Mawaziri waliosimama kama Mawaziri awamu ya Sita, Wengine hamna kitu kabisa

Mawaziri waliosimama kama Mawaziri awamu ya Sita, Wengine hamna kitu kabisa

Tatizo ni mfumo tuna walaumu bure maana wote wanategemea mawazo ya mtu mmoja ambaye hakosei
 
Tuwe wakweli tu....Huyu MHAGAMA sijui JENI ni moja ya watu ambao unajiuliza aliwezaje kuwa Waziri....sio tu waziri huyu hana uwezo hata wakuwa katibu kata... UMMY alipaswa kwenda kupractice na kukifanyia kazi alichosomea huko, akiwa competent aishie huko huko.... Ndalichako huyu alipaswa kukaa huko kwenye utendaji wizarani sio kuwa Waziri.... Mulamula naye alipaswa kubaki kuwa Personal secretary wa mtu sio level ya uwaziri...

Tuache sasa kuwapa watu nyadhifa kwa connection, tujitahidi kupima uwezo wao na ikiwezekana kushindanisha na wengine...Mifumo imejaa VILAZA ndio maana kila siku tunalialia...
kwa hiyo umewakomalia wamama tu....mbona huwasemi wababa?
 
Ukweli kabisa kwangu mimi ni mawaili tu mpaka sasa!
Mohamedi Mchengerwa na Geofrey Mwambe.

Hawa wamezishika nafasi zao kwa kujiamini na wanaendasha kazi za Uwaziri kama ipasavyo.

Mohamed Mchengerewa mpaka nimeanza kumfikia come 2030 akae pale juu. Huyu bwana anajitambua sana. Mwambe anajua nini anafanya.

Mwambe kapewa lidude very complex lakini ninamwona kabeba hali ya kujiamini kwa kiasi kinachopaswa huku akiwa makini sana kuendana na Bosi wake.

Anafafanua mambo kwa uelewa mkubwa bila hata ya kusababishiwa kashfa.

Wengine waliokuwa wanaenda vizuri ni Simbachawene ingawa kwa kiasi ninaona ile hali ya kujiamini ilipunguzwa na awamu ya tano. Anatakiwa arudi kawaida yake.

Mkenda alikuja vizuri lakini Mwezi Novemba, 2021 kwake umekuwa mchungu kwa kiasi na ninahisi kapunguziwa confidence kwa kiasi kikubwa ingawa ni Mtendaji mzuri.

Hawa wengine hawa wameshindwa kabisa! Mziki waliokuwa wanaucheza awamu ya tano unawachanganya.

Wanashindwa kubadilika kwa sababu ya kuona aibu. Dr. Mwigulu alikuja na staili ya kuanza kusimama kwenye gari na kutoa mastatement kama Mkuu wa Nchi akifikiri awamu ya sita haitamshtukia.

Baada ya kuona Ndugulile katunguliwa kama kunguru aliyekuwa anavizia vifaranga naye kaufyata! Tatizo la Dr. Mwigulu ni kusaka umaarufu wa kinchi badala ya wa kijimbo. Na 2025 kule jimboni kwake Iramba hapati.

Mawaziri wengine bado sana, akina Kitila Mkumbo, Ndumbaro, Mhagama, Ummy, Ndalichako, Mulamula, wapo wapo tu. Mbaya zaidi ni akina Kabudi ambao wamejificha pangoni, hawana impact yeyotena wapo kama maksai aliyehasiwa!

Mama yangu SSH zingatia sana thread hii, fanya mabadiliko, akina Kabudi, Mkuchika sio vibaya ukiwaondoa. Ukiwaacha kwa nafasi zao kwa muda mrefu kama akina Mhagama wameshajitengenezea networks hatari sana katika potifolios wanazozisimamia na ndiyo maana wana viburi hatari.

Hawa watu watakuja kukuangusha mchana kweupe! Angalau uwafanyie hata reshuffle basi!
Poa. Ila tambua tu kuwa hakuna mpakwa mafuta hata mmoja hapo. Kwa ivo wengine ni viwete ama wakuchechemea wameshindwa kusimama. Ni hayo tu.

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Lukuvi inaisimamia vizuri tu wizara ya ardhi.
Kivipi sasa ikiwa ujenzi holela bado upo
Ukiwa na heka yako moja unaweza kuuzia watu hata 20 na nyumba zikajengwa hapo ovyo
Angekuwa na akili maeneo nje ya mji yangepimwa na kuzingatia mipango miji ili baadaye
 
em ngoja kwanza!
kwani tumeshafanya uchaguzi wa awamu ya sita na kumpata raisi wa awamu ya sita?!!
 
Kweli , hao uliowataja hamna kitu, Ndalichako anafaa kwenye utendaji kuliko kuwa waziri, Ummi Mwalimu nae hamna kitu, kazi matamko tu ili aonekane anaupiga mwingi, huyu mama Mulamula nae haeleweki, Jeni ndo sijui kwa nn bado yupo? Alitakiwa aendelee kufundisha VeTA huko.
Tuwe wakweli tu....Huyu MHAGAMA sijui JENI ni moja ya watu ambao unajiuliza aliwezaje kuwa Waziri....sio tu waziri huyu hana uwezo hata wakuwa katibu kata... UMMY alipaswa kwenda kupractice na kukifanyia kazi alichosomea huko, akiwa competent aishie huko huko.... Ndalichako huyu alipaswa kukaa huko kwenye utendaji wizarani sio kuwa Waziri.... Mulamula naye alipaswa kubaki kuwa Personal secretary wa mtu sio level ya uwaziri...

Tuache sasa kuwapa watu nyadhifa kwa connection, tujitahidi kupima uwezo wao na ikiwezekana kushindanisha na wengine...Mifumo imejaa VILAZA ndio maana kila siku tunalialia...
 
Mhagama pale yupo tu kama mpini ambao hauna jembe .......kati ya vilaza hata huyu yumon...... hangaya
 
Tuwe wakweli tu....Huyu MHAGAMA sijui JENI ni moja ya watu ambao unajiuliza aliwezaje kuwa Waziri....sio tu waziri huyu hana uwezo hata wakuwa katibu kata... UMMY alipaswa kwenda kupractice na kukifanyia kazi alichosomea huko, akiwa competent aishie huko huko.... Ndalichako huyu alipaswa kukaa huko kwenye utendaji wizarani sio kuwa Waziri.... Mulamula naye alipaswa kubaki kuwa Personal secretary wa mtu sio level ya uwaziri...

Tuache sasa kuwapa watu nyadhifa kwa connection, tujitahidi kupima uwezo wao na ikiwezekana kushindanisha na wengine...Mifumo imejaa VILAZA ndio maana kila siku tunalialia...
Kwa hii tathmini yako ni kama hatuna baraza la mawaziri kabisa
 
Back
Top Bottom