assadsyria3
JF-Expert Member
- Apr 9, 2013
- 6,905
- 4,054
Na sio kwa watuhumiwa wa ugaidi pekee, hata kwa raia wanaokamatwa kwa makosa mbalimbali. Sidhani kama raia aliyewahi kupitia mikononi mwa polisi anaweza kutoa habari za uhalifu mahaliNaomba hili liangaliwe.
upo ushahidi mwingi umetolewa si vizuri kuuweka hapa.
kuna haja ya jeshi la polisi kuzingatia haki Za binadamu wakati WA kutekeleza majukumu yao hasa kwa wanaokamatwa kwa kesi Za ugaidi.
Wanabodi,
Taifa bado liko kwenye shock ya nini haswa kilichotokea kwa askari wetu?.
Mauaji haya ya Polisi Wetu ni Ujambazi tuu, ni Ugaidi au Retaliation?. Wakati vyombo vya uchunguzi vikiendelea na kazi yake, Sisi Watanzania kama taifa lazima tujiulize, Nini Kifanyike Kukomesha Hali Hii?,
Kwanza nikiri nimesikitishwa na vifo hivi vya vijana wetu askari polisi kushambuliwa na kuuwawa na majambazi wenye silaha.
Swali ni jee huu ni ujambazi tuu wa kawaida, uvamizi kwa lengo la kuiba silaha, ni ugaidi, ambush au nini haswa?.
Hili kuwaweka polisi wetu kwenye risk na kuwa an easy target, kwa majambazi wanaotumia silaha, niliwahi kulizungumza hapa kwa kirefu Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na kupandishwa vyeo limekaaje?
Kwa tukio kama la jana,jee mnadhani huu sasa ni wakati muafaka wa kuzibadili sheria zetu za jeshi la polisi ili kuwalinda polisi wetu wawe licenced to kill officially na serikali itangaze rasmi kuwa ujambazi wa kutumia silaha adhabu yake ni kifo cha papo kwa papo, no prosecution no kesi, bali ni hukumu ya kifo there and then ili kuwaogofya kabisa majambazi wote wanaotumia silaha wasithubutu?!.
Kama ni ugaidi au retaliation, tufanye nini?.
Natoa pole kwa rais wetu wa JMT, waziri wa Mambo ya Ndani, IGP na familia za askari hao!
RIP Askari Wetu.
Nini Kifanyike? .
Ijumaa Kuu Chungu!.
Paskali
Update 1.
Thanks very objective.
Paskali
Update 2 ya michango very objective
Thanks kwa mchango huu, very objective
Paskali
Update 3.
Huu ni mchango very objective
Thanks for this.
Paskali
MUNGU HUYU!Kisifanyike chochote juzi kuna Wabunge wameomba hilo swala lijadiliwe bungeni kuna wanawake jenista mhagama na mwenzie bila hata aibu wanasema ni uchochezi!
Yakasikika makofi ya Wabunge wa ccm waaaa...waaaa....waaaa....
Acha tuendelee hivi hivi
Mkuu Pascal heshima kwako. Kwanza nitoe pole kwa jeshi la polisi na kwa familia na ndugu wote waliopatwa na misiba hii. Mimi nitachangia upande wa recruiting and training za polisi wetu. Mkuu, utaratibu wa kuajiri na mafunzo kwa vijana wetu nadhani haupo sawa, huwezi kuajiri watu kwa kujuana, watu wenye elimu zao halafu, wasio na wito, utayari, kujitoa halafu unawapeleka kwenye mafunzo ambayo kimsingi hayaendani na wakati tulionao. Unamchukuaje mtu ambaye amemaliza chuo, hajaoa, hajamaliza hata mkopo wake wa bodi, ambaye kwao waliuza rasilimali zilizokuwepo akasomea halafu unampeleka kwenda kupambana na jambazi. Automatically ndo maana linapotokea tukio la uhalifu polisi hufika baada ya nusu saa au saa moja na wakikaribia hupiga risasi hewani ili kukwepa kukabiliana na majambazi live. Inawezekana mbinu za mafunzo , aina ya askari wetu (watoto wa wakubwa) hawawez kuifanya hii kazi kwa ufanisi au wanaogopa kutokana na kwenda huko kama sehemu ya kukulia au kutafta kipato na si vinginevyo. Naamini utaratibu wa zaman uliokuwa unatumika kuajiri wana usalama ilikuwa nzuri, huko mitaani kuna watu ukiwapeleka huko kufanya kazi kama hiyo wataifanya vyema. Mkoa wa Mara kwa mfano kuna watu wakiskia risasi ya jambazi wanaanza kukimbia kwenda inapotokea, huku Pwani hawa waswahili ni kinyume. Sikatai jeshi kuwa la wasomi, ila wasomi wawepo wachache wenye kupanga mipango ila wale rapid responders si lazima wawe wasomi amabao huenda huko huku akikumbuka amesoma miaka mingi hajatimiza malengo yake n.k. Tuachane na huu utaratibu wa sasa wa kuajiri kwa kujuana huku tukijaza watoto wa vigogo kwenye majeshi yetu ambao wakifika huko akili zao ni kuzichanga na si vinginevyo, hivi mmewahi kujiuliza Kwanini polisi wakitumwa kwenda kumkamata mwanasiasa wanaenda kwa mbwembwe ilihali shughuli kama hii ya kupambana na wahalifu /majambazi kabla ya kufika eneo la tukio huanza kufyatua risasi hewani ili kuwa alert majambazi kukwepa kupambana nao? Mtaala wa mafunzo ndani ya jeshi letu ubadilishwe ili kuendana na wakati na ufocus miaka mingi ijayo. Jeshi letu inawezekana ni worse kulikon tunavyofikiria, wamejaa wapiga dili, watoto wa vigogo, wavivu na watu wasiokuwa na mori, uzalendo. Tutengeneze kikosi imara, wenye ari. Kuna vijana huko vijijin ukiwachukua na kuunda kikosi maalum ndani ya jeshi letu let's say "First Responders" na mbinu mpya tutasonga mbele. Asante.Wanabodi,
Taifa bado liko kwenye shock ya nini haswa kilichotokea kwa askari wetu?.
Mauaji haya ya Polisi Wetu ni Ujambazi tuu, ni Ugaidi au Retaliation?. Wakati vyombo vya uchunguzi vikiendelea na kazi yake, Sisi Watanzania kama taifa lazima tujiulize, Nini Kifanyike Kukomesha Hali Hii?,
Kwanza nikiri nimesikitishwa na vifo hivi vya vijana wetu askari polisi kushambuliwa na kuuwawa na majambazi wenye silaha.
Swali ni jee huu ni ujambazi tuu wa kawaida, uvamizi kwa lengo la kuiba silaha, ni ugaidi, ambush au nini haswa?.
Hili kuwaweka polisi wetu kwenye risk na kuwa an easy target, kwa majambazi wanaotumia silaha, niliwahi kulizungumza hapa kwa kirefu Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na kupandishwa vyeo limekaaje?
Kwa tukio kama la jana,jee mnadhani huu sasa ni wakati muafaka wa kuzibadili sheria zetu za jeshi la polisi ili kuwalinda polisi wetu wawe licenced to kill officially na serikali itangaze rasmi kuwa ujambazi wa kutumia silaha adhabu yake ni kifo cha papo kwa papo, no prosecution no kesi, bali ni hukumu ya kifo there and then ili kuwaogofya kabisa majambazi wote wanaotumia silaha wasithubutu?!.
Kama ni ugaidi au retaliation, tufanye nini?.
Natoa pole kwa rais wetu wa JMT, waziri wa Mambo ya Ndani, IGP na familia za askari hao!
RIP Askari Wetu.
Nini Kifanyike? .
Ijumaa Kuu Chungu!.
Paskali
Update 1.
Thanks very objective.
Paskali
Update 2 ya michango very objective
Thanks kwa mchango huu, very objective
Paskali
Update 3.
Huu ni mchango very objective
Thanks for this.
Paskali
Viongozi wakiislamu tena? Umepotoka mkuu. Hapo hakuna uislamu na mwenye mawazo kama haya siku mkiwaandama hao waislamu waziwazi (kwa sasa wanaandamwa kwa kificho) huo moto mtaupiga petroli na yatakuwabkama yale ya garissa.Nionavyo mimi ni makundi ya maharifu yanakusanya silaha.
Halfu kitu kingine kule yanakotokea haya ni kule kule kwenye pwani isiyokuwa na ulinzii. Ulinzi uimarishwe katika njia chocho za bahari.
Ninaomba JWTZ wafanye operation maalumu katika misitu iliyokatika maeneo hayo. Kunaweza kuwa na kambi maalumu ya uahrifu.
Tatu viongozi wa dini ya kiisilam, wale wanaowaza mema, wakae na wajadili namna ya kukomesha mitazazmo mibovu ya baadhi ya watu walio nao juu ya maisha. Bila shaka wanafahamu haya ni kwa nini yanatokea kwa kuwa eneo yanakotokea haya ni kule kwenye wingi wa wafuasi wao ambao wameshindwa maisha. Wanatakiwa wawape elimu sahihi namna wataboresha maisha yao badala ya kutafuta njia za kiharamia au kutaka kuharibu nchi ili wakose wote. Hii ni roho ya shetani yule mwenye wivu.
Nne jeshi la polisi lirudi katika misingi ya kutenda haki. Waacha uharamia wa kudhulumu na kuonea raia. Polisi waache unyanganyi wa mali na haki za raia ili jamii iwaone kuwa ni sehemu yake na iwape ushirikiano. Polisi wamejitenga na wananchi ki malengo na ndiyo sababu wananchi wako kimya hata wanapoona mipango miovu inatokea. Ninasema hivi kwa sababu, bila shaka hata katika tukio hili kulikuwa na watu karibu. Hao jambazi hakutoka hewani na hakuyeyeyuka baada ya ushetani wake. Watu walimwona akiingia na alikoelelkea wanajua. Jeshi la polisi linahitaji kuhamasisha umoja kati yake na raia ili raia walisaidie kuzuia matukio ya kishetani kama haya.
Tano serikali iache kuwatumia polisi vibaya. Inawajengea chuki dhidi ya wananchi. Wanachi wanaoan polisi ni watesi wao na si wasaidizi n ahivyo kujitenga nao mbali. Viongozi wa ccm na serikali wawekeane mikakati ya kudhibiti matumizi ya jeshi la polisi yasiyo halali. Yanalidhalilisha jeshi letu na kuliweka katika wakati mgumu sana wa kutengwa na umma.
Serikali itambue kwamba hii ni karne nyingine. Budget za serikali ziangalie suala la technolojia ya ulinzi na usalama ndani na nje ya mipaka ya nchi yetu. Ikiwa tetemeko lilitokea Bukoba na hapakuwa na hata kipimo cha kutambua kabla hatua stahiki zikachukuliwa, na bado serikali ikasema haikuleta tetemeko, niina mashaka na uwepo wa technolojia ya ulizini wa mipaka yetu hasa katika bahari na sehemu zisizokaliwa na watu. Kuliko kutumia nguvu kubwa kudhibiti wapinzani, ninaomba serikali iwekeze kweney technolojia surveillance ndani na nje ya mipaka yetu. Polisi wanaoonyesha uharamia kama kunyang'anya mali za mahabusu kwa nguvu, kutetea uharlfu ndani ya jeshi, kuonea na kusingizia raia, wanatakiwa kuondolewa kwenye kikosi hivi kwa sababu hawa ini hatari kwa jeshi lenyewe. Wanaweza kuuza taarifa hata mipango ya dani ya jeshi kwa maslahi ya 1000,000. Ondoeni maharamia kati ya polisi, sukeni jeshi letu upya, kisha liwezeshwe kwa technolojia inayoona na kutoa taarifa ya matukio hasa katika maeneo yenye wasialam wengi kama huko pwani na mkuranga.
Watanzania ninaomba sana tuendelee kuishauri serikali japo inakataa kushauriwa. Hii la kukataa ushauri wa wanaoongozwa tulichukue kama tatizo linalohitaji tiba kama maradhi lakini hatwezi kujenga taifa pasipo kushauriana na kusikilizana. Ccm ninyi ndio wenye viburi, ninaomba muwe wa kwanza kujirekebisha. Tambueni bila taifa lenye amani ccm haipo.
Viongozi acheni kujenga matabaka miongoni mwa wananchi. Acheni kuwadharau watanzania na kuwabagua, huku mkifanya kebehi za wazi kwa viburi. Migawanyikio mnayoijenga ndiyo inayoondoka mishkikamano na mioyo ya uzalendo . Bila kuwa na umoja na uzalendo, hakuna suluhu rahisi ya matatkzo yanayoinuka.
NINAOMBA NISIITWE MCHOCHEZI MAANA SERIKALI INADHANI IKIWAUNGA WATU VINYWA NDIYO INASHINDA, KUMBE INAJENGA ROHO MBAYA ZA KIKATILI NA MTAWANYIKO UANOANZA KULIGHARIMU TAIFA KWA KASI HII YA AJBU.
Nini maana ya Gaid?Wachangiaji msifanyie hili suala mzaha Gaidi hana chama wala dini ni mnyama akivaa vesti ya kujilipua huwa hajui ataua nani. Wiki iliyopita huko Misri katika kanisa la Copti mliona jinsi raia wasiokuwa na hatia walivyouliwa.
Tuweke pembeni tofauti zetu na tujadili adui yetu mkubwa Gaidi. Leo tumepoteza vijana wetu saba tunatakiwa tufarijii familia zao sio kutoa comments za mzaha.
Kuna jambo lingine linashangaza sana. Mtu anakamata lori la mkaa, linataifishwa alafu mkaa ule ule unauzwa na mwenye mali hapati kitu. Kwanini msimbwambie mkaa wako tutauza na utapewa nusu ya mali yako. Badala yake mtu anabaki masikini milele.Mheshimiwa paschal mayalla,kuna siku nilileta Uzi humu kuwa kauli za Rais zitahatarisha usalama wa Taifa, maana kutatokea magaidi na majambazi . thread ilifutwa faster,anyway sikulalamika maana ilikuwa ni sensitive issue sana lakini ukweli utabaki kuwa pale pale kuwa kauli za Rais na kumkumbatia Bashite zitaliangamiza Taifa. Utekaji unaofanywa na taasisi muhimu za serikali nazo zinachangia haya yote,kinachofanyika ni visasi dhidi ya serikali.