Matumizi yako kwa siku ni sh. ngapi? Je, niko vizuri au mimi ni mwananchi mnyonge?

Matumizi yako kwa siku ni sh. ngapi? Je, niko vizuri au mimi ni mwananchi mnyonge?

Prakatatumba abaabaabaa

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2022
Posts
1,842
Reaction score
6,087
Kwenda kazini natumia nauli ya 2000, kwenda 1000 kurudi 1000, asubuhi haiwezi kuzidi 1000 chai na harakati zingine, mchana hapa napiga sahani ya wali na nyama/dagaa/migebuka daily, ni 2000 nashushia na juice ya buku, kwa hiyo mchana jumla ni 3000, usiku ratiba yake ni kama mchana tu, 3000 lazima nitumie, kwa hiyo kwa siku nzima natumia 8000/= vocha natumia 5000 kwa week japo week haifiki mwisho, kwa hiyo kwa siku lazima nitumie 10,000/=

Hapo sina familia, kwa mwezi natumia 300,000/= ...nyumba nakaa ya 80,000/= hapo sijapiga mahesabu ya zaka na sadaka na michango mingine ya kanisa na jumuiya, kwa hiyo kwa mwezi natumia 450K hata nijibane kivipi, kila mwezi kwenye account nabakiza kiasi cha laki moja kama akiba so tokea nimepata hiki kibarua nina akiba ya 1.5m kipato changu kwa mwezi ni laki tano tu,

Sina cha kujivunia sana kwa sababu sina plot ninayomiliki, wala asset yoyote ile, nachukia sana kwenda church Jumapili nakutana na watu wengi wakiendesha magari n.k najiona kama myonge sana lakini najipa matumaini tu kwamba ipo siku moja, Age bado sijafika 30, nina 26.

Wewe mdau matumizi yako kwa siku ni yapi? Shusha Nondo zako tupate kujifunza na sisi.
 
Ni ngumu kukwepa hizo gharama,
Tafuta mishe ya pembeni ya kukuza kipato chako ili uongeze akiba.

Hao wenye magari wasikutie unyonge, hawakuzaliwa nayo, muhimu kuza kipato chako na wewe utamiliki kwa wakati wako.

Mungu ni wetu sote!
 
Ni ngumu kukwepa hizo gharama,
Tafuta mishe ya pembeni ya kukuza kipato chako ili uongeze akiba.

Hao wenye magari wasikutie unyonge, hawakuzaliwa nayo, muhimu kuza kipato chako na wewe utamiliki kwa wakati wako.

Mungu ni wetu sote!
Ndio kilichobaki, naumiza kichwa sana nifanye nini kama side hustle mpaka nachanganyikiwa, kinachonichanganya zaidi ni hapa kigoma sioni tobo.
 
Kigoma matumizi yote hayo?? Ungekuwa dar ungeolewa. Review matumizi yako ni makubwa mno na isitoshe ww ni ticha
Nimeishi Dar mzee, nimesoma Mugabe secondary japo nimezaliwa Morogoro, usijifanye mjuaji, nimeishi kwa kwa kipato cha laki 3, kabla sijaajiriwa, nimesoma hapo udsm miaka 3, nikamaliza nikabaki kupambana hapo mpaka nilipoajiriwa mwaka jana, kwa hiyo Dar sio kigezo cha matumizi makubwa.
 
Ndio kilichobaki, naumiza kichwa sana nifanye nini kama side hustle mpaka nachanganyikiwa, kinachonichanganya zaidi ni hapa kigoma sioni tobo.
Usikate tamaa usiache kwenda kanisani Jumapili. Fanya survey kwa makini ni fursa gani iliyopo unayoweza kufanya unaweza kuomba ushauri pia kwa watu waliofanikiwa hapo.
 
Back
Top Bottom