makubwa yanayoathiri jamii? Kwa sababu kama uchawi unafanya kazi kwenye mambo madogo, basi ungetarajiwa ufanye kazi pia kwenye mambo makubwa.

Je, unaweza kunipa ushahidi wa mambo hayo makubwa yanayofanyika kwa uchawi?

Mimi naamini katika sayansi kwa sababu imeleta maendeleo makubwa karibu katika kila nyanja—michezo, tiba, mawasiliano, ujenzi, sanaa, na hata safari za anga, Sayansi haina mipaka, inatumika popote na kwa yeyote anayejifunza na kuitumia.

Lakini uchawi unaonekana kuwa na mipaka mingi sana , Kwanini? Mbona hauwezi kutumika kutatua matatizo makubwa kama ukame, maradhi, au hata kushinda mashindano makubwa kama World Cup? Mbona kila mara unapokuwa na changamoto kubwa, watu huja kutegemea sayansi badala ya uchawi?

Kama uchawi kweli upo na unaweza kufanya lolote, mbona hakuna hospitali ya wachawi, magari ya wachawi, au hata kompyuta za wachawi?
 
Back
Top Bottom