Chumvi ni dawa. Chumvi ni tiba.
Ktk jadi chumvi ni kama stimulant yaani inaweza kufukuza kitu kibaya ama kuzuia ubaya but if combined with other related materials related with prayer.
Naiamini chumvi ya mawe daima si ktk jadi tu hata maji ya baraka huandaliwa na chumvi na ikiwa huamini jaribu kulamba maji ya baraka hasa yale yaandaliwayo na kanisa letu la Vatican.
Shida kubwa kwa waafrika wengi dini hamuijui wala biblia mmevichukua bila kuelewa kwa propaganda fake za wazungu.
Ukweli mila na biblia havipishani ni sawa.
Mungu alileta upatanisho kwa damu ya mnyama baadaye kwa damu ya yesu kristo hakukosea ni sawa. Tunafanya upatanisho wa familia kwa njia ya damu mnyama kuleta amani ktk koo si kosa ni sawa.
Yesu hakutibu watu kwa maombi tu bali hata kwa kuwaogesha waondoe mikosi ila leo ukioga dawa unaitwa mchawi, rejea mwenye ukoma kuambiwa ajichovye mtoni mara saba ili atakasike kwani yesu hakuwa na uwezo wa kumuombea?.
Ni vema tukaheshimu mila na desturi zetu zisizopingana na sheria za nchi hata Mungu.
Chumvi ni dawa na kitu pekee cha kujivunia alotupa Mungu.
Hii hapana, kama unamuamini Yesu usiwaambie watu damu ya mnyama inapatanisha ukoo,
Soma Bible agano la kale kwa misingi ya aga jipya ukisoma kwa mtindo huo Bible itakupoteza mno,
Lazima uwe na macho ya ndani
Tofauti ya mila na desturi unazo sema jiulize swali
Kwa nguvu ipi wanaitumia ili kupata vyote hivyo
Kuna vitu viwili vinavyo tumika
Ukikosa kumtumia Mungu basi upo kwa shetani
Ndio maana siku hiz hatumwagi damu ya wanyama kuwasailiana na Mungu kama zamani na hii ndio ambayo ufalme wa giza wameweza kuiga na baba yao shetani
Sisi tunao amini tunatumia damu ya Yesu hii shetani kashindwa ku I copy
Sasa hiv tupo chini ya neema si chini ya sheria
Mwenye ukoma aliye ambiwa kaoge alikuwa naamani wakati wa agano la akale
Hawa wa agano jipya tofauti na naamani alicho ambiwa
Naamani
Kuna mila haziendani na neno la Mungu tena nyingi tu, ndani yake kuna nguvu za giza zimejificha,
Chumvi inatumika kwa upande wa Mungu sikatai kabisa hata mimi nikitaka kufanya kitu nikihitaji chumvi natumia kwa Neno la Mungu na naweka ktk matendo
Sababu wakati mwingine bila matendo imani imekufa, naweza kutamka au kuchukua kitendo husika
Mungu akulinde