Mauaji ya Polisi wetu ni Ujambazi, Ugaidi au Retaliation? Nini kifanyike kukomesha hali hii?

Mauaji ya Polisi wetu ni Ujambazi, Ugaidi au Retaliation? Nini kifanyike kukomesha hali hii?

Naomba hili liangaliwe.

upo ushahidi mwingi umetolewa si vizuri kuuweka hapa.

kuna haja ya jeshi la polisi kuzingatia haki Za binadamu wakati WA kutekeleza majukumu yao hasa kwa wanaokamatwa kwa kesi Za ugaidi.
 
Naomba hili liangaliwe.

upo ushahidi mwingi umetolewa si vizuri kuuweka hapa.

kuna haja ya jeshi la polisi kuzingatia haki Za binadamu wakati WA kutekeleza majukumu yao hasa kwa wanaokamatwa kwa kesi Za ugaidi.
Na sio kwa watuhumiwa wa ugaidi pekee, hata kwa raia wanaokamatwa kwa makosa mbalimbali. Sidhani kama raia aliyewahi kupitia mikononi mwa polisi anaweza kutoa habari za uhalifu mahali
 
Jeshi la Polisi la Tanzania ni kama Mbwa na bwana wake akiamrishwa anatekeleza bila kujiuliza nn impact ya haya wanayofanya
 
Wanabodi,
Taifa bado liko kwenye shock ya nini haswa kilichotokea kwa askari wetu?.

Mauaji haya ya Polisi Wetu ni Ujambazi tuu, ni Ugaidi au Retaliation?. Wakati vyombo vya uchunguzi vikiendelea na kazi yake, Sisi Watanzania kama taifa lazima tujiulize, Nini Kifanyike Kukomesha Hali Hii?,

Kwanza nikiri nimesikitishwa na vifo hivi vya vijana wetu askari polisi kushambuliwa na kuuwawa na majambazi wenye silaha.

Swali ni jee huu ni ujambazi tuu wa kawaida, uvamizi kwa lengo la kuiba silaha, ni ugaidi, ambush au nini haswa?.

Hili kuwaweka polisi wetu kwenye risk na kuwa an easy target, kwa majambazi wanaotumia silaha, niliwahi kulizungumza hapa kwa kirefu Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na kupandishwa vyeo limekaaje?
Kwa tukio kama la jana,jee mnadhani huu sasa ni wakati muafaka wa kuzibadili sheria zetu za jeshi la polisi ili kuwalinda polisi wetu wawe licenced to kill officially na serikali itangaze rasmi kuwa ujambazi wa kutumia silaha adhabu yake ni kifo cha papo kwa papo, no prosecution no kesi, bali ni hukumu ya kifo there and then ili kuwaogofya kabisa majambazi wote wanaotumia silaha wasithubutu?!.

Kama ni ugaidi au retaliation, tufanye nini?.

Natoa pole kwa rais wetu wa JMT, waziri wa Mambo ya Ndani, IGP na familia za askari hao!

RIP Askari Wetu.
Nini Kifanyike? .
Ijumaa Kuu Chungu!.
Paskali
Update 1.

Thanks very objective.

Paskali
Update 2 ya michango very objective

Thanks kwa mchango huu, very objective
Paskali
Update 3.
Huu ni mchango very objective

Thanks for this.
Paskali

Wafunguwe kanda maalum kama ilivyo kule tarime.
 
Kisifanyike chochote juzi kuna Wabunge wameomba hilo swala lijadiliwe bungeni kuna wanawake jenista mhagama na mwenzie bila hata aibu wanasema ni uchochezi!
Yakasikika makofi ya Wabunge wa ccm waaaa...waaaa....waaaa....
Acha tuendelee hivi hivi
MUNGU HUYU!
 
jeshi lijali haki Za binadamu, ripoti Za tume Za haki Za binadamu tz karibia kila mwaka Hawa hawakosekani ,kwanini?
 
Kimtazamo wangu hii ongoing operation ya kukusanya silaha inayofanywa na kikundi ambacho hakuna akijuaje.Vyombo vya ulinzi wanatakiwa wawe makini sana,wanatumika na wanasiasa hadi watu hawawapendi.Kwenye ukweli wao wamekuwa wakipindisha,kwenye haki wao wanafanya dhulma,kumekua na kuteswa na watu wasiojulikana kila kukicha,wapo radhi kukesha mtaandaon kujua nan katukana nani ili wampate kuliko kudeal na core functions zao,kwa nini hao wasiwashindwe?.Watu wamekua wakipotea huku majibu yanayotelewa na zaid ya vituko.Chuki hii si nzu kabsa maana wanakosa support pind wanapoihitaj na kwa kua wote tupo kwenye jamii moja what goes around,comes around..lazma nao yawakute tu.
Kuna mambo ambayo ukiangalia na kusikiliza unaona kabisa kuna watu wana. misuse wanausalama wetu,na cha ajabu wao wamekubali kuwa upande mmoja na kukandamiza wengine.
Niseme tu death is real,na wote tutakufa,ila vyombo vyetu vinatakiwa vitende haki na vifanye kaz kwa weled si "mzuka" na watapata support nzur tu.
Huu mtindo wa kuuwa askar na viongoz wengne kwenye huo mkoa kwangu naona si just ujambaz,waende watafute sabab ni nini na wajirekeshe ili raia wawape taarifa sahihi kwenye kila tukio.Raina wapenda aman bado tupo weng,watupe support na wawe fair tu.Above all,R.I.P kwa fallen servicemen wote wa hili tukio
 
unaongolea polisccm

saivi polis akifa watu wanashangilia polis punguzeni kutumika pia hamtendi haki.
 
Tukiwa vijana wadogo wakati huo kijijini,kuna Mzee alikuwa mtemi sana,anapiga mpaka wazee wenzake mbele za watoto na wake zao.Ilikuwa nj zile enzi za "wababe" ndio wanaheshimika,kuna siku aliwahi kumpiga kerebu mzee mwenzake mbele ya mwanae wa kiume.

Kile kitendo kilimuuma sana yule dogo,akakaa na kinyongo moyoni bila kusema,siku ya siku Mzee mbabe tukasikia ameokotwa korongoni kijiji cha Muhunze akiwa hana kaptula ya ndani wala shati,na jana usiku alionekana kilabuni akinywa pombe,miaka kumi baadae ikaja kugundulika alitandikwa na yule dogo ambaye alishuhudia baba yake akitandikwa kerebi kama miaka mitano iliyopita.

Binadamu ni kiumbe wa ajabu sana,saikolojia ya binadamu ni ngumu kuielewa.Unapofika na kusikia kuwa Masheikh ambao ni mababa wa familia na viongozi wa dini wamelawitiwa na kuminywa korodani mpaka kupoteza uwezo wa kusimamisha,unategemea hii chuki inakaa wapi?

Unapombambikia mtu kesi ya uwizi,anasota rumande kwa mateso na karaha,tambua huyu ana ndugu na watu wanaompenda walio tayari kulipa kisasi ili kuridhisha nafsi zao.

Wapo watu wanaofungwa bila makosa,wapo wanaobambikiwa kesi kwa sbb za kisiasa,haya yote yanajenga chuki kati ya raia na askari polisi.

Polisi unafika kwenye kijiwe cha bodaboda unasomba pikipiki 20 kisa wamezidi muda wa "serikali" wa saa sita usiku,na ili wazitoe pikipiki zao,basi kila mtu anatakiwa kutoa elfu50....hii chuki inamea kama mmea kando ya kijito
 
polisi waweke siasa pembeni wafanye kazi kwa kutumia taratibu za kazi zao watafanikiwa
 
Wanabodi,
Taifa bado liko kwenye shock ya nini haswa kilichotokea kwa askari wetu?.

Mauaji haya ya Polisi Wetu ni Ujambazi tuu, ni Ugaidi au Retaliation?. Wakati vyombo vya uchunguzi vikiendelea na kazi yake, Sisi Watanzania kama taifa lazima tujiulize, Nini Kifanyike Kukomesha Hali Hii?,

Kwanza nikiri nimesikitishwa na vifo hivi vya vijana wetu askari polisi kushambuliwa na kuuwawa na majambazi wenye silaha.

Swali ni jee huu ni ujambazi tuu wa kawaida, uvamizi kwa lengo la kuiba silaha, ni ugaidi, ambush au nini haswa?.

Hili kuwaweka polisi wetu kwenye risk na kuwa an easy target, kwa majambazi wanaotumia silaha, niliwahi kulizungumza hapa kwa kirefu Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na kupandishwa vyeo limekaaje?
Kwa tukio kama la jana,jee mnadhani huu sasa ni wakati muafaka wa kuzibadili sheria zetu za jeshi la polisi ili kuwalinda polisi wetu wawe licenced to kill officially na serikali itangaze rasmi kuwa ujambazi wa kutumia silaha adhabu yake ni kifo cha papo kwa papo, no prosecution no kesi, bali ni hukumu ya kifo there and then ili kuwaogofya kabisa majambazi wote wanaotumia silaha wasithubutu?!.

Kama ni ugaidi au retaliation, tufanye nini?.

Natoa pole kwa rais wetu wa JMT, waziri wa Mambo ya Ndani, IGP na familia za askari hao!

RIP Askari Wetu.
Nini Kifanyike? .
Ijumaa Kuu Chungu!.
Paskali
Update 1.

Thanks very objective.

Paskali
Update 2 ya michango very objective

Thanks kwa mchango huu, very objective
Paskali
Update 3.
Huu ni mchango very objective

Thanks for this.
Paskali
Mkuu Pascal heshima kwako. Kwanza nitoe pole kwa jeshi la polisi na kwa familia na ndugu wote waliopatwa na misiba hii. Mimi nitachangia upande wa recruiting and training za polisi wetu. Mkuu, utaratibu wa kuajiri na mafunzo kwa vijana wetu nadhani haupo sawa, huwezi kuajiri watu kwa kujuana, watu wenye elimu zao halafu, wasio na wito, utayari, kujitoa halafu unawapeleka kwenye mafunzo ambayo kimsingi hayaendani na wakati tulionao. Unamchukuaje mtu ambaye amemaliza chuo, hajaoa, hajamaliza hata mkopo wake wa bodi, ambaye kwao waliuza rasilimali zilizokuwepo akasomea halafu unampeleka kwenda kupambana na jambazi. Automatically ndo maana linapotokea tukio la uhalifu polisi hufika baada ya nusu saa au saa moja na wakikaribia hupiga risasi hewani ili kukwepa kukabiliana na majambazi live. Inawezekana mbinu za mafunzo , aina ya askari wetu (watoto wa wakubwa) hawawez kuifanya hii kazi kwa ufanisi au wanaogopa kutokana na kwenda huko kama sehemu ya kukulia au kutafta kipato na si vinginevyo. Naamini utaratibu wa zaman uliokuwa unatumika kuajiri wana usalama ilikuwa nzuri, huko mitaani kuna watu ukiwapeleka huko kufanya kazi kama hiyo wataifanya vyema. Mkoa wa Mara kwa mfano kuna watu wakiskia risasi ya jambazi wanaanza kukimbia kwenda inapotokea, huku Pwani hawa waswahili ni kinyume. Sikatai jeshi kuwa la wasomi, ila wasomi wawepo wachache wenye kupanga mipango ila wale rapid responders si lazima wawe wasomi amabao huenda huko huku akikumbuka amesoma miaka mingi hajatimiza malengo yake n.k. Tuachane na huu utaratibu wa sasa wa kuajiri kwa kujuana huku tukijaza watoto wa vigogo kwenye majeshi yetu ambao wakifika huko akili zao ni kuzichanga na si vinginevyo, hivi mmewahi kujiuliza Kwanini polisi wakitumwa kwenda kumkamata mwanasiasa wanaenda kwa mbwembwe ilihali shughuli kama hii ya kupambana na wahalifu /majambazi kabla ya kufika eneo la tukio huanza kufyatua risasi hewani ili kuwa alert majambazi kukwepa kupambana nao? Mtaala wa mafunzo ndani ya jeshi letu ubadilishwe ili kuendana na wakati na ufocus miaka mingi ijayo. Jeshi letu inawezekana ni worse kulikon tunavyofikiria, wamejaa wapiga dili, watoto wa vigogo, wavivu na watu wasiokuwa na mori, uzalendo. Tutengeneze kikosi imara, wenye ari. Kuna vijana huko vijijin ukiwachukua na kuunda kikosi maalum ndani ya jeshi letu let's say "First Responders" na mbinu mpya tutasonga mbele. Asante.
 
Hii nchi iko salama nyie mnoendelea kujadili hili sua mtakua wapiga diri au wauzaji waunga mnataka kumkwamisha Rais acheni uchochezi kati ya Raia na Serikali aya ndo maneno ya Awamu ya Tano
 
Umeanza vizuri lakin umwpoteza mwelekeo ,he una maana kuwa RAIA na polisi na we kama RAIA haupo tayari kuwasaidia polisi kwa namna yyte?
 
Unajua kupukutika kirahisi? Kweli RAIA mzalendo WA nchi hiii unasema hivyo namheshimu mzee WA nyuki WA kanda ya NYANDA za juu.
 
Nionavyo mimi ni makundi ya maharifu yanakusanya silaha.

Halfu kitu kingine kule yanakotokea haya ni kule kule kwenye pwani isiyokuwa na ulinzii. Ulinzi uimarishwe katika njia chocho za bahari.

Ninaomba JWTZ wafanye operation maalumu katika misitu iliyokatika maeneo hayo. Kunaweza kuwa na kambi maalumu ya uahrifu.

Tatu viongozi wa dini ya kiisilam, wale wanaowaza mema, wakae na wajadili namna ya kukomesha mitazazmo mibovu ya baadhi ya watu walio nao juu ya maisha. Bila shaka wanafahamu haya ni kwa nini yanatokea kwa kuwa eneo yanakotokea haya ni kule kwenye wingi wa wafuasi wao ambao wameshindwa maisha. Wanatakiwa wawape elimu sahihi namna wataboresha maisha yao badala ya kutafuta njia za kiharamia au kutaka kuharibu nchi ili wakose wote. Hii ni roho ya shetani yule mwenye wivu.

Nne jeshi la polisi lirudi katika misingi ya kutenda haki. Waacha uharamia wa kudhulumu na kuonea raia. Polisi waache unyanganyi wa mali na haki za raia ili jamii iwaone kuwa ni sehemu yake na iwape ushirikiano. Polisi wamejitenga na wananchi ki malengo na ndiyo sababu wananchi wako kimya hata wanapoona mipango miovu inatokea. Ninasema hivi kwa sababu, bila shaka hata katika tukio hili kulikuwa na watu karibu. Hao jambazi hakutoka hewani na hakuyeyeyuka baada ya ushetani wake. Watu walimwona akiingia na alikoelelkea wanajua. Jeshi la polisi linahitaji kuhamasisha umoja kati yake na raia ili raia walisaidie kuzuia matukio ya kishetani kama haya.

Tano serikali iache kuwatumia polisi vibaya. Inawajengea chuki dhidi ya wananchi. Wanachi wanaoan polisi ni watesi wao na si wasaidizi n ahivyo kujitenga nao mbali. Viongozi wa ccm na serikali wawekeane mikakati ya kudhibiti matumizi ya jeshi la polisi yasiyo halali. Yanalidhalilisha jeshi letu na kuliweka katika wakati mgumu sana wa kutengwa na umma.

Serikali itambue kwamba hii ni karne nyingine. Budget za serikali ziangalie suala la technolojia ya ulinzi na usalama ndani na nje ya mipaka ya nchi yetu. Ikiwa tetemeko lilitokea Bukoba na hapakuwa na hata kipimo cha kutambua kabla hatua stahiki zikachukuliwa, na bado serikali ikasema haikuleta tetemeko, niina mashaka na uwepo wa technolojia ya ulizini wa mipaka yetu hasa katika bahari na sehemu zisizokaliwa na watu. Kuliko kutumia nguvu kubwa kudhibiti wapinzani, ninaomba serikali iwekeze kweney technolojia surveillance ndani na nje ya mipaka yetu. Polisi wanaoonyesha uharamia kama kunyang'anya mali za mahabusu kwa nguvu, kutetea uharlfu ndani ya jeshi, kuonea na kusingizia raia, wanatakiwa kuondolewa kwenye kikosi hivi kwa sababu hawa ini hatari kwa jeshi lenyewe. Wanaweza kuuza taarifa hata mipango ya dani ya jeshi kwa maslahi ya 1000,000. Ondoeni maharamia kati ya polisi, sukeni jeshi letu upya, kisha liwezeshwe kwa technolojia inayoona na kutoa taarifa ya matukio hasa katika maeneo yenye wasialam wengi kama huko pwani na mkuranga.

Watanzania ninaomba sana tuendelee kuishauri serikali japo inakataa kushauriwa. Hii la kukataa ushauri wa wanaoongozwa tulichukue kama tatizo linalohitaji tiba kama maradhi lakini hatwezi kujenga taifa pasipo kushauriana na kusikilizana. Ccm ninyi ndio wenye viburi, ninaomba muwe wa kwanza kujirekebisha. Tambueni bila taifa lenye amani ccm haipo.

Viongozi acheni kujenga matabaka miongoni mwa wananchi. Acheni kuwadharau watanzania na kuwabagua, huku mkifanya kebehi za wazi kwa viburi. Migawanyikio mnayoijenga ndiyo inayoondoka mishkikamano na mioyo ya uzalendo . Bila kuwa na umoja na uzalendo, hakuna suluhu rahisi ya matatkzo yanayoinuka.

NINAOMBA NISIITWE MCHOCHEZI MAANA SERIKALI INADHANI IKIWAUNGA WATU VINYWA NDIYO INASHINDA, KUMBE INAJENGA ROHO MBAYA ZA KIKATILI NA MTAWANYIKO UANOANZA KULIGHARIMU TAIFA KWA KASI HII YA AJBU.
Viongozi wakiislamu tena? Umepotoka mkuu. Hapo hakuna uislamu na mwenye mawazo kama haya siku mkiwaandama hao waislamu waziwazi (kwa sasa wanaandamwa kwa kificho) huo moto mtaupiga petroli na yatakuwabkama yale ya garissa.

Hao majambazi na hapo kuna uhasama wa wananchi na vyombo vya usalama na viongozi wa hayo maeneo. Si uliona waliwaua askari kisha wakaamuru wananchinwakachukue vitu vyao kama mbao, mkaa n.k. Hapo hakuna ugomvi wakidini, acha kichochea mengine tusiyoyaweza.

We unadhani Alshababi wakifika hapa kwetu siku utasikia central imetekwa na mjengo wote umewaka moto. Tusiombee hayo na tuache fitna hii. Mawazo hayo yakizoeleka na kuanza kuwatesa wasiohusika, vijana waliokata tamaa wataungana na hao majambazi na mziki wake mtahama dar.

Vita yao hawa sio kama ile ya kagera. Wanavizia na kuuwa na wanasepa. Nakusihi acha kupandikiza haya mambo ya chuki za kidini, hata wewe kutapona.
 
Wachangiaji msifanyie hili suala mzaha Gaidi hana chama wala dini ni mnyama akivaa vesti ya kujilipua huwa hajui ataua nani. Wiki iliyopita huko Misri katika kanisa la Copti mliona jinsi raia wasiokuwa na hatia walivyouliwa.
Tuweke pembeni tofauti zetu na tujadili adui yetu mkubwa Gaidi. Leo tumepoteza vijana wetu saba tunatakiwa tufarijii familia zao sio kutoa comments za mzaha.
Nini maana ya Gaid?
 
Tuanze kwanza kukomesha utekaji...haya ya mauaji yatakoma endapo utekaji watu utakwisha..na usipokwisha basi polic wajiandae
 
Mheshimiwa paschal mayalla,kuna siku nilileta Uzi humu kuwa kauli za Rais zitahatarisha usalama wa Taifa, maana kutatokea magaidi na majambazi . thread ilifutwa faster,anyway sikulalamika maana ilikuwa ni sensitive issue sana lakini ukweli utabaki kuwa pale pale kuwa kauli za Rais na kumkumbatia Bashite zitaliangamiza Taifa. Utekaji unaofanywa na taasisi muhimu za serikali nazo zinachangia haya yote,kinachofanyika ni visasi dhidi ya serikali.
Kuna jambo lingine linashangaza sana. Mtu anakamata lori la mkaa, linataifishwa alafu mkaa ule ule unauzwa na mwenye mali hapati kitu. Kwanini msimbwambie mkaa wako tutauza na utapewa nusu ya mali yako. Badala yake mtu anabaki masikini milele.

Mtu unakamata mbao, zinataifishwa na wauza tena kwa bei ya hovyo kabisa, mtu mwenye mali anabaki kiwa masikini na anamuona askari aliyetaifisha mali anakunywa mipombe na kubadilisha mademu. Hatari sana.

Safari moja (hiki kisa sikisahau), tulipanda fuso ya jamaa alibeba nazi anakuja temeke, kufika katikati hapo kwenye kizuizi jamaa wakazuia gari kisa dereva aliweka vigunia viwili vya mkaa vya 25kg. Dereva akajitetea kuwa jamani mm natoka pori kila siku kule mkaa rahisi, naenda kutumia huu mm sifanyi biashara. Au nilipe ushuru basi.

Askari wakagoma wakataka kuchukua mkaa, tukawekwa pembeni 2hrs. Dereva akabembeleza sana. Jamaa wamekomaa kwelikweli.

Dereva akawaita wote askari wakaja. Akapanda kwenye gari akawaambia haya shusheni huo mkaa niondoke lakini nawahakikishieni mkiiona hii gari kaeni mbali ntakuja kuwasaga wote hapahapa na kesi yake ni elfu 30.

Jamaa alifoka sana kuwa mnatuonea sisi watu wa pwani tu mbona ndugu zenu wanapita nao mkaa hapa hamwashiki, mm kila siku ndio kazi yangu napita njia hii kufuata mihogo na nazi sasa shusheni mm niondoke lakini mkae sawa.

Alikua askari mmoja akamwambia ondoa gari yako uende.

Haya mambo yapo na watu wanajenga chuki sana.
 
Back
Top Bottom