Tetesi: Mazungumzo yaanza Bakhressa kuinunua Channel Ten

Tetesi: Mazungumzo yaanza Bakhressa kuinunua Channel Ten

Bora aiuze tu,a ukiangalia chanel 10 unajua kabisa kuna kitu hakiko sawa,either wafanyakazi hawalipwi mishahara au haina wafanyakazi at all,unaweza kuwa unatazama habari,mtangazaji anasema "ngoja tuungane na mwandishi wetu alieko mahakamani kwa taarifa zaidi" lkn cha ajabu inakuja habari ya nzige kushambulia shamba la mahindi Rukwa,na hali hii huwa sio siku moja ila ni Kila siku
wengine hua wanaongea wenyewe tena wako live on air
 
Bora, maana Chanel 10 ilikuwa hoi kabisa

Afadhali sasa biashara ifanyike ili Watangazaji na Waandishi wao waache kuja ' Kugongea ' chai, chakula na maji ya kunywa huku katika Vibanda vyetu vya Mama Ntilie ambako ' Walalahoi ' wengi akiwemo GENTAMYCINE ndiyo viwanja vyetu vya kujidai. Na kuna Mtangazaji wao mmoja ( jina kapuni ) ukimkaribisha tu Kula usidhani labda ataonja kidogo na ' Kuuchuna ' bali mtaenda nae sawa hadi Sahani inakuwa nyeupe na mnanawa pamoja maji na kuanza kuangaliana huku ' minyoo ' ya kutokushiba ikianza kuchanja mbuga matumboni mwenu.
 
Mimi nilijuwa tu ...maana channel ten tangia walivyo anza kumpromote bashite na Jiwe ndipo walipo poteza wateja ...wakaanza kukosa wadhamini ...wakabaki kulusha mahubiri tu.. ukiingiza siasa kwenye media uwezi kuendelea.... simnaona na E tv sahv wanspumulia ICU...kama sio kukwepa kodi wangekuwa wameshaifunga...zamani ... kiukweli hapa bongo Eatv ndo tv bora ...maana nivigumu kukutana na sura za wanasiasa... ovyo ovyo.
 
Wadau, Katika Hali ya kutaka kuinusuru kampuni ya Africa Media Group ambayo ipo hoi kiuchumi. Mmilikiwa Azamtv na makampuni ya Ssb Salim Bakhera ameanza rasmi mazungumzo mazito na mmiliki wa Channelten Ndugu Rostam Azizi kwa lengo la kuinunua kampuni Hiyo.
Inadaiwa pia kwamba Reginald Mengi pia alikuwa akiimendea Channelten.
Mengi nitawajuza zaidi kadiri mazungumzo yanavyoendelea



Bado ni miaka ya kununua second hand!!?
 
Yule si alimfadhili mamvi akasubiri gawiwo pale mh atakaposhinda urais...ungekuta leo amebinafsishiwa hata mbuga ya serengeti ili kufidia pesa alizotumia!!!.
hahaa..lakini mbona kwenye top list ya natajiri wa tz yupo kwenye namba 2"" so inakuwaje yaani ""? mpka ashindwe kuiendesha hiyo kampuni??
 
Wadau, Katika Hali ya kutaka kuinusuru kampuni ya Africa Media Group ambayo ipo hoi kiuchumi. Mmilikiwa Azamtv na makampuni ya Ssb Salim Bakhera ameanza rasmi mazungumzo mazito na mmiliki wa Channelten Ndugu Rostam Azizi kwa lengo la kuinunua kampuni Hiyo.
Inadaiwa pia kwamba Reginald Mengi pia alikuwa akiimendea Channelten.
Mengi nitawajuza zaidi kadiri mazungumzo yanavyoendelea
Get the facts right, mmiliki wa Channel Ten ni Shabbir Abji, yule mwenye New Africa Hotel na washirika wake akiwemo Tanil Somaiya na sio Rostam Aziz, Rostam yeye anamiliki New Habari ambayo nayo iko hoi!.

Mmiliki wa kwanza wa Channel Ten ikiitwa DTV alikuwa Shabir Dewji na mdogo wake Murtaza Dewji, wakaiuza kwa Mtaliano Franco Tramonatana akaibadili kuwa Channel Ten ndipo akataka kuiuza na mnunuzi wa mwanzo alikuwa ni Mzee Reginald Mengi, TCRA wakazuia kwa hoja kuwa tayari anamiliki vituo vitatu vya TV, ITV, EATV NA Capital TV, Vituo 3 vya Redio, Radio One, EARadio na Capital FM, na magazeti zaidi ya 10, The Guardian, Nipashe, The Financial Times, Kulikoni, Lete Raha, Alasiri, ambayo yako chini ya kampuni ya The Guardian Limited, pia kuna magazeti chini ya kampuni ya Media Solution na shirika la habari la PST, hivyo akakataliwa, ndipo Shabbir Abdji aliyekuwa anamiliki kituo cha CTN akainunua na kuinganisha.

Hivyo Mengi hawezi tena kutaka kuinunua unless TCRA wamebadili kanuni.

P
 
Laana yao ni pale walipotangaza ushindi wa Maalim Seif kuwa ni mshindi wa urasi uchaguzi wa mwaka 1995 ilipokuwa inaitwa DTV
 
Get the facts right, mmiliki wa Channel Ten ni Shabbir Abji, yule mwenye New Africa Hotel na washirika wake akiwemo Tanil Somaiya na sio Rostam Aziz, Rostam yeye anamiliki New Habari ambayo nayo iko hoi!.

Mmiliki wa kwanza wa Channel Ten ikiitwa DTV alikuwa Shabir Dewji na mdogo wake Murtaza Dewji, wakaiuza kwa Mtaliano Franco Tramonatana akaibadili kuwa Channel Ten ndipo akataka kuiuza na mnunuzi wa mwanzo alikuwa ni Mzee Reginald Mengi, TCRA wakazuia kwa hoja kuwa tayari anamiliki vituo vitatu vya TV, ITV, EATV NA Capital TV, Vituo 3 vya Redio, Radio One, EARadio na Capital FM, na magazeti zaidi ya 10, The Guardian, Nipashe, The Financial Times, Kulikoni, Lete Raha, Alasiri, ambayo yako chini ya kampuni ya The Guardian Limited, pia kuna magazeti chini ya kampuni ya Media Solution na shirika la habari la PST, hivyo akakataliwa, ndipo Shabbir Abdji aliyekuwa anamiliki kituo cha CTN akainunua na kuinganisha.

Hivyo Mengi hawezi tena kutaka kuinunua unless TCRA wamebadili kanuni.

P
Nafikiri hii ni sheria ya tume ya ushindani wa kibiashara (FCC). Hii kumzuia Mengi ni sehemu ya wajibu wao kuangalia madhara kibiashara kwenye Mergers and Acquisitions. Kisheria kabla kampuni hazijaungana au kuchukuliwa na nyingine lazima mtoe notice kwa FCC. Mergers and Acquisitions zisipokuwa closely monitored zinaweza kuleta monopoly kwenye biashara kitu ambacho ni hatari.
 
Radio yao Magic FM ndio usiseme, mara kwa mara sauti inabadilika, inakuwa kama imeminywa, mara sauti inakata kabisa, inabidi msubiri,,,,,,,,,,, Halafu matatizo yote haya yakitokea hamna kuwataka radhi wasikilizaji.
Hapo ndio huwa wananishangza,yaani huwa hawaombi radhi kabisa,sijui ndio sabotage yenyewe
 
Hii kampun kumbe Bado ipo hai
Waliuwa tu ile dtv yao
 
Waongee vizuri na mkuu wa mkoa ata wasaidai

Kimsingi chanel ten imezidiwa.yaani huwa wanatoa taarifa zilizopitwa na wakati.habari za juzi unaziona leo
Kuna siku niliona habari a ITV j4 channel 10 nikaona jpili,nilichokiona kwa kweli
 
Daah itakua bora maana sisi wengine tusipolipia king'amuzi tunabakiwa na channel 10 na TBC, yaan inakua kero mpaka unalazimika kulipia tu hata kama bajeti zinagoma.
Kama ikiwezekana wauziane hata kesho tuuu.[emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3]
 
Nafikiri hii ni sheria ya tume ya ushindani wa kibiashara (FCC). Hii kumzuia Mengi ni sehemu ya wajibu wao kuangalia madhara kibiashara kwenye Mergers and Acquisitions. Kisheria kabla kampuni hazijaungana au kuchukuliwa na nyingine lazima mtoe notice kwa FCC. Mergers and Acquisitions zisipokuwa closely monitored zinaweza kuleta monopoly kwenye biashara kitu ambacho ni hatari.
Nimekumbuka, transition of competitive to monopoly capitalism
 
Nadhani sababu ziko wazi sana kwa sasa, nitajaribu kuziweka hapa.
1/Umiliki wa chombo cha habari kwa sasa ni jambo la hatari kimaisha na kibiashara kwa mmiliki mwenyewe.
(Watawala wanaweza kumuandama mmiliki katika maisha yake yake ya kila siku kutokana tu na habari wasioipenda kurushwa katika kituo chake. Mzee Mengi analijua sana hili).

2/Biashara ya matangazo imedorora sana kwenye vituo vingi.
(Makampuni mengi makubwa ya kibiashara yamedorora sana kwa sasa, hayaoni tena umuhimu wa kuendelea kutumia pesa nyingi kufanya promotion za biashara zao kwao nguvu ya manunuzi kwa watanzania umeshuka kwa zaidi ya 50% ukilinganisha na hapo kabla).

3/Hakuna tena uwezekano wa chombo cha habari kwa sasa kuweza kutengeneza Brand yenye nguvu kupitia habari na mijadala huru ili kujenga Huge Capital Bundle width viewer ili uwe ndio mlango wa kuvuta matangazo ya biashara yenye pesa nyingi.

4/Gharama za uendeshaji ni kubwa mno kwa sasa kwa vyombo vya habari. (Kodi imekuwa msumari wa moto, makato ya TCRA nk vinawaumiza wamiliki).

5/Vyombo vya habari vimekuwa vingi mno, na watazamaji wamepungua sana, wako busy na mitandao zaidi.
 
Nadhani sababu ziko wazi sana kwa sasa, nitajaribu kuziweka hapa.
1/Umiliki wa chombo cha habari kwa sasa ni jambo la hatari kimaisha na kibiashara kwa mmiliki mwenyewe.
(Watawala wanaweza kumuandama mmiliki katika maisha yake yake ya kila siku kutokana tu na habari wasioipenda kurushwa katika kituo chake. Mzee Mengi analijua sana hili).

2/Biashara ya matangazo imedorora sana kwenye vituo vingi.
(Makampuni mengi makubwa ya kibiashara yamedorora sana kwa sasa, hayaoni tena umuhimu wa kuendelea kutumia pesa nyingi kufanya promotion za biashara zao kwao nguvu ya manunuzi kwa watanzania umeshuka kwa zaidi ya 50% ukilinganisha na hapo kabla).

3/Hakuna tena uwezekano wa chombo cha habari kwa sasa kuweza kutengeneza Brand yenye nguvu kupitia habari na mijadala huru ili kujenga Huge Capital Bundle width viewer ili uwe ndio mlango wa kuvuta matangazo ya biashara yenye pesa nyingi.

4/Gharama za uendeshaji ni kubwa mno kwa sasa kwa vyombo vya habari. (Kodi imekuwa msumari wa moto, makato ya TCRA nk vinawaumiza wamiliki).

5/Vyombo vya habari vimekuwa vingi mno, na watazamaji wamepungua sana, wako busy na mitandao zaidi.
hizi ndizo facts
 
Back
Top Bottom