Mauzauza: Nasumbuliwa na ndoto za kuhusu wazee wangu

Mauzauza: Nasumbuliwa na ndoto za kuhusu wazee wangu

Ndugu yangu sifahamu namna ya kuziombea ndoto kibibilia,na isitoshe ndoto za wazee wangu naziota sana,sielewi tatizo ni nini,nimeuliza baadhi ya watu wazima wamenambia Nina mizimu ya ukoo,so sielewi ndugu,labda unisaidie jinsi ya kudil nazo.
 
Ndugu yangu sifahamu namna ya kuziombea ndoto kibibilia,na isitoshe ndoto za wazee wangu naziota sana,sielewi tatizo ni nini,nimeuliza baadhi ya watu wazima wamenambia Nina mizimu ya ukoo,so sielewi ndugu,labda unisaidie jinsi ya kudil nazo.
Mizimu=WAFU=KUZIMU.

Kujitenga na Roho ya ukoo na Mizimu Si KAZI ndogo.

Watafute waliookoka mfanye maombi kama team.

Ni vita Hasa, Si mchezo. Lakini nikutir moyo hutapigana pekeako. Malaika wa YESU watapamvanabpia kuwasaidia.

Ubarikiwe.

Amen
 
Kuna maelezo natamani nkuandikie ila nahs huta nielewa ila nenda kanisan waombee Misa hata zile za asubh kwa majina Yao mana kuota wanakuomba soda n kwamba wanakiu ya kua karbu na ww au kujumuika pamoja na ww waombee Misa wapate kupumzika mahali pema na roho zao zkae toharan pili udi na uban n chakula kwa viumbe wanao onekana na wasioonekana kwaio acha kutumia mana n kama unawaendekeza watakusumbua sana mwsho wa siku wataivuta nafs yako walipo mana wao n roho,nafs kwa sasa ndio mana mpka ulale ndio nafs yako inaweza kuwasiliana nao kama kwenu mna mila na amjasimama vzur katiba ibada chukua maziwa kwa ajil ya uyo anaeomba soda na pombe kwaajili ya baba kama alikua anatumia kunywa kidogo uku ukinena Kisha mwaga chin ardhin ukiwataja majina like wazee wangu karibuni kwa hik kidogo japo mpate na nyie Kisha mkapumzke kwenye makao yenu unakunywa na kumwaga chin apo shughuli imeisha na pombe ya mazao sio kvant
 
Pole, ila Usichanganye Imani kama unatumia udi, chumvi, ubani, hirizi na vinginevyo tumia hivyo tu.

Na kama unamkiri Yesu Kristo Bwana au damu yake hakikisha una uhalali wa kulitumia. Uwe safi hakuna chochote kitakacho kusumbua maana yeye hachangamani na yeyote.

Jina lake na Damu yake linajitoshereza kukusaidia maana yeye ndio njia ya kweli na uzima huwezi fika kwa Baba bila kupita kwake.

Halafu hayo mandoto ya mababu, wazazi, mke au ndugu waliokufa kiimani sio ishara nzuri kwani hakuna ushirika kati ya wafu na walio hai ni roho zinazotaka kukurudisha nyuma na kupooza mambo na mipango yako
 
Sijachanganya lolote,damu ya Yesu nilitamka usingizi wakati nakabwa.Hii nyumba nimeambiwa aliyekuwa anaishi alikuwa mganga na alikuwa anaitumia kuagulia watu.Muda sio mrefu katoka kunipigia,sikuwa kwenye mazingira ya kupokea,nikitoka job ntampigia nione alikuwa ananitafutia nini.
Kama tatizo ni nyumba, basi yakupasa kuvunja maagano yote yaliyowekwa kwenye hiyo nyumba,, mtumaini Bwana kwa moyo wako wote naye atayanyoosha mapito yako.
 
Mie ni mkristo Mkatoliki,mwanachama wa Shirika la moyo mtakatifu wa Yesu,naamin katika ukombozi kupitia damu ya Yesu iliyomwagika msalaban na kuleta wokovu.Sala nyingi nisalizo zinaangukia ktk kuitaja damu ya Yesu 🙏
UKWELI ni mchungu,

Toka kwenye Dini hiyo Ili upambane katika Kweli. IBADA ya Rozali na misaafu ni IBADA isompendeza Mungu. Dini hiyo Ina nakandokando mengi na Machukizo mbele ya Mungu hivyo huwezi PATA ushirikiano mzuri Kutoka Kwa Mungu wa Kweli.

Dini hiyo walipokufa wazazi wako mliwasha mishumaa na Huwa mnawaombea Wafu, hiyo ni IBADA ya wafu, ndiyo sababu kuu ya wafu kukufuatilia, wapo kuzimu hao.

Kama unataka Ukombozi wa Kweli, Funga na uombe Mungu atakuonyesha namna sahihi ya kupambana vita hiyo.

In short, Madhabahu ya Dini Yako Haina ushirika na Mungu wa Kweli.

Amen
 
Kama tatizo ni nyumba, basi yakupasa kuvunja maagano yote yaliyowekwa kwenye hiyo nyumba,, mtumaini Bwana kwa moyo wako wote naye atayanyoosha mapito yako.
Solution ni kuhama.

Nyumba hakuijenga Yeye iweje avunje mikataba ya nyumba ya mtu mwingine ambaye anaamini mikataba hiyo ni halali sawasawa na miungu yake?

Tupambanie tujenge nyumba zetu na tumkabidhi Mungu wetu azilinde, au ahamie nyumba ya watu wenye mikataba na madhabahu inayoendana na Imani ya Mungu wake.

Amen
 
Kuna maelezo natamani nkuandikie ila nahs huta nielewa ila nenda kanisan waombee Misa hata zile za asubh kwa majina Yao mana kuota wanakuomba soda n kwamba wanakiu ya kua karbu na ww au kujumuika pamoja na ww waombee Misa wapate kupumzika mahali pema na roho zao zkae toharan pili udi na uban n chakula kwa viumbe wanao onekana na wasioonekana kwaio acha kutumia mana n kama unawaendekeza watakusumbua sana mwsho wa siku wataivuta nafs yako walipo mana wao n roho,nafs kwa sasa ndio mana mpka ulale ndio nafs yako inaweza kuwasiliana nao kama kwenu mna mila na amjasimama vzur katiba ibada chukua maziwa kwa ajil ya uyo anaeomba soda na pombe kwaajili ya baba kama alikua anatumia kunywa kidogo uku ukinena Kisha mwaga chin ardhin ukiwataja majina like wazee wangu karibuni kwa hik kidogo japo mpate na nyie Kisha mkapumzke kwenye makao yenu unakunywa na kumwaga chin apo shughuli imeisha na pombe ya mazao sio kvant
Hizo ni IBADA za mizimu.

Mungu amekataza ushirika kati ya Walio hai na waliokufa.

Ukiendelea na IBADA hizo, utakapokufa, utaenda direct KUZIMU.

Dini hiyo haikutokana na Mungu, wameingiza IBADA za kipepo zifanyike na Wana wa Mungu mkiaminishwa kuwa zinaruhusiwa na Mungu ambapo Si Kweli.
 
Habari za asubuhi wanaJF, hope tumeamka salama kwa uweza wa manani🙏

Wiki kama mbili nilikuwa nasumbuliwa na ndoto za kuhusu wazee wangu (RIP, manake wote walishatangulia mbele za haki), walikuwa wananijia ndotoni wakiomba niwapatie vinywaji, sehemu nyingine niliota napeleka vyakula,wakaniomba na vinywaji, specifically soda, aliniomba Bibi mzaa mama.

Yani nilikuwa naona ndoto za kuwahusu wao na ndugu wengine walio hai katika familia. Ni wiki niliyokuwa najihisi huzuni na upweke sana bila sababu.

Basi Jumatatu nilipotoka job nikaenda kwenye msikiti wa jiran Kuna duka la dawa za kisuna nikanunua udi flan hivi huwa unatumika kuombea watu waliotangulia mbele za haki. Nikarudi nyumbani nikaoga, nikala then nikauchoma nikiwaombea pumziko hasa Bibi na mama, then kwenye saa kumi na moja nikalala,nimejiwekea utaratibu wa kulala mchana nikiwa free.

Ndani ya nusu saa toka nilale nikaota mwanamke mmoja mtu mzima kavaa upande wa kanga kajifunika Hadi kifuani, kasimama dirishani mwa chumba changu lakini kanipiga mgongo, hivyo sikumwona sura,then nikastuka toka usingizini, nikabadil upande nikarud kulala, this time kama nusu saa baadae nikaota nakabwa pumzi na mtu nisiyemwona huku amenikandamiza kichwa chini,nikawa napambana kujinasua huku nikitaja damu ya Yesu niokoe, nilihangaika kwa muda then akaniachia na nikaamka ghafla. Sikulala tena, nikaamka na kuendelea na ratiba nyingine ya kumalizia siku.

Kulipopambazuka, nikajiandaa, nikachoma udi then nikaingia mzigon, then saa 11 baada ya muda wa mkoloni, nikaenda sokon nikanunua chumvi ya mawe nikarudi home nikaipigia deki chumbani na sebuleni. Nikachoma na udi ule wa kuwaombea wazee wangu, nikaendelea na ratiba nyingine na hali ikaendelea kuwa shwari hata zile ndoto zikakata.

Kimbembe nimeamka leo nikajiandaa niende job, kabla sijatoka natafuta udi zangu zilizobaki nichome sizioni, nimekagua kote sijaziona, na ninaishi peke yangu, hii nyumba Ina usalama wa kutosha, nimebaki na bumbuwazi. Hapa nimepanga nikitoka job nikanunue za kutosha pamoja na ubani, manake hii nyumba nina wiki tu toka nihamie. Maoni yenu wadau.
Umeianzisha vita ngumu ambayo hutaishinda.
Unachanganya vitu sana.
Kuna ibada ya sanamu na Mungu hivi viwili havichangamani.

Chagua kimoja...udi au Yesu
 
Nimesema unachanganya sbb unatumia udi!
Ww unaemwamimi Yesu hutakiwi kutumia hivyo vitu.
Sawa mpendwa, nyumba Ina madhabahu za kiganga hiyo km kulikuwa na hizo kazi hapo, lkn na we hizo ndoto Zinaonyesha Kuna shida!

Kuna mdau kakuuliza swali zuri hapo unaufahamu ,uelewa kuhusu damu ya Yesu na namna ya kuitumia?

Mi nakuuliza una uelewa kuhusu ndoto kibiblia na namna ya kuziombea?
Nami nimemwambia kuwa vita hii hataishinda.
Mungu hachanganywi na miungu
 
Ndugu yangu sifahamu namna ya kuziombea ndoto kibibilia,na isitoshe ndoto za wazee wangu naziota sana,sielewi tatizo ni nini,nimeuliza baadhi ya watu wazima wamenambia Nina mizimu ya ukoo,so sielewi ndugu,labda unisaidie jinsi ya kudil nazo.
Sawa,Kuna ushauri juu hapo juu wa mdau ,uzingatie pia kadri unavyosikia ndani yako.
Biblia inasema ...hakuna ushirika kati walio hai na wafu....
Lkn pia kuota watu waliokufa,inaweza kuwa ni roho ya mauti inakufuatilia!
Na hiyo roho ya mauti sio lzm iwe kufa Kifo Cha kimwili tu hata kiroho hata kwenye mambo yako ,km uchumi, familia unaweza ona Kila kitu hakiendi...nk

Wakati mwingine inakuwa Kuna kitu wanataka kukurithisha vitu....
Biblia inasema kwenye Waebrania ....agano la urithi lilipo Iko mauti..
Soma Waebrania 9 yote, itakusaidia..
Nami nimemwambia kuwa vita hii hataishinda.
Mungu hachanganywi na miungu
Ngoja tumsaidie
 
Nami nimemwambia kuwa vita hii hataishinda.
Mungu hachanganywi na miungu
Sina miungu ndugu yangu 🙏 nahisi huo udi umeenda kuamsha ishu za watu🤣saiv nimetoka kuongea na mwenye nyumba kanambia atakuja hapo home kesho tuongee,manake yeye anaishi kijijin huko,hii nyumba kaijenga mjini ya kupangisha🙏 ni msukuma🤣🤣
 
Hakuna vya kunirithisha wazee wangu walikuwa watu wa ibada sana 🙏 nahisi hii nyumba Ina kitu hakiko sawa
Sawa,Kuna ushauri juu hapo juu wa mdau ,uzingatie pia kadri unavyosikia ndani yako.
Biblia inasema ...hakuna ushirika kati walio hai na wafu....
Lkn pia kuota watu waliokufa,inaweza kuwa ni roho ya mauti inakufuatilia!
Na hiyo roho ya mauti sio lzm iwe kufa Kifo Cha kimwili tu hata kiroho hata kwenye mambo yako ,km uchumi, familia unaweza ona Kila kitu hakiendi...nk

Wakati mwingine inakuwa Kuna kitu wanataka kukurithisha vitu....
Biblia inasema kwenye Waebrania ....agano la urithi lilipo Iko mauti..
Soma Waebrania 9 yote, itakusaidia..

Ngoja tumsaidie
 
Back
Top Bottom