KERO Mawaziri wa Elimu na TAMISEMI, Shule ya Msingi Nyerere, Moshi kuna shida kubwa. Tunaomba mtusaidie

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Elimu NI pesa.Hakuna Elimu bure.ndo muelewage.ndo maana wakwao hutawakuta huko mnakoambiwa elimu bure.akili za kuambiwa changanya na zako.mtabakia kuwa na watu wanaojua kupiga kura tu.wenzenu wanatengeneza wapigiwa kura.
Ni kweli hakuna elimu bure. Lakiji wanancjo ndio wanaolipia kupitia kqenye kodi wanazolipa, Wasimamizi wake hawawezi kugeuza jambo hili kuwa wanatufanyia hisani.
 
Unalijua eneo husika na makazi ya wazazi? Hili jambo lilitakiwa lifanyike mwaka jana kabla ya shule kufunga.
Isingeleta tofauti, umbali utazingatiwa, wasiliana na mkuu wa shule na Afisa Elimu Kata kwa usaidizi zaidi.
 
Ndugu John Maviatu, mtaala mpya hauanzi mwaka huu, mbona huelewi? Huko shuleni ulienda kusomea ujinga?
 
Nendenikwamkuuwamkoaaaa acheniujinga

Wawilayaa hana.msaadaa kwahili
 
Afisa elimu amechukua ushauri toka kwa mchepuko wake ambaye hajasoma.
Hivi hivyo vyumba vingine alitaka mchepuko wake ufanye sehemu ya mamma ntilie?
Hawa watu wasio na upeo wanapewaje vyeo?
Hebu hamisheni huyo mtu kwenda wilaya ya same kule Chome au Mbaga.
 
Elimu NI pesa.Hakuna Elimu bure.ndo muelewage.ndo maana wakwao hutawakuta huko mnakoambiwa elimu bure.akili za kuambiwa changanya na zako.mtabakia kuwa na watu wanaojua kupiga kura tu.wenzenu wanatengeneza wapigiwa kura.
Kuongea kiingereza kwako ni elimu na inatakiwa ilipiwe zaidi! Nyerere angekuwepo angesema neno moja tu "UPUMBAVU", yaani kusema "yes sir" nilipie! Nchi ya majuha tumefanya kusema kiingereza ni sawa na kuangalia mechi ya ManU na Man City! Tulipie.
 
Hayo si maamuzi yake yeye anatekeleza maagizo ya mama.
 
Kuongea kiingereza kwako ni elimu na inatakiwa ilipiwe zaidi! Nyerere angekuwepo angesema neno moja tu "UPUMBAVU", yaani kusema "yes sir" nilipie! Nchi ya majuha tumefanya kusema kiingereza ni sawa na kuangalia mechi ya ManU na Man City! Tulipie.
Kwenye mchango wangu nimezungumzia kiingereza?kiingereza NI lugha Tu kama kisandawe.mi nimesema elimu inahitaji pesa kama mnalijua Hilo waacheni watt wenu hapo na mlipie au wahamisheni kama mlivyoambiwa,wapelekeni kule kwa bure.
 
Mleta Mada ameelekeza swala lake kwa Waziri TAMISEMI.
Yupo sahihi kwa mtazamo wangu,aingilie kati kuepusha usumbufu kwa wazazi.
Halmashauri ya manispaa Ina maeneo mengi,wajenge Shule mpya kuepusha kadhia kwa wazazi.
Afisa Elimu anatekeleza maagizo toka kwa mwajiri wake,hawezi kwenda tofauti na maelekezo aliyopewa
 
Mabadiliko ni Jambo la kawaida katika harakati za maendeleo shida inayooneka hapa ni ucheleweshwji wa Taarifa ya kuhamisha wanafunzi wakati shule zinakaribia kufunguliwa.
kwa hakika mabadiliko hayakwepeki. Lakini je? Hayo mabadiliko yamelenga nini? Ni mabadiliko kutoka hasi kwenda chanya?

Na je, na hili mi la msingi. Ingekuwa mabadiliko ndani ya famolia ya DED hakuna ambaye angehoji. Lakini kwa kuwa yanahusisha jamii, hakuna budi kuwa SHIRIKISHI. Haipendezi kwa wanaojiita maofisa kutoa maamuzi bila kuwashirikisha wananchi ambao ndio wanufaika.
 
Kwenye mchango wangu nimezungumzia kiingereza?kiingereza NI lugha Tu kama kisandawe.mi nimesema elimu inahitaji pesa kama mnalijua Hilo waacheni watt wenu hapo na mlipie au wahamisheni kama mlivyoambiwa,wapelekeni kule kwa bure.
Hoja, yaani walipie kwa ajili ya kiingereza tu! Ni upumbavu. Mimi sikubaliani na kuwaambia walipie ili wajue kiingerza au wawsondoe watoto wao kama hawana hela ya kujifunza kiingereza wawaondoe wawapeleke uswahilini!
Wewe unaposema waioweza kulipa wawaondoe watoto wao ni kuunga mkono biashara ya lugha ya kiingereza kuwa ni elimu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…