- Thread starter
- #21
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Jambazi asikii chochote zaidi ya risasi
Je kuna maandamano huko Mara? Kama ni kweli basi shida iko
Ikithibitika chakula chako ni chuma Ili iwe fundisho.Tofautisha "mchawi, jambazi, mganga" na "mshukiwa mchawi, jambazi, mganga" kama ulivyoorodhesha.
Kwenye fungu la pili hata wewe unaweza kuwamo.
Au nasema uongo ndugu zangu?
Pinga pinga FC.
Unamtisha nn!!! Kweli hujisimamia.sometimes its difficult to find truth until a man in the long black coat knocks on your Door .
Kuna time Huwa nawaza viongozi tuliowapa uongozi wanatuona kama sie ni watoto wadogo tutambaao...Mara yameonekana maandamano ya kuwapongeza polisi kuuwa wanaosemekana majambazi.
Kwamba maandamano hayo yamekuwa ya amani yakipokelewa na RPC wa huko, ni jambo la kupongezwa kwani haki ya kikatiba imetamalaki.
Hata hivyo kuna tashwishi za kutosha kuwa maandamano haya yameasisiwa na kuratibiwa na polisi wa huko kwa lengo la kuficha maovu yao au kujaribu kujisafisha.
View attachment 2371340
Tuhuma hizi katika hali yoyote ile si za kupuuzwa.
Ikumbukwe kazi ya polisi ni kukamata watuhumiwa na kuwafikisha kunakohusika. Katu si kuwauwa kinyama kama inavyosemekana ilitendeka.
Wakati kunaitishwa uchunguzi kwenye kadhia tata hii, ni vyema polisi wakatarajia kuyapokea maandamano mengine ya amani pia, yenye kuwafikishia ujumbe wa malalamiko.
Ni muhimu wakaliona hilo kuwa ni jambo la kheri kwani wao "kama ma taxi dereva sisi sote ni abiria wao."
Ni vyema wakafahamu wengine tulikaa kwa kutulia wengine walipoandamana kuwaunga wao mkono. Hivyo iwe wakati wao nao wa kukaa kwa kutulia ili kuyapokea malalamiko yetu.
Tunaamini kwa mujibu wa sheria, mkuki hauwezi kuwa mtamu kwa nguruwe tu.
Shime waungwana.
Ikithibitika chakula chako ni chuma Ili iwe fundisho.
Kama jambazi anaenda fungwa haimfundishi aliye nje atafanya uhalifu then ataenda jela atatoka.
hizo nchi zinazowaua wahalifu ni baada ya kustudy kwamba sheria haina uwezo wa kumfunza mwanadamu wapo watu wamezaliwa always ni criminal hata uwape shilingi bilioni moja Katu awaaji ujambazi, hawa dawa ni kuwatenga na jamii na sio kumuweka jela anakula bure kodi zetu.
Si Kweli, minyororo itakatikatika soon, mateka watakuwa huru kwenda ktk njia Yao.Inawezekana ni sisi ndiyo tunaowakubalia kuwa sie tu watoto wadogo ...
Unamtisha nn!!! Kweli hujisimamia.
Pinga pinga FC.
Kuna ndugu yeyote ametoa tamko kwamba ndugu yako kauwawa na sio jambazi?
Kama hakuna basi polisi imefanya kazi nzuri. Jambazi hana huruma
Jamii inayo uwezo wa kuthibitisha.Ikithibitika. Nani anathibitisha? Goodluck, Mahita, Jumanne, yule mwenzao au wewe?
Jamii inayo uwezo wa kuthibitisha.