Mauaji Salenda: Wahusika wote, Waziri na Sirro Wawajibishwe

Mauaji Salenda: Wahusika wote, Waziri na Sirro Wawajibishwe

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Maisha ya watu 5 wakiwamo wasiokuwa na hatia yamepotea jana, wengine wakijeruhiwa.

Haya yakitokea katika kinachosemekana kuwa ni mwendelezo wa matukio ya dhuluma tokea kwa watu wenye dhamana ya kutoa ulinzi kwa watu.

Aliyesemekana kuwa ni gaidi anasemekana hakuwa gaidi bali alikuwa ni raia wa kawaida. Hata katika tukio lenyewe hakuonekana kujificha wala kuwa tatizo na watu.

Bwana yule alionekana kukereka na jambo, alitembea wazi wazi akionekana kulalama. Yawezekana hakuwa gaidi wala jambazi. Labda kama alikuwa ni mwenda wazimu.

Taarifa zinazoeleza uwepo wa tashwishi ya dhuluma toka kwa waliokuwa wamemkamata si za kupuuzwa.

Hata hivyo, ni nani mwenye kumfunga paka kengele? Polisi hawa wanaweza kujichunguza wenyewe? Kwa fursa ipi ya kuaminika waliyoiwekeza kwa raia?

Kwani ilikuwaje kwenye:

1. Tukio la wafanya biashara wa madini wa Ifakara?
2. Matukio lukuki ya dhuluma kwenye vituo vya polisi?
3. Matukio lukuki ya akina Sabaya?
4. Matukio lukuki ya watu wasiojulikana?
5. Matukio ya lukuki ya watu wanaopigwa, kuteswa, kufa na hata kupotea mikononi mwa polisi?

Walaaniwe wahusika wote kwenye tukio la jana.

Wawajibishwe wahusija wote kwenye tukio la jana.

Kwamba tumefika hapa kwa sababu ya ukikwaji wa haki, haikubaliki.
 
Maisha ya watu 5 wakiwamo wasiokuwa na hatia yamepotea jana, wengine wakijeruhiwa. Haya yakitokea katika kinachosemekana kuwa ni mwendelezo wa matukio ya dhuluma tokea kwa watu wenye dhamana ya kutoa ulinz...
Hakuna wa kuyafanya, Sammy ni hasara tupu, hatuna Rais! Lazima wananchi watetee maisha yao, wakilala watateswa mpaka waseme poooo
 
Polisi polisi polisi
Wizara ya mambo ya ndani inabidi kuweka uchunguzi huru ili kujua pumba na mchele maana polisi wanamtindo wa kudhulumu Kisha wanakupa kesi kubwa ili wazidi kukutoa hela

Nani wa kumfunga paka kengele? Polisi hawawezi kujichunguza wenyewe. Hata hili watalifunika funika.

Apumzike kwa amani bwana Hamza na wahanga waliojikuta kwenye mahali sipo kwenye muda siyo.
 
Hakuna wa kuyafanya, Sammy ni hasara tupu, hatuna Rais! Lazima wananchi watetee maisha yao, wakilala watateswa mpaka waseme poooo

Sirro wala polisi hawakustahili pole wala pongezi.

Wanastahili laana na kuwajibishwa.

Ni wazi juu hakuna mtu bali pana kipindi cha watu wanaotupeleka kama gari bovu.
 
LUKUVI alisema pale Kanisani Magaidi wanapitia Zanzibar hivi Mbowe ametokea Zanzibar na kuingia Tanganyika kwa Njia za Panya,CCM waua mwana CCM.
 
kwaiyo mkuu hapo polisi sjui ni usalama unacheo gani?
 
Mtu ukijiona una Bundle na simu basi ndio unajiona unaakili kweli kweli , mnakuja kumwaga upupu wenu huku bila kufikiri na mnaleta habari za kufikirika , mnataka yule mtu aue watu wangapi ndio mridhike?

Kwa akili zenu unaweza kumkamata mtu anayejua kutumia tena akiwa na silaha za kivita tena AK 47 mbili ? mjitafakari kabla ya kutoa upupu wenu.

Jueni kuwa magazine moja risasi zaidi ya 30 waacheni polisi wafanye kazi yao.
 
Kuwajibishwa kuko nchi za wenzetu, hapa kwetu ni kulindana.

Kwa kuyajua hayo hatuna sababu ya kuwahi kuwatumia salamu za pole majahili hawa.

Hadi tutakapokuwa japo na katiba mpya hakuna aliye salama.
 
Mtu ukijiona una Bundle na simu basi ndio unajiona unaakili kweli kweli , mnakuja kumwaga upupu wenu huku bila kufikiri na mnaleta habari za kufikirika , mnataka yule mtu aue watu wangapi ndio mridhike? Kwa akili zenu unaweza kumkamata mtu anayejua kutumia tena akiwa na silaha za kivita tena AK 47 mbili ? mjitafakari kabla ya kutoa upupu wenu.
Jueni kuwa magazine moja risasi zaidi ya 30 waacheni polisi wafanye kazi yao.

Kuna mtu hapa kadhulumiwa. Si kila mtu anaweza ku react katika namna unayotaka wewe akiwa kadhulumiwa.

Wewe huioni tuhuma ya dhuluma iliyotufikisha huku?

Kwa hiyo wewe umekuja kumwaga upupu humu kwa sababu huna bundle?

Kazi za polisi si kudhulumu watu mali wala haki zao. Kabla ya kuwaonyesha uthabiti wetu katika kuyapinga hayo, hayupo aliye salama.
 
Gaidi ni gaidi hata km angedhulumiwa dhahabu adhhabu yake ni kifo
 
polosi sijui wamepatwa na nini wanafanya watakavyo saivi rushwa ndo usiseme dhuluma kumbambikia kesi.

mama sijui anakwama wapi jeshi LA polisi lilipofikia sio sehemu nzuri.

kuna hitaji mabadiliko.
 
kwaiyo mkuu hapo polisi sjui ni usalama unacheo gani?

Haihitaji kuwa polisi au usalama kutambua kuwa kuna maisha yamepotea bila sababu na nani ni wa kulaumiwa
 
Back
Top Bottom