Maumivu ya wamiliki wa European cars!


All the best
 
Issue ya air_flow meter tu kwenye japanise hua inawatoa jasho mafundi, wanakununulisha ma_coil, mara plugs, filter, wanafungua mpaka tank_ badilisha pump, hapo mbele wana fumua kote mpaka top_cover, mara valve [emoji2962] alafu unakuja ishu ipo kwenye ki_thermometre kidogo ndani ya air cleaner[emoji16][emoji16][emoji55] fundi maiko ana choshaga sana
 


Upo sahihi mkuu. Na siyo kwa air flow tu... kuna vitu vingi kwenye mijapani hasa toyota.

Nimewahi ongea humu mara kadhaa, kwamba gari za japan hususan toyota zinasifika kwamba siyo mti wa Christmass, that is too bad kwa sababu kuna matatizo yanatokea na hayawashi warning light. Likikukuta hakuna rangi utaacha kuona.

Unlike European ambazo zipo very sensitive kuwasha warning lights.
 
Yeap! Matatizo mengi ya mjep hayana warning light kabisa mpaka uihisi ua izime kabisa hata kwa dignosis hupati maana hakuna switch wala sensor za ku detect hizo kasoro, ila hawa wengine, muda wote gari inakua inaongea na wewe inakua kama mtoto wako kabisa, zingine zinasoma mpaka kiwango cha upepo kwenye tire, zina soma mpaka aligment sio mjep hana muda huo
 
Fix zipi? Tatizo mnatumia gari za kijapan mainly Toyota na za zamani, sasa ungejua ya kuwa gari ya mjapani latest model spare parts genuine ni gharama sana usingekuja kucomment upuuzi hapa.
hata iwe nagarama vipi haiwezi kufikia gari yaulaya. ukijua bei yagari ndio utachanganua beiya spare zake.
 
hata iwe nagarama vipi haiwezi kufikia gari yaulaya. ukijua bei yagari ndio utachanganua beiya spare zake.
Tatizo lako umekariri. Sisi wakati tunakua miaka ya 80 hapa Bongo yalikuwa yamejaa magari ya kizungu BMW, Peugeot , Renault , Opel nk. Sasa jiulize miaka ya 80 na sasa kipindi gani ilikuwa rahisi kupata Spare Parts za ulaya? Usichokifahamu ni kwamba Biashara tu imebadilika baada ya Soko la Mjapani used kushika tamu, ila European car makers wakubwa kama Landrover, Peugeot, na wengine kibao wote walikuwa na ofisi hapa Dar na mikoa yote mikubwa. Mabadiliko ya kibiashara yalikuja hadi kubadili mindset za watu juu ya magari ya Ulaya. Baba zetu walitumia magari ya Ulaya 80's kipindi hata internet hakuna na walimudu..leo hii kuna kila kitu lakini kijana wa kisasa anaogopa gari la Ulaya. its a big Joke.🤣🤣
 
Hizi gari zetu laiti zingekuwa na sensor kama European cars wengi tungekuwa tunapaki Tu na ishu kubwa inakuja pale gari inapoleta shida ukienda Kwa fundi unaweza kubadilisha spare zaidi ya 5 kumbe tatizo lipo sehemu nyingine kitu ambacho Kwa magari ya ulaya tatizo lingejulikana moja Kwa moja.

Wabongo sisi tunashindwa Tu kupiga hesabu vizuri ukiangalia huku kwenye Toyota huwa tunatumia pesa nyingi kutibu tatizo dogo Sana tena sometimes unaweza kwenda Kwa mafundi zaidi ya tano na Huko kote unapita kuachia pesa
 
Mafundi wetu huwa wanachosha sana.

Sent from my CPH2219 using JamiiForums mobile app
 
Kama ni hii umepigwa


Badili mtazamo wako kuhusu BMW
 
NDUGU ACHA UONGO KWANI UNAPOLETA UONGO UNAPATA FAIDA GANI AU LIKES NA COMMENT'S ZIKIWA NYINGI UNALIPWA SIKU HIZI JF.

1, UNAPOSEMA MADALALI WA BIAFRA NDO WALIKUUZIA HYO BMW UNA MAANISHA NI OFISI YETU YA MACHACHU ENTERPRISES AMBAYO IKO HAPO BIAFRA NA NDO HUWA TUNAPAKI GARI ZETU HAPO UWANJANI AMBAKO NIMEFANYA KAZI KWA MIAKA 5 NA HATUJAWAHI KUINUNUA WALA KUIUZA HIYO GARI.

2,NA TOKA TUMEANZA KUUZA GARI HAKUNA GARI AMBAYO ILISHAWAHI KURUDISHWA AU KULETEWA MALALAMIKO YOYOTE REFER KWENYE THREAD YETU YA MAGARI USED TZ KAMA UTAPATA LALAMIKO LA MTEJA HATA MOJA

3, HAKUNA GARI YA JAPAN WALA EUROPEAN CARS AMBAYO ITAKUSUMBUA ENDAPO UTAKUWA UNAIFANYIA SERVICE SAHIHI KWA WAKATI SAHIHI,HIVYO USIOGOPESHE WATU,UNAWEZA KUWA NA RUNEX IKAKUPASUA KICHWA HALI YA KUWA MWENYE BM X3 AKAWA ANAPETA.
 
Mkuu, gari yenyewe used unataka spare parts mpya za nini?
 
mkuu ukiingia bara barani majibu unayapata live wengi wanamiliki gari zakijapani.kwamaana hio hizo ndio gari zahali yachini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…