Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)

MAUMIVU YASIYO KWISHA(ENDLESS PAIN)...!!

Sehemu ya Kumi na Nane
.
#Ilipoishia:
Careen aliniuliza maswali mengi mfululizo ambayo yalinifanya niuone mdomo mzito.
Sikujua nini cha kumjibu wakati aliponiuliza kama nampenda.
.
Kauli yake ya "Matendo yako yanafanana na Peter" ilizidi kunipunguza nguvu ya kunyanyua mdomo kumjibu.
.
Nilibaki kimya huku nikiwa nimeinamia chini, nilikua na maswali mengi sana kichwani.
Careen atanichukuliaje nikimuambia "Ndio nakupenda ", je atanitenga kama Peter?
Itakuwaje nikimuambia ukweli halafu anikatae?.
Nilijikuta mdomo mzito kama nimefungwa mzigo wa tani 1000.
.
#Inaendelea:
Careen akanishika bega, na kuniambia "Chris, niweke wazi leo hii".
.
Moyo ukanipiga paaah, nikainua kichwa juu na kuzidi kupata wasiwasi.
Mikono yangu ilikosa nguvu na kuanza kutetemeka, nikajitahidi kujizuia ili Careen asigundue wasiwasi wangu.
Kuna sauti ndani yangu ikawa inaniambia "Kuwa mwanaume, funguka ya rohoni ".
Na sauti nyingine ilikua na nguvu zaidi, ilikua ikiniambia "Chris usiseme lolote, acha kabisa, atakukataa na kukutenga kama Peter".
.
Nilikaa kimya kwa muda zaidi, lakini mwisho nikajisemea kimoyo moyo "Liwalo na liwe, leo namuambia".
Nikataka kufungua kinywa, lakini bado nikasita.
.
Nikajisemea kimoyo moyo "Chris sema".
Nikanyanyua kinywa, na kumjibu "Yeah, ndio nakupenda. Tena zaidi ya sana".
Careen alistuka, akanitazama.
.
Inasemekana kuwa mwanzo huwa mgumu, nililiamini hilo.
Japo nilipata ugumu kutamka kauli ya kwanza, lakini baada ya kutamka hiyo kauli, ndipo nilipoanza kupata nguvu ya kunena zaidi.
.
"Careen nakumbuka nilikupenda tangu siku ya kwanza nakuona darasani, siku yetu ya kwanza kuja chuo.
Niliwaza mengi sana kukuhusu, na nilitamani kufanya mengi sana na wewe." - (Nilinyanyua kinywa na kumtamkia Careen).
.
Careen alikosa ujasiri wa kunitazama usoni kama mwanzo, akashusha uso wake na kutazama chini.
Nikampigilia misumali zaidi.
"Najua unajiuliza kwanini sikukwambia siku zote hizo.
Mwanzoni sikutaka kuzungumza sababu nilijua tayari una boyfriend, sikutaka kuharibu mahusiano yako.
Na hata mlipoachana sikutaka kukugusia hili jambo, nilitaka nikupe muda wa kuyasahau mapito yako kwanza". - (Nikanyamaza kidogo, na kumeza mate).
.
Niliiona mikono ya Careen ikitetemeka kwa mbali, sikutaka kupoteza nafasi hiyo.
Nikajisogeza karibu na kumshika mikono yake.
Careen alizidi kutazama chini.
.
Nikaendelea kuzungumza kwa hisia zaidi ili maneno yapenye moyoni mwake.
Nikamwambia "Careen, najua unapitia maumivu ya kutendwa. Najua umekosa kabisa imani juu ya mapenzi, na wala huwaamini tena wanaume.
Lakini kusema ukweli wanaume wenye upendo wa kweli wapo, wanaojua thamani yako wapo, wanaokupenda wapo, wanaotamani wangekua wako milele wapo.
Usiyachukie mapenzi, Usinichukie hata mimi ninayekueleza hisia zangu leo.
Nipe nafasi nikuonyeshe maana halisi ya upendo, nikuonyeshe thamani yako halisi.
Siwezi kukupa ahadi za uongo, nipe nafasi nikuonyeshe kwa vitendo.
Na kama bado haupo tayari kuingia kwenye mahusiano, niko tayari kukusubiri kipenzi hata ukichukua miaka ".
.
Nikanyamazia hapo, Careen akanigeuzia macho na kunitazama.
Akaniambia "Chris wanaume mmebarikiwa maneno mazuri mwanzoni, lakini matendo sifuri.
Leo unazungumza maneno mazuri, unalia, unanyenyekea, lakin ukishapewa nafasi tu unabadilika.
Chris, mimi si mtoto, nawajua wanaume vilivyo".
.
Alianza kuniletea vikwazo, lakini sikukata tamaa.
Nikamjibu "Kipenzi, hii ni Africa.
Wanaume wengi hawajui thamani ya wanawake, wala jinsi ya kuishi nae.
Ila wachache tu ndo wanaojua.
Tatizo ni moja tu Careen wangu, unapopewa kiroba kilichojaa mawe, ni ngumu sana kutambua kama kuna kipande kimoja cha dhahabu ndani.
Careen wewe mrembo sana, umebarikiwa kwa mengi, lazima utasumbuliwa na wengi walaghai ambao watakutumia na kukuacha.
Lakini hiyo isiwe sababu ya wewe kushindwa kutafuta dhahabu ndani ya kiroba kilichojaa mawe.
Niamini na unipe nafasi, hutojutia. Nakupenda sana.". - (Niliishia hapo, na kuamua kumsikiliza).
.
Careen alikaa kimya kwa muda mrefu sana akiwa kama anatafakari.
Lakini mwisho nilimuona anashika mkoba wake.
Na kuniuliza "Naweza kuondoka??? ".
.
Nikatingisha kichwa kuashiria ndio.
.
Akanijibu "Itakua vizuri kama hatutozungumzia hizi mada tena. Siko tayari kuwa na mahusiano na yeyote yule".
.
Jibu lake lilinistua sana, likaniumiza na kunifanya nianze kujilaumu kwanini nimemwambia ukweli kama nampenda.
.
Pindi anataka kuondoka, nikamuita "Careen".
Akageuka na kunitazama.
Nikamwambia "Baada ya yote tuliyozungumza, naomba usinitenge.
Tuendelee kuwa kama kaka na dada, usinichukie".
.
Careen akaniangalia sana, mwisho akanijibu "Siwezi kukutenga, kuwa na amani ".
Kisha akageuka na kuanza kuondoka.
.
Nilibaki nimekaa kwenye benchi, hata nguvu ya kunyanyuka sikuwa nayo tena.
Maswali mengi kichwani, ina maana leo ndio namkosa Careen??
Inamaana na mimi nimeshindwa kama Peter??
Inamaana na mimi nitavaa dera??
Niliumia sana.
.
Sikupata hamu ya kufanya lolote lile, nilinyanyuka na kuanza kutembea kama mtu aliyetembea umbali mrefu.
Sikuwaza kupanda boda boda, wala kufanya nini, njiani nilikua kama sioni watu.
Kichwa kilikua kizito, nilihisi maumivu ambayo sikuwahi kuhisi.
.
Nilijilaumu kwa mengi, na hapo niliamini kuwa mapenzi sio mchezo wa kubashiri.
Nilijiona mjinga sana kuwekeana mechi na Peter, nikajiona mjinga kumcheka Peter.
Nikakumbuka mateso na misukosuko niliyopitia juu ya Careen, sikuamini, baada ya mateso yote nakuja kutoka mikono mitupu.
Uvumilivu wote ule, leo nimekosa mbivu na kupata maganda.
.
Nilipofika hostel, nilikuwa naona kama chumba kikubwa.
Kitandani hapalaliki, kwenye kiti hapakaliki.
Nilizunguka chumba kama chizi.
Usiku wangu ulikua mrefu sana, nilianza kuelewa kwanini baadhi ya watu huamua kujinyonga baada ya kuachwa, maumivu hayavumiliki.
.
Kesho yake asubuhi nilikumbuka kumtafuta kwenye simu Dr Leonard, angalau anipe tulizo la moyo kwa maneno yake yenye kufariji.
.
Alipokea simu, na kuniomba nimuelezee vizuri.
Nilipomaliza kueleza akanipa pole kwa yote yaliyojiri lakini alikuja kuzungumza mambo yaliyonipa nguvu mpya na kujikuta nikianza kupata amani.
.
Dr Leonard: Kwanza nikupe pole kwa maumivu ambayo unapitia. Lakini pili nikupe hongera kwa kuchukua hatua kubwa sana ya kumpa ukweli wa moyo wako.
Usijutie kwa jambo ulilofanya, unatakiwa kufurahia mambo mawili.
1: Umemweleza hisia zako, sababu mwanzo kila jambo ulilokua unafanya alikua akidhani ni kama kaka yake. Lakini kuanzia sasa ataanza kurudisha mawazo nyuma na kukumbuka mambo yote uliyowahi kumfanyia, ndipo hapo ataanza kutengeneza picha mbalimbali kichwani mwake kukuhusu wewe.
Na jambo lolote utakalokuwa unamfanyia kuanzia sasa litakua linamfanya ahisi kuwa unafanya sababu unampenda.".
.
Alinyamaza kidogo, nikaanza kupata hamu ya kumsikiliza zaidi.
Akakohoa kidogo na kuendelea kuongea "Namba mbili: Furahi sababu amekuhakikishia nafasi ya urafiki, hiyo itakupa wepesi wewe wa kuendelea kumfanyia vitu vitakavyo mfanya akupende zaidi. Kwahiyo itumie vizuri hiyo nafasi, usikate tamaa mapema, mwanaume huwa hachoki kupambana.
Hiki ndo kipindi unachotakiwa kumfanya aamini upendo ulionao kwake kwa vitendo.
Ametoka kutendwa, hebu usikate tamaa, muonyeshe utofauti kati yako na boyfriend wake aliyemtenda, hakika atakupenda bila kutegemea".- (Alizungumza kwa kujiamini na kumaanisha alichokuwa anasema).
.
Hapo nikaanza kupata mwanga juu ya kitu nachotakiwa kufanya, lakini bado nikawa na hofu kuwa tayari nilishakataliwa, itabadilikaje zile kauli alizosema.
.
Dr Leonard: Chris unahofia kukataliwa, tena umekataliwa kwenye jaribio la kwanza tu.
Kama ulikua hujui, mwanamke yeyote mwenye misimamo na kuhitaji mahusiano serious, kamwe hawezi kukukubalia kiurahisi rahisi.
Anahitaji muda wa kukuwazia, kukutafakari na kutoa maamuzi.
Sasa kama umekata tamaa mapema, jua kwamba utamkosa.
Lakin kama hautokata tamaa mapema, na uko tayari kumfanya awe wako, basi jione kuwa kuanzia sasa uko ndani ya nusu fainali, bado fainali yenyewe.
Pambana Chris, mi naona ushindi kabisa hapo.
Angekua hakupendi, hata hiyo nafasi ya urafiki usingepewa".
.
Alimaliza kwa kusema hivyo, nilipata amani sana na nguvu mpya.
Nikasema sasa, Careen atakua wangu tu, sikati tamaa kamwe.
.
Nikaagana na Dr Leonard, akanipa maneno ya mwisho tu "Unakumbuka niliwahi kukwambia mwanamke anapenda nini? Basi usifanye makosa wakati huu" kisha akakata simu.
.
Wakati huo huo, nikaanza kwa kumtumia sms Careen, lakini hakujibu.
Sikukata tamaa, nikatuma tena jioni, lakini sikujibiwa.
.
Majira ya saa 2 usiku, ikabidi nimpigie simu, akapokea.
Alikua kapoa mwanzoni, lakini kila muda ulivyozidi kwenda nilizidi kunogesha maongezi na kujikuta tukizungumza kwa muda mrefu zaidi.
.
Siku kadhaa zilipita huku nikiwa nazidi kumsogeza Careen karibu.
Sikuleta papara nyingi, ilibidi nitumie akili zaidi kuliko kukurupuka.
Nilianza kuona mabadiliko kwa Careen, alianza kunizoea zaidi ya mwanzo na kuniweka karibu zaidi.
Nilijenga nae ukaribu kiasi cha kula nae, kufurahi nae, kumshauri, kusoma nae.
.
Nakumbuka niliwahi mwomba anisindikize hostel, akakubali.
Tulipofika sikutaka kufanya nae lolote zaidi ya kuweka movie, na kumuandalia kinywaji na biscuits.
Nikamuuliza angependa kula nini, akasema "Hapana nitaenda kula nyumbani".
.
Sikutaka aondoke hivi hivi bila kula, nikamlazimisha sana mwisho akakubali na kuniambia angependa kula wali na samaki.
.
Kwavile nilifunzwa vyema kwetu, suala la kupika wala halikunipa tabu.
Nilimuacha ndani na kwenda kununua vinavyohitajika, kisha kumuandalia chakula.
.
Tulikaa kwa pamoja na kula, hakula sana, akajifanya ameshiba.
.
Sikutaka kuipoteza nafasi hiyo, nikamwambia "mmh umekula kidogo tu,"
.
Careen: Kweli nimeshiba.
.
"Hujashiba bwana, kula hata kidogo, au nikulishe" - (Nikazungumza kimasikhara huku nimechota chakula kwenye kijiko na kumpelekea mdomoni.).
.
Akawa kama anaona aibu, lakini mwisho akanyanyua kinywa na kula huku anatoa tabasamu.
Nilifurahi sana na kumuongeza vijiko kadha wa kadha mpaka aliposhiba na kunipa shukrani kwa chakula kitamu.
.
Mazoea yalizidi, kuna siku nilimwomba Careen nitoke nae out usiku angalau tupate wasaa wa kuzungumza pamoja, na nilitaka nitumie nafasi hiyo kumkumbusha Careen jinsi gani nampenda sana.
.
Alikataa sana, na kusema kuwa hawezi kutoka usiku na wala si mazoea yake na wazazi wake hawataruhusu.
Nilizidi kuvutiwa zaidi na misimamo yake, na kuona kuwa Careen ni wife material.
.
Nikabadilisha maamuzi na kumuomba tutoke mchana, iwe mahala tulivu ambapo tunaweza zungumza na kufurahi pia.
Akakubali na kuniambia "Twende South Beach, jumamosi hii".
Nilifurahi sana baada ya kusikia maneno hayo.
.
Ni wiki 2 sasa tangu Abdulrahman na Peter watengane.
Na bado mnafki hajajulikana, ambaye anatoa siri zetu kwa Peter na Nasra.
.
Siku ya Alhamisi ya juma hilo, nilikua maeneo ya KBG nikipata kinywaji na mishikaki pamoja na Abdulrahman huku tukiwasubiria marafiki zetu wengine nao waje.
.
Tukawa tukipiga story mbalimbali, lakini ghafla ikaingia simu kutoka kwa Careen.
Tukazungumza kwa dakika kadhaa, na kuagana na kukata simu.
.
Abdulrahman akazungumza kwa kingereza akimaanisha "Naona siku hizi unazidi kumnogesha".
.
Nikacheka na kumjibu "Dah acha yani, mambo yanazidi kunoga".
.
Abdulrahman akanisisitiza nisijicheleweshe sana, nikajikuta namweleza "Usijali bro, na jumamosi naenda nae South Beach, nitamfungukia tena''.
.
Akafurahi sana kusikia hivyo, na kunipa $100(dollar 100) kama kilinda wallet kwa siku hiyo.
Walipokuja marafiki zetu(Ivan, Ramadhan, Hasheem) tukaendelea kufurahia kwa vinywaji na mishikaki.
.
Majira ya saa 3 usiku tukaagana na kutaka kuondoka, lakini jambo la kushangaza Ivan akaomba lift kwenye gari la Abdulrahman.
.
Nilipatwa na maswali mengi kichwani nikiwaza itakuwaje wawili hawa wakienda pamoja, nikahofia siri isifichuke kuwa wote wanamtaka msichana mmoja.
.
Nikajipa moyo kuwa haitowezekana, na tukaagana na kuondoka.
.
Siku ya Jumamosi ya miadi ilifika, na kukutana na Careen maeneo ya South Beach.
Nililipa kiingilio na sote tulienda kutafuta mahala pazuri pa kupumzika ili tuweze kuyazungumza vizuri.
Nikamchukua Careen mpaka maeneo ya ufukweni na kupumzika nae.
Tukapiga story mbalimbali, za vituko na matani, mwisho nikaanza kuleta story za hisia.
Nilimuona akianza kuonyesha utofauti, nikamshika mkono wake na kuanza kuubusu busu huku nikimweleza jinsi gani ananivutia.
Jinsi gani nampenda na natamani angekuwa wangu siku zote za maisha yangu.
Alinitazama na kuonyesha utofauti wake na siku ile ya kwanza, leo alinitazama na kuonyesha tabasamu lake, akaniambia "Chris nakupenda sana, na umenifanya nikuone utofauti kati yako na wanaume wengine ".
Akazungumza mengi sana, na hasa kunisifia.
Nilimkamata na kumpiga denda kwa dakika 5.
Na nilipomaliza nilimkombatia kwa nguvu sana.
.
Baada ya yote hayo tulianza kuchekeshana mambo mbalimbali yaliyopita kati yetu, lakini ghafla akaniambia "Tusimame".
.
Nikashangaa, "Tusimame tena?".
Nilipatwa na mshangao, lakini hakunijibu, akanyanyuka na kunishika mikono na kuninyanyua.
.
Nikanyanyuka, akanitazama usoni.
Akawa kama mtu anayenivizia hivi, kisha kunibusu shavuni na kukimbia huku akicheka.
.
Nikacheka sana, lakini niliamini kuwa lile busu lilikuwa na maana kubwa sana.
Nikamtazama na kumuuliza "Unaenda wapi sasa?? "
.
Akanijibu "Narudi sasa hivi, naenda kuchukua vinywaji".
.
Nikabaki namtazama huku nacheka, akaenda kuchukua vinywaji na wakati anarejea, akiwa kama hatua 15 kabla ya kunifikia.
.
Ghafla nilistukia kuna mtu kanikombatia kwa nyuma huku akisema kwa nguvu "Wow baby wangu".
.
Careen alistuka na kusimama baada ya kuona tukio lile.
Nami nilistuka na kutazama ni nani aliyenikombatia.
Nikatupa macho nyuma yangu, sikuamini macho yangu niliyemuona.
.
Akaongea tena kwa sauti "Chris baby wangu, nilikumiss sana ".
.
Hapo nilihisi kuwa pilau tayari limeingia mafuta ya taa baada ya kumuona Careen akiwa ameviachia vinywaji vilivyokuwa mikononi mwake na kuvidondosha chini huku akionekana akiwa haamini kile alichokiona.
.
Nilirudia tena kuitazama sura ya aliyenikombatia, sikuwa nikimjua hata kidogo, wala sijawahi kuonana nae hata mara moja.
Nikamsukumiza, akadondoka chini.
.
Kutazama mbele, nilimuona Careen akianza kuondoka kwa hasira.
Nikaanza kumkimbilia ili nimueleweshe kuwa huyo dada aliyenikombatia simjui
.
.
Je ni nani aliyemkombatia Chris?? Na kwanini au katumwa na nani??? Careen atamuelewa tena Chris??? Na nini kitajiri hapo baadae???
.
Usikose sehemu ya 19

Sehemu ya Kumi na tisa soma hapa Maumivu Yasiyo kwisha (Endless Pain)
 
Broo ingekuwa mm ningekimbia tuu, yaan nisingejali watanionaje, mm nngechanganya miguu tuu
 
Broo ingekuwa mm ningekimbia tuu, yaan nisingejali watanionaje, mm nngechanganya miguu tuu
Maamuzi ya mtu hua yanatofautiana sana hivyo kwako ni kawaida ila kwa wengine ni ngumu.
 
Mkuu hii ni bonge la story ila ungefanya kuwa tag wapenda story wote humu jukwaani ili na wenyewe waje waipitie
 
Mkuu hii ni bonge la story ila ungefanya kuwa tag wapenda story wote humu jukwaani ili na wenyewe waje waipitie
Asante mkuu kwa taarifa pia tunaweza saidiana kuwaita wahusika.
 
Nimewahi kurudi kazini kwa ajili ya story hii [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1319][emoji1319][emoji1319][emoji1319]
 
Bando litaisha kwa kuchungulia chungulia jàman[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…