Na walimu kabisa wanakatisha masomo kwamba leo saa nne mwisho...asb mstarini tunapigwa trela kwamba picha yenyewe baadaeDah!umenikumbusha mbali sana,miaka ile ya tisini akija mtu wa mazingaombwe masomo yanasimama mnaingia kwa kulipa kiingilio kuanzia sh moja mpaka sh.tano.
Hivi wale ma POWER wa Mazingaombwe wa zamani walikuwa wanatembelea mashule wako wapi siku hizi?
Namkumbuka Power Mabula
Wengi wamechoka au wamekufa isitoshe michezo yenyewe imepoteza mvuto. Walikuwa wengi kina power sangandele,power Bernad,Tx chaka.
Teh, teh, teh! Umenikumbusha mbali sana. Kulikuwa na mwana mazingaombwe maarufu sana kule Lindi alikuwa anaitwa Jeki Magongo!
Inabidi humu ndani tuanze kuamkiana humu hata kama hatuonani, yaani miaka ya Tisini bado mlikuwa praimari tu?Dah!umenikumbusha mbali sana,miaka ile ya tisini akija mtu wa mazingaombwe masomo yanasimama mnaingia kwa kulipa kiingilio kuanzia sh moja mpaka sh.tano.
Angalia trick zao kwenye Channel e ya startimes kipindi kinaitwa breaking the magician's code kila jumamosi saa 1usiku.
kunaa jamaa mmoja alikuwa anaitwa kababa yeeee....anakalia misumari atoboki hahaaa,kuna masi ya mote....KATIKA VITUKO VILIVYO JIRI NIHICHIA.waliitwa wanafunzi wawili mbele wa kike na kiume...jamaa akafanya mambo yake akawapa ndizi za kuiva wakala THEN wakaambiwa waondoke wakasahau kusema thanx.ebana eeh wakaambiwa warudi wakaulizwa kwanini hamjasema asante haya ninipeni ndizi zangu.....akaanzwa demu akaambiwa aruke juu kuruka ndizi ikatoka kupitia njia ya sehemu ya siri...duh nouma[note,dada mwenyewe sister du kweli yanii nikimuona now nacheka sana]mwanaume nae akaanza kutoka coin kupitia njia ya haja kubwa coin kibaoEnzi zile nasoma shule ya msingi kulikuwa na vijana waliokuwa wakija shule kwa ajili ya mazingombwe. Walikuwa wakifika shuleni mara kwa mara kwa ajili ya maonyesho hayo.
Walikuwa wakipewa kibali na mwl mkuu/mwl wa michezo pamoja na kupewa darasa la kufanyia mazingambwe yao kama ukumbi. Pia kulikuwa kiingilio ili kuweza kuingia ukumbini (darasani) kwa ajili ya kuangalia mazingaombwe hayo.
Ndani ya ukumbi, wanaofanyia mazingaombwe walikuwa wakifanya vituko mbalimbali ambavyo baada ya kuvikumbuka nikaamua kuleta uzi huu kwenye hili jamvi la chitchat ili tukumbushane. Nakumbuka:
Naombeni tukumbushane vituko vyilivyokuwa vikifanyika kwenye mazingaombwe
- Kuna siku walimuita mvulana mmoja wakampasua tumbo hadi utumbo ukawa unaonekana kwa nje, baadae wakaongea maneno fulani yule mtu akazinduka na hakuwa na kovu lolote lile
- Siku nyingine wilimuita mtoto aliyekuwa mdogo kuliko wote darasani wakamuweka ndani ya gunia lililokuwa tupu mara baada ya dakika kadhaa... pipi na biskut zikajaa kwenye lile gunia...
Vilevile nimejiuliza maswali yafuatayo:
Mtazamo wako ukoje katika haya?
- Nini kilikuwa kinasababisha tuone mtu aliyepasuliwa tumbo hana hata kovu eneo lililopasuliwa?
- Mazingaombwe bado yanafanyika mashuleni mpaka sasa?
- Je Wizara ya Elimu ilikuwa inakuridhia mazingaombwe kufanyika mashuleni?
Ok mko fine wana JF!!
Nilikua mtaani nkakuta kundi kubwa limekusanyika na kila mmoja akiwa na different facial expression i.e wengine mshangao; wengne wakifurahi; wengine wakiwa makini kufuatilia kila anachokfanya kijana mmoja wa umri wa kati ya 30-40s.ile kuuliza kuna nni nakajibiwa ni mwana mazingaombwe!!!! Nkajpenyeza na kuanza kufuatilia kwa makini but 2 b sure majanga yalifanyika nisijue anatumia ujanja ujanja au ni branch of science which deals with jujue??? Wakuu plz naomba kujulishwa wanamazingaombwe wanatumia uchawi au ni sayance ya kizungu?????