Maulid Kitenge, huoni aibu kuwasaliti Watanzania wenzako? Hatimaye ukweli umefichuka

Maulid Kitenge, huoni aibu kuwasaliti Watanzania wenzako? Hatimaye ukweli umefichuka

Mwanzoni mwa mwezi huu wa pili 2022 kuliibuka ghafla na kwa kasi ya ajabu jitihada za makusudi za kujaribu kuwaondoa wamasai katika ardhi zao za kimila huko Ngorongoro kwa madai ya kwamba binadamu wamekuwa wengi huko Ngorongoro na hivyo wanaharibu ekolojia.

Vita hii ya kuwaondoa wamasai ilikuwa spear headed na nguli wa habari za michezo ndugu MAULID KITENGE ambapo alifanya ziara huko Ngorongoro na kutuambia WaTz kwamba eti ‘HALI INATISHA HUKO NGORONGORO’;

Wengi wetu tulihisi kuna jambo nyuma ya pazia, kwamba ghafla tu mtu wa michezo anaenda kushikia bango jambo lisilo la kimichezo; kiasi tulipata hisia kwamba amaelipwa pesa ili kueneza propaganda kwa maslahi ya waliomtuma.

Haya sasa, imekuja kugundulika kwamba hilo eneo la Ngorongoro anataka kuuziwa kampuni ya uwekezaji toka Falme za kiarabu inayomilikiwa na ‘Royal family’ kwa ajili ya kuendesha uwindaji wa kujifurahisha (game hunting), kampuni hiyo inaitwa OBC.

Sasa namuuliza ndugu yangu Kitenge, HUONI AIBU kuwasaliti WaTanzania wenzako?!

Nadhani Kuna Jambo halipo sawa hapa.

OBC anataka kununua Loliondo au Ngorongoro?
 
Kwahiyo kisa umeshawahi kulawitiwa tukuache tu uendelee na huo mchezo kisa sio mara yako ya kwanza, what nonsense is this?! Pia uwindaji at what cost?! Displacing thousands of Tanzanians?!
Rubbish,kalia hapa utulizw mihemko👇

20220216_225742.jpg
 
kuna siku magu alisema kuna kipande cha nchi kimeuzwa nikawa najiuliza ni wapi kumbe loliondo imeuzwa uuuuwiii jamaa wameichukua milele nasikia mswahili hutakiwi kuonekana huko waarabu wameweka hadi uwanja wao binafsi wa ndege
Na cellphone network zinasoma kama vile haupo TZ. KARIBU UARABUNI
 
Walipouza Loliondo gazeti la kwanza kuripoti taarifa ile (Motomoto) lilifunguwa mazima hadi leo.. Na hilo hilo lilifungiwa pia kwa kusema Zanzibar ilipojiunga na OIC. Kama kawa, ilipingwa kwanza na Serikali na watu kadhaa kuliwa vichwa.. LAKINI HADI LEO LOLIONDO SIYO YETU TENA.. Hao hao akina so called royal family walifanya yao.

LEO WAMERUDI TENA
Kuna ushahidi wa Wilaya ya Loliondo kuuzwa?
 
Hivi umeelewa vizuri hiyo habari? Au kiingereza kimekupiga chenga? Naona umewakamata wajinga wenzako..
Kwa kukusaidia wewe na mazwazwa wenzako, hiyo habari haihusiani na alichoongea Kitenge(i.e Ngorongoro), bali inaongelea kuwaondoa wamasai kutoka Loliondo.
..
.
Wewe ndio hujui chochote rudia kusoma vizuri na dictionary,kwa kifupi loliondo ilishapigwa mnada tangu enzi za mwinyi OBC inawinda wanyama na kusafirisha walio hai U.A.E kila wanapojisikia mwaka huu wameongezewa km 1500 kwa upande wa loliondo na akapewa na discount price kuchukua ngorongoro kwa hiyo maskini wapishe wenye pesa zao huu ndio ukweli mchungu.
 
Wewe ndio hujui chochote rudia kusoma vizuri na dictionary,kwa kifupi loliondo ilishapigwa mnada tangu enzi za mwinyi OBC inawinda wanyama na kusafirisha walio hai U.A.E kila wanapojisikia mwaka huu wameongezewa km 1500 kwa upande wa loliondo na akapewa na discount price kuchukua ngorongoro kwa hiyo maskini wapishe wenye pesa zao huu ndio ukweli mchungu.

Hopeless
 
Pamoja na hayo mbuga zetu zinapaswa kulindwa sana , hizo ni rasilimali za taifa. Ni rahisi kuanzisha makazi mapya ya binadamu kuliko kuanzisha mbuga za wanyama zenye hadhi. Siungi mkono uwepo wa maasai kuharibu mbuga wala wawekezaji.
Tuna jukumu la kulinda urithi wetu kwa miaka hadi mia ijayo sio kuendekeza siasa zisizojali masilahi ya taifa. Wanasiasa wengi wanaagalia tu kura za wamasai bila athari za shughuli za binadamu kuongezeka ndani ya Mbuga za wanyama.
Karne ya ishirini moja turuhusuje binadamu kuishi maisha ya zama za kale na kuwa kivutio kama wanyama
Watafutiwe eneo zuri wawekewe huduma za kijamii wanzishe maisha ya kisasa na ufugaji wenye tija
 
Nadhani Kuna Jambo halipo sawa hapa.

OBC anataka kununua Loliondo au Ngorongoro?
Ulichouliza ni sawa na kusema “OBC anataka kununua Tabata au Ilala?” Hapo utajibu nini, ukizingatia Tabata iko ndani ya ilala, na Tabata ziko nyingi humo humo ndani ya Tabata.
 
Pamoja na hayo mbuga zetu zinapaswa kulindwa sana , hizo ni rasilimali za taifa. Ni rahisi kuanzisha makazi mapya ya binadamu kuliko kuanzisha mbuga za wanyama zenye hadhi. Siungi mkono uwepo wa maasai kuharibu mbuga wala wawekezaji.
Tuna jukumu la kulinda urithi wetu kwa miaka hadi mia ijayo sio kuendekeza siasa zisizojali masilahi ya taifa. Wanasiasa wengi wanaagalia tu kura za wamasai bila athari za shughuli za binadamu kuongezeka ndani ya Mbuga za wanyama.
Karne ya ishirini moja turuhusuje binadamu kuishi maisha ya zama za kale na kuwa kivutio kama wanyama
Watafutiwe eneo zuri wawekewe huduma za kijamii wanzishe maisha ya kisasa na ufugaji wenye tija
Ufaransa inapata watalii milioni 100 kwa mwaka na haina mbuga za wanyama, tourist attraction walinayo ni heritage tourism.Waacheni wamasai waendelee kuishi kwenye maeneo yao ukizingatia pia kuwa utamaduni wao ni cultural heritage na kivutio cha utalii.
Kama ni wanyama tunazo mbuga nyingi tu za kutosha tuheshimu utu wa watu kuna nchi hazina mbuga za wanyama lakini maisha yanaendelea na wanapata watalii wengi ikumbukwe kuwa vivutio vya utalii siyo uwepo wa wanyama tu twende extra mile na tufikirie nje ya box.
 
Tulieni tulieni.....mlimtukana sana baba wa watu hadi mkamwita shetani. Tulieni mambo hayajaanza bado
Kwakweli, WaTz tutubu, la sivyo tutauzwa utumwani kwa waarabu kama miaka ya utumwa
 
Pamoja na hayo mbuga zetu zinapaswa kulindwa sana , hizo ni rasilimali za taifa. Ni rahisi kuanzisha makazi mapya ya binadamu kuliko kuanzisha mbuga za wanyama zenye hadhi. Siungi mkono uwepo wa maasai kuharibu mbuga wala wawekezaji.
Tuna jukumu la kulinda urithi wetu kwa miaka hadi mia ijayo sio kuendekeza siasa zisizojali masilahi ya taifa. Wanasiasa wengi wanaagalia tu kura za wamasai bila athari za shughuli za binadamu kuongezeka ndani ya Mbuga za wanyama.
Karne ya ishirini moja turuhusuje binadamu kuishi maisha ya zama za kale na kuwa kivutio kama wanyama
Watafutiwe eneo zuri wawekewe huduma za kijamii wanzishe maisha ya kisasa na ufugaji wenye tija
Watafutiwe eneo zuri ili kulinda hifadhi au ili kupisha mwarabu aje kuuwa wanyama kwa kujiburudisha?
 
Hopeless hata taahira anaweza kutyoe hilo neno, jibu hoja kama alivyokifafanulia yeye, kwamba kaongezewa km 1500 za Loliondo, pia kapewa offer ya Ngorongoro kama nyonheza kwa bei ya kutupa, jobu hoja.

Hakuna hoja yoyote ya kujibu hapo..!
Kwa kukusaidia tu:
Rudia alichokisema Kitenge, halafu soma hiyo habari yako uliyoweka "link", ukimaliza soma ulichoandika hapa kwenye huu uzi wako. Halafu uone ulipoingia chaka.
 
Kila
Ufaransa inapata watalii milioni 100 kwa mwaka na haina mbuga za wanyama, tourist attraction walinayo ni heritage tourism.Waacheni wamasai waendelee kuishi kwenye maeneo yao ukizingatia pia kuwa utamaduni wao ni cultural heritage na kivutio cha utalii.
Kama ni wanyama tunazo mbuga nyingi tu za kutosha tuheshimu utu wa watu kuna nchi hazina mbuga za wanyama lakini maisha yanaendelea na wanapata watalii wengi ikumbukwe kuwa vivutio vya utalii siyo uwepo wa wanyama tu twende extra mile na tufikirie nje ya box.
Kila nchi ina vivutio vyake vya utalii so kujilinganisha na Ufaransa ni kushindwa kuweka ulinganifu mzuri.

Sijui kama unajua madhara ya shughuli za binadamu kwenye mbuga za wanyama ?
Ni sawa na kusema tuwaachie watu
Wae deleze shuguli zao kwenye
vyan zo maji kwa sababu tu ni wazaliwa pale
Binadamu lazima awekee mipaka kwenye kila jambo maana ana ubinafsi wa asili,
Tunaweza kuangalia maslahi ya wachache lakini tukaleta hasara kubwa kwa taifa
Embu fikiri kama mbuga na misitu zisingelindwa kila jamii iliyo karibu nazo ikavamia na kuendeleza shughuli zake huko , nini kingetokea ?
Tuache siasa zisizo na faida kwa rasimali za taifa na kizazi kijacho
 
Watafutiwe eneo zuri ili kulinda hifadhi au ili kupisha mwarabu aje kuuwa wanyama kwa kujiburudisha?
Sijui kama umesoma vizuri post
Nimeeleza kwamba siungi mkono uwepo shughuli za wamasai wala za wawekezaji zinazoleta madhara kwenye mbuga
So rasilimali zetu tu najukumu la kuzilinda dhidi ya wenyeji au wawekezaji
 
Back
Top Bottom