Maumivu ya mwanamke kusalitiwa: Hana wa kumtetea, jamii inaona ni haki yake

Maumivu ya mwanamke kusalitiwa: Hana wa kumtetea, jamii inaona ni haki yake

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Maumivu ya mwanamke anaposalitiwa yanaweza kuwa na athari kubwa sana kihisia. Hali hii inaweza kusababisha machungu na kuumiza moyo. Kila mwanamke anaweza kuhisi maumivu tofauti na kuonesha hisia tofauti kulingana na uzoefu wake binafsi na mazingira ya kijamii.

Mbaya zaidi mwanamke amezungukwa na jamii ambayo inamjenga kuwa yeye kusalitiwa au kuumizwa kihisia ni sehemu yake na hapaswi kuonesha hisia za kukataa hali hiyo, mwanamke kajengwa kuvumilia usaliti kutoka kwa wanaume huku akidanganywa kwa kusifiwa kuwa ndiye mwanamke bora na anapaswa kukubali hali hiyo.

Imekuwepo kampeni kuwa mwanamke anayevumilia mwanaume wake kuwa na michepuko ni mke anayefaa kwani hujenga familia, bila kujali kuwa anaumia kihisia na kuteseka kwa msongo wa mawazo kwani hana sehemu ya kupeleka lawama wala kulalamikia kwa kuwa jamii imeshamtengenezea mazingira kuwa hayo ndiyo maisha yake na akienda kinyume na hapo hushambiliwa kuwa hana uvumilivu na kwamba hafai kuwa mke wa mtu.

Jamii imekuwa ikihubiri kuwa mwanaume anahaki ya kuchepuka na kwamba huo ndio uanaume na ndio fahari kwao kitu ambacho kina athari sana kwa ustawi wa familia na kinamuathiri sana mwanamke japo hana namna kwa kuwa tayari kashawekewa mazingira ya kukubaliana nacho japo kinamuumiza sana.

Baadhi ya maumivu ya kihisia yanayoweza kujitokeza ni pamoja na:
  1. Kuvunjika kwa uaminifu: Kusalitiwa kunaweza kuharibu msingi wa uaminifu katika uhusiano. Mwanamke anaweza kuhisi kuvunjika moyo na kuhisi kama imani yake imesalitiwa.
  2. Kukosa thamani: Mwanamke anaweza kuanza kuhisi kuwa hana thamani na kuanza kujidharau. Hii inaweza kusababisha kupungua kwa kujiamini na kujiona kuwa si wa kuvutia au wa kustahili.
  3. Hasira na huzuni: Kusalitiwa kunaweza kusababisha hisia za hasira na huzuni. Mwanamke anaweza kuhisi kuvunjika moyo, kuhisi kudhalilishwa, au kuwa na ghadhabu kuelekea mwenzi wake au mtu aliyehusika katika usaliti huo.
  4. Kupoteza imani katika mahusiano: Kusalitiwa kunaweza kusababisha mwanamke kupoteza imani katika mahusiano na kuwa na wasiwasi kuhusu uwezekano wa kusalitiwa tena. Hii inaweza kusababisha ugumu katika kuamini watu wapya na kujenga uhusiano mpya.
Ni muhimu kutambua kuwa kila mtu anaweza kuhisi maumivu tofauti na kuharibika kihisia kwa njia tofauti. Kwa wengine, maumivu yanaweza kupungua kadri muda unavyosonga na kupitia mchakato wa kupona, huku wengine wanahitaji msaada wa ziada kutoka kwa marafiki, familia, au wataalamu wa ustawi wa akili kusaidia kupitia maumivu hayo.
 
"Jamii imekuwa ikihubiri kuwa mwanaume anahaki ya kuchepuka"

"Imekuwepo kampeni kuwa mwanamke anayevumilia mwanaume wake kuwa na michepuko ni mke anayefaa na kwani hujena familia,

Kwa haya sikubaliani nawe kwani wenye hofu ya Mungu hatuwezi kushabikia haya wala kusema kuwa ni haki ya mwanaume kuchepuka

Hao wanaofanya kampeni au hiyo jamii unayoisema labda ni secret society lakini hawapo hadharani na mabango au hiyo kampeni unayosema

Mwanamke aheshimiwe kama mama na mzazi pia Ana heshima yake kwenye jamii na anaemdharau na kuchepuka eti ni haki yake basi atakuwa ana laana huyo
 
Tunachepuka kwa sababu ya ny*g* tu tunaoa kwa sababu ya maisha.

Shida nae wanawake wanatofautiana sana unakuta ana akili za maisha tabia njema lkn hana amsha amsha kitandan unapiga tu kupata watoto.

Kuna wengn aisee kitandan unamtafuna mpaka unatosheka lkn kwingineko kote hana jipya mitazamo yake ya kimaisha imekaa kitikotokitikitoki.

Dili ni kuchepuka lkn usigundulike ili usimuumize mtoto wa watu
 
Tunachepuka kwa sababu ya ny*g* tu tunaoa kwa sababu ya maisha.

Shida nae wanawake wanatofautiana sana unakuta ana akili za maisha tabia njema lkn hana amsha amsha kitandan unapiga tu kupata watoto....
We unaona mwenye akili hakuridhishi,ushawahi jiuliza kama wewe unamridhisha?itakuaje siku ujue anachepuka alafu akwambia humridhishaji kitandani?utamsamehe?
 
Sio kwamba jamii imemjengea mwanamke huo mtazamo, hii ni nature tokea dunia imeanza mpaka leo hii kuanzia kwenye vitabu vya dini mpaka kwenye history za kiafrika polygamy ndo utaratibu.

Hivyo jamii imemnyanganya mwanaume haki ya kuwa na wake wengi na matokeo yake ndo haya uliyoyaandika.
Haki tunyimwe sisi nyie ndo mnalalamika
 
Naposema jamii namaanisha kundi kubwa la watu, kama upo wewe unayeona si vyema basi una heri na uendelee ivyo, kampeni si lazima iwe ya kutembea na mabango, angalia hata kwenye mitandano kijamii wanaume wanavyojiproud kwa uchepukaji huku wakitoa sababu kuwa wao wameumbiwa kuwa na tamaa za kutamani wanawake wapya nk hiyo ni kampeni kwani huwafanya waliokuwa wametulia waone kuwa ni sawa kuchepuka
 
Back
Top Bottom