Mavazi ya Mchungaji Tony Kapola yachunguzwe

Mavazi ya Mchungaji Tony Kapola yachunguzwe

Nimeshawahi sikiliza sermons zake jamaa anamadini sema yupo rational sana stori nyingi. Mavazi sio inshu mbona jamaa yupo smart tu, kupiga sneaker na jinsi sio kigezo cha ku criticise mafundisho yake
 
Nilipohoji kuhusu uvaaji wa mchungaji Tony Kapola kuna watu hususan wanawake walinivaa kwa ukali kwamba nina wivu niwaachie mchungaji wao, kwamba uvaaji wake ni wa kawaida, kwamba uvaaji wa kisasa kwa Watumishi wa Mungu sio tatizo. Binafsi niwaambie UTUMISHI WA MUNGU ni mgumu na unahitaji usiriaz kuliko wengi mnavyofikiri, Yohana alijinyima hadi kuvaa magunia na kula nzige jangwani mnafikiri utumishi ni mwepesi?

Tunarahisisha mno utumishi wa Mungu miaka hii ndio maana wahubiri nao wanahubiri injili mpya nyepesi ya kisasa iliyopakwa maneno matamu ya miujiza, utajiri na mafanikio, hawaihubiri ile injili pure ya Ufalme wa Mungu, ile ya kukemea dhambi kwa ukali wake.

Ndio maana tunaskia Watumishi wengine wanasema hata dukani sigara weka biashara sio ibada, wengine wanasema ndoa sikuiz sio mwili mmoja, wengine wameenda mbali na kusema pesa za majini sio haramu. Utumishi wa Mungu umeonekana ni simple tu hadi kina Irene Uwoya wanataka kufungua makanisa sasa huku bado miili imejaa tattoo.

Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na nchi anahitaji Watumishi VIELELEZO KWAO WAAMINIO. Katika uvaaji, unenaji, utendaji na mwenendo mzima wa maisha kwa ujumla

Kwa Mungu hakuna usasa, sheria zake ni zile zile WAACHE DHAMBI NA KUNIABUBU

Mahubiri ya utajiri, pesa, miujiza na mahusiano yasitutoe kwenye mstari, Mungu sio mrahisi kama tunavyoaminishwa na Watumishi hawa wa kisasa

Tunapaswa kusali kwa imani, kutubu, kufunga na kuomba, Tunapaswa kumuogopa Mungu na kumuabudu kweli. Tunapaswa kuyaheshimu madhabahu yake. Tunapaswa kutambua Mungu ni mtakatifu hadhihakiwi wala kuchanganywa na aina yoyote ya uchafu

Nawasilisha.
Na nani TAKUKURU?
 
hao ni motivational speakers, sio wahubiri, ndio maana wasikilizaji wengi ni wanawake, wanacheka hadi jino la mwisho na wao wanajiona wanaongea vitu vya pointiiii. wala usiwaite wachungaji.
Sasa tuwaache hao wanawake waendelee kuliwa au tuwashtue?
 
Kuna mmoja jana jumapili siku ya pentekoste nilimshangaa sana akihubiri injili ambayo hakuipokea tangu akiwa kijana, najua ujana wake alikuwa moto ila sasa anahubiri injili nyepesi ya kuridhia urembo uliopigwa marufuku enzi hizo. Alimuinua mama mama mmoja alisuka rasta na kujipaka lipstick na wanja akimsifia kuwa anafanya vema kuonekana ana hela za kununua mapambo hayo, hivyo wanawake wote kanisani wawe na hela za kufanya maendeleo ikiwemo kujipamba kwa mapambo ya gharama si dhambi. Tuje kwa hawa vijana wa kileo watumishi wa mungu akina kapole na masanja wanavaa hovyo sana. Ni wachungaji lakini uvaaji wao ni utata mtupu, watasababisha hata mabinti wa makanisa ya nao watavaa hovyo kama wachungaji wao.
 
Back
Top Bottom